Ruzuku kwa vyama vya Siasa: Mnaonaje tumshauri Rais Magufuli aifutilie mbali ruzuku hii? Ni ufisadi

Mkuu Kilimba, ni kweli ruzuku ni haki ya vyama vya siasa, lakini hata mikutano pia ni haki ya vyama vya siasa, baada ya kuonekana mikutano haina maslahi kwa taifa, imefutwa, why not ruzuku? .
Jee kutoa ruzuku kwa vyama vya siasa ni jambo jema kuliko hizo fedha zingetumika kwenye shughuli nyingine za maana zaidi.
Pasco
Mkuu Pasco hizo shughuli za maana ambazo ili zifanyike ni lazima ruzuku ifutwe ni zipi? Na kama ni za maana kweli kuliko hiyo ruzuku ya vyama kwa nini zisipangiwe bajeti yake? Tumekuwa na huu mtazamo sana kwamba kwa nini pesa fulani isiende kufanya mambo ya maana. Hata ndege zilizonunuliwa tulidai pesa zake zingeenda kufanya hayo maana kwani ni watz wangapi wana uwezo wa kutumia huo usafiri? Kupanga ni kuchagua mkuu, tumekubali ruzuku iwepo tena kisheria. Nani kakuambia hii nchi ni maskini? Hivyo vijisenti tu vya ruzuku ndio vinakusumbua?
 
Basi CCMMM peke yake itagobga ruzuku za kimya kimya.
Mkuu Bokoyoka, CCM ina vitega uchumi kibao ilivyo loot toka kwa Watanzania enzi za chama kimoja hivyo itasurvive, pia Magufuli akaamua kwa vile CCM ndio chama Tawala, na ni chama dola, ni halali kuendeshwa kwa fedha za umma na vikao vya chama kuendeshewa ikulu.
Paskali
 
Ni mawazo mazuri sana Pasco. Ni busara Vyama vya Upinzani vifutiwe Ruzuku na ibaki kwa Chama Tawala tu ili haki itendeke maana hivyo Vyama havina la maana zaidi ya maandamano tu!!
Mkuu Gango, naunga mkono hoja, tena nashauri sio ruzuku tuu ifutwe hata hiyo ofisi ya Msajili wa Vyama nayo ifutwe tuu haina lingine la maana la kufanya baada ya kuisajili CCM, ruzuku ifutwe, vyama vingine vyote vinavyotegemea ruzuku vife,ibaki CCM pekee ndicho chama pekee chenye hati miliki ya kuitawala Tanzania milele kufuatia ni CCM pekee ndio yenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa urais wa muungano.
Pasco
 
Mkuu Bavaria, Tanu ilianzishwa kwa michango ya kujitolea.
Siasa sio ajira ni kazi ya kujitolea.
Ruzuku kwa vyama vya siasa ni ufisadi tuu kama ulivyo ufisadi mwingine wowote.
Pasco
Mkuu Pasco ya TANU ni historia, tunaweza kujifunza mengi kutokana na historia hiyo. Lakini sasa hivi mambo yamebadilika, hatuko enzi za TANU, sasa hivi siasa ni zaidi ya ajira, hakuna mwenye huo moyo kujitolea kama enzi za TANU. Tuko kizazi kingine kabisa ambacho pesa ndio kila kitu. Ikitokea muujiza hili suala la kufuta ruzuku likapelekwa bungeni utashangaa jinsi wabunge watakavyokuwa wamoja kulipinga tena kwa nguvu zao zote bila kujali itikadi zao.
 
Naunga mkono kabisa, hata hizo mali za umma zinazosadikika ziko ccm zirudishwe serikalini kisha anayetaka uongozi wa kisiasa ajitolee tu.maana yaweza kuwa kazi ya wito pia.
Mkuu Getrusa naunga mkono hoja, uongozi ni kujitolea, uongozi ni wito na sio ajira ya kuchumia au kufisidi kodi za Watanzania masikini wa kutupwa kwa kisingizio cha ruzuku.
Pasco
 
Mkuu Kilimba, ni kweli ruzuku ni haki ya vyama vya siasa, lakini hata mikutano pia ni haki ya vyama vya siasa, baada ya kuonekana mikutano haina maslahi kwa taifa, imefutwa, why not ruzuku? .
Jee kutoa ruzuku kwa vyama vya siasa ni jambo jema kuliko hizo fedha zingetumika kwenye shughuli nyingine za maana zaidi.
Pasco
Mkuu Pasco hiyo mikutano unayodai imepigwa marufuku mbona jana PROPESA LIPUNBAVU alifanya mkutano wa hadhara Lindi tena akapewa na ulinzi wa Polisi? Mikutano iliyopigwa marufuku ni ile ambayo ni tishio kwa CCM lakini vibaraka wa CCM ruksa kufanya mikutano. Vivyo hivyo ruzuku ikifutwa CCM na vibaraka wake wataendelea kupewa lakini si vyama tishio kwa CCM!
 
Anzisha mchakato wa kisheria,kama kwenda mahakamani kuiomba mahakama ifute sheria ya ruzuku,vyama vya siasa vijitegemee mbona vyama vya michezo,vyama vya ushirika havipati ruzuku kutoka serikalini na vimeweza kuendesha shughuli zao.
Hayo mamilioni ya ruzuku wanaopewa vyama vya siasa zipelekwe kuwasaidia wakulima,wafugaji,wavuvi,wafanyabiashara wadogo wadogo nk.
Mkuu Kitulo, naunga mkono hoja, mchakato niliuanzisha ni huu wa kutoa ushauri kwa Magufuli.
Pasco
 
jamani sasa kama hao viongozi wamesoma na wana elimu acheni wale pesa za ruzuku usitegemee hata siku moja mtu usiesoma na aliyesoma wakawa sawa,
 
Mkuu Gango, naunga mkono hoja, tena nashauri sio ruzuku tuu ifutwe hata hiyo ofisi ya Msajili wa Vyama nayo ifutwe tuu haina lingine la maana la kufanya baada ya kuisajili CCM, ruzuku ifutwe, vyama vingine vyote vinavyotegemea ruzuku vife,ibaki CCM pekee ndicho chama pekee chenye hati miliki ya kuitawala Tanzania milele kufuatia ni CCM pekee ndio yenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa urais wa muungano.
Pasco
Teh! Teh! Teh! Thanks a lot for being sarcastic!
 
CCM bila ruzuku haiwezi kujiendesha Hata kwa miezi miwili.Vyama kama CHADEMA na CUF vilianza bila ruzuku na viliweza kujiendasha na kukuwa mpaka vikaanza kupata ruzuku,CCM haina uzoefu huo.CCM ilikuwa inaendeshwa na fedha za serikali mpaka mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa na ruzuku kuanza kutolewa kwa vyama vya siasa. CCM iliendelea kukomba ruzuku yote kwa kuwa vyama vingine havikuwa na sifa ya kupata ruzuku mpaka baada ya uchaguzi mkuu wa 1995 ndipo baadhi ya vyama kama NCCR,CUF, CHADEMA na UDP vikaanza kupata ruzuku tena kidogo sana huku CCM ikikomba 90% ya ruzuku yote!
 
Ushauri mzuri ni kumwomba JPM aviache vyama vyenye usajiri na vinavyopata ruzuku kutumia ruzuku hizo kwa kufanya kazi za kisiasa ambazo wamesajiriwa kufanya. Kinyume cha hapo, sikukuu ya tarehe 10 October itakuwa inatuhusu!
 
Mkuu Zero, kwani rais Magufuli alipofuta mikutano ya hadhara ya kisiasa aliifuta kwa sheria gani?.
Rais aliposema atapunguza mishahara, atapunguza kwa sheria gani? .
Au alipotaka Maalim Seif anyimwe mafao, anyimwe kwa sheria gani? .
Ruzuku ni ufisadi, rais akiamua kuifuta hiyo ruzuku anaifuta tuu kwa sababu ni ufisadi tuu kama ulivyo ufisadi mwingine wowote.
Pasco
Mkuu sikupingi!

Nilitaka uutoe ufafanuzi direct ili na wenzetu wakuelewe!
 
Wasipo jitia, watatiwa hicho kidole watake wasitake, huu ni ufisadi tuu kama ulivyo ufisadi mwingine wowote.
Pasco

Acha Dharau Mkuu..
Inamaana hawa walioweka hiki kipengele ndani ya katiba walikua dhaifu zaidi yako??
Au zaidi ya huyo mtukufu wako..??punguza kuhemka
 
Wanabodi,
Kuna hii kauli ya "asiyefanya kazi na asile". Jee siasa nayo ni kazi ya kustahili mshahara kwa jina la ruzuku kwa vyama vya siasa? . Ruzuku hii iendelee kuwepo watu waendelee kuitafuna au ifutwe? .

Japo sijafanya utafiti wa ni nchi ngapi zinagawa ruzuku kwa vyama vya siasa lakini kwa nchi masikini kama Tanzania , serikali inayowajibika kwa watu wake na kuheshimu rasilimali kiduchu za taifa, haiwezi fedha zinazokamuliwa kama kodi kwa wananchi masikini wa kutupwa wanaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, halafu fedha hizo zinakuja kugawiwa bure kama ruzuku kwa watu wazima wenye nguvu zao! .

Je Huu sio ufisadi? .

Katika kuunga mkono juhudi za rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli za kubana matumizi ikiwemo kupunguza safari za nje, kuwaengua watumishi hewa, kufanya tumbua tumbua majipu ya ufisadi, namshauri rais wetu azifutilie mbali ruzuku za vyama vya siasa, huu ni ufisadi tuu kama ulivyo ufisadi mwingine wowote! .

Enzi za Nyerere kulitolewa ruzuku ya mbolea, mbegu bora na pembejeo za kilimo ili kuimarisha uzalishaji mali, sasa ruzuku hizo zimefutwa na badala yake mijitu mizima isiyo na matatizo yoyote, ndio inakaa bure kutafuna ruzuku ya bure bure huku masikini wakitaabika.

Aliyefanya kazi na asile! . Siasa sio kazi ya mshahara bali ni kazi ya kujitolea, ruzuku kwa vyama vya siasa ni ufisadi, jee is it just au ifutwe?.

Angalizo.
Japo ruzuku ni haki ya vyama vya siasa na inatolewa kwa mujibu wa katiba, lakini kiukweli ruzuku ni ufisadi tuu kama ulivyo ufisadi mwingine wowote na japo rais hana mamlaka ya kufuta jambo lolote lililoruhusiwa na katiba, lakini kwenye vita vya ufisadi akiamua anaweza.

Hata mikutano ya hadhara ya kisiasa popote uliruhusiwa na katiba lakini kufuatia ufisadi wa matumizi mabaya ya muda, badala ya vyama kuhamasisha watu wafanye kazi, vyama vinakalia kuhamasisha uzururaji kwa jina la maandamano na uvivu wa watu kukaa bure bila kufanya kazi kwa kisingizio cha kuhudhuria mikutano ya hadhara ya kisiasa nchi nzima. Rais Magufuli amepiga marufuku mikutano ya hadhara ya kisiasa popote na amefanikiwa.

Mishahara ni haki ya mwajiriwa, wakati wangine wakilipwa mishahara ya Shilingi 150,000 kwa mwezi, wengine wanalipwa shilingi milioni 40 kwa mwezi. Hiyo ni mishahara ya peponi. Rais Magufuli amebaini kuwa huo pia ni ufisadi hivyo ameamuru mishahara hiyo ikatwe na kima cha juu kubaki sii zaidi ya TZS 15.M.

Sasa kama haya yote rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli ameweza, anawezaje kuachia huu ufisadi mkubwa kabisa kwa jina la ruzuku uendelee kufanywa na serikali yake kwa kuwakamua kodi watu masikini wa nchi yake na kuwagawia bure bure watu matajiri kuitafuna? !.

Hakuna hata kuzisubiri Bunge kuifuta sheria ya ruzuku kwa vyama vya siasa, rais Magufulli kwavile ameamua kapambana na ufisadi na kubana matumizi, then apambane na ufisadi wote bila double standards na kubana matumizi yote yasiyo ya lazima zikiwemo ruzuku kwa vyama vya siasa.

Pasco

Rejea
Ushauri : Ruzuku za vyama vya siasa kwa mwaka 1 zipelekwe kusaidia maafa Bukoba
Rais apitie upya ruzuku za vyama vya siasa, ni zaidi ya laana
Ruzuku kwa vyama vya siasa ifutwe
MAONI: Serikali isitishe ruzuku kwa vyama vya siasa hadi 2020
Waanze kufuta ya CCM kwani wao ndiyo wanapata Ruzuku kubwa kuliko vyama vyote na wamekuwa wakiitumia vibaya Mpaka walikosa pesa za kuendesha mkutano mkuu Dodoma hadi setikali wakachukua pesa hazina kimya kimya kuendesha mkutano, kumbuka CCM wao wana vyanzo vingi vya mapato pia wanaongoza serikali wanaweza kuchukua pesa Hazina bila vyama vingine kujua kwa maana kwamba hata wakifutiwa ruzuku live bado watapata ruzuku kwa Syle ingine ya kimafia. Kwa sasa Ruzuku ya CCM inatumika kudhoofisha Ukawa kupitia kwa wakala wao Pro-pesa Lipumba huku msajili akila njama wampatie Ruzuku lipumba wagawane pesa zote chapchap na lipumba apate kuzitumia hizo pesa kuwanunua wafuasi zaidi na kutimiza lengo lao la kuuzika ukawa ili mwaka 2020 CCM watawale kama chama kimoja.
 
CCM bila ruzuku haiwezi kujiendesha Hata kwa miezi miwili.Vyama kama CHADEMA na CUF vilianza bila ruzuku na viliweza kujiendasha na kukuwa mpaka vikaanza kupata ruzuku,CCM haina uzoefu huo.CCM ilikuwa inaendeshwa na fedha za serikali mpaka mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa na ruzuku kuanza kutolewa kwa vyama vya siasa. CCM iliendelea kukomba ruzuku yote kwa kuwa vyama vingine havikuwa na sifa ya kupata ruzuku mpaka baada ya uchaguzi mkuu wa 1995 ndipo baadhi ya vyama kama NCCR,CUF, CHADEMA na UDP vikaanza kupata ruzuku tena kidogo sana huku CCM ikikomba 90% ya ruzuku yote!
Ruzuku ya CCM nyingi inapigwa na Kitengo cha uchakachuaji, propaganda, kamati za Ufundi na uchonganishi kinachoongozwa na mr February , Mfano sasa hivi wamekula pesa nyingi sana pesa zote za kubana matumizi kuzuia safari za nje, pesa za maafa, pesa za madawa, pesa za watumishi hewa nk , hiyo pesa yote inaliwa na Wajanja baada ya kugundua kuwa Mkulu hapendi kusikia Ukawa inapiga hatua ndipo wakaitumia fursa hiyo kupenyeza bajeti zao na kupewa pesa nyingi ambazo hupigwa panga mpaka kufika kwa lipumba zinakuwa robo ni aina fulani ya ufisadi hatari kuliko Escrow, inashangaza mkulu kutumia pesa nyingi kupambana na ukawa kuliko kujenga viwanda, Madalali wa siasa baada ya kuzikosa Safari za nje sasa wanakula pesa kupitia mladi wa siasa za maji taka ambao unaigharimu serikali pesa nyingi kuliko Safari za nje.
 
Back
Top Bottom