GE2025 Said Soud: Hakuna Chama chenye uwezo wa kuiangusha CCM

GE2025 Said Soud: Hakuna Chama chenye uwezo wa kuiangusha CCM

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,448
Reaction score
2,099
Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama cha Wakulima (AAFP), Said Soud, amesema hakuna chama cha siasa chenye uwezo wa kuiondosha Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani kutokana na uimara na umoja wa chama hicho.

Soud alibainisha kuwa AAFP ipo tayari kushirikiana na CCM na kumuunga mkono mgombea wake wa Urais, Dk. Hussein Ali Mwinyi, kutokana na rekodi nzuri aliyoionesha katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Zanzibar.

Aidha, mgombea huyo alikitaka chama cha ACT Wazalendo kuacha kuhamasisha fujo kwa kisingizio cha kura ya mapema, akisema kufanya hivyo ni dalili ya uchu wa madaraka.

Akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake Mwera, alisema hakuna namna ya kuzuia kura ya mapema kwani jambo hilo lipo kisheria na siyo Zanzibar pekee yenye utaratibu huo.

Soud alimuomba Msajili wa Vyama vya Siasa kufuta usajili wa chama chochote kitakachohamasisha fujo na uvunjifu wa amani hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu

Soma pia



 
1756988078603.png
 
Kuna haja gani kupoteza kodi kubwa kwaajili ya uchaguzi,kwa mamluki km hawa?
 
Back
Top Bottom