Songambele
JF-Expert Member
- Nov 20, 2007
- 4,695
- 2,553
Serikali ya Rwanda imepiga marufuku sauti kama zilivyoitwa makelele yanayotoka katika nyumba za ibada kwa madai ya kuleta bugudha kwa wasiohusika na ibada hizo. Marufuku hiyo inahusu adhana kutoka katika misikiti yote na midundo ya miziki kutoka katika makanisa mbali mbali na mahubiri kupitia vipaza sauti. Nukuu kutoka BBC asubuhi leo.
Waumini wameshaanza kuchukua hatua ya kupambana na amri hiyo kali ya serikali, kwa waislamu wameahidi kutumia radio kwa ajili ya adhana na kuhakikisha kila muumini anakuwa na Radio ili kupata taarifa za ibada na mahubiri.
Serikali ya Rwanda inatofautiana sana na serikali nyingine za Afrika Mashariki katika kusimamia maagizo yake, ikipiga marufuku manake ni marufuku kweli hakuna compromise wala kuandamana ni utekelezaji tu na atakae kaidi hatua kali za kisheria zinachukuliwa. Kwa mfano mifuko ya nylon(rambo) na jamii yake maruku Rwanda maana yake hutaona mfuko huo kigali ukikutwa nao lupango tu.
Kama ilivyo ada baadhi ya waumini hawajakubaliana na marufuku hiyo lakini hakuna namna nyingine ya wananchi kupinga kama ambavyo ingetokea Tz au Kenya watu wangepinga, wanaharakati wangetoka lakini wanaharakati hakuna Rwanda na waliokuwepo ni kuunga mkono mamlaka.
Waumini wameshaanza kuchukua hatua ya kupambana na amri hiyo kali ya serikali, kwa waislamu wameahidi kutumia radio kwa ajili ya adhana na kuhakikisha kila muumini anakuwa na Radio ili kupata taarifa za ibada na mahubiri.
Serikali ya Rwanda inatofautiana sana na serikali nyingine za Afrika Mashariki katika kusimamia maagizo yake, ikipiga marufuku manake ni marufuku kweli hakuna compromise wala kuandamana ni utekelezaji tu na atakae kaidi hatua kali za kisheria zinachukuliwa. Kwa mfano mifuko ya nylon(rambo) na jamii yake maruku Rwanda maana yake hutaona mfuko huo kigali ukikutwa nao lupango tu.
Kama ilivyo ada baadhi ya waumini hawajakubaliana na marufuku hiyo lakini hakuna namna nyingine ya wananchi kupinga kama ambavyo ingetokea Tz au Kenya watu wangepinga, wanaharakati wangetoka lakini wanaharakati hakuna Rwanda na waliokuwepo ni kuunga mkono mamlaka.