Safari yangu ya Rwanda

Safari yangu ya Rwanda

sanjo

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2010
Posts
943
Reaction score
271
Wakuu,

Katika kufunga Mwaka 2011 nilisafiri kwenda Rwanda kwa ajili ya kuona mambo mbalimbali ya nchi hiyo baada ya Mauaji ya 1994. Baadhi ya vitu nilivyoona ni kama ifuatavyo:

(1) Mpakani Rusumo:
Kwa upande wa Tanzania (hakuna benki wala Bureau de change) kuna maduka madogo madogo na Wamachinga wakiwa na fedha zao mkononi kwa ajili ya kubadilisha fedha mbalimbali (Shilingi ya Tanzania, Dollar na Faranga ya Rwanda) kutoka kwa wasafiri. Kwa upande wa Rwanda, ukivuka daraja la Akagera unakutana la Bango lisemalo "Investment Yes, Corruption No." Kuna tawi la benki na Bureau de change kadhaa.

(2) Ukitoka tu Mpakani kuelekea Kigali mara moja utaona tofauti kati ya nchi hizi:
(i) Sijaona nyumba ya NYASI au TEMBE kwa upande wa Rwanda hata baada ya Kwenda Butare kusini mwa nchi.
(ii) Umeme hadi vijijini hata kama nyumba ni ndogo tu.
(iii) Nchi ya Rwanda ina idadi kubwa sana ya watu ukilinganisha na eneo la nchi (high population density). Huwezi kuona mapori kama ya upande wa Tanzania. Kwani kutoka Benaco mpaka Rusumo ni mapori tu.
(3) Usafi: Miji ya Kigali, Gitarama, Kayonza na Butare ni misafi, bustani zikiwa zimetunzwa sana.
(4) Rushwa ni kidogo. Trafic police wa Rwanda akimkamata dereva hufanya miwili tu kumwandikia adhabu ili akalipe au kumsamehe.
(5) Nini kichocheo cha mabadiliko hayo.
Baada ya kudadisi watu mbalimbali kwa nini nchi imebadilika sana katika miaka 16 iliyopita wengi wametaja ni Uongozi madhubuti wenye nia ya kuleta maendeleo ya watu. Rushwa inapingwa kabisa na mkuu wa nchi na kila mwananchi anahamasishwa kujiletea maendeleo katika eneo lake kwa juhudi na maarifa bila kuvunja sheria.

Wakuu, haya ni baadhi ya mambo niliyoyaona katika ziara hii. Kinachonisikitisha kwa upande wa Tanzania (nchi yangu) ni kuwa pamoja na rasirimali nyingi tuliyonayo bado nchi inazidi kudodora katika nyanja mbalimbali.
 
umetembelea kigali memorial centre?...kisha nenda Kigali bussiness centre ukaone watoto...baada ya hapo nenda Gisenyi ukaone utalii wa sokwe na Ndege..ukimaliza nitafute tukae pale Sports View tule Mutzing,skol .primus
 
tanzania bado tunajifunza namna ya kusuluhisha migogoro na kutoka kwenye usingizi tuliolala
 
"Baada ya kudadisi watu mbalimbali kwa nini nchi imebadilika sana katika miaka 16 iliyopita wengi wametaja ni Uongozi madhubuti wenye nia ya kuleta maendeleo ya watu. Rushwa inapingwa kabisa na mkuu wa nchi na kila mwananchi anahamasishwa kujiletea maendeleo katika eneo lake kwa juhudi na maarifa bila kuvunja sheria".

Hivi vitu tulikuwa navyo miaka ya mwanzoni baada ya uhuru,azimio la Arusha lakini tulipoliuwa ndio ikawa basi tena.
 
Kagame ni mwanajeshi tofauti na Kanali wetu wa maneno na mapambo lazima uone tofauti hii .
 
hayo maendeleo yanasababishwa na viongozi wenye nia hasa na nchi yao'mkuu vipi kuhusu ule ubaguzi wa mtusi na mhutu'bado upo?
 
Tanzania ya baada ya Baba wa Taifa, inayo mengi ya kuwatenganisha Watanzania kuliko kuwaunganisha. Maendeleo makubwa yanayoweza kutarajiwa kwa mfumo wa sasa ni jua kuchwa na kuzama. Mengine kama barabara nzuri, maji safi na salama, elimu bora ni yatokanayo; yanatokea kwa nasibu na hayajali ubora. Siasa zimekuwa za chuki, udini, ukanda, wenye nacho, ushirikina, n.k Wakuu wa Serikali na chama tawala wamepotea dira. Nchi inakwenda tu bila kujua inaelekea Kaskazini na je ndiko ilikopanga kwenda au inashuka kusini zaidi na kujipongeza! Hata tukifarakana, tukapigana, tukakatana mapamnga, Tanzania haitoweza kuamka na kusimama ili ianze kufuata vema njia ya maendeleo kama Rwanda. Sababu ziko nyingi lakini za haraka ni uwepo wa makundi kinzani mengi (udini, siasa, maskini na matajiri) ambayo chuki zake zimejengeka taratibu na kwa muda mrefu na sababu ya pili uwepo wa rasilimali (mafuta, uranium, gas achana na dhahabu) zilizoadimika katika ulimwengu wa mabeberu na ambazao faida yake kubwa haipatikani kama uchimbwaji wake unafanyika katika jamii yenye amani. Hivyo kiberiti kikiwaka, hawa mabeberu watakuja haraka sana kusaidia pande hasimu kuingia vitani ili wao wauze silaha, nyinyi muendelee kumwaga damu, na wao waendelee kuvuna rasilimali kwa urahisi zaidi.

Naijionea huruma siku hiyo ikinikuta ningali hai......
 
umetembelea kigali memorial centre?...kisha nenda Kigali bussiness centre ukaone watoto...baada ya hapo nenda Gisenyi ukaone utalii wa sokwe na Ndege..ukimaliza nitafute tukae pale Sports View tule Mutzing,skol .primus

Asante kwa ushauri huo. Nitakutafuta baada ya kufanya safari nyingine. Nilikaa sana pale Butare Museum na NUR.
 
Asante kwa ushauri huo. Nitakutafuta baada ya kufanya safari nyingine. Nilikaa sana pale Butare Museum na NUR.

Fika pale Bungeni ukaone matundu ya risasi ni historia nzuri sana ..katika kujua yale mauaji ya kimbari....tembelea shule zao uone

mkuu kila la kheri..tutafutane
 
hayo maendeleo yanasababishwa na viongozi wenye nia hasa na nchi yao'mkuu vipi kuhusu ule ubaguzi wa mtusi na mhutu'bado upo?

Kwa muda mfupi niliokaa sijauona. Watu wanaongea lugha moja (Kinyarwanda) watawala waliopo hawataki ubaguzi wa kikabila.
 
Kwa Tanzania hakuna kiongozi wenye nia ya kuendeleza watanzania wala kuwaletea maendeleo
Wapo pale kujineemesha matumbo yao na familia zao
hakuna kiongozi mwenye utashi wa kusema hili nalifanya kwa maendeleo ya nchi yangu na watu wake ila analifanya kwa kuwa kabla ya kusaini mktaba wa kufanya hilo jambo kashapokea cha kwake. matokeo yake ni zile barabara ambazo zinabomoka kabla ya kukabidhiwa maana lami haina kiwango, mradi wa maji unakwama kabla ya kuanza, bwawa la maji linapasuka kabla ya kuanza kutumika, madarasa yana nyufa kabla hayajaanza kutumika, jengo limebomoka na vitasa kuachia kabla halijaanza kutumika, miradi hewa kibao ambayo hata waliopitisha na kuidhinisha matumizi ya fedha hawachukuliwi hatua zozote, au wanawashtaki wale waliofichua uozo na ulaji huo.
Kila sehem imeoza kuanzia ngazi ya kijiji mpaka taifa kw aulaji usio na kikomo na usio na mkemeaji maana kwenye kutafuna kila mmoja wao ana fungu lake.
Tutabaki kushangilia Rwanda inaendelea wakati sisi ndo tunazidi kurudi nyuma kimaendeleo
Hadi hapo kwenli tutakapopata viongozi ambao wana utashi na nia haswa ya kutupeleka kule tunakotaka na wananchi watakapoamka kudai kuwa haya madudu yanayofanyika sasa yaishe na watakapokuwa na nguvu za kumwajibisha kiongozi kwa madudu yake aliyoyafanya.
 
Kwa muda mfupi niliokaa sijauona. Watu wanaongea lugha moja (Kinyarwanda) watawala waliopo hawataki ubaguzi wa kikabila.

Rwanda hakuna ukabila kabisa wote wanaongea lugha moja,wote ni wanyarwanda ..wanajenga taifa lao...
kwanza usiku nchi inalindwa na jeshi..au unasemaje mkuu sanjo
 
Tanzania ya baada ya Baba wa Taifa, inayo mengi ya kuwatenganisha Watanzania kuliko kuwaunganisha. Maendeleo makubwa yanayoweza kutarajiwa kwa mfumo wa sasa ni jua kuchwa na kuzama. Mengine kama barabara nzuri, maji safi na salama, elimu bora ni yatokanayo; yanatokea kwa nasibu na hayajali ubora. Siasa zimekuwa za chuki, udini, ukanda, wenye nacho, ushirikina, n.k Wakuu wa Serikali na chama tawala wamepotea dira. Nchi inakwenda tu bila kujua inaelekea Kaskazini na je ndiko ilikopanga kwenda au inashuka kusini zaidi na kujipongeza! Hata tukifarakana, tukapigana, tukakatana mapamnga, Tanzania haitoweza kuamka na kusimama ili ianze kufuata vema njia ya maendeleo kama Rwanda. Sababu ziko nyingi lakini za haraka ni uwepo wa makundi kinzani mengi (udini, siasa, maskini na matajiri) ambayo chuki zake zimejengeka taratibu na kwa muda mrefu na sababu ya pili uwepo wa rasilimali (mafuta, uranium, gas achana na dhahabu) zilizoadimika katika ulimwengu wa mabeberu na ambazao faida yake kubwa haipatikani kama uchimbwaji wake unafanyika katika jamii yenye amani. Hivyo kiberiti kikiwaka, hawa mabeberu watakuja haraka sana kusaidia pande hasimu kuingia vitani ili wao wauze silaha, nyinyi muendelee kumwaga damu, na wao waendelee kuvuna rasilimali kwa urahisi zaidi.

Naijionea huruma siku hiyo ikinikuta ningali hai......

Mkuu Omutwale, hapa umenena nchi inapokosa dira na viongozi watumishi wa watu hata kama itakuwa na rasilimali nyingi nchi hiyo utakuwa uwanja wa fujo na shamba la bibi.
 
Bila shaka utakuwa umeshaiona tofauti, wananchi wa Rwanda wanatafuta maendeleo wao wenyewe while watanzania wanasubiri serikali iwaletee
 
Rwanda hakuna ukabila kabisa wote wanaongea lugha moja,wote ni wanyarwanda ..wanajenga taifa lao...
kwanza usiku nchi inalindwa na jeshi..au unasemaje mkuu sanjo

Mkuu ni kweli, kila kwenye mkusanyiko wa watu kuna Askari Jeshi na SMG mkononi. Hawaongei au kubugudhi mtu.
 
Back
Top Bottom