Sakata la Corona: BBC acheni unafiki, heko (KM) Wizara ya Afya, Prof. Mchembe kwa nyundo yako jana

Weka ushahidi mkuu maneno matupu hayavunji mfupa.
Mnachekesha sana. Kwa kusudi kabisa, hamuweki kumbukumbu za waliokufa kwa corona wala kupima, ili mkiulizwa muweze kusema leta ushahidi.
Kuna nyuzi nyingi tu humu za watu waliofiwa na ndugu zao kutokana na corona, mfano kifo cha Padre Shewiyo kama sikosei.
 
Hao viongozi unao waamini, ndio hao hao wanaenda nje kuifuata kwa ajili yao na familia zao,ambao wanaogopa wanawatumia watu.kama wote tunakaa tu ingekuwa poa, ila tunachezeana viini macho
 
Mnachekesha sana. Kwa kusudi kabisa, hamuweki kumbukumbu za waliokufa kwa corona wala kupima, ili mkiulizwa muweze kusema leta ushahidi.
Kuna nyuzi nyingi tu humu za watu waliofiwa na ndugu zao kutokana na corona, mfano kifo cha Padre Shewiyo kama sikosei.
Kuna mwingine lecture UDSM nasikia nimonia
 


Ni matangazo ya biashara wakati ata huko kwao wana watu wenye akili kama zetu, awataki chanjo; mbona wana report.

Kuizuia covid sidhani kama ni mission ndogo, chanjo kwa sasa ni kwa ajili ya over 50 years, front line worker na watu wenye magonjwa mengine serious.

Lengo ni kuyalinda hayo makundi kwa sababu wakipata ndio wenye chance kubwa za kuathirika zaidi au kupoteza maisha.

Wakishachanja hayo makundi maisha yaendelee wewe kama ujafika umri huo na wala auna maradhi ya muda mrefu inabidi upambane na COVID tu kwa mtindo wako hata huko kwao hiyo ndio plan wakishamaliza kuwachanja wanaokusudiwa.
 
Mnachekesha sana. Kwa kusudi kabisa, hamuweki kumbukumbu za waliokufa kwa corona wala kupima, ili mkiulizwa muweze kusema leta ushahidi.
Kuna nyuzi nyingi tu humu za watu waliofiwa na ndugu zao kutokana na corona, mfano kifo cha Padre Shewiyo kama sikosei.
Kwa hiyo huo dio ushahidi wako? Grow up!
 
Kama chombo cha habari kazi yake ni ku report sioni kosa lao...kama wamefikisha ujumbe kama walivyopokea.

Kama korona ni janga la dunia na Tanzania ni moja ya hizo nchi za duniani kwani kupokea ushauri kuna tatizo gani.. Kama nyie hamtaki basi sawa..tambulisheni chanjo yenu na dunia ijue ...tuwasaidie na wengine pia.
Heshima yako mkuu. Hebu chukulia mfano huyu ni baba jukumu lake ni kuilinda familia yake sasa baba anakataa chanjo hana mpango wowote wa kuinusuru familia yake na hii shida inayotokea yeye anaona bora siku ziende tu. Tumchukuliaje baba wa aina hii SHIDA KUBWA
 
Ndio maana hatupokei haraka haraka ,tunataka kujiridhisha
Kwakwel bila hivyo tunacheza na Bill Gate atatuangamiza.kwann watupangie aina ya chanjo wakati nchi nyingi zimetengeneza chanjo. Tunaweza kuagiza hata Iran, Russia au popote kwa uwezo wetu na kwa kujiridhisha.

Tunaweza kuharakisha badala ya kujitibu tukajimaliza.
 
Tusifanye utani ugonjwa upo na unaua,, tuendelee kumuomba Mungu bila kusahau kutumia njia za asili_kujifukiza,,mazoezi,,n.k
 
BBC wamekua wepesi sana kurusha matamko dhidi ya Tanzania yatolewayo na shirika la afya duniani kupitia wakurugenzi wake kuhusiana na ugonjwa wa covid 19 hasa yale yenye kuonyesha mbinyo kwa nchi yetu.

Jana pia dira ya mchana lilitolewa tamko na mkurugenzi mkuu kanda ya Afrika lenye kuitaka Tanzania ijitafakari kuhusu chanjo na iwe tayari kushirikiana na nchi za kiafrika, kwangu mimi hili ni debe la biashara tu.

Jana hiyohiyo KM wa afya, professor Mchembe aliipangua kauli ya MD huyo kanda ya Afrika. Ufafanuzi wa Mchembe ulikuwa makini na wenye kufikirisha sana kwa anae jitambua.

