Sakata la Joshua Nassari: Mtazamo wangu

Sakata la Joshua Nassari: Mtazamo wangu

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,348
Reaction score
26,144
Ubunge wa aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari umesitishwa/umefutwa katika kile kinachotajwa kuwa hakuhudhuria mikutano mitatu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila ruhusa ya Spika wa Bunge. Katika kutekeleza hilo, Ofisi ya Spika imeijenga hoja yake kwa kutumia Ibara ya 71(1)(c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (kama ilivyofanyiwa marekebisho mara kwa mara)ambayo nainakili hapa chini:

71.-(1) Mbunge atakoma kuwa Mbunge na ataacha kiti chake katika Bunge litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo-
(a).……………………………….(haihusiki)

(b).……………………………….(haihusiki)

(c) ikiwa Mbunge atakosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge Mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika;

Ni dhahiri kuwa Ibara niliyoinakili hapo juu inazungumzia sababu mojawapo ya kukoma kwa Ubunge wa Mbunge yeyote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.ababu hiyo ni kukosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge Mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika. Kulingana na Ibara hiyo, kuna mambo muhimu.

Mosi, Mbunge husika anakosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge mitatu mfululizo. Kulingana na sakata la Nassari, Nassari hakuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge mitatu mfululizo. Ni jukumu lake Nassari nje au ndani ya Mahakama kuthibitisha kuwa alihudhuria vikao vya mikutano hiyo ya Bunge ambayo anadaiwa kuwa hakuihudhuria. Katika hilo, hakutakiwi porojo wala siasa, ushahidi unatosha.

Pili, Ibara tajwa inazungumzia ruhusa ya Spika. Ruhusa ni kibali cha kufanya au kutofanya au kusema au kutosema jambo. Katika uga wa kiutumishi, ruhusa huombwa kwa fomu au barua maalum. Mwombaji wa ruhusa huhakikisha kuwa fomu au barua yake imemfikia ipasavyo mtoa ruhusa na hatimaye amepata ruhusa hiyo kupitia fomu hiyo au barua ya mtoa-ruhusa. Hapo ndipo ruhusa ya kufanya au kutofanya au kusema au kutosema huanza.

Tatu, kwa mujibu wa Ibara niliyoinakili hapo juu na sakata zima la Joshua Nassari, mtoa-ruhusa ni Spika wa Bunge. Ni ruhusa ya kutohudhuria vikao vya mikutano ya Bunge ima chini ya mitatu au mitatu. Joshua Nassari, kwa mujibu wa jambo lake, alipaswa kuomba na kupata ruhusa ya Spika wa Bunge ili kutohudhuria vikao vya Mikutano mitatu mfululizo ya Bunge. Kama aliipata ruhusa hiyo, ni wakati wake nje au ndani ya mahakama kuianika ruhusa hiyo. Kulialia na kuomba huruma kutafuata baadaye.

Kwa uelewa wangu, neno 'mfululizo' limetumika kuonyesha ukubwa wa jambo hilo la kukosa kuhudhuria vikao vya mikutano ya Bunge kwakuwa Miukutano ya Bunge hufanyika kila baada ya miezi kadhaa. Kimsingi, mikutano mitatu mfululizo hubeba kipindi kirefu cha kutosha na ndiyo maana Mbunge anapokosa bila ruhusa ya Spika anapaswa kukoma kuwa Mbunge. Joshua Nassari, pamoja na kuiweka mbele hoja ya kumuuguza mkewe, anapaswa kuuambia umma, wapigakura wake na hata Mahakama (kama atakwenda) kuhusu ruhusa yake kutoka kwa Spika.

Kwakuwa suala la Joshua Nassari ni suala nyeti na linaloweza kujengewa nadharia mbalimbali sahihi na potofu, ni wajibu wake kuweka mambo sawa kwa kuanika ruhusa yake kutoka kwa Spika au ushahidi wake kuwa si kweli kuwa hakuhudhuria vikao vya mikutano mitatu mfululizo ya Bunge.Amasivyo, Katiba, Sheria, Kanuni na Taratibu za Bunge zitampiga kumbo kirahisi sana.
 
