Sakata la Loliondo lamvuruga Kikwete

Sakata la Loliondo lamvuruga Kikwete

Walidhani wamasai wangalikuwa bado usingizini, kumbe wenzao walishamshwa siku njyingi. Mtwara kulishindikana hata Loliondo nako kutashindikana. Watanzania wanaamka kwa kasi ya ajabu. Mungu ibariki Tanzania kwa kutuondolea hawa mafisadi wanaotutesha na kuiuza nchi yetu kwa bei ya suti!
 
Pesa ya mwarabu walishakula tangu enzi za kampeni na mikataba binafsi ya biashara yao ya mafuta, return mali ya umma kupitia ardhi ya Loliondo.

Kazi kweli, wana wa Loliondo komaeni mpaka kieleweke na hii itawafungua macho kwingine, kama Dodoma kwenye uranium na kwingineko.

Huu ndio ugaidi wa CCM!
 
Jamani naomba mnikumbushe. Ni tukio gani kweli ambao jk amewahi kuingilia kati na kutoa tamko ama uamuzi rmgogoro wowote ile, uamzi ambao una ladha ya tamko la mkuu wa nchi?​
 
*Sakata la mgogoro unaorindima kwa sasa kuhusu unyang'anywaji wa Ardhi ya Loliondo kwa lengo la kumpa mwekezaji wa kiarabu umemvuruga sana Rais Kikwete na kusita kujitokeza hadharani kulitolea kauli.

*Hapo awali Kupitia kikao cha baraza la mawaziri iliamriwa kuwa WAKAZI WA LOLIONDO WANYANG'ANYWE ENEO HILO na kumtuma Waziri wa Maliasili na Utalii Hamisi Kagasheki kwenda kulisimamia kwa nguvu zote, lakini Kauli ya hivi karibuni iliyotolewa rasmi na CCM kupitia kwa Naibu katibu mkuu wake Mwigulu Nchemba ambaye alitumwa na Secretariety ya CCM akiwa kama mjumbe mkuu wa kamati maalum aliyotumwa kwenda Loliondo kujaribu kutafuta suluhu kwa njia za Kisiasa ya kuwa 'WANANCHI WA LOLIONDO WANA HAKI NA ARDHI YAO NA WAZIRI KAGASHEKI ALIKOSEA KATIKA MAAMUZI YAKE YA KUTAKA KUWANYANG'ANYA ENEO HILO' imemchanganya zaidi rais Kikwete kwa kuwa yeye pia ni mwenyekiti wa CCM na hata mtu aliyewahi kutoa Kibali(Kimakosa?) cha kisheria cha umiliki wa Ardhi hiyo wa wakazi wa Loliondo alikuwa pia waziri wake!!

*Habari za ndani kabisa zinasema kuwa, Rais alikuwa tayari ameamua kumtuma Waziri mkuu Pinda kwenda Loliondo ama kupitia Bunge Kutoa Kauli juu Mgogoro wa Loliondo lakini dakika za mwisho mwisho Pinda alizuiwa(Alikataa?) kufanya jambo lolote maana ingechafua Upepo wote, badala yake Alitumwa Kagasheki aendelee kufa nalo huku Serikali ikipima upepo!!
Sidhani kama ile kauli ya mwigulu ilikuwa kauli rasmi ya ccm...
 
kinachoendelea ni muendelezo wa usanii, ambao ytumeshaushuhudia kwa miaka nane sasa. Kikwete akiwa raisi ambaye ni mwenyekiti wa baraza la mawaziri ameamua ardhi ya watu wa loliondo ipokonywe, mtu huyuhuyu ni mwenyekiti wa chama ambacho kinapinga ardhi ya wa watu wa loliondo kupokonywa.Huu ni mwendelezo wa siasa za kisanii zinazofanyika kwa mtindo wa KUSOMA UPEPO.Kikwete alisoma upepo kipindi cha vuguvugu la kutaka katiba mpya akamuumbua mama selina kombani, akasoma upepo kipindi cha sakata la jairo akamuumbua pinda na alivyoona upepo una kasi kubwa ikamlazimu jairo ang'oke.Kila mara amekuwa akifanya hivyo na alipofanya hivyo, yeye alibaki kuwa mwema na kuumbua viongozi waandamizi wenzake,tusubiri na tuone safari hi nani atakaye umbuliwa.
 
Nimsomapo Rais Kikwete nadhani hajawahi kuvurugwa wala kuumwa au kuumizwa na baya lolote liwapatalo watanzania au Tanzania; kwa hili jamaa namsifu na ataendelea kula sana maisha ya dunia hii kama mzee madiba vile-ni stress-less kabisa jamaa. Nyie mnaodhani hivyo ndio mnaumwa na Tanzania au watanzania, 'any one should come to prove me wrong'
 
Kipande cha ardhi ni zaidi ya hiyo mita za mraba unazosema wewe.

Kitakachomfanya Raisi aingilie kati ni kushindwa kwa watendaji wake kutatua tatizo kwa kufuata haki, sheria na katiba ya nchi, na zaidi kuweka MASLAHI ya nchi na WANANCHI mbele.
mkuu nimeiweka hiyo figure makusudi kuonyesha kwamba ardhi inayoongelea ni ndogo sana ukilinganisha na ardhi yote ya Tz. Ukichukulia kuwa sheria inampa rais mamlaka ya kuwa na final say ya ardhi yeyote hapa nchini sidhani kama kipande cha loliondo kinamuumiza kichwa kama anavyotaka tuamini huyo Tanu.
 
Uzuri wa CCM inazo K@ND-M nyingi sana za kutumia hivyo tusubiri tuone iliyokwisha kutumika ikitupwa pembeni!.

Na utawala huu umevunja rekodi kwa kuzitumia ipasavyo kabla ya kuzi-Damp. Namkumbuka EL, M-K-M -A, MK-MA etc.
 
Jamani naomba mnikumbushe. Ni tukio gani kweli ambao jk amewahi kuingilia kati na kutoa tamko ama uamuzi rmgogoro wowote ile, uamzi ambao una ladha ya tamko la mkuu wa nchi?​
wewe utakua wa 2005...

Tamko la mbayuwayu nadhani utakua ulilisikiasikia japo ulikua bado mdogo.
 
Kauli ya Mwigulu ni changa la macho! Ilichokusudia serikali ndicho kitatekelezwa!

Kwa hili la ardh,i wamasai wako pamoja na watakomaa nalo ikibidi serikali iwamalize wote; pamoja na wale wa kutoka Kenya!!! Itabidi warudishe fedha na hizo suti za waarabu!!
 
kwahiyo wewe unadhani rais ni mtu wakuongea kila siku?kama atahitajika ataliongelea kwa mda atakaotaka ,rais hawezi umizwa kichwa na kipande cha ardhi cha mita 4000 za mraba.

“Dear Guest, Welcome to the UAE.
Enjoy the best network coverage
and other unmatched services only
with Etisalat. Please use<+> or
<00>before the country code for
international calls. For directory services call 181, for availability of
GPRS, MMS 3G roaming services call
Etisalat Travellers help line 8002300
& for inquiries on Tourism,
entertainment, shopping, etc call
7000-1-7000(Roaming rates apply) Have a pleasant stay in the UAE.”
 
Sidhani kama ile kauli ya mwigulu ilikuwa kauli rasmi ya ccm...
Ndugu yangu Tuko wewe unadhani Ile kauli ya Mwigulu Nchemba ni Kauli ya nani? na Kauli ya CCM ni ipi mpaka sasa?

*Jaribu kuunganisha haya ndio utajua kauli ya Mwigulu ndio kauli ya CCM:

1/Mwigulu Nchemba ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM(Mahali popote anakuwepo pasipo Katibu mkuu basi Atakuwa anakaimu nafasi ya katibu mkuu wa CCM ambaye ndiye mtendaji/mratibu mkuu wa CCM)

2/Mwigulu Nchemba alitumwa rasmi na Secretariety ya CCM kama mjumbe mkuu rasmi kwenda kutatua mgogoro wa Loliondo Kisiasa!!(Alienda kujadiliana, kushawishi au kuhitimisha kiini cha mgogoro ule kwa niaba ya CCM, kwa hivyo ni lazima alitakiwa kutoa kauli)

3/Kauli ile aliitoa kwenye mkutano rasmi wa Kichama mbele ya Wananchi(WanaCCM!!), watendaji wote muhimu wa CCM na Serikali.

4/Kabla na hata baada ya Kauli ya Mwigulu Nchemba kutoka hakuna kauli nyingine yoyote uliyowahi kutolewa na CCM taifa kuhusiana na mgogoro wa Loliondo.

5/Toka Secretariety mpya ya CCM kuundwa mwishoni mwa mwaka jana, walikuja na mtindo wa kuwaadabisha viongozi wa serikali hadharani ili kukinusuru Chama mbele ya wananchi(Kauli mbiu ya Chama kuidabisha serikali!!)
 
Last edited by a moderator:
Wakati anakula kiapo alisema hiki kipande si ardhi ya Tanzania? Vinginevyo akiri hadharani kuwa ameshindwa kulinda katiba ya nchi kama alivyoapa. Rais kumpuuza Mtanzania na kumthamini Mwarabu aliyewatumikisha babu zetu kama watumwa na kuwauza kama bidhaa, hii si bure.
hivi unaelewa nini kuhusu loliondo?.

Mi navojua miaka mingi iliyopita kuna waarabu walikodi kitalu cha uwindaji hapo loliondo.
Sasa kinachoendelea sasa sijui,AU KUNA ALMASI IMEGUNDULIKA HAPO hadi kelele zimeanza kuwa toomuch.
 
“Dear Guest, Welcome to the UAE.
Enjoy the best network coverage
and other unmatched services only
with Etisalat. Please use<+> or
<00>before the country code for
international calls. For directory services call 181, for availability of
GPRS, MMS 3G roaming services call
Etisalat Travellers help line 8002300
& for inquiries on Tourism,
entertainment, shopping, etc call
7000-1-7000(Roaming rates apply) Have a pleasant stay in the UAE.”
hiyo tulishaisikia karibu miaka 20 iliyopita.inaonekana hao jamaa waliamua kutumia mtandao wa kwao.kwani hapo pakoje?i mean hapo loliondo,kuna raia wa kiarabu wanaishi,infrastructure zote za kuirate loliondo kama nchi au ni hiyo msg ya simu.?
 
mkuu nimeiweka hiyo figure makusudi kuonyesha kwamba ardhi inayoongelea ni ndogo sana ukilinganisha na ardhi yote ya Tz. Ukichukulia kuwa sheria inampa rais mamlaka ya kuwa na final say ya ardhi yeyote hapa nchini sidhani kama kipande cha loliondo kinamuumiza kichwa kama anavyotaka tuamini huyo Tanu.
Mkuu Elungata nafikiri bado huelewi kabisa dhana nzima ya migogoro ya umiliki wa Ardhi dunia nzima.

*Thamani ya Ardhi sio ukubwa wake tu bali ni;
1/MAHALI ilipo.
2/MAZINGIRA yanayoizunguka ardhi hiyo.
3/RASIMALI inayopatikana katika Ardhi hiyo.
4/HISTORIA katika umilikishaji ardhi hiyo.
5/HALI YA HEWA katika eneo hilo.

*Sasa embu jiulize maswali haya;
1/Kwanini Mwarabu alitoka Kwao Falme za kiarabu na kuja moja kwa moja Tanzania eneo la Loliondo kuja kutaka KUIMILIKI ardhi hiyo unayoiita 'ndogo sana' kwa gharama yoyote?

2/Kwanini Mmasai wa Tanzania hayuko tayari kwa gharama yoyote kuhamishwa eneo hilo Loliondo unaloliita 'dogo sana' kwenda mahali pengine Tanzania kuishi?
 
Last edited by a moderator:
hivi unaelewa nini kuhusu loliondo?.

Mi navojua miaka mingi iliyopita kuna waarabu walikodi kitalu cha uwindaji hapo loliondo.
Sasa kinachoendelea sasa sijui,AU KUNA ALMASI IMEGUNDULIKA HAPO hadi kelele zimeanza kuwa toomuch.
Mkuu Elungata nani alikwambia mwarabu ''alikodi'' hiyo ardhi?

Katika uhalisia ni kwamba Mwarabu ''Alimilikishwa'' ardhi hiyo, ndio maana yuko huru nayo kwa kitu chochote anachokitaka kufanya juu ya ardhi hiyo.
Toka lini Uwindaji ukafanyika kwa ndege za kijeshi, Uchimbaji wa madini, ujenzi wa kiwanja cha ndege, ujenzi wa mikonga ya mitandao ya simu za mkononi nk.

Kama unabisha iambie serikali yako imtimue huyo mwarabu sasa, ili uone moto wake.
 
Last edited by a moderator:
viongozi wetu wa sasa ni tatizo ,mfumo unamlinda zaidi mwekezaji .na mwekezaji huyu anapewa tax holiday ya 5 years ,miaka ikiisha anauza au anabadili jina kwa kweli hapa sioni mantiki ya kumlinda mwekezaji tuwajali wananchi wetu kwanza kwa kuwa investors anaweza kuwekeza popote na si lazima loliondo hata nje ya tanzania wanachojali ni faida bila kujali serikali imepata kodi au la .tujali watu wetu kwanza kama yupo mwenye mtaji apewe nafasi awekeze atoe ajira kwa watz na jamii kwa ujumla alipe kodi taifa lisonge mbele .
 
Natamani kama 2015 ingekuwa kesho wakatutua hili zigo...huu ni wendawazi..
 
Nchemba is out of his mind .. yaani anazuia utekelezaji wa ahadi walizotoa kwa mfadhili wao?
Hivi kwanini kwenye kampeni za urais hawatoi ahadi za kunyang'anya maeneo ya wananchi na kuwapa wageni? hawatekelezi waliyoyatolea ahadi wanatekeleza wasiyoyatolea ahadi..........
 
Back
Top Bottom