zwangandaba
JF-Expert Member
- Jan 31, 2023
- 750
- 1,425
Nimepanda basi la Songea. Ni New force linapitia mikoa ya kusini.
Kilichonishangaza nikuona abiria wenzangu karibia 10 wamenunua maembe pale Mbagara na kuanza kuyafakamia.
Huyu dada niliekaa nae pamoja na kuwa sista duu nae yuko bize na maembe yake kutafuna na kutema maganda nje ya kioo. Nyie wangoni kwani huko Songea hakuna maembe? Halafu hii tabia ya kula vyakula hovyohovyo mbona kama imekaa kishamba sana?
Kama ni njaa, maembe yanatibu njaa? Kwanini usivumilie mpaka Nangurukuru kwenye restaurant ukapate breakfast.
Nimesafiri sana na mabasi ya kaskazini, Iringa, mpaka Mwanza sikuwahi kuona abiria wakila maembe tena kwa kung'ata na meno ndani ya usafiri wa umma.
Kilichonishangaza nikuona abiria wenzangu karibia 10 wamenunua maembe pale Mbagara na kuanza kuyafakamia.
Huyu dada niliekaa nae pamoja na kuwa sista duu nae yuko bize na maembe yake kutafuna na kutema maganda nje ya kioo. Nyie wangoni kwani huko Songea hakuna maembe? Halafu hii tabia ya kula vyakula hovyohovyo mbona kama imekaa kishamba sana?
Kama ni njaa, maembe yanatibu njaa? Kwanini usivumilie mpaka Nangurukuru kwenye restaurant ukapate breakfast.
Nimesafiri sana na mabasi ya kaskazini, Iringa, mpaka Mwanza sikuwahi kuona abiria wakila maembe tena kwa kung'ata na meno ndani ya usafiri wa umma.