Kichwa Ze Don
Senior Member
- Jun 7, 2017
- 174
- 298
Mzee Baba Shusha Nondo Tupate Madini
Nashauri msimuliaji aendelee na utaratibu wake wa usimuliaji....
Asi yumbishwe na mtu yeyote.....just focus
Kuna kipindi niliwai kuandika maoni yangu hapa JF akatokea jamaa mmoja aka ni attack ALINITOLEA KAULI NILITAMANI NI INGIE KWENYE SIMU NIMFUATE TUPIGANE...SIO SIRI NILIPATA JAZBA KUU
All in all nilimwelewesha na hakurudia Tena mungu ni mwema thanks is Friday.
Mkuu nadhani content inaeleweka mkuu...ila wajuaji nyinyi Huwa hamuwez kukaa kimya....Mkuu siyo vizuri kuandika Mungu kwa herufi ndogo
endeleaTunaendelea.
Kuna mtu ameuliza kuhusu mavazi. Jibu ni kwamba hatukuwa na nguo zilezile tulizotoka nazo downtown Dar es salama. Tulichokuwa tunafanya ni kujiepusha n'a mzigo wowote ule, tuliamini mzigo utatujengea shida na mashaka kwa sehemu tunazopitia, hivyo kwenye issue ya nguo ilikuwa ni kuvaa na kama kuna safari basi unaondoka nazo mbele kwa mbele na ukibadilisha ndio inakuwa mwisho wake.
Ijapokuwa pale tunduma kidogo nguo tulidumu nazo kutokana na kwamba tulikaa muda kidogo.
Unajua tuliishije pale? Pale kulikuwa kuna watu wengi sana mchanganyiko, kuna watu walikuwa wanakula bata mbaya sana, sasa yule jamaa yetu mmoja aliyebakia Tunduma alikuwa na upepo mkali sana wa kukubaliwa na watu, hususa wakina Dada, pia kutokana na hali ya ujanja ujanja wa umjini mjini tuliweza kuwateka mawazo zaidi wenyeji wa pale kuliko hats vijana wengine wajinga wajinga waungaji na wazamiaji tuliowakuta pale. Tulitumia sana gia ya kuwa kwanza sisi ni watoto wa polisi na hatuma mashida makwetu huko ila tumeamua tu kutafuta maisha mbele kwa mbele.
Ujanja huo ulitufanya tuishi kibosi ndani ya bar moja hivi maeneo Yale iliyokuwa inamilikiwa na jimama moja toka Mbeya huku warembo wengi wa pale wakiwa mabinti toka mbeya na sehemu nyingine kwa uchache, tulikuwa tunalala kwenye kichumba kimoja hivi kilichokuwa kama stoo ya dharura hapo mjengoni.
Na hapo hapo ndipo yule mwenzetu mmoja alipobadilisha mawazo ya kusonga mbele baada ya kunogewa na penzi mtoto wa kinyakyusa na kutuacha njia panda.
Kwa msaada wa ndugu Boipelo tulifika katika mji wa kihistoria kwetu na Botswana, mji wa Francistown usiku kidogo na kiukweli hatukuwa na uelekeo wowote baada ya hapo.
Tulikuwa tunaogopa sana. Kwanza kwasababu Boi alitueleza kuwa watu wengi wa pale wanapendelea kuzungumza lugha ya kwao hivyo kwetu kama tungekutana na wanausalama au watu wabaya ingekuwa hatari sana kwetu.
Lakini uzuri ni kwamba kwa miaka ile hakukuwa na usumbufu sana kwa Botswana kuhusiana na swala la wahamiaji haramu ndani ya nchi yao kwa kuwa kwanza haikuwa vizuri ki uchumi na haikuwa chaguo kabisa kwa wajanja kuishi pale kutokana na kwamba hata wakazi wa pale siku zote walikuwa wakitamani kuondokea Afrika ya kusini kutafuta maisha bora zaidi.
Hivyo brother Boi aliamua kutusaidia tu kwa uwezo wake wote. Yeye alikuwa akifanyia kazi kwenye issue za utalii utalii na masuala ya Sanaa za asili pamoja na matamasha ya ngoma na mengineyo kama hayo. Na kwa kule Botswana wana penda sana tamaduni zao hata ukiwakuta kanisana wanaweza wakapiga nyimbo mpaka ukafurahi mwenyewe. Pia wanapenda sana kutumia majina yao ya asili kuliko Yale ya kigeni hapo sijui kwa miaka ya sasa kama wamebadilika.
(Naleta mwendelezo hapa muda huu)
(Naleta mwendelezo hapa muda huu
Mkuu Mailman usimfokee atuletee mautamu.Muda huu ni muda gani?