Safari ya Mtwara hadi Songea

Safari ya Mtwara hadi Songea

Kama njia ya Tunduru ikishindikana; hakuna njia nyingine maeneo ya Lindi kwenda Songea au Njombe? au ni lazima nirudi Dsm, kisha nianze safari kupitia Morogoro, Iringa, Njombe, hadi Songea?
 
Nasikia yupo mjenzi wa barabara anasaidia kukwamua mkikwama; bado sielewi masika huko kusini inaishia mwezi gani
Ndugu mpaka mje mvutwe ni masaa zaid ya matatu we jitose tu
 
Kama kumbukumbu zangu ziko sawa barabara ya Tunduru - Songea ni mojawapo ya barabara iliyopata ufadhili wa kujengwa kwa kiwango cha lami na serikali ya Marekani kupitia mfuko wa MCC; ni kitu gani tena kilichelewesha ujenzi?
 
Ujenzi unaendelea mkuu na sasa wapo pale Kilimasela mlimani
 
Kama huna kazi ya maana tunduru ningekuambia kwa msisitizo pita Dar songea.
Barabara toka Mangaka mpaka Namtumbo ni majanga japo niliacha wachina wakiwa kazini.
Sio barabara ya kujaribu.
Mi nilikuwa na prado kali lakini ukiangalia madaraja, barabara. Lo.
Songea lala Ugabe iliyoko mitaa ya stendi.
 
Ndio tunapata picha halisi ya kusahuliwa kwa kusini, sababu watawala wetu walikuwa wabinafsi kwenye keki ya taifa
 
Songea zipo nyumba salama za kulala wageni? Hotel & Lodge

SONGEA ni kati ya miji yenye lodge nyingi nchini toka zamani...kila baada ya nyumba Gest japo zenye hadhi sio nyingi sana.
 
Ulizia kama Tunduru mvua inanyesha kama inanyesha Pitia Dar- Songea,hiyo Barabara ya Tunduru -Songea ni moja kati ya Barabara mbovu kuwepo hapa duniani.
Duniani.dah. sio aijaunganishwa kimkoa.yani hapo nakumbuka movie flani inaiwa WRONG TURN.. Ni hatari kwa matumizi ya binadamu
 
Mvua zimeisha mkuu, njia inapitika vizuri jadi Songea. Guest zipo nzuri mno na kwa bei rahisi mfano Ugabe, heritage cottage, top one inn, ziwani nk. Karibu mkuu ILA Kuna ki baridi Fulani hivi kimeanza. Ni vizuri uje na jacket au mkoti
 
nimewahi dozi Ugabe. ilikuwa 25000 wako vizuri na mgahawa mzuri.
 
Mvua zimeisha mkuu, njia inapitika vizuri jadi Songea. Guest zipo nzuri mno na kwa bei rahisi mfano Ugabe, heritage cottage, top one inn, ziwani nk. Karibu mkuu ILA Kuna ki baridi Fulani hivi kimeanza. Ni vizuri uje na jacket au mkoti

Asante Mshua's kwa taarifa
 
Naona wadau wanakupa maoni kirahisi sana,nimepita mara mbili mwez uliopita hali ni mbaya mvua ikinyesha,ukitaka uhalisia niPM namba yako ila usisahau mkate,maji na juis pia uvae sendo au mabuti kwan kuna kusukuma gari in case mvua ikinyesha
Akitaka uhalisia akupm? duh!
 
kama lami imefika mpaka kilimasera safi sana mwaka Jana tulikuwa na Lori tulilala huria siku mbili maana mvua ilikuwa inanyesha na mvua ikinyesha pale mlimani palikuwa hapapitiki
 
Halafu hii way ina fulsa kibao,lakini ndio hivo tena vijana wao wengi wapo Dar.
 
Back
Top Bottom