Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Tofauti na tunavyoona hali ya mambo ndani ya CHADEMA ambacho kipo busy na shughuli za kisiasa nchini kwa kutumia vijipesa kidogo vya ruzuku na michango ya wananchi; chama cha mapinduzi chenye matrioni ya ruzuku kila mwaka hakijulikani kinazitumiaje hizo fedha.
Wadadisi wa mambo wanahoji, kama CHADEMA pamoja na uchanga wake, na karuzuku kadogo inakopata inaweza kufanya mambo mengi na makubwa kiasi hiki yanayoashiria ushiriki wa kweli katika shughuli za siasa, CCM yenye matrioni ya fedha si ilipaswa kufanya zaidi ya hapo?
CCM inatumia ofisi zilizojengwa na watanzania wote nchi nzima, hakilipi kodi ya pango la ofisi; CCM inakusanywa hela kutoka kwenye miradi iliyochangiwa na watanzania wote wakati wa chama kimoja: kama vile viwanja vya mipira, majengo ya kukodisha, pamoja na viwanda, na hivi sasa inajineemesha kutokana na kipato kitokanacho na miradi hiyo.
Kwa haraka haraka kama ukifanya tathimini ya kile ambacho CCM inauwezo wa kukusanya kwa mwaka na matumizi yake, matrioni ya fedha yanabaki mfukoni. Lakini chama hiki hakijishughulishi na jambo lolote linalohusu affairs za watu.
Hakijishughulishi kwenda kusikiliza kero za wananchi na kutoa maelezo juu ya masuala ambayo kiliahidi kutekeleza mwaka 2010 na hakikutekeleza. Hakijishughulishi na ukusanyaji wa maoni ya katiba (taarifa za ndani zinaonyesha kwamba kuna kikosi kazi kinatengeneza hayo maoni, badala ya kuyakusanywa kwa wananchi kama inavyofanya CHADEMA), na zaidi ya yote, chama hiki hakionyeshi kuguswa na matatizo yanayowakabili wananchi hata japo kwa kujaribu kuwa nao na kushirikiana nao kuyatatua.
Mimi najiuliza hapa, hizi ruzuku kubwa ambayo chama hiki kinaipata, inatumika wapi, na inatumikaje? Na pesa zile zinazokusanywa kwenye miradi mbalimbali ambayo ilijengwa na watanzania wote inatumika wapi?
Tunataka majibu yanayojitosheleza siyo longolongo. Kuna taarifa za ndani zinazoonyesha kwamba ruzuku ya chama chenu inawaneemesha baadhi ya vigogo ndani ya chama. Kama mtaleta hadidhi za sungura na paka mimi nitamwaga mboga hapa. Tayari nina data za matawi yenu ambayo yameripoti kutokupata hela yoyote kutoka makao makuu huku kila tawi likipangiwa kiasi cha fedha cha kuchangia makao makuu. Mtueleze ni kwanini huko makao makuu kunahitaji kuongezewa hela tu ilihali hakuna cha maana kinachoendelea katika harakati za kisiasa?
cc. HAMY-D, Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba, Ritz, ZeMarcopolo, babayako utaifakwanza, FaizaFoxy, etc.
Wadadisi wa mambo wanahoji, kama CHADEMA pamoja na uchanga wake, na karuzuku kadogo inakopata inaweza kufanya mambo mengi na makubwa kiasi hiki yanayoashiria ushiriki wa kweli katika shughuli za siasa, CCM yenye matrioni ya fedha si ilipaswa kufanya zaidi ya hapo?
CCM inatumia ofisi zilizojengwa na watanzania wote nchi nzima, hakilipi kodi ya pango la ofisi; CCM inakusanywa hela kutoka kwenye miradi iliyochangiwa na watanzania wote wakati wa chama kimoja: kama vile viwanja vya mipira, majengo ya kukodisha, pamoja na viwanda, na hivi sasa inajineemesha kutokana na kipato kitokanacho na miradi hiyo.
Kwa haraka haraka kama ukifanya tathimini ya kile ambacho CCM inauwezo wa kukusanya kwa mwaka na matumizi yake, matrioni ya fedha yanabaki mfukoni. Lakini chama hiki hakijishughulishi na jambo lolote linalohusu affairs za watu.
Hakijishughulishi kwenda kusikiliza kero za wananchi na kutoa maelezo juu ya masuala ambayo kiliahidi kutekeleza mwaka 2010 na hakikutekeleza. Hakijishughulishi na ukusanyaji wa maoni ya katiba (taarifa za ndani zinaonyesha kwamba kuna kikosi kazi kinatengeneza hayo maoni, badala ya kuyakusanywa kwa wananchi kama inavyofanya CHADEMA), na zaidi ya yote, chama hiki hakionyeshi kuguswa na matatizo yanayowakabili wananchi hata japo kwa kujaribu kuwa nao na kushirikiana nao kuyatatua.
Mimi najiuliza hapa, hizi ruzuku kubwa ambayo chama hiki kinaipata, inatumika wapi, na inatumikaje? Na pesa zile zinazokusanywa kwenye miradi mbalimbali ambayo ilijengwa na watanzania wote inatumika wapi?
Tunataka majibu yanayojitosheleza siyo longolongo. Kuna taarifa za ndani zinazoonyesha kwamba ruzuku ya chama chenu inawaneemesha baadhi ya vigogo ndani ya chama. Kama mtaleta hadidhi za sungura na paka mimi nitamwaga mboga hapa. Tayari nina data za matawi yenu ambayo yameripoti kutokupata hela yoyote kutoka makao makuu huku kila tawi likipangiwa kiasi cha fedha cha kuchangia makao makuu. Mtueleze ni kwanini huko makao makuu kunahitaji kuongezewa hela tu ilihali hakuna cha maana kinachoendelea katika harakati za kisiasa?
cc. HAMY-D, Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba, Ritz, ZeMarcopolo, babayako utaifakwanza, FaizaFoxy, etc.
Last edited by a moderator: