Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,954
- 20,463
Timu yetu ya taifa Taifa Stars inajiandaa na mechi ya kuamua ni nani aongoze kundi na kuwa na nafasi kubwa ya kuliwakilisha bara la Afrika katika fainali za kombe hilo la Dunia zitakazofanyika nchini razil mwakani.
Endapo timu yetu itafanikiwa kuifunga Morocco tarehe 8 mwezi June mjini Marrakechi na kutoa sare na Ivory Coast, basi kuna uwezekano mkubwa wa timu yetu kwenda Brazil kucheza fainali hizo kwa mara ya kwanza kabisa katika historia ya mpira nchini Tanzania.
Taifa Stars inafunzwa na kocha Kim Poulsen kutoka nchini Denmark na ni hivi karibuni tu mkataba wake na TFF uliongezewa miaka miwili ili ainoe vizuri zaidi timu hiyo. Kim alichukua nafasi ya kocha mwingine Jan Poulsen ambae alirudi nchini kwao Denmark.
Kim Poulsen ameiwezesha Taifa Stars kucheza mpira mzuri unaovutia ukionyesha mpangilio wa safu za mabeki, sehemu ya kiungo na ushambulaji na uchezaji wake umekuwa ni wa kisasa zaidi. Ushahidi wa uchezaji huo ni kuona Taifa Stars sasa imepanda ngazi kwenye orodha ya FIFA inayoonyesha timu zenye ubora wa usakataji kabumbu kutoka nafasi ya 145 nafasi ya 124 hadi ya 116 jambo ambalo ni la kujivunia sana. Endapo Taifa Stars itafanikiwa kwenda Brazil basi inaweza kupanda nafasi moja au mbili zaidi juu.
Pia endapo Taifa Stars itafanikiwa kwenda Brazil basi wachezaji wake wengi wanaweza kutambulika zaidi duniani na kuweza kupata nafasi ya kucheza kwenye ligi mbalimbali duniani zenye kuweza kuwapatia kipato cha kuboresha maisha yao na familia zao.
Timu ya Morocco au Simba wa Atlas (Atlas Lions) kama inavyoitwa, imeshiriki kwenye fainali hizo maarufu duniani mara ya mwisho ikiwa ni mwaka 1998 nchini France na ikatolewa kwenye hatua za awali.
Katika mechi yake na Tanzania Morocco ilichapwa magoli 3-1 na kushtukizwa kabisa na magoli hayo.Tokea mwanzo wa mchezo hali ya timu hiyo kimchezo haikuwa sawa kabisa, hakukuwa na mpangilio na wachezaji wake walionekana kutojiamini. Wachezaji wa timu hiyo walishindwa kabisa kumiliki mpira na hata walipopata nafasi za wazi za kufunga magoli walizipoteza.
Timu zilipokwenda mapumziko kocha wa timu hiyo Eric Gerets aligomba sana kwa wachezaji wake na akawaambia kwamba ufanisi wao kiuchezaji ulikuwa ni mbovu haijapata kutokea.
Lakini kama alikuwa amepigilia misumali jeneza la timu hiyo, kipindi cha pili Morocco walishangaa kutundikwa goli la kwanza mara tu kipindi cha pili kilipoanza na Ulimwengu Thomas kwenye dakika ya 46, kala hawajakaa sawa Mbwana Samata akatundika goli la pili na baadae dakika ya 79 akatundika goli la tatu, Morocco wakawa chali!
Morocco walijitahidi kujitutumua kutafuta goli na walikuja kuambulia goli pekee la kufutia machozi dakika ya nyongeza ya 93 liliofungwa na Youssef El Arabi.
Waliporudi nchini kwa kocha Gerets akafukuzwa kazi na nafasi yake ikachukuliwa na Rachid Taoussi ambae ni Mmoroko.
Kwenye orodha ya FIFA Morocco inashika nafasi ya 74 kutoka nafasi ya 77 iliyokuwa miaka miwili iyopita na katika kutaka kutetea nafasi yake hiyo kwenye ulimwengu wa soka timu hiyo ina wachezaji wanaocheza soka kwenye ligi mbalimbali barani Ulaya kama Marouane Chamakh wa Arsenal (anachezea West Ham kwa mkopo) na Adel Taarabt wa Qeens Park Rangers ambayo imeshuka daraja msimu huu kwenye ligi kuu ya Uingereza.
Marouane Chamakh wa sasa si yule Chamakh aliekuwa akichezea Bordeaux ya France kiasi cha kuwavutia Arsenal kumsajili na hakuweza kuchezea timu hiyo mara zote. Chamakh amecheza mechi 67 na kufunga magoli 14 tu. Arsenal ikamtoa kwenda West Ham kwa mkopo hadi mwisho wa msimu wa 2012/13 na amecheza mechi tatu tu na hajafunga goli hata moja.
Kocha wa Morocco Taoussi alikwishamtoa mshambuliaji huyo kwenye timu hiyo kwa sababu za kwamba hajacheza mechi nyingi kwenye ngazi ya klabu.
Mchezaji mwingine ni Taarabt ambae nae amezunguka kwenye timu za Tottenham na QPR nchini Uingereza ambae nae hana rekodi nzuri ya ufungaji magoli inagwa kwa Taifa Stars ni lazima waangalie hili.
Wapo wachezaji wengine wanaocheza Ulaya kama Youssouf Hadji mchezaji wa kiungo anaechezea Al Arabi ya Qatar, mshambuliaji Youssef El Arabi anaechezea Granada ya Spain ambae alicheza mechi na Taifa Stars na mshambuliaji Mounir El Hammoudi anaechezea Fiorentina ya Italy kwenye ligi ya Serie A.
Itakumbukwa mshambuliaji huyu ndie alieifunga Taifa Stars goli pekee kwenye uwanja wa Taifa kwenye mchezo wa kufuzu kucheza fainali za mataifa huru ya Afrika yaliyofanyika mwaka 2012.
Pia kwenye timu hiyo alikuwemo Younes Belhanda mchezaji wa kiungo anaechezea Motepellier ya France ambae aliondolewa na kocha wa sasa Taoussi ambae amewapa kipaumbele wachezaji wanaotoka ndani ya nchi hiyo. Yumo Oussama Assaidi ambae ni mshambuliaji wa pembeni wa timu ya Liverpool ya Uingereza na Karim El Ahmadi ambae huchezea nafasi ya mlinzi kiungo (defensive midfielder) wa timu ya Aston Villa pia ya Uingereza.
Wapo walinzi Mehdi Benatia wa Udinese ya Italy na Ahmed Kantari ambae ni mkoba anaechezea timu ya Stade Brest ya France.
Kocha Taoussi ana rasilimali ya kutosha kuchezesha timu nzima ya wachezaji kutoka mamtoni lakini katika timu yake yenye wachezaji 24, 16 kati yako wanatoka nchini Morocco. je alikuwa anajaribu wachezaji hao na jariio limegonga mwamba?
Safari ya kwenda Brazil si ya kuichezea hata kidogo na Taifa Stars ian wajibu wa kukaza uzi uleule iliyoukaza kwenye uwanja wa nyumbani wa Ben Mkapa mpaka kufikia kuwatungua Morocco 3-1.
Kama kawaida ya waarau hawa wakiwa kwao ni lazima Taifa Stars wajiandae kukabiliana na vitimbwi na kelele za kuwachanganya kutoka kwa maelfu ya wamoroko ambao watakuwa nyuma ya timu yao kutaka ifidie magoli hayo matatu.
Lakini nina imani na kocha Poulsen ataiandaa timu yetu vizuri na kuhakikisha kwamba malengo yetu ya kuwadhibiti Morocco kwenye mtindo wao wa kutumia kona, mipira ya adhabu na mashambulizi ya kushtukiza yanatimizwa.
Kila la kheri timu yetu ya Taifa Stars.
Endapo timu yetu itafanikiwa kuifunga Morocco tarehe 8 mwezi June mjini Marrakechi na kutoa sare na Ivory Coast, basi kuna uwezekano mkubwa wa timu yetu kwenda Brazil kucheza fainali hizo kwa mara ya kwanza kabisa katika historia ya mpira nchini Tanzania.
Taifa Stars inafunzwa na kocha Kim Poulsen kutoka nchini Denmark na ni hivi karibuni tu mkataba wake na TFF uliongezewa miaka miwili ili ainoe vizuri zaidi timu hiyo. Kim alichukua nafasi ya kocha mwingine Jan Poulsen ambae alirudi nchini kwao Denmark.
Kim Poulsen ameiwezesha Taifa Stars kucheza mpira mzuri unaovutia ukionyesha mpangilio wa safu za mabeki, sehemu ya kiungo na ushambulaji na uchezaji wake umekuwa ni wa kisasa zaidi. Ushahidi wa uchezaji huo ni kuona Taifa Stars sasa imepanda ngazi kwenye orodha ya FIFA inayoonyesha timu zenye ubora wa usakataji kabumbu kutoka nafasi ya 145 nafasi ya 124 hadi ya 116 jambo ambalo ni la kujivunia sana. Endapo Taifa Stars itafanikiwa kwenda Brazil basi inaweza kupanda nafasi moja au mbili zaidi juu.
Pia endapo Taifa Stars itafanikiwa kwenda Brazil basi wachezaji wake wengi wanaweza kutambulika zaidi duniani na kuweza kupata nafasi ya kucheza kwenye ligi mbalimbali duniani zenye kuweza kuwapatia kipato cha kuboresha maisha yao na familia zao.
Timu ya Morocco au Simba wa Atlas (Atlas Lions) kama inavyoitwa, imeshiriki kwenye fainali hizo maarufu duniani mara ya mwisho ikiwa ni mwaka 1998 nchini France na ikatolewa kwenye hatua za awali.
Katika mechi yake na Tanzania Morocco ilichapwa magoli 3-1 na kushtukizwa kabisa na magoli hayo.Tokea mwanzo wa mchezo hali ya timu hiyo kimchezo haikuwa sawa kabisa, hakukuwa na mpangilio na wachezaji wake walionekana kutojiamini. Wachezaji wa timu hiyo walishindwa kabisa kumiliki mpira na hata walipopata nafasi za wazi za kufunga magoli walizipoteza.
Timu zilipokwenda mapumziko kocha wa timu hiyo Eric Gerets aligomba sana kwa wachezaji wake na akawaambia kwamba ufanisi wao kiuchezaji ulikuwa ni mbovu haijapata kutokea.
Lakini kama alikuwa amepigilia misumali jeneza la timu hiyo, kipindi cha pili Morocco walishangaa kutundikwa goli la kwanza mara tu kipindi cha pili kilipoanza na Ulimwengu Thomas kwenye dakika ya 46, kala hawajakaa sawa Mbwana Samata akatundika goli la pili na baadae dakika ya 79 akatundika goli la tatu, Morocco wakawa chali!
Morocco walijitahidi kujitutumua kutafuta goli na walikuja kuambulia goli pekee la kufutia machozi dakika ya nyongeza ya 93 liliofungwa na Youssef El Arabi.
Waliporudi nchini kwa kocha Gerets akafukuzwa kazi na nafasi yake ikachukuliwa na Rachid Taoussi ambae ni Mmoroko.
