Watanzania wenzangu sote tumekua tukisikia jinsi ndugu zetu wanaofanya biashara ya kusafirisha Watalii wanavonyanyaswa na kunyanyapaliwa kutoka kwa jirani zetu hawa. Kwa maneno ya kawaida tu ni vigumu kuona usumbufu unaowakabiri ndugu zetu aswa unaposikia ya kwamba Waziri anayehusika na maswala ya utalii amekwisha wasiliana na waziri mwenza katika kutafuta suruhu.kwa maoni yangu na hii ni baada ya kupata ushuhuda wa aliyekutwa na kadhia endapo nawe utapata nafasi ya kumsikiliza basi suruhisho ni kuamua kuufunga mpaka wetu mara moja na ndipo sasa juhudi za waziri husika zianze kwani kwa maneno ya shuhuda hata chakula ama kinywaji kama soda sasa madereva wa wakitanzania hawauziwi wanapokuwa katika foleni ya kuakikisha wageni wao wanafika Jomo Kenyatta Int Airport.Unyama gani huu, jamani kwa ndugu zetu ambao tukiwa nao uku kwetu wanaimba u afrika mashariki!!? TUFUNGE MPAKA NDIO TUANGALIE NAMNA YA SURUHISHO PERID