Wapinzani wamekuwa wakilalamika na kuona wanaonewa katika kila jambo linalotokea kwao. Inawezekana ni kweli mke wake alikuwa na changamoto, je ni mwanamke huyo tu mwenye changamoto za uzazi? Hivi kama kila mwanaume ataamua kukaa nyumbani kulea mimba ya mke wake kwa miezi tisa kazi zitafanyika kweli? Wakati mwingine tuwe serious bhana, Joshua hapa amechemka.
Japo naona baadhi ya viongozi wake wamejaribu kukubeba na kukutetea, lakini kiuhalisia kukutetea kwenye hili inabidi uwe umekunywa gongo kidogo. Lissu nae ameamua hadi kutoa ujumbe wa uongo kwamba Nassari alimpigia kuomba ushauri na akamwambia vikao vya Novemba alikuwepo lakini kwenye press umesema Novemba ni kweli hakuwepo. JE,
1. Ni kwa nini alikataa kuulizwa maswali na waandishi wa habari ambao amewaita yeye mwenyewe?
2. Ni kwamba viongozi wake wanakurupuka hasa Lissu?
3. Ameona ni njia bora ya kuhama chama bila kuzomewa na kuitwa msaliti?
4. Viongozi wake wamewahi kumuonya juu ya utoro wake Bungeni?
5. Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni kupitia kwa mnadhimu hawakuwa na taarifa juu ya dharura alizokuwa nazo Mbunge wao?
6. Barua anayodai ametuma kwa Spika, kwa nini haikupita kwenye ofisi ya Kambi rasmi ya Upinzani?
 
Wapinzani wamekuwa wakilalamika na kuona wanaonewa katika kila jambo linalotokea kwao. Inawezekana ni kweli mke wake alikuwa na changamoto, je ni mwanamke huyo tu mwenye changamoto za uzazi? Hivi kama kila mwanaume ataamua kukaa nyumbani kulea mimba ya mke wake kwa miezi tisa kazi zitafanyika kweli? Wakati mwingine tuwe serious bhana, Joshua hapa amechemka.
Japo naona baadhi ya viongozi wake wamejaribu kukubeba na kukutetea, lakini kiuhalisia kukutetea kwenye hili inabidi uwe umekunywa gongo kidogo. Lissu nae ameamua hadi kutoa ujumbe wa uongo kwamba Nassari alimpigia kuomba ushauri na akamwambia vikao vya Novemba alikuwepo lakini kwenye press umesema Novemba ni kweli hakuwepo. JE,
1. Ni kwa nini alikataa kuulizwa maswali na waandishi wa habari ambao amewaita yeye mwenyewe?
2. Ni kwamba viongozi wake wanakurupuka hasa Lissu?
3. Ameona ni njia bora ya kuhama chama bila kuzomewa na kuitwa msaliti?
4. Viongozi wake wamewahi kumuonya juu ya utoro wake Bungeni?
5. Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni kupitia kwa mnadhimu hawakuwa na taarifa juu ya dharura alizokuwa nazo Mbunge wao?
6. Barua anayodai ametuma kwa Spika, kwa nini haikupita kwenye ofisi ya Kambi rasmi ya Upinzani?
Hapa Chadema wamethibitisha wao ni chama kidogo!
 
