safi sana mzee sabodo kwa kuyaumbua CCM yaliyodhani kwamba utayapatia fedha za bwerere. yalidhani yatapewa fedha za kutunishia matumbo yao...........hayooooooooooooooooooooo...yameumbuka!Kwa ufupi
Akizungumza jana katika mahojiano maalumu nyumbani kwake Upanga jijini Dar es Salaam, Sabodo alisema hana fedha za kutoa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa miundombinu mkoni Dodoma.
Dar es Salaam,
Mfanyabiashara maarufu nchini, Mustafa Sabodo ameitaka Serikali kuwachangisha wananchi ili kupata fedha za kuhamishia makao makuu ya Serikali mjini Dodoma.
Akizungumza jana katika mahojiano maalumu nyumbani kwake Upanga jijini Dar es Salaam, Sabodo alisema hana fedha za kutoa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa miundombinu mkoni Dodoma.
“Nataka niweke suala hili vizuri, sina fedha za aina hiyo popote pale. Ninazo mali kadhaa lakini sina fedha zote hizo. Watu wengi wanakuja kwangu, wanakuja hapa, nipe pesa, nipe pesa, hakuna pesa hapa,” alisema Sabodo na kuongeza:
“Mimi ni kama kichocheo tu, kama ndimu unatia kwenye soda. Nilichosema ni kutafuta juhudi kutoka kwa kampuni za India na Singapore kufanikisha ujenzi wa makao makuu ya Dodoma, lakini sina kiasi chote hicho cha fedha,” alisema.
Chanzo: Mwananchi
Hahaha msemaji ukweli ageuka kuwa msemaji uongoHaaaaah hii nayo Kali!!
Hawa wanaokopa timu?Sabodo hana uzalendo wowote, watu hawajiulizi kwa nini biashara zake kubwa kubwa ziko nje ya nchi? Ajifunze kwa wenzie kama kina Dewji family, Bakhresa, Rostam au Manji
Walipokua wanatoa pesa zao za udhamini mbona hukukuuliza?Hawa wanaokopa timu?
Usipende kupotosha! Gazeti la serekali Habari Leo liliripoti kwa mapana na marefu kwamba Sabodo atatoa bilioni 5 USD na atawashawishi na marafiki zake waje wawekeze kwenye viwanda hapo Dodoma! Tena wakasema ataanza na uwekezaji kwenye shule, hospitali na real estate! Hawakuishia hapo, wakasema Sabodo aamua kuachana na CHADEMA na hatawapa tena fedha! Waje hapa watuambie hiyo habari waliitoa wapi?Sabodo anasema atawaleta wawekezaji kuja kuwekeza Tanzania hususan Dodoma yeye akiwemo. Na taarifa ya awali ilieleza hivyo. Sasa wewe kwa kuwa hujui unakuja na hisia binafsi unaandika uongo na manyumbu wenzako wanakuunga mkono
Haya magazeti ni kinyaa!!Usipende kupotosha! Gazeti la serekali Habari Leo liliripoti kwa mapana na marefu kwamba Sabodo atatoa bilioni 5 USD na atawashawishi na marafiki zake waje wawekeze kwenye viwanda hapo Dodoma! Tena wakasema ataanza na uwekezaji kwenye shule, hospitali na real estate! Hawakuishia hapo, wakasema Sabodo aamua kuachana na CHADEMA na hatawapa tena fedha! Waje hapa watuambie hiyo habari waliitoa wapi?
Waandishi wa Tanzania ukishawapa bahasha ya khaki umemaliza , hata kama ina elfu 5Dola b5 waandishi mliichukulia powa? Hiyo ni hela haswa Sabodo huyu angeipata wapi?
Ila kuna mwandishi mmoja aliliweka sawa kwamba sabodo atashawishi marafiki zake wa Italy, Egypt, India n.k. ili wawekeze Dodoma ambapo wakikubali investment zao itafikia hizi $b5
Maneno tuu huyu hata $B3 anaweza asiwe nayo....Kwa ufupi
Akizungumza jana katika mahojiano maalumu nyumbani kwake Upanga jijini Dar es Salaam, Sabodo alisema hana fedha za kutoa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa miundombinu mkoni Dodoma.
Dar es Salaam,
Mfanyabiashara maarufu nchini, Mustafa Sabodo ameitaka Serikali kuwachangisha wananchi ili kupata fedha za kuhamishia makao makuu ya Serikali mjini Dodoma.
Akizungumza jana katika mahojiano maalumu nyumbani kwake Upanga jijini Dar es Salaam, Sabodo alisema hana fedha za kutoa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa miundombinu mkoni Dodoma.
“Nataka niweke suala hili vizuri, sina fedha za aina hiyo popote pale. Ninazo mali kadhaa lakini sina fedha zote hizo. Watu wengi wanakuja kwangu, wanakuja hapa, nipe pesa, nipe pesa, hakuna pesa hapa,” alisema Sabodo na kuongeza:
“Mimi ni kama kichocheo tu, kama ndimu unatia kwenye soda. Nilichosema ni kutafuta juhudi kutoka kwa kampuni za India na Singapore kufanikisha ujenzi wa makao makuu ya Dodoma, lakini sina kiasi chote hicho cha fedha,” alisema.
Chanzo: Mwananchi
MsemajiUkweli Mzee Mwanakijiji Pasco joka kuu The Boss Mag3