Sakata la IPTL na ESCROW: Kafulila aanza kuumbuka, sasa kusambaza umeme MW 2000 Kenya

KAFULILA AUMBUKA KWA KUSEMA SETH HATAKIWI KENYA
View attachment 186998
mmililki wa IPTL na mwakandege mwanasheria wa IPTL

KAMPUNI ya kufua umeme ya Pan African Power Solution inayoimiliki kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) imezidi kung’aa katika nchi za jumuia ya Afrika Mashariki katika kusambaza nishati ya umeme.

Hatua hiyo inasababishwa na serikali ya Kenya kuipatia barua kampuni hiyo ya kufanya nao kazi ya usambazaji umeme katika mradi unaohusisha nchi mbili za jumuia hiyo, ambazo ni Tanzania na Kenya.

Barua ya Kenya iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Petroli, Injinia Joseph .K. Njoroge ya tarehe 19, Agosti 2014 kwenda kwa Mwenyekiti Mtendaji wa PAP, Harbinder Sing Sethi.

Taarifa zaidi kuhusiana na barua hiyo, yenye kumbukumbu namba ME&D/CONF/3/2/73A iliyokuwa na kichwa cha habari Expression of interest for IPP for 2000MV power generations and supply to Kenya and Tanzania.

Barua hiyo, ilieleza kuwa inazitaka pande tatu hizo ikiwemo PAP, Tanzania na Kenya kukutana haraka kuona ni namna gani uzalishaji huo utaanza haraka iwezekanavyo.
Akithibitisha barua hiyo, Katibu na Mwanasheria Mkuu wa IPTL/PAP, Joseph Makandege alisema kampuni yao inaendelea kuchapa kazi na haitishiki na kauli za wanasiasa kwa kuwa wao si wanasiasa.

‘’Tunafurahi kuwa tunazidi kuaminiwa na serikali mbalimbali ndani na nje ya Tanzania. Hii inadhirisha ufanisi na ueledi wetu katika tasnia nzima ya nishati,’’alisema.

Hivyo, alisema anaamini maneno yote yanayoenezwa juu yao kuwa yanatawaliwa na chuki na wivu wa kibiashara kutoka kampuni zingine za usambazaji wa umeme.

Kutolewa kwa barua hiyo kwa IPTL kutaweza kuondoa sintofahamu iliokuwepo, baada ya Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila(NCCR- Mageuzi) kudai kuwa Seth anayeongoza kampuni hiyo amepigwa marufuku kufanya biashara ya aina yoyote Kenya.

Kafulila alinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini hapa, kuwa Seth ni fisadi na kwamba Kamati ya Bunge ya nchini Kenya imempiga marufuku kufanya biashara nchini humo.
===================================



Chanzo: habarileo
Kafulila amefeli kutofautisha Kampuni ya IPTL iliyotokana na Muungano wa kampuni ya Mechmar (Malaysia) Berhard (70%) na VIP(30%), na kampuni ya PAP/IPTL iliyoundwa baada ya kununuliwa kampuni kwa kampuni hizo hapo juu,hivyo kitendo cha kuzungumzia utendaji kazi wa kampuni ya IPTL(CHINI YA PAP) kwa kuihusisha na kampuni ya IPTL chini ya Mechmar na VIP ni kuionea PAP na kuikosea kampuni hii ya PAP/IPTL.
 
Toka mwanzo nilijua kuwa hii filimbi inayopulizwa na kaka yangu Kafulila ni ya udongo wa kinyesi. Ahh! Kafulila chimba shimo la kujifukia mapema maana huko mbele tuendako wananchi watakutambua kwa true colour yako, sisimizi/Tumbili.
Kafulila amefeli kutofautisha Kampuni ya IPTL iliyotokana na Muungano wa kampuni ya Mechmar (Malaysia) Berhard (70%) na VIP(30%), na kampuni ya PAP/IPTL iliyoundwa baada ya kununuliwa kampuni kwa kampuni hizo hapo juu,hivyo kitendo cha kuzungumzia utendaji kazi wa kampuni ya IPTL(CHINI YA PAP) kwa kuihusisha na kampuni ya IPTL chini ya Mechmar na VIP ni kuionea PAP na kuikosea kampuni hii ya PAP/IPTL.
 
Eheee! Kweli mungu amfich mnafiki
Nilisema mimi jaman huyu kafulila ataumbuka vibaya aya ona sasa anavyo anza kuumbuka
Aya acha move iendele

Hapana kafulila hajafeli kutofautisha kati ya hayo makampuni, anajua fika kila kitu shida ni kuwa ameamua kwa makusudi kuchafua taswira ya IPTL baada ya PAP/IPTL kukataa kumpa fedha aliyoiomba kwao eti ili afunge mdomo,sasa kinachofuata IPTL wameamua sharia itawale wamempeleka mahakamani na watapeleka ushahidi wa jinsi alivyoomba fedha ili anyamaze, na bilioni 300 atawalipa IPTL, ILI LIWE FUNZO KWA WABUNGE WENYE UCHU WA FEDHA ZA HARAKA HARAKA,
 
Pap/iptl kwa kipindi kilichoanza kufanya kaziz nchini wamejitahidi sana kusahihisha makosa yaliyokuwa yamefanywa na iptl ya mechmar na vip,ambayo gharama ya uzalishaji ilikua juu na pia pap/iptl imejitahidi kumaliza migogoro mingi iliyokuta tanesco wanayo juu ya iptl
 
Duuh! mkuu rechosawe! Kafulila atapenyea wapi jamani hii si aibu? hafu hii tabia ya kuwa msemaji wa serikali ya kenya alianza lini kafulila? maana siku ile bungeni mpaka mishipa ilikuwa inamtoka utafikiri yeye ndo msemaji wa serikali ya kenya, aya sasa hata jua halijazama IPTL wamepewa kazi na serikali hiyohiyo alosema SETH hawezi kupewa kazi nchini kenya. Ukiwa muongo jitahidi kuwa na kumbukumbu utafedheheka mjini hapa. hao akina mkono wamekuingiza chaka bovu

Pap/iptl kwa kipindi kilichoanza kufanya kaziz nchini wamejitahidi sana kusahihisha makosa yaliyokuwa yamefanywa na iptl ya mechmar na vip,ambayo gharama ya uzalishaji ilikua juu na pia pap/iptl imejitahidi kumaliza migogoro mingi iliyokuta tanesco wanayo juu ya iptl.
 
naomba niulize wana jamvi hivi kati ya symbion na iptl hipi hipi inatoza chaji kubwa kwenye kuiuzia tanesco umeme
 
huu uzi wote umejaa vibaraka wa PAP mpaka kina MTV wanajisahau na kusema " mlitaka tuwape umeme bure tanesco" mi nawashauri muache kupiga kelele na tusubiri ripoti itoke ili tujue nani mwizi nani tumbili
 
Kwa kijana wa Tanzania ya leo, kupata hela ndiyo kila kitu kwenye maisha na ndiyo maana si ajabu kuona kwamba Taifa letu sasa limeanza kujipatia sifa ya kupuuzia wizi unaokandamiza maisha ya Watanzania.Tumeyasikia na kuyashuhudia yaliyotokea huko nyuma ambayo ni matokeo ya wizi dhidi ya mali ya umma - See more at: Raia Mwema - UKAWA: Mbona hamsemi kitu kuhusu IPTL?

oja yangu hii inawahusu viongozi wa juu wa UKAWA. Wameikalia kimya Escrow, hatuisikii sauti ya Freeman Mbowe, Profesa Ibrahim Lipumba na James Mbatia. Wapo wananchi ambao tayari wameanza kuhoji kuhusu ukimya huu.
Mwanasiasa pekee wa upinzani ambaye anaonekana kuguswa na suala hili ni Mbunge wa Kigoma Kusini kupitia NCCR, David Kafulila. Wanashindwa hata kujifunza kutoka kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ambaye ingawa si mjumbe wa UKAWA, ameungana na Kafulila katika kupigania pesa ya Escrow iliyochotwa BOT irejeshwe
- See more at: Raia Mwema - UKAWA: Mbona hamsemi kitu kuhusu IPTL?
 
huu uzi wote umejaa vibaraka wa PAP mpaka kina MTV wanajisahau na kusema " mlitaka tuwape umeme bure tanesco" mi nawashauri muache kupiga kelele na tusubiri ripoti itoke ili tujue nani mwizi nani tumbili

Member km mtv yupo hapa kuchafua tu hali ya hewa hajui asemacho yeye anatafuta kutupandikiza hukumu zilizotoka kimakosa na kuziona ni haki
Kwanza ukiona mahali kaingia Mangi au Manka au Singasinga ujue wanalinda pesa tena ya kipuuzi hata ya kumuua mtu
attachment.php

naona unapangia watu watete nini acaha kushika mawazo ya watu wewe acha watu wachangie wanavyo weza
sasa hapa Kekuu unataka ninyamaze km Kafulila? mm nilimwambia mwenzako Manka kajiunga humu juzi kwa ID fake ili kuja kutetea UOZA wenu
Iko siku itafika ukweli utajulikana kwani hata TTCL walikuwa na ukiritimba wa namna hiyohiyo
 
Last edited by a moderator:
Hapana kafulila hajafeli kutofautisha kati ya hayo makampuni, anajua fika kila kitu shida ni kuwa ameamua kwa makusudi kuchafua taswira ya IPTL baada ya PAP/IPTL kukataa kumpa fedha aliyoiomba kwao eti ili afunge mdomo,sasa kinachofuata IPTL wameamua sharia itawale wamempeleka mahakamani na watapeleka ushahidi wa jinsi alivyoomba fedha ili anyamaze, na bilioni 300 atawalipa IPTL, ILI LIWE FUNZO KWA WABUNGE WENYE UCHU WA FEDHA ZA HARAKA HARAKA,
Kuliko mlipwe ni bora tuwafutilieni mbali, maana mmezidi na wizi wa kiajabuajabu
Mara umeme unakatikakatika
mara Gesi haitoshi kuzungusha mitambo
yaani humu jamvini mnajionesha msivyo na Uzalendo kabisa
Maji ya mito ni yetu, Gesi ni yetu
hao Mabwana zenu wamekuja na Mabrief-case tu ndio mje mumdai Kafulila Bilioni 300
sasa tutaandamana na hivyo vyama 2 vya siasa vilivyotangaza kuwa wataandamana Nchi nzima mpaka Ripotu hiyo ya Utooh isomwe Bungeni
na Muondoke kabisa turudi kwenye umeme wa Generator au wa jua
 
huu uzi wote umejaa vibaraka wa PAP mpaka kina MTV wanajisahau na kusema " mlitaka tuwape umeme bure tanesco" mi nawashauri muache kupiga kelele na tusubiri ripoti itoke ili tujue nani mwizi nani tumbili
kweli humu vibaraka wa kafulila wamejaaa sana ngoja tusubiri ripot ya CAG then tuone na mwenye makosa
kingine mkaka kuchagua nupande wa kutetea sio kuwa kibaraka kama unavyo fikilia kwa mfano mimi nimefatili huu mchako toka A-Z na nikajua kwamba hapa kuna ugomvi wa kibiashara kati ya wafanyabiashara wakubwa na haohao wanatumia weakness za baadh ya wabunge wetu ili wajalibu kuongopea umma lakini sasa watz tumestukia mchezo
Kwani wewe mbona ujiulizi toka issue ianzee ni kafulila tu ndo anaifatilia inamaana wa bunge wa upinza ni yeye au yeye ndo mzalendo peke yake
kuna kitu hapo nyuma pazia hapo
 
Kuliko mlipwe ni bora tuwafutilieni mbali, maana mmezidi na wizi wa kiajabuajabu
Mara umeme unakatikakatika
mara Gesi haitoshi kuzungusha mitambo
yaani humu jamvini mnajionesha msivyo na Uzalendo kabisa
Maji ya mito ni yetu, Gesi ni yetu
hao Mabwana zenu wamekuja na Mabrief-case tu ndio mje mumdai Kafulila Bilioni 300
sasa tutaandamana na hivyo vyama 2 vya siasa vilivyotangaza kuwa wataandamana Nchi nzima mpaka Ripotu hiyo ya Utooh isomwe Bungeni
na Muondoke kabisa turudi kwenye umeme wa Generator au wa jua
tatizo la wabongo tunakalili na sio kuelewa sasa wewe ushamezeshwa kamwe uwezi kubadilika
ndo maana watz weng sio compitenty
 
safari hii mtang'oka nawaambieni Kafulila si mchezo hata km kuna Wasaliti wa Nchi yetu lakini wizi mnaotuibia tutaandamana, msijifanye kubadili ID zenu kuja kutoa 'Like'
Kafulila Go go go go

Wajinga ndiyo waliwao

Ezekiel Kamwaga
Toleo la 373
1 Oct 2014

373_iptl.jpg


  • IPTL yanunuliwa kwa fedha zake yenyewe
KAMPUNI ya Pan African Power (PAP) iliinunua Kampuni ya Independent Power (IPTL) siku chache baada ya kulipwa mabilioni yaliyokuwepo katika Akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwapo katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Raia Mwema limebaini.
Ushahidi wa nyaraka ambao gazeti hili limeupata wiki hii, unaonyesha kwamba tayari mmoja wa wabia wa IPTL alikuwa amelalamika na kuomba PAP wasilipwe fedha za Escrow kwa vile hawajamlipa fedha zake, lakini alilipwa baada ya BoT kulipa fedha kwa PAP.
Taarifa hizi mpya zinaibua uwezekano kwamba huenda PAP ilitumia fedha za IPTL ‘kuinunua',
Kafulila pia aliwahi kulieleza gazeti hili kwamba kwa vile serikali inalipa gharama za uendeshaji wa mitambo kwa IPTL, Seth na PAP wana uhakika wa kujipatia walau shilingi bilioni nne kila mwezi kutoka serikalini. -
See more at: Raia Mwema - Wajinga ndiyo waliwao
 
Member km mtv yupo hapa kuchafua tu hali ya hewa hajui asemacho yeye anatafuta kutupandikiza hukumu zilizotoka kimakosa na kuziona ni haki
Kwanza ukiona mahali kaingia Mangi au Manka au Singasinga ujue wanalinda pesa tena ya kipuuzi hata ya kumuua mtu
attachment.php


sasa hapa Kekuu unataka ninyamaze km Kafulila? mm nilimwambia mwenzako Manka kajiunga humu juzi kwa ID fake ili kuja kutetea UOZA wenu
Iko siku itafika ukweli utajulikana kwani hata TTCL walikuwa na ukiritimba wa namna hiyohiyo
daaa!!!!!!! kweli mkaka unakalili vibaya sana pole mwaya
lakini ukweli utabaki kuwa ukweli kama
kafulila anadiliki kutumika kwa wafanyabiashara wakubwa ili kuongopea umma hii dhambi itamgharimu maisha yake yote
 
Kwa kijana wa Tanzania ya leo, kupata hela ndiyo kila kitu kwenye maisha na ndiyo maana si ajabu kuona kwamba Taifa letu sasa limeanza kujipatia sifa ya kupuuzia wizi unaokandamiza maisha ya Watanzania.Tumeyasikia na kuyashuhudia yaliyotokea huko nyuma ambayo ni matokeo ya wizi dhidi ya mali ya umma - See more at: Raia Mwema - UKAWA: Mbona hamsemi kitu kuhusu IPTL?

oja yangu hii inawahusu viongozi wa juu wa UKAWA. Wameikalia kimya Escrow, hatuisikii sauti ya Freeman Mbowe, Profesa Ibrahim Lipumba na James Mbatia. Wapo wananchi ambao tayari wameanza kuhoji kuhusu ukimya huu.
Mwanasiasa pekee wa upinzani ambaye anaonekana kuguswa na suala hili ni Mbunge wa Kigoma Kusini kupitia NCCR, David Kafulila. Wanashindwa hata kujifunza kutoka kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ambaye ingawa si mjumbe wa UKAWA, ameungana na Kafulila katika kupigania pesa ya Escrow iliyochotwa BOT irejeshwe
- See more at: Raia Mwema - UKAWA: Mbona hamsemi kitu kuhusu IPTL?

Sasa hapo ndo uamini kwamba kafulila anafungu lake kashamegewa na kinarostam ili kuwaalibia iptl
mkuu hi issue ni ya kibiashara baina ya wafanyabiashara wakubwa wale walio shindwa kupata tenda kwa tanesco leo hii ndo wamegeuka kuwa maadu wa iptl
Sas hapo ndo tunakuja kujua weakness ya mkuu kafulila na ndo maana huu mchako yupo peke yake
Mbona richmond wanasiasa wengi walilivalia njuga ,epa mbona weng walilivamia yani hapo kuna kitu nyuma ya pazia wewe anza kufatilia ndo utaanza kugundua kwamba huu mchezo ni wakuchafuana tu na wengine kutengeneza majina yao kisiasa
 
safari hii mtang'oka nawaambieni Kafulila si mchezo hata km kuna Wasaliti wa Nchi yetu lakini wizi mnaotuibia tutaandamana, msijifanye kubadili ID zenu kuja kutoa 'Like'
Kafulila Go go go go

Wajinga ndiyo waliwao

Ezekiel Kamwaga
Toleo la 373
1 Oct 2014

373_iptl.jpg

Tatizo mkuu hoja zako azina mashiko ya kumshawishi mtu
bali ni za kulazimisha tu ebu rudi nyuma chambua mambo then uje na hoja zilizo shiba ok mkuu
 
daaa!!!!!!! kweli mkaka unakalili vibaya sana pole mwaya
lakini ukweli utabaki kuwa ukweli kama
kafulila anadiliki kutumika kwa wafanyabiashara wakubwa ili kuongopea umma hii dhambi itamgharimu maisha yake yote
unajua ID za kutunga zitakudhiri kwani ww sio mchagga ila umeingia kwenye tamaa ya fedha ya kutumaliza Watanzania tunaotetewa na kafulila
wa kawaida hizi ni fedha zinazowekwa katika benki wakati pande mbili zinazozana mahakamani. Huwa zinatolewa kufuatia uamuzi wa mahakama.
Kwa mujibu wa Kafulila "Muhongo alisema uongo mbele ya Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwamba uamuzi wa kutoa fedha za Escrow kwa IPTL ulikuwa wa Mahakama na serikali isingeweza kwenda kinyume."
Haya yanapingwa na Kafulila ambaye anasema katika hukumu hiyo ya Septemba mwaka jana, hakuna mstari hata mmoja unaosema kuwa fedha za Escrow wapewe kampuni ya IPTL.
Kafulila anadai Profesa Muhongo aliliambia Bunge kuwa serikali ililipa fedha hizo ili kuondokana na kesi hiyo lakini yeye Kafulila anadai ana nyaraka za Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kuteua kampuni mbili za uwakili kwenda kuiwakilisha katika kesi nchini Uingereza.
Ndipo hali ilianza kuchafuka
- See more at: Raia Mwema - Umma wastahili kujua ukweli wa fedha za IPTL

Kafulila anasema Mahakama haikutoa hukumu kuwa fedha za Escrow zichukuliwe. Hii inakaririwa na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe ambaye anasema ameangalia hukumu iliyotolewa na Jaji Utamwa na hakuona chochote kuhusu Escrow.
Halafu akaangalia muhtasari wa mkutano baina ya Tanesco, IPTL na Wizara. Humo akaona tafsiri yao ya hukumu ya Mahakama, ikisema fedha za Escrow zilipwe kwa kampuni ya PAP ambayo inamilikiwa nusu na Bw Harbinder Singh na nusu na hifadhi ya Simba iliyosajiliwa Australia.
Zitto anapaswa ashukuriwe kwa kusambaza katika mtandao uamuzi wa Mahakama pamoja n
- See more at: Raia Mwema - Umma wastahili kujua ukweli wa fedha za IPTL
 
Kafulila anafahamu fika
kuanzia tangu kusaniwa kwa makubaliano ya
ESCROW Julai 5, 2006, TANESCO walikuwa
wanaendelea kupatiwa umeme kila siku, kwa
kiasi kilekile wanachokihitaji wao mpaka leo
hii na anajua kwamba, TANESCO walikuwa
hawailipi IPTL na badala yake fedha walikuwa
wanaziweka katika akaunti ya ESCROW, Je
Kafulila alitaka tuwape umeme bure TANESCO.
Je yeye anapofanya kazi bungeni halipwi?,
Anapokaa katika vikao vyake hapewi posho au
wanaomtuma kueneza uongo hawamlipi?.
Kafulile aache kutumika vibaya.

Nimekuelewa mkuu tena sana

Mafuta yalikuwa yananunuliwa na Serikali na ndio maana ule mpango wa Serikali wa kukabiliana na upungufu wa nishati ya umeme ulizua utata sana kuhusu kiwango cha mafuta yaliyonunuliwa
 
Tatizo mkuu hoja zako azina mashiko ya kumshawishi mtu
bali ni za kulazimisha tu ebu rudi nyuma chambua mambo then uje na hoja zilizo shiba ok mkuu
pesa mbaya ndugu yangu kwani WaTZ tunazungukana wenyewe kwa wenyewe
sijui mpaka hapo hajaelewa nini hasa cha kufafanuliwa kuwa tunaibiwa wakati Umeme na maji ni rasilimali zetu
Hapa Ponjoro anawahonga Waandishi wa Habari kuwanyamazisha kwanini asiende kuchimba visima km SABODO
IPTL 2.jpg
Na humu JF wanaolipwa wanaionesha OLE WAO
IPTL 1.jpg
 
unajua ID za kutunga zitakudhiri kwani ww sio mchagga ila umeingia kwenye tamaa ya fedha ya kutumaliza Watanzania tunaotetewa na kafulila
wa kawaida hizi ni fedha zinazowekwa katika benki wakati pande mbili zinazozana mahakamani. Huwa zinatolewa kufuatia uamuzi wa mahakama.
Kwa mujibu wa Kafulila “Muhongo alisema uongo mbele ya Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwamba uamuzi wa kutoa fedha za Escrow kwa IPTL ulikuwa wa Mahakama na serikali isingeweza kwenda kinyume.”
Haya yanapingwa na Kafulila ambaye anasema katika hukumu hiyo ya Septemba mwaka jana, hakuna mstari hata mmoja unaosema kuwa fedha za Escrow wapewe kampuni ya IPTL.
Kafulila anadai Profesa Muhongo aliliambia Bunge kuwa serikali ililipa fedha hizo ili kuondokana na kesi hiyo lakini yeye Kafulila anadai ana nyaraka za Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kuteua kampuni mbili za uwakili kwenda kuiwakilisha katika kesi nchini Uingereza.
Ndipo hali ilianza kuchafuka
- See more at: Raia Mwema - Umma wastahili kujua ukweli wa fedha za IPTL

Kafulila anasema Mahakama haikutoa hukumu kuwa fedha za Escrow zichukuliwe. Hii inakaririwa na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe ambaye anasema ameangalia hukumu iliyotolewa na Jaji Utamwa na hakuona chochote kuhusu Escrow.
Halafu akaangalia muhtasari wa mkutano baina ya Tanesco, IPTL na Wizara. Humo akaona tafsiri yao ya hukumu ya Mahakama, ikisema fedha za Escrow zilipwe kwa kampuni ya PAP ambayo inamilikiwa nusu na Bw Harbinder Singh na nusu na hifadhi ya Simba iliyosajiliwa Australia.
Zitto anapaswa ashukuriwe kwa kusambaza katika mtandao uamuzi wa Mahakama pamoja n
- See more at: Raia Mwema - Umma wastahili kujua ukweli wa fedha za IPTL

Du kweli mkuu noma kumbe unaotea mpaka makabila ya watu
Mmmmhhhhhh umetisha mtabiri
 
Back
Top Bottom