Rushwa imetamalaki, uzembe umekithiri

Rushwa imetamalaki, uzembe umekithiri

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,602
Reaction score
830,350
Ifike mahali tusionekane wapingaji na wakosoaji wa kila kitu,! Jamani tuna hoja tusikilizwe! Tutapongeza panapostahili, tutakosoa penye mushkeli.... Tunajenga boma moja hatuna haja ya kufanyiana hujuma.

Ukweli mchungu ni kwamba hali ni mbaya taasisi za serikali hasa zile zinazohusika na wananchi moja kwa moja, kuna taasisi zimesahauliwa na nyingine kukumbukwa sana TRA ARDHI na MIUNDOMBINU pengine huku ndio kumewekewa jicho kali sana.

Lakini huku kwengine hali ni mbaya sana. Jeshi la polisi na vitengo vyake vyote , huduma za afya, serikali za mitaa, elimu hakufai hakufai hakufai.... Trafiki barabarani utadhani wamepewa kibali rasmi, huko kwenye vituo vya polisi magereza, idara za mahakama unaambiwa live kabisa ni ama A au B! La usipoambiwa itabidi tu ujiongeze.

Huduma za afya kwenye hospital na vituo vya afya vya serikali huduma zimezidi kuwa mbovu, uzembe ndio usiseme, rushwa ndio kama imezaliwa upya! Yako wapi yale MADUKA YA DAWA YA SERIKALI? Yameishia wapi yale???? wananchi wanaumizwa huko jamani.

Wafanyakazi hawana morali wa kazi tena! Hawana hakika na kesho yao hakuna kupandishwa madaraja, na kila uchao ni uhakiki usiokoma NI VