Safari ya mapenzi na vikwazo vyake

Safari ya mapenzi na vikwazo vyake

kigori wa kilwa

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
483
Reaction score
149
BAADA YA KUCHUNIANA KWA MUDA MREFU,
MPENZI WA KIKE ANAAMUA KUMPIGIA MSELA
WAKE SIMU.
Simu inaita kwa mara kwanza hadi inakatika
bila kupokelewa. Manzi hakati tamaa, anapiga
tena na baada ya ngrii ngrii kama sita, jamaa
ndo anapokea simu.
Hata baada ya kupokea, jamaa haongei neno
hata la HALOO. Manzi inabidi alianzishe.
MANZI: Hey Frank, mambo.
LI-FRANK: Poa.
MANZI: Mbona hupokei simu jamani.
LI-FRANK: Hii imejipokea, au?
MANZI: Hee yaishe basi. Mbona kimya sana
siku hizi.
LI-FRANK: Unataka nimpigie nani makelele.
MANZI: Mbona unanijibu hîvyo Frankie.
LI-FRANK: Kukujibuje.
MANZI: Hivyo kifupi na majibu ya chooni.
LI-FRANK: Unataka nikujibuje sasa kama jibu la
swali lako ni hilo.
MANZI: Kwa hiyo hilo ndo jibu la swali langu.
LI-FRANK: Ndo màana yake. Kama unataka
majibu marefu na yenye maelezo, nenda kapime
UKIMWI kisha ombea uwe nao. Hapo utapata
majibu uyatakayo na maelezo mengi tu.
Manzi anakaa kimya kama dakika 1 hivi.
Anashusha pumzi ndefu ya kuchoka au kukata
tamaa tuseme.
MANZI: Hivi Frank nimekukosea nini?
LI-FRANK: Kunipigia simu.
MANZI: (huku kama anataka kulia) Jamaniii.
LI-FRANK: Nyo nyo nyooo. Msyuuu.
Manzi anasikika anavuta vikamasi ila hakati
simu.
LI-FRANK: Unakunywa supu.
MANZI: (Huku akiwa na sauti ya kilio). Hivi
Frank kweli umebadilika hivi?
LI-FRANK: Kwa hiyo unanitukana. Nimekuwa
Zombie mimi, au mzimu. Unanitukana Marry, si
ndio eeh.
MANZI: Hapana si hivyo.
LI-FRANK: Ila.
MANZI: Basi nisamehe.
LI-FRANK: Umepiga simu ili iweje.
MANZI: Leo ni siku yako ya kuzaliwa Frank.
LI-FRANK: Kwa hiyo.
MANZI: Happy Birthday.
LI-FRANK: Kingine.
MANZI: Nakupenda Frank.
LI-FRANK: Umemaliza?
MANZI: (Akiwa kakata tamaa juu ya Frank).
Nimekumiss pia, naomba urudi uwe nami.
LI-FRANK: Umemaliza?
MANZI: Ndio.
LI-FRANK: Haya kata simu.
MANZI: Frank please. Usinifanyie hivyo jamani.
LI-FRANK: Sibadili neno, kata simu.
MANZI: Ok. Aaah! Poa, asante Frank.
Simu inakatwa.
Baada ya dakika kumi, simu ya Manzi inaita.
Kucheki, ni Frank. Hata sekunde haiishi,
inapokelewa.
FRANK: Umekasirika?
MANZI: Hapana, ila nimeumia.
FRANK: Chungulia dirishani.
Manzi ananyanyuka na kufungua mapazia ya
dirisha laké. Uso kwa uso na tabasamu la Frank
pale dirishani.
FRANK: Naamini utadumu na mimi maishani
mwangu mwote. Kama umeweza kuvumilîa
haya madogo, na kuficha hisia zako kuwa
hujakasirika, naamin utavumilia na makubwa na
kuficha ya ndani. I miss you too, Marry. Ni
wewe pekee uliyenitakia siku yangu ya
kuzaliwa. Ukiwatoa dada na mama yangu,
wewe ndiye mwanamke pekee nitakae kuelewa.
Unajua Marry alikuwaje? Nisikumalizie uhondo.
Jaribu na wewe kufata njia ya LI-FRANK uone
kama Manzi wako atakuwaje.homewrk kwa nyie ambao hamjaoa cc wenye ndoa tunasoma tu, wenye michepuko ruksa tutest hahahaha
 
kwa kizazi hiki cha BRN unafikiri utakutana na mioyo ya chuma kama hiyo?

kwanza hupigiwi simu.. unatumiwa please recharge me, halafu anapigiwa mwingineeeee!

Unatuma sms ya Goodmorning, unajibiwa Mchana bila aibu.. wakati kifurushi/vocha umemnunulia wewe! dadeki..

Mnunulie simu, nimnunulie vocha!..
 
mmh hayo majibu ya shombo hivo kuvumilia ni ngumu
 
nimeshakosa mambo mangapi ila bado kanipa nafasi na ukasema kwamba uniachi utanipenda milele

Chozi lako mola kasikia nami nimekiri upendo nitatulia
nitakupenda milele daima daima X 2


naimba tyu
 
mh!!" huu ujumbe umenikumbusha mbali my x nilimwambia nakupenda sana akasonya eti UNAJUA KUPENDA WEWE!!!! WAPO WANAOJUA KUPENDA SIO WEWE.... nililia na wala hakushtuka na vimachozi vyangu
 
Back
Top Bottom