Kwenye orodha ya FIFA Morocco inashika nafasi ya 74 kutoka nafasi ya 77 iliyokuwa miaka miwili iyopita na katika kutaka kutetea nafasi yake hiyo kwenye ulimwengu wa soka timu hiyo ina wachezaji wanaocheza soka kwenye ligi mbalimbali barani Ulaya kama Marouane Chamakh wa Arsenal (anachezea West Ham kwa mkopo) na Adel Taarabt wa Qeens Park Rangers ambayo imeshuka daraja msimu huu kwenye ligi kuu ya Uingereza.
Marouane Chamakh wa sasa si yule Chamakh aliekuwa akichezea Bordeaux ya France kiasi cha kuwavutia Arsenal kumsajili na hakuweza kuchezea timu hiyo mara zote. Chamakh amecheza mechi 67 na kufunga magoli 14 tu. Arsenal ikamtoa kwenda West Ham kwa mkopo hadi mwisho wa msimu wa 2012/13 na amecheza mechi tatu tu na hajafunga goli hata moja.
Kocha wa Morocco Taoussi alikwishamtoa mshambuliaji huyo kwenye timu hiyo kwa sababu za kwamba hajacheza mechi nyingi kwenye ngazi ya klabu.
Mchezaji mwingine ni Taarabt ambae nae amezunguka kwenye timu za Tottenham na QPR nchini Uingereza ambae nae hana rekodi nzuri ya ufungaji magoli inagwa kwa Taifa Stars ni lazima waangalie hili.
Wapo wachezaji wengine wanaocheza Ulaya kama Youssouf Hadji mchezaji wa kiungo anaechezea Al Arabi ya Qatar, mshambuliaji Youssef El Arabi anaechezea Granada ya Spain ambae alicheza mechi na Taifa Stars na mshambuliaji Mounir El Hammoudi anaechezea Fiorentina ya Italy kwenye ligi ya Serie A.
Itakumbukwa mshambuliaji huyu ndie alieifunga Taifa Stars goli pekee kwenye uwanja wa Taifa kwenye mchezo wa kufuzu kucheza fainali za mataifa huru ya Afrika yaliyofanyika mwaka 2012.
Pia kwenye timu hiyo alikuwemo Younes Belhanda mchezaji wa kiungo anaechezea Motepellier ya France ambae aliondolewa na kocha wa sasa Taoussi ambae amewapa kipaumbele wachezaji wanaotoka ndani ya nchi hiyo. Yumo Oussama Assaidi ambae ni mshambuliaji wa pembeni wa timu ya Liverpool ya Uingereza na Karim El Ahmadi ambae huchezea nafasi ya mlinzi kiungo (defensive midfielder) wa timu ya Aston Villa pia ya Uingereza.
Wapo walinzi Mehdi Benatia wa Udinese ya Italy na Ahmed Kantari ambae ni mkoba anaechezea timu ya Stade Brest ya France.
Kocha Taoussi ana rasilimali ya kutosha kuchezesha timu nzima ya wachezaji kutoka mamtoni lakini katika timu yake yenye wachezaji 24, 16 kati yako wanatoka nchini Morocco. je alikuwa anajaribu wachezaji hao na jariio limegonga mwamba?
Safari ya kwenda Brazil si ya kuichezea hata kidogo na Taifa Stars ian wajibu wa kukaza uzi uleule iliyoukaza kwenye uwanja wa nyumbani wa Ben Mkapa mpaka kufikia kuwatungua Morocco 3-1.
Kama kawaida ya waarau hawa wakiwa kwao ni lazima Taifa Stars wajiandae kukabiliana na vitimbwi na kelele za kuwachanganya kutoka kwa maelfu ya wamoroko ambao watakuwa nyuma ya timu yao kutaka ifidie magoli hayo matatu.
Lakini nina imani na kocha Poulsen ataiandaa timu yetu vizuri na kuhakikisha kwamba malengo yetu ya kuwadhibiti Morocco kwenye mtindo wao wa kutumia kona, mipira ya adhabu na mashambulizi ya kushtukiza yanatimizwa.
Kila la kheri timu yetu ya Taifa Stars.