Ubunge wa aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari umesitishwa/umefutwa katika kile kinachotajwa kuwa hakuhudhuria mikutano mitatu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila ruhusa ya Spika wa Bunge. Katika kutekeleza hilo, Ofisi ya Spika imeijenga hoja yake kwa kutumia Ibara ya 71(1)(c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (kama ilivyofanyiwa marekebisho mara kwa mara)ambayo nainakili hapa chini:

71.-(1) Mbunge atakoma kuwa Mbunge na ataacha kiti chake katika Bunge litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo-
(a).……………………………….(haihusiki)

(b).……………………………….(haihusiki)

(c) ikiwa Mbunge atakosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge Mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika;

Ni dhahiri kuwa Ibara niliyoinakili hapo juu inazungumzia sababu mojawapo ya kukoma kwa Ubunge wa Mbunge yeyote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.ababu hiyo ni kukosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge Mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika. Kulingana na Ibara hiyo, kuna mambo muhimu.

Mosi, Mbunge husika anakosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge mitatu mfululizo. Kulingana na sakata la Nassari, Nassari hakuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge mitatu mfululizo. Ni jukumu lake Nassari nje au ndani ya Mahakama kuthibitisha kuwa alihudhuria vikao vya mikutano hiyo ya Bunge ambayo anadaiwa kuwa hakuihudhuria. Katika hilo, hakutakiwi porojo wala siasa, ushahidi unatosha.

Pili, Ibara tajwa inazungumzia ruhusa ya Spika. Ruhusa ni kibali cha kufanya au kutofanya au kusema au kutosema jambo. Katika uga wa kiutumishi, ruhusa huombwa kwa fomu au barua maalum. Mwombaji wa ruhusa huhakikisha kuwa fomu au barua yake imemfikia ipasavyo mtoa ruhusa na hatimaye amepata ruhusa hiyo kupitia fomu hiyo au barua ya mtoa-ruhusa. Hapo ndipo ruhusa ya kufanya au kutofanya au kusema au kutosema huanza.

Tatu, kwa mujibu wa Ibara niliyoinakili hapo juu na sakata zima la Joshua Nassari, mtoa-ruhusa ni Spika wa Bunge. Ni ruhusa ya kutohudhuria vikao vya mikutano ya Bunge ima chini ya mitatu au mitatu. Joshua Nassari, kwa mujibu wa jambo lake, alipaswa kuomba na kupata ruhusa ya Spika wa Bunge ili kutohudhuria vikao vya Mikutano mitatu mfululizo ya Bunge. Kama aliipata ruhusa hiyo, ni wakati wake nje au ndani ya mahakama kuianika ruhusa hiyo. Kulialia na kuomba huruma kutafuata baadaye.

Kwa uelewa wangu, neno 'mfululizo' limetumika kuonyesha ukubwa wa jambo hilo la kukosa kuhudhuria vikao vya mikutano ya Bunge kwakuwa Miukutano ya Bunge hufanyika kila baada ya miezi kadhaa. Kimsingi, mikutano mitatu mfululizo hubeba kipindi kirefu cha kutosha na ndiyo maana Mbunge anapokosa bila ruhusa ya Spika anapaswa kukoma kuwa Mbunge. Joshua Nassari, pamoja na kuiweka mbele hoja ya kumuuguza mkewe, anapaswa kuuambia umma, wapigakura wake na hata Mahakama (kama atakwenda) kuhusu ruhusa yake kutoka kwa Spika.

Kwakuwa suala la Joshua Nassari ni suala nyeti na linaloweza kujengewa nadharia mbalimbali sahihi na potofu, ni wajibu wake kuweka mambo sawa kwa kuanika ruhusa yake kutoka kwa Spika au ushahidi wake kuwa si kweli kuwa hakuhudhuria vikao vya mikutano mitatu mfululizo ya Bunge.Amasivyo, Katiba, Sheria, Kanuni na Taratibu za Bunge zitampiga kumbo kirahisi sana.
Kuhusu suala hili Chadema hawataki kanuni, sheria au katiba itumike; wanataka ''busara za Spika''.
 
Inahitaji uwe na ujasiri wa kipekee kumtetea Joshua Nassari. Analiingiza tu Taifa hasara kurudia uchaguzi kutokana na sababu za kizembe. Labda kama alifanya tu kwa makusudi ili baadae apate sababu ya kurudi nyumbani.
 
Kinachozungumzwa ni ukwel mtupu embu tuone ikutano ya Bunge kwa mwaka..

Bunge limeundwa na vipindi viitwavyo Mikutano. Mkutano wa Bunge ni mfululizo wa vikao vya Bunge, kuanzia kikao cha kwanza hadi cha mwisho. Kuna Mikutano 20 katika Bunge moja.

Kuna mikutano minne katika Bunge.
Mkutano wa kwanza, kati ya Oktoba hadi Novemba;
Mkutano wa pili, kati ya Januari hadi Februari;
Mkutano wa tatu, kati ya Aprili hadi Juni;
Mkutano wa nne, kati ya Augosti hadi Septemba.

So kwa tafsir ya mfano hapo ya Vikao vitatu ni kuanzia October mpka June ya mwaka unaofuatia,
Kwa maelezo ya Nasari ni kwamba alikua anamuuguza Mkewe so naamin Ugonjwa wa zaid ya miez 10 naamin kwa nafas yake na elimu yake Nassari alitakiwa kupta ruhusa ya Ndugai kama sheria inavyosema ili asiingie kwenye haya matatzo ya sasa
 
Ndugu zangu watanzania naomba niwaambie jambo moja kubwa sana lina tesa taifa hili. Nalo sio jingine ni maadili na kuheshim wakati.
Hivi karibuni tumesikia vilio vingi vya watu wakilia kutotendewa haki lakini ukichunguza unakuta mtu mzembe na asie na maadili.
Nassari ameita vyombo vya habari nakusoma vitu mm naweza sema havikuwa na utaratibu.
Huu ndio ukweli..
Kabla mbunge hajaenda nje ya nchi kwa matibabu kuna vibal anapewa je muulizen anacho?
Pili kama nikweli ina maana Tz hapakuwa na Dr wakumsaidia mke wake?
Mengi tutasikia ila ukweli ni mzito
 
Nasari ana machaguo mawili tu, Aendeelee kula maisha kwa kuunga mkono juhudi ili arudi bungeni, au akomae kikamanda akisubiri 2020 ili asitaafu siasa akiwa kijana.
 
Una uhakika? Bila shaka unakerekwa sana na uanasheria wangu? Ndiyo imeshakuwa Mkuu, vumilia. Kama unaamini sina uwezo, endelea kuamini hivyo.
Kwanini nikelwe na uanasheria wako, hivi umesoma vema comment yangu? Irudie soma tena
 
Ubunge wa aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari umesitishwa/umefutwa katika kile kinachotajwa kuwa hakuhudhuria mikutano mitatu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila ruhusa ya Spika wa Bunge. Katika kutekeleza hilo, Ofisi ya Spika imeijenga hoja yake kwa kutumia Ibara ya 71(1)(c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (kama ilivyofanyiwa marekebisho mara kwa mara)ambayo nainakili hapa chini:

71.-(1) Mbunge atakoma kuwa Mbunge na ataacha kiti chake katika Bunge litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo-
(a).……………………………….(haihusiki)

(b).……………………………….(haihusiki)

(c) ikiwa Mbunge atakosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge Mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika;

Ni dhahiri kuwa Ibara niliyoinakili hapo juu inazungumzia sababu mojawapo ya kukoma kwa Ubunge wa Mbunge yeyote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.ababu hiyo ni kukosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge Mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika. Kulingana na Ibara hiyo, kuna mambo muhimu.

Mosi, Mbunge husika anakosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge mitatu mfululizo. Kulingana na sakata la Nassari, Nassari hakuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge mitatu mfululizo. Ni jukumu lake Nassari nje au ndani ya Mahakama kuthibitisha kuwa alihudhuria vikao vya mikutano hiyo ya Bunge ambayo anadaiwa kuwa hakuihudhuria. Katika hilo, hakutakiwi porojo wala siasa, ushahidi unatosha.

Pili, Ibara tajwa inazungumzia ruhusa ya Spika. Ruhusa ni kibali cha kufanya au kutofanya au kusema au kutosema jambo. Katika uga wa kiutumishi, ruhusa huombwa kwa fomu au barua maalum. Mwombaji wa ruhusa huhakikisha kuwa fomu au barua yake imemfikia ipasavyo mtoa ruhusa na hatimaye amepata ruhusa hiyo kupitia fomu hiyo au barua ya mtoa-ruhusa. Hapo ndipo ruhusa ya kufanya au kutofanya au kusema au kutosema huanza.

Tatu, kwa mujibu wa Ibara niliyoinakili hapo juu na sakata zima la Joshua Nassari, mtoa-ruhusa ni Spika wa Bunge. Ni ruhusa ya kutohudhuria vikao vya mikutano ya Bunge ima chini ya mitatu au mitatu. Joshua Nassari, kwa mujibu wa jambo lake, alipaswa kuomba na kupata ruhusa ya Spika wa Bunge ili kutohudhuria vikao vya Mikutano mitatu mfululizo ya Bunge. Kama aliipata ruhusa hiyo, ni wakati wake nje au ndani ya mahakama kuianika ruhusa hiyo. Kulialia na kuomba huruma kutafuata baadaye.

Kwa uelewa wangu, neno 'mfululizo' limetumika kuonyesha ukubwa wa jambo hilo la kukosa kuhudhuria vikao vya mikutano ya Bunge kwakuwa Miukutano ya Bunge hufanyika kila baada ya miezi kadhaa. Kimsingi, mikutano mitatu mfululizo hubeba kipindi kirefu cha kutosha na ndiyo maana Mbunge anapokosa bila ruhusa ya Spika anapaswa kukoma kuwa Mbunge. Joshua Nassari, pamoja na kuiweka mbele hoja ya kumuuguza mkewe, anapaswa kuuambia umma, wapigakura wake na hata Mahakama (kama atakwenda) kuhusu ruhusa yake kutoka kwa Spika.

Kwakuwa suala la Joshua Nassari ni suala nyeti na linaloweza kujengewa nadharia mbalimbali sahihi na potofu, ni wajibu wake kuweka mambo sawa kwa kuanika ruhusa yake kutoka kwa Spika au ushahidi wake kuwa si kweli kuwa hakuhudhuria vikao vya mikutano mitatu mfululizo ya Bunge.Amasivyo, Katiba, Sheria, Kanuni na Taratibu za Bunge zitampiga kumbo kirahisi sana.
kama itathibitika kweli kuwa Nassari hakufuata taratibu kwenye sakata hili, atakuwa amedhihirisha the highest level of irresponsibility na sidhani kama hata anastahili tena kuvaa hadhi ya uwakilishi wa wananchi mahala popote, labda akienda CCM ambao wao ni zoazoa tu bora liende!
 
Kwanini nikelwe na uanasheria wako, hivi umesoma vema comment yangu? Irudie soma tena
Una uhakika mimi sina uwezo wa kubishana na Mawakili wenzangu mahakamani? Kwahiyo kazi zangu za kila siku nazifanyia wapi? Mkuu, jifunze kuheshimu kazi na tasnia za watu. Achana na huyo Ibambasi anayelazimisha mabishano
 
Una uhakika mimi sina uwezo wa kubishana na Mawakili wenzangu mahakamani? Kwahiyo kazi zangu za kila siku nazifanyia wapi? Mkuu, jifunze kuheshimu kazi na tasnia za watu. Achana na huyo Ibambasi anayelazimisha mabishano
Alafu mkuu mtu professional kama wewe inabidi uwe makini sana endapo mtu ana ku provoke kwenye nyuzi zako, wengine tupo kuwatoa mtu kwenye mood, na wengine kejeli ni nyingi, na wengine tupo kuchochea kejeli kuona muhusika ata react vipi,

Comment nyingine unaachana nazo mkuu,
 
Back
Top Bottom