Nzenzu
JF-Expert Member
- Aug 10, 2011
- 858
- 164
Siku tatu kabla ya mkutano wa Morogoro Nape Nnauye akongea kwenye radio moja, alisikika akishauri wananchi wa Morogoro wasiende kwenye mkutano wa CDM kwani kutatokea vurugu na wanaweza kuumia.. alikuwa anaongea kama vile kuna mpango funali, nilikuwa namsikiliza na watu wengine , kuna mtu akasema mbona anaongea hivi , au wamepanga kufanya vurugu.. kilichotokea baada ya hapo wote tunajua...
Binafsi namini huu ni mkakati wa serikali kutaka ama kufuta CDM, au kupiga vita mikutano ya CDM kabisa.
Hawawezi kufuta, wanataka kuwaaminisha wananchi kuwa CDM NI CHAMA CHA VURUGU!