Rutabanzibwa amtunishia msuli Waziri Huvisa

Rutabanzibwa amtunishia msuli Waziri Huvisa

Nchi hii inasonga kwa mizuka chini ya uongozi wa vibaka watanashati.Tofauti ya hawa vibaka na wale wa Tandale na Manzese ni uvaaji wa suti tu.Anaposema kwamba anamtetea kwa sababu anaonewa kwani kuna wananchi wangapi wadhurumiwa Ardhi na hao mnaowaita wawekezaji kupitia serikali za vijiji?,ni wananchi wangapi wanalipwa fidia ndogo ukilinganisha na mali zao chini ya wizara iyoiyo anayoiongoza?.ZIDUMU FIKRA ZA NDUGU KATIBU MKUU RUTABANZIBWA,KWANI NI FIKRA SAHIHI??????
 
Poor Ruta! unamtunishia misuli waziri mwanamke? wewe ni PS wa miaka mingi you should know better. Unyanyasaji wa ki-jinsia???? Tume ya maadili mmulikeni!
 
Hivi huyu ndiye anayetajwa tajwa kwenye maskendo mengi ya kifisadi? Hiyo Wizara wamepangana, Waziri Mhaya, Katibu Mhaya mtuhumiwa Mhaya. Hivi hapo NEMC itapeleka tingatinga?
Hivi huwezi kuwaza zaidi ya ukabila jamani???
 
Maswali yangu kwa Rutabanzibwa;
1:Kama huyo raia wa kigeni unayedai alipatiwa hati kwa mgongo wa rushwa kwa watumishi wa ofisi yako je huyo Mhaya mwenzio una uhakika gani kuwa hakupata hati kwa mgongo wa rushwa na ukabila kwako mwenyewe na watumishi wako?
2.Tatizo hapa sio kuwa na vibali halali wala feki bali ni kujenga katika maeneo ambayo siyo sahihi kwa mazingira,na vibali vyote vinatoka katika ofisi yako,kwa nini wasibanwe hao waliotoa vibali hivyo?
Hivi huwezi kujenga hoja nzito bila kuingia kwenye ukabila? Tusione fahari sana kutaja makabila ya watu bila sababu, unaweza kukuta mambo yametokea by coincidence lakini hapa ikaonekana kama ukabila ndio msingi wa suala lenyewe hasa,.
 
Ukabila: waziri wa ardhi mhaya katibu mhaya mvamizi mhaya. yamenitokea baraza la ardhi na nyumba kibaha, mvamizi wangu mhaya mwenyekiti wa baraza mhaya wakili wamvamizi mhaya. najua umeshafaham kilichonitokea.

Mkuu
Umenifurahisha sana hebu nipe kilichotokea kwn matokeo yanaweza yakawa mengi,na vp kwn baraza la ardhi na nyumba ndio mwisho wa maamuzi?
 
Hivi huwezi kujenga hoja nzito bila kuingia kwenye ukabila? Tusione fahari sana kutaja makabila ya watu bila sababu, unaweza kukuta mambo yametokea by coincidence lakini hapa ikaonekana kama ukabila ndio msingi wa suala lenyewe hasa,.

Samahani mkuu,hata sikupenda kuweka hilo suala la ukabila lakini ukisoma vizuri majibu ya Katibu Ruta namnukuu''Sio kwa sababu ni MHAYA....''yanaonyesha wazi alivyotumia ukabila ,alikuwa anajishuku!Hakuna aliyemuuliza swali hilo!Ukiwa askari unatembea then unakutana na jamaa,ambaye kukuona tu anasema''Mi hata sijaiba hizo hela''Kamata hilo,litakuwa mwizi hilo!!Kauli zake mkuu zilionyesha ukabila!!
Samahani kwa kueleweka vibaya!
 
RUTABANZIBWA....Rutabanzibwa....HUYU NI FISADI KWELI KWELI.... na hata hapa onaona jeuri yake HE DOESN*T CARE ABOUT MINISTER...HE IS PURELY FISADI LONG TIME..

===>> Mama Tibaijuka kashindwa kumtimua kisa MHAYA MWENZAKE...na bado hapa anamkingia kifua mhalifu MHAYA mwenzake....
na huku yeye ni katibu wa Wizara ya ardhi....unategemea nini hapa...???

===>> HUYU NI KUPIGA KELELE KILA KONA KTK MIKUTANO YA MIHADHARA NA MITANDAONI NA MAGAZETINI HADI RAIS AMTUPE NJE NA KUSHTAKIWA....

===>> Fisadi papa huyu Rutabanzibwa amezorotoshe sana maendeleo ya wizara kwa rushwa kubwa kubwa...na mama Tibaijuka kwacha sbb ni UKABILA...

==>> JK mfukuze huyu haraka na umechelewa...plz

We kweli mpuuzi kweli kweli !!!!!!!!! Waziri anawezaje kumtimua Katibu Mkuu ?? Watu wengine mpo jamvini ka ------- tu , Katibu mkuu ni uchaguliwa na Rais , hata Waziri Mkuu hawezi kumtimua sembuse Waziri
 
Unakumbuka kauli zilizotolewa na wanahisa wa IPTL dhidi ya huyo bwana kuhusiana na ripoti ya WB.

.........wewe hujui kuwa WB kuna wala rushwa wakubwa pia..........nimesha wahi kuhudhuria vikao vya bodi WB......
 
Nimesoma comments za watu hapa....kweli watanzania wengine ni vichekesho...

Inatakiwa watanzania tujifunze utawala wa sheria...mimi namtetea huyu katibu mkuu kwa anavyojitahidi kufanya kazi kwenye mazingira magumu....hiyo wizara ni ngumu na ina ufisadi mwingi lakini anajitahidi kuchukua hatua za kuupunguza...shida ya watanzania wanataka mtu anayepiga kelele kwenye vyombo vya habari ndio wajue anafanya kazi...kwa taarifa huyu alikua against IPTL kwa msiofahamu, lakini ikaletwa kwa nguvu za JK....huyu huyu amewahi kushtakiwa mara nyingi na kuna wakati mafisaidi walikua wamfunge jela kama sio jaji mkuu kuingilia hukumu....alichofanya hapa ni kuhakikisha sheria inafuatwa labda alikua anamfahamu anayeonewa....kama mnakumbuka hata lile soo la rose garden na manispaa ya kinondoni walipotaka kukurupuka tu kuvunja ikabidi magufuli aingilie kati akawaambia kavunjeni tu kama hamtalipa mabilioni.....hawa wadau wanaopiga kelele mbona hamuendi kuvunja nyumba ya lwakatare sababu wanaogopa kulipa .....hii wizara imejaa ufisadi wa kufa mtu na ulianza tangu serikali ya awamu ya pili....

....hiyo iko kwenye makaratasi....ili Wadanganyika mumuone shujaa....lakini behind the scene....huyu alituingiza mkenge...ni MAFIA

.....hilo la Mama Lwakatare........Waziri Huvisa alishalitolea ufafanuzi.......
 
Jamaa kweli ni mtetezi wa wanyonge,hili la Uhaya limekuja by the way

Mkuu Nzi kwenye taratibu za uandishi ukimquote mtu unastahili kumquote hadi mwisho,..nimeandika sentence nzima ukijichukulia kipande ukataka ufafanuzi nadhani sio sahii...ujumbe wangu uko kwenye kipande ulichoacha

Chifu, niliomba uthibitisho wa kuonyesha huyu jamaa unayemtetea, kuwa ni mzalendo. Sasa unaposema uthibitisho wako ni huo wa kusema, "hili la Uhaya limekuja by the way" ndilo linaonyesha kwamba huyo jamaa ni mtetezi wa wanyonge?!?

Weka uthibitisho hapa wa kuonyesha namna huyu jamaa alivyotetea wanyonge.

1. Thibitisha ni namna gani ametetea wanyonge kwa kuondoa uozo wa watumishi wa ardhi kugawa na kuuza viwanja vya raia mara mia mia!!
2. Thibitisha alivyoweza kuona maeneo ya wazi, maeneo ambayo watoto wangecheza, raia wangejipumzisha, maji yangepita kufuata mkondo wake n.k.
3. Thibitisha jinsi anavyotetea wakulima na wafugaji wanaofukuzwa sasa kila mahala kwa wimbo wa uwekezaji mkubwa wa kilimo!!
4. Thibitisha jinsi anavyotetea watu wanaoishi kando kando ya hifadhi za misitu na wanyama, wanavyonyanyaswa kwa wimbo wa uhifadhi wa bionuai!!

Thibitisha chifu, siyo ulete stori za "hili la Uhaya limekuja by the way"
 
BAK, hii yote inaonesha jinsi utendaji serikalini ulivyokuwa at its lowest level ever. Waziri analalamika Katibu mkuu wa wizara anafanya mambo shaghalabagala hachukui hatua ili Katibu mkuu awajibishwe, Katibu mkuu wa wizara hiyohiyo kwa miaka 17 anasema kuna rushwa sana wizarani kwake na bado anaendelea na ukatibu mkuu bila kuchukua hatua yoyote. Sanasana anasema ameenda mahakamani bila kutaja alikuwa anamtetea nanai kwenye kesi iliyofunguliwa na nani. Wizara hii (ardhi) iko ICU sio utani.
Nasikia harufu ya choo
 
Iviiiii, Naomba kuuliza, Mh. Naziri Karamagi yuko wapi, alikuwa waziri wa wizara gani vile

Kumbe alikuwepo pia Wilson Masilingi, mnakumbuka?
 
Embu taja yale Mashamba makubwa kule Babati anamiliki nani? Ji...Tuuuu

Mbu ngeee
 
Mimi ninashangaa sana nchi hii kuwa huyu bwana bado yumo serikalini; kwanza afya yake ni ya mgogoro licha ya kuhusika na tuhuma nyingi za rushwa!! Sasa huyo anayesema alimuwekea dhanana kwasababu alikuwa anaonewa na sio kwasababu ni muhaya mwenzie; wananchi wangapi wameonewa na yeye hakuenda kuwawekea dhamana? Alikwenda kumuwekea dhamana Mugishagwe kwasababu ni muhaya mwenzie na wanafanya biashara pamoja period!! Wizara hii itazidi kuwatesa wananchi kwasababu ya lack of management prowess ya Mkweree kwa kufanya makosa ya kuwaweka Tibaijuka na Rutabanzibwa wakiwa wote washomile kuongoza wizara moja nyeti kama hiyo!!!
Waziri muhaya na katibu Mkuu mhaya kisha mtuhumiwa ni muhaya unategemea nini?
 
Ukabila: waziri wa ardhi mhaya katibu mhaya mvamizi mhaya. yamenitokea baraza la ardhi na nyumba kibaha, mvamizi wangu mhaya mwenyekiti wa baraza mhaya wakili wamvamizi mhaya. najua umeshafaham kilichonitokea.

Wakili wako alikua kabila gani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom