sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,032
Maada hii inahusu spidi za kuzunguka mjini na mitaani sio barabara kuu za safari ndefu
Nikiwa mimi ni moja wapo wa waliostaafu hii tabia nimeona niweke huu mjadala, Nakumbuka nlikuwa napenda sana kutembea barabarani na mitaani kwa spidi ambayo watu walilalamika nakimbiza gari na kuweka maisha ya raia hatarini.
Nikaja kugundua kwamba hakuna sehemu nayowahi zaidi zaidi tu ya ushamba wa gari, sifa na kuigana.
Mwaka 2015 (miaka 23) nilienda driving school na nikapewa leseni ya udereva, baada ya hapo nikawa na gari ya kwanza Carina TI nilyoshauriwa na nafundi kwa bajet yangu, niliipenda niliiwekea rim sport, kuweka tint kwenye vioo, mziki mnene, n.k ili tu nionekane 😁😁
kuanzia hapo kila gari niliyokuwa nayo niliipenda sana kwa kuiremba sambamba na kuipa moto / kukimbiza, Ila nikiri wazi tu huu ushamba umeniisha mwaka huu mwezi wa february nilipokuwa nampeleka dada yangu sehemu fulani akawa analalamika kwani nawahi wapi na spidi yangu inampa kizunguzungu, nilimpeleka hio sehemu asubuhi na kumrudisha jioni kwa muda wa wiki mbili.
Nilianza kuona kwakweli spidi niliyozoea kuendeshea gari ipo juu japo mimi niliona kawaida, Nikaona hakuna sehemu nayowahi na nikaona nahatarisha maisha ya watu wanaokatiza barabara hasa watoto.
Kwa sasa spidi yangu nayopenda kutembelea ni haivuki 40 kph na kwenye barabara ya vumbi haizidi 20 ili nisitimue vumbi na kuwachafua raia.
Kwa spidi hii nimeanza kuona raha ya kiendesha gari, akili yote inakuwa inaweza kumudu gari na mazingira ya barabara na kusikiliza muziki bila wasi wasi.
Uendeshaji wa gari kwa spidi kubwa ni hatari kwako na wengine, chukua hatua
Nikiwa mimi ni moja wapo wa waliostaafu hii tabia nimeona niweke huu mjadala, Nakumbuka nlikuwa napenda sana kutembea barabarani na mitaani kwa spidi ambayo watu walilalamika nakimbiza gari na kuweka maisha ya raia hatarini.
Nikaja kugundua kwamba hakuna sehemu nayowahi zaidi zaidi tu ya ushamba wa gari, sifa na kuigana.
Mwaka 2015 (miaka 23) nilienda driving school na nikapewa leseni ya udereva, baada ya hapo nikawa na gari ya kwanza Carina TI nilyoshauriwa na nafundi kwa bajet yangu, niliipenda niliiwekea rim sport, kuweka tint kwenye vioo, mziki mnene, n.k ili tu nionekane 😁😁
kuanzia hapo kila gari niliyokuwa nayo niliipenda sana kwa kuiremba sambamba na kuipa moto / kukimbiza, Ila nikiri wazi tu huu ushamba umeniisha mwaka huu mwezi wa february nilipokuwa nampeleka dada yangu sehemu fulani akawa analalamika kwani nawahi wapi na spidi yangu inampa kizunguzungu, nilimpeleka hio sehemu asubuhi na kumrudisha jioni kwa muda wa wiki mbili.
Nilianza kuona kwakweli spidi niliyozoea kuendeshea gari ipo juu japo mimi niliona kawaida, Nikaona hakuna sehemu nayowahi na nikaona nahatarisha maisha ya watu wanaokatiza barabara hasa watoto.
Kwa sasa spidi yangu nayopenda kutembelea ni haivuki 40 kph na kwenye barabara ya vumbi haizidi 20 ili nisitimue vumbi na kuwachafua raia.
Kwa spidi hii nimeanza kuona raha ya kiendesha gari, akili yote inakuwa inaweza kumudu gari na mazingira ya barabara na kusikiliza muziki bila wasi wasi.
Uendeshaji wa gari kwa spidi kubwa ni hatari kwako na wengine, chukua hatua