Ghiti Milimo
JF-Expert Member
- Jul 18, 2011
- 5,134
- 7,651
Basi la Sabena,lililokuwa linatoka Mwanza,kuelekea Tabora,limepata ajali,na kwa uchache watu saba wamefariki papo hapo,maeneo ya Busanda,nje kidogo ya mji wa Shinyanga. Kwa mujibu wa ndugu yangu,aliyekuwepo eneo la tukio,ajali yenyewe,imetokea hivi:-
Basi la Air Time,lilikuwa linafuatwa nyuma na Sabena. Pia,mbele kulikuwa na farasi wawili,wakiendeshwa na wazungu,kila mmoja na farasi wake,wote wakielekea njia ya kuelekea Nzega,kutokea Shinyanga.
Wakati huo huo,mbele kulikuwa na SEMI lililobeba cement,kuelekea Shinyanga. Sabena,bila tahadhari,dereva akaamua kulipita Air Time,ghafla,akaliona hilo SEMI mbele yake! Akalirudisha kushoto,na kuligonga Air Time kwa nyuma,baada ya hapo,likarudi tena kulia,na kukutana uso kwa uso na SEMI,ambalo baada ya kugongana,lilitoka nje ya barabara,na kuiacha Sabena barabarani,likiwa limepondeka vibaya!
Lile Air Time,lilipogongwa nyuma,lilienda kumgonga farasi mmoja,likamvunja mguu,na kumuua mzungu aliyekuwa ameipanda!
Hilo Air Time,hakuna aliyeumia!
Ajali hii,imetokea leo saa 2 asubuhi.
Source: Ndugu yangu,aliyekuwepo eneo la tukio,na kutoa msaada kwa majeruhi!
Basi la Air Time,lilikuwa linafuatwa nyuma na Sabena. Pia,mbele kulikuwa na farasi wawili,wakiendeshwa na wazungu,kila mmoja na farasi wake,wote wakielekea njia ya kuelekea Nzega,kutokea Shinyanga.
Wakati huo huo,mbele kulikuwa na SEMI lililobeba cement,kuelekea Shinyanga. Sabena,bila tahadhari,dereva akaamua kulipita Air Time,ghafla,akaliona hilo SEMI mbele yake! Akalirudisha kushoto,na kuligonga Air Time kwa nyuma,baada ya hapo,likarudi tena kulia,na kukutana uso kwa uso na SEMI,ambalo baada ya kugongana,lilitoka nje ya barabara,na kuiacha Sabena barabarani,likiwa limepondeka vibaya!
Lile Air Time,lilipogongwa nyuma,lilienda kumgonga farasi mmoja,likamvunja mguu,na kumuua mzungu aliyekuwa ameipanda!
Hilo Air Time,hakuna aliyeumia!
Ajali hii,imetokea leo saa 2 asubuhi.
Source: Ndugu yangu,aliyekuwepo eneo la tukio,na kutoa msaada kwa majeruhi!