MwanaDiwani naona tumekutana hapa tena!!!Wewe utakuwa mwanaCHADEMA lakini huifahamu CHADEMA katika mazingira ya jana na leo!.
Hao unaodai warudishwe lazima ufahamu kuwa hawahitaji kurudishwa kwa sasa kama fikra zako zinavyodhani kwa sababu wameishajirudisha wenyewe.
Mh. Mbowe na Dkt. Slaa kwa sasa wameishajenga mazingira ambayo hayahitaji hata kupigiwa kura ili kurudi katika nafasi zao za uongozi.
Mh. Mbowe na Dkt. Slaa wameishawafukuza na wanaendelea kuwafukuza wanachama wale ambao andiko lako ndiyo lilitakiwa liwaombe wawarudishe kina Mbowe na Dkt. Slaa katika nafasi zao.
Kwani hufahamu sababu iliyopelekea uchaguzi wa ndani wa CHADEMA Taifa kupigwa tarehe mara tatu ili waendelee kujenga mazingira ya kujirudisha wenyewe katika uongozi.
Kama unafahamu sababu zake, basi wewe utakuwa umetumwa pia kujenga mazingira ili ionekane kama kuna uwanja ulio sawa katika chaguzi za nafasi ya kitaifa ndani ya CHADEMA.
Kila siku ninasema, CHADEMA kimejengwa katika misingi ya kilaghai.
Vyama vya upinzani ni tofauti na chama kilichopo madarakani.
Gharama za kubadili viongozi kila baada ya miaka kumi zina faida na hasara yake na kuna wakati hasara inazidi faida.
Wakati wa Mtei,Bob Makani ungeweza kubadili uongozi bila athari kubwa kwa chama.Labda nikueleweshe kwa njia nyingine nayo ni kuwa mashambulizi yaliyokuwa yanavurumishiwa CDM wakati wa Mtei na Bob Makani ndiyo kama ya leo ya kufikia kuweka vinasa sauti chini ya kitanda?
Kwa nini CCM wanapenda uongozi wa CDM ubadilike,what is so special?