Sababu Kwanini Ethiopian Airlines inazidi kutawala anga la Afrika

mcshonde

Member
Jul 15, 2022
66
152
5835FA47-4B56-4961-B78A-8D00F60218DB.png


Septemba 2022 shirika la ndege la Ethiopia (Ethiopian Airlines Group) lilisaini mkataba wa kumiliki 49% ya shirika la ndege la Nigeria.

Hatua hiyo ikalifanya Shirika hili linalomilikiwa na serikali ya Ethiopia kwa 100% kuendelea kutawala anga la Afrika, kwani linamiliki mashirika mengine kama:-

24% ya hisa African Airline (ASKY) la Lomé Togo.
49% ya hisa katika Shirika la Ndege la Malawi.
45% ya shirika la ndege la Zambia
49% ya mashirika ya ndege ya Tchadia kutoka Chad.
99% ya umiliki wa hisa Ethiopian-Mozambique Airlines LTD
51% ya Umiliki wa Hisa wa DHL-ET Huduma za Usafirishaji mizigo.

Upo mpango wa kuingia mkataba na Air Djibouti pamoja na Guinea Ecuatorial Airlines.
Kwanini shirika hili lenye wafanyakazi 17000 linazidi kukua zaidi!?

Licha ya kumilikiwa na serikali kwa asilimia 100, Ethiopian Airlines yenye ndege 178 inazidi kukua kwa sababu:-

a) Serikali imeliruhusu kufanya biashara na kutoingilia utendaji wa bodi hasa inapomchagua mkurugenzi mtendaji/CEO (sio kawaida sana barani Afrika)
b) Ufanisi wa usimamizi wake (hakuna ujanja ujanja na upigaji, viongozi wake ni wataalamu wanaoijua biashara)
c) Nafasi yake ya kijiografia
d) Ukosefu wa washindani wanaofaa ndani ya Afrika
e) Kwa ujumla ni “mbinu kali” za kuwaweka washindani nje ya mstari.

Kipindi cha janga la Uviko-19 mashirika mengi yalitangaza kupata hasara mwisho wa mwaka 2020, lakini Ethiopian Airline lilikuwa kati ya mashirika machache duniani yaliyopata faida.
 
Ethiopia airline ndo kiboko ya noisy neibours airline wenyewe wanajionaga smart kwenye biashara na kutuona waTanzania wanyonge ila kwa ethiopia air hawatambai.
 
Air hostesses wana miaka 60, viajuza vinapiga wall putty usoni na bado sura hazina shukrani
Wakishuka ndege mkuu nakwambia wengine wanatembea kwa shida, sasa hapo nashangaa ikitokea emergency je. Wale nina uhakika wanachoka kusimama kwenye ndege lazima watakuwa wanapenda kupumzika na kutojichosha
 
Acha ATCL iendelee na kununua ndege kisiasa na kuzipaki viwanjani. Wanasiasa ndio wanaofanya biashara ya ndege na biashara nyingine tutegemee nini?
 
Waethipia pia Raia wao waliopo nje ya kwao wanafanya vizuri kwa sababu Serikali yao inawatambua kwa sasa ukiondoa Wachina SA wanaofata Wageni wenye uchumi mkubwa ni hao ET na pia hawana masharti magumu ya kurudi na fedha kwao hata kodi za bidhaa kwao ni rafiki daah Bongo daslm hao TRA wanaanza kupata faida kabla jata ya bidhaa kufika sokoni unategemea nini?safari yenye abiria wengi ni SA ila Air Tanzania inawashinda miaka mingi kwa sababu ya kukosa Uzalendo...
 
Ethiopian airlines kiboko ya KQ. Anambana kupitia wingi wa Ndege, kununua Malawian Airlines (hapo anambana safari za Southern Africa-Malawi, Tanzania, South Africa, Zambia, Zimbabwe) pia Nigerian air na ASKY maana yake West Africa kule atakimbiza pia.
 
Back
Top Bottom