Sababu tano za kufa kwa Bongo movie

Mimi nisichopenda..

1. Kila movie lazima ina mambo ya uchawi na ushirikina.. Yani zinaboa kwwli .

2.Kukosa akili na ubunifu..... Watafute vipanga wwnye vipaji na akli za darasani, makalio tunayaona mitaani huku, hatutaki ya kwenye TV
Yaani unajiuliza hivi kila BM actress lazima afungashe?
 
Wajuzi husema kama huna KIPAJI basi jitahidi uwe na hata Experience maana mtu mwenye experience akichanganya na juhudi, ubunifu na maarifa huwa ni bora zaidi ya mwenye kipaji sasa Bongo muvi wamekosa vyote hivyo na ndio maana kila siku wanalalamika. Embu jaribu kuchukua mfano huu angalia wasanii wengi wa bongo muvi wa sasa ni wale waliongia kwenye tasnia kwa kuwa tu ni wazuri wa muonekano pasi na kuangalia uwezo wa ndani wa mtu husika matokeo yake ni kazi mbovu ambayo hutupelekea watazamaji kuwa watabiri muvi itaishia vipi.
 
Nadhani haikuwa sahihi kuita movie, wangebaki kwenye kucheza maigizo yao kama zamani tu
 
Hii ya 5 kwangu ilinigusa sana na 2015 nilijiridhisha kabisa kuwa hiyo namba 3 wanayokabisa maana mtu aliyenauwezo mzuri wa akili awezi kuendeshwa akili na makundi et mara MAMA ONGEA NA MWANAOA au NIMESTUKA SASA!! huu ni umburula na nikajiapiza tutakutana kwenye hizo kazi zao wanazoringia zilizowatia kiburi binafsi sitakaa kuja kununua hizo movie tena!!
 
Mkuu upo sawa kbsa. Hiyo namba 1, 2 na 5 umepiga msumari wa inchi 6 kbsa. Tamaa ya pesa huwa mbaya sana. Wengi wanajikuta wamenunuliwa na chama. Tangu JB aingie kweny kampen za ccm hata kumuona tu sihitaji.
Wakina marlaw leo hii wamejichokea.
Kazi za kibongo huwa siangalii kbsa. Zinaanza kiajabu ajabu na zinaisha kiajabu ajabu km chuma ulete vile
 
Hii ya 5 kwangu ilinigusa sana na 2015 nilijiridhisha kabisa kuwa hiyo namba 3 wanayokabisa maana mtu aliyenauwezo mzuri wa akili awezi kuendeshwa akili na makundi et mara MAMA ONGEA NA MWANAOA au NIMESTUKA SASA!! huu ni umburula na nikajiapiza tutakutana kwenye hizo kazi zao wanazoringia zilizowatia kiburi binafsi sitakaa kuja kununua hizo movie tena!!
Mwaka 2015 niliaga rasmi kuangalia bongo movie! Walinichafua roho sana!
Mkuu upo sawa kbsa. Hiyo namba 1, 2 na 5 umepiga msumari wa inchi 6 kbsa. Tamaa ya pesa huwa mbaya sana. Wengi wanajikuta wamenunuliwa na chama. Tangu JB aingie kweny kampen za ccm hata kumuona tu sihitaji.
Wakina marlaw leo hii wamejichokea.
Kazi za kibongo huwa siangalii kbsa. Zinaanza kiajabu ajabu na zinaisha kiajabu ajabu km chuma ulete vile
Yaani kujiingiza kwenye siasa ndio ilikuwa mwanzo wa kifo chao.
Hawakuwa na uwezo wa kufikiri maisha miaka miwili ijayo yatakuwaje.
 
Pia wadada ndio sehemu ya kufanyia biashara ya ukahaba,atavaa vibaya,ataonyesha miguu,kila kitu,halafu anakaa anasubiri ma director wa movie wawatafutie wanaume.

Kuna mmoja alishapelekwa Congo Drc baada ya kupendwa huko,Dalali alikuwa mwanamuziki mmoja wa FM Academia "tajiri"
 
Pia wadada ndio sehemu ya kufanyia biashara ya ukahaba,atavaa vibaya,ataonyesha miguu,kila kitu,halafu anakaa anasubiri ma director wa movie wawatafutie wanaume.

Kuna mmoja alishapelekwa Congo Drc baada ya kupendwa huko,Dalali alikuwa mwanamuziki mmoja wa FM Academia "tajiri"
Sure! wadada wengi wanatumia movie kutangaza biashara ya ukahaba kwa kusaka ma sponsors.
 
Spot on!

Kila binti aliyeshiriki umiss lazima aingie Bongo Movie

Akina Mercy Johnson, Uche Jombo walishiriki wapi umiss?

Si kila mtu anaweza Director au script writer mzuri
Kumbuka Nollwood ambae ana elimu ndogo ni degree moja. Ijapokuwa Hollywood kuna ambao hawana elimu, lakini hii tansia ilianza kabla ya karne ya 19, lakini bado wanaangalia vipaji. Hapa nyumbani kuna watu wenye vipaji kama Mercy Johnson ambao wana fit kila sehemu. Na pia kuna wengine wana fit sehemu moja tu. Tatizo wao wanaweza kumuweka sehemu ambayo hafit hivyo anaonekana si muigizaji.
 
Kinadada/ wanawake wa Bongo Movie wanatumia sanaa kama sehemu ya kutangaza Biashara yao Umalaya..


Wanaume nao wanashindana na dada zao kujiremba . ..



Bongo Movie lkn ina mahadhi ya Ulaya... Kwanini nisiangalie hizo tu Ulaya moja kwa moja..



Bongo Movie Bongo lala
 
Hiyo namba 5 ndo sababu kubwa , siwezi nunua movie ya mtu alikuwa anamtukana Lowasa na kututukana wapinzani malofa, tena wanatukejeli kwa vicheko....yaani nna hasira nao balaa

Hao milioni 6 tuliompigia Lowasa ambao wengi tupo mjini hatuwataki kabisa ...

Hao milioni 8 wa ccm waliowashabikia wengi wapo Mpitimbi hata umeme hawana na hata kununua movie hawawezi
nimecheka
 
Namba 5 napendekeza katika list yako iwe ya 1 and vice versa kama ningepanga kwa uzito....!
Mtoa mada asituzungusheeee! Wakati anajua sababu No.1 kaiweka mwisho. Wengine wanasema kuondoka ghafla kwa mtu aliyeipandisha chati bongo movie (Kanumba) kulisababisha hali hii, nakubali imechangia lakini kwa kiwango Fulani tu maana baada ya kifo cha Kanumba waliendelea kusikika na pengo lake halikuonekana sana. Bongo movie wameanza kupotea hewani Sept 2015 walipoacha Kazi yao ya msingi na kuingia mwili mzima kwenye siasa bila kutathmini kuwa kundi kubwa la washabiki wao wako upande gani. Kama kuna msanii anayepaswa kulaumiwa kuliko wote ni Vincent Kigosi (Ray). Kuyumba kwake Mara huku Mara kule kuliua kila kitu.
 
Watanzania tunazidi kuandika rekodi, ndani ya miaka mitano JB ana Movie 50 lakini Anold Schwarzenegger alianza miaka ya 1970 ila hadi leo hajafikia movie 50
 
Ngoja Lumumba waje wakuletee Povu. Kingine kumtegemea BASHITE kama ndio Thinktank wao.
Hili la Bashite ni kosa la kujifunga goli kwa mkono. Maana Refa anaweza kukubali goli lakini akakutoa nje kwa kadi nyekundu. Badala ya kutafuta wapi walipojikwaa wanahangaika na daktari wa mafua wakati wana kidonda.
 
Hili la Bashite ni kosa la kujifunga goli kwa mkono. Maana Refa anaweza kukubali goli lakini akakutoa nje kwa kadi nyekundu. Badala ya kutafuta wapi walipojikwaa wanahangaika na daktari wa mafua wakati wana kidonda.
Ha ha ha haaaaaa... Asante sana Mkuu.
 
Back
Top Bottom