jMali
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 8,379
- 4,899
- Thread starter
- #41
Huyu padri kawashika pabaya, chama kinaundwa na vijana kwa hiyo gia ya kuwasema ni genocidaires haipo, halafu kimejaa watutsi na wahutu kwa hiyo kuwasingizia ukabila nako haiwezekani. Vijana wenyewe wamekulia nje ni wasomi watupu sio vilaza, wanapiga hoja balaa! Ndio maana wamewazuia juu kwa juu wasiingie nchini. Wakiingia itakuwa tabu kuwazuia usajili kwa kuwa hakuna kisingizio chochote kwao. Wakisajisajili kifuatacho mzee wa 97% atapata namba za viatu!Shangaa mkuu,kimsingi paka na Watusi wenzie hawana chao Rwanda iwapo wataruhusu vyama vya siasa vifanye kazi za kisiasa kwa ukweli! Rejea jinsi mama victoire ingabire anavyonyanyaswa na serikali ya Watusi ni kwa sababu alikuja Rwanda katika sura ya upinzani halisi na angeruhusiwa kugombea tu,paka saahizi angekuwa jela. Hata padri Nahimana,amezuiliwa kuingia Rwanda kwa sababu paka hawezi kushindana nae maana ndani ya uchaguzi paka atagaragazwa kama mende. Nashangaa ile %97 iliyomuunga mkono kugombea kwa mara ya tatu IPO wapi maana angejivunia hiyo kama mtaji wake wa kumshinda Nahimana kwenye uchaguzi.