Professor Mchembe alisema Tanzania haiko tayari kwa chanzo hizo, kwani nchi nyingi zimetengeneza chanjo ya virus hivi, China, Amerika, Russia, German, Brazil, India nk, Je? Tutumie chanjo ipi ambayo ni salama ikizingatiwa virus hawa wanajibadilisha kila uchao.

Kwakuwa professor Mchembe maelezo yake yalimfunika MD wa WHO kanda ya Afrika, BBC wakaipotezea habari hii yenye kufumbua macho waafrika.

Kwangu mimi hii ni kauli thabiti sana,

Na ndipo suala la uharaka wa chanjo hizi zilizogunduliwa kwa kukiuka kanuni utajua zimelenga biashara, yaani tatizo limetengenzwa ili kujipatia faida kubwa huku baadhi ya wanadamu wakiangamia pasi hatia yoyote.

Naipongeza serikali kwa kua makini sana katika kucheza ngoma hii ya ma babylon.

Namalizia kwa kusema BBC na DW ni radio za wakoloni zenye kazi moja tu ya propaganda mfu dhidi ya anayepinga udhalimu wa mabeberu, chukua tahadhari
Wewe na huyo profesa wako wote vibuyu tu,ningemuona wa maana kama angesema hatutaki chanjo zenu kwa kuwa tunayo ya kwetu ambayo ni bora kuliko hizo za kwenu. Hoja yake ni kuwa zipo chanjo nyingi hivyo hajui tutumie ipi,huu ni uhuni tu kwani kwa vyovyote vile mwisho wa siku lazima tuchanjwe.
 
Ni chanjo ya ugonjwa gani ambayo tumewahi kukugundua sisi kama taifa?
Mbona nilichoandika kinaeleweka? Mm nimehoji kwann tupangiwe Aina ya chanjo.Tunaweza kununua Ya Iran,China,Russia kwa uwezo wetu na baada ya kujiridhisha.

Nashangaa wew unakuja na hoja za ss kugundua chanjo.Nani kaongelea hizo.
 
Wewe na huyo profesa wako wote vibuyu tu,ningemuona wa maana kama angesema hatutaki chanjo zenu kwa kuwa tunayo ya kwetu ambayo ni bora kuliko hizo za kwenu. Hoja yake ni kuwa zipo chanjo nyingi hivyo hajui tutumie ipi,huu ni uhuni tu kwani kwa vyovyote vile mwisho wa siku lazima tuchanjwe.
Shida ya Watanzania lawama na ujuaji mwingi.Sisi Ni nchi Lazima tunachokifanya tujiridhishe.Haiwezekani tunaletewa chanjo tunaambiwa chukuen hii, kwanini Africa tupangiwe aina fulani ya chanjo.Na kwann tupangiwe.

Kuna chanjo ya Iran, Russia, China na zote zinafanya kazi kwa ufanisi,kwani lazima kutumia HIYO ya Bill Gate.Na lichanjo tunalolazimishiwa hata halijathibitishwa.

HOJA hapa ni serikali kuharakisha kupatikana chanjo haraka,ambayo tumejiridhisha nayo.
 
hivi dawa za TB/KIFUA KIKUU tunatengeneza wenyewe eeeehhh!au hizi nazo tunaagiza kwa mabeberu
 
Kongole sana mwamba

Napenda watu wanaojiamini kama wewe
Unajua mkuu,sisi WATZ ujuaji mwingi, lawama nyingi.Kimsingi hakuna taifa ambalo halichukui tahadhari kuwalinda raia wake.

Kuna chanjo zenye ufanisi za Russia, Iran, China , Brazili. Sisi km nchi tunaweza kuagiza kutoka popote Kati ya hizo. Kwanini Waafrika tunaletewa tunalazimishwa kuchukua hiyo ya Bill Gate.

Tuna uhakika wanayochanjwa wazungu ndiyo hiyohiyo tuliyoletewa sisi. Na hii chanjo halijathibitishwa.

LA MSINGI:
Ni kwamba korona IPO na INAUWA tuchukue tahadhari zote zinazopaswa.

Pili, Serikali iharakishe upatikanaji wa chanjo ambayo tumejiridhisha ni salama toka popote pale. Na serikali ionyeshe utashi wa kutekeleza Hilo.

Tatu, Watanzania tupunguze ujuaji, km tunaona serkali inachelewa tupaze sauti na si kulazimisha kupokea chanjo ambayo hatuna uhakika na usalama wake. Tukidhurikarau kupata madhara ni Watanzania nyie nyie mtakuja hapa kusema Serikali ilikurupuka. Seikali ina wajibu wa kutulinda.

Nne, Tumeambiwa tupige nyungu, hiyo ni plan ya kwanza, je, kwa hii korona toleo la pili ambayo inauwa ghafla, plan ya nyungu inapofeli, plan b Ni nn kwa serikali.Na serikali imejipanga namna gani ikitokea hali imekuwa mbaya.

Pia, tuihoji serkali ikiwa ina mpango wa kuagiza chanjo au la.Au plan ya serikali Ni kupiga nyungu basi haijalishi Hali Ni mbaya kiasi gani.
 
Unajua mkuu,sisi WATZ ujuaji mwingi, lawama nyingi.Kimsingi hakuna taifa ambalo halichukui tahadhari kuwalinda raia wake.

Kuna chanjo zenye ufanisi za Russia, Iran, China , Brazili. Sisi km nchi tunaweza kuagiza kutoka popote Kati ya hizo. Kwanini Waafrika tunaletewa tunalazimishwa kuchukua hiyo ya Bill Gate.

Tuna uhakika wanayochanjwa wazungu ndiyo hiyohiyo tuliyoletewa sisi. Na hii chanjo halijathibitishwa.

LA MSINGI:
Ni kwamba korona IPO na INAUWA tuchukue tahadhari zote zinazopaswa.

Pili, Serikali iharakishe upatikanaji wa chanjo ambayo tumejiridhisha ni salama toka popote pale. Na serikali ionyeshe utashi wa kutekeleza Hilo.

Tatu, Watanzania tupunguze ujuaji, km tunaona serkali inachelewa tupaze sauti na si kulazimisha kupokea chanjo ambayo hatuna uhakika na usalama wake. Tukidhurikarau kupata madhara ni Watanzania nyie nyie mtakuja hapa kusema Serikali ilikurupuka. Seikali ina wajibu wa kutulinda.

Nne, Tumeambiwa tupige nyungu, hiyo ni plan ya kwanza, je, kwa hii korona toleo la pili ambayo inauwa ghafla, plan ya nyungu inapofeli, plan b Ni nn kwa serikali.Na serikali imejipanga namna gani ikitokea hali imekuwa mbaya.

Pia, tuihoji serkali ikiwa ina mpango wa kuagiza chanjo au la.Au plan ya serikali Ni kupiga nyungu basi haijalishi Hali Ni mbaya kiasi gani.
mother mdogo alienda kutembea kwa sister London 2019 ilikuwa arudi julai 2020
Ilipozuka tena waka block tena.
Ivo ameshindwa kurudi.

Yupo hukohuko tu na limenenepa balaa

Anasema kiukweli wazungu wanakufa ila African wanadunda tu.

Mm namwambia waendelee tu kublock ili uzidi kuchana.
Ameanza kutema kile cha kimalkia.
 
BBC wamekua wepesi sana kurusha matamko dhidi ya Tanzania yatolewayo na shirika la afya duniani kupitia wakurugenzi wake kuhusiana na ugonjwa wa covid 19 hasa yale yenye kuonyesha mbinyo kwa nchi yetu.

Jana pia dira ya mchana lilitolewa tamko na mkurugenzi mkuu kanda ya Afrika lenye kuitaka Tanzania ijitafakari kuhusu chanjo na iwe tayari kushirikiana na nchi za kiafrika, kwangu mimi hili ni debe la biashara tu.

Jana hiyohiyo KM wa afya, professor Mchembe aliipangua kauli ya MD huyo kanda ya Afrika. Ufafanuzi wa Mchembe ulikuwa makini na wenye kufikirisha sana kwa anae jitambua.

Professor Mchembe alisema Tanzania haiko tayari kwa chanzo hizo, kwani nchi nyingi zimetengeneza chanjo ya virus hivi, China, Amerika, Russia, German, Brazil, India nk, Je? Tutumie chanjo ipi ambayo ni salama ikizingatiwa virus hawa wanajibadilisha kila uchao.

Kwakuwa professor Mchembe maelezo yake yalimfunika MD wa WHO kanda ya Afrika, BBC wakaipotezea habari hii yenye kufumbua macho waafrika.

Kwangu mimi hii ni kauli thabiti sana,

Na ndipo suala la uharaka wa chanjo hizi zilizogunduliwa kwa kukiuka kanuni utajua zimelenga biashara, yaani tatizo limetengenzwa ili kujipatia faida kubwa huku baadhi ya wanadamu wakiangamia pasi hatia yoyote.

Naipongeza serikali kwa kua makini sana katika kucheza ngoma hii ya ma babylon.

Namalizia kwa kusema BBC na DW ni radio za wakoloni zenye kazi moja tu ya propaganda mfu dhidi ya anayepinga udhalimu wa mabeberu, chukua tahadhari
Western Media ziko kwa ajili ya Biashara, wakishalipwa wanafanya kazi, taarifa zao lazima uwe makini sana kuzichuja bahati mbaya watu wengi duniani wanafuata mkumbo tu. hizo chanjo zenyewe wanapigana vikumbo .
 
Back
Top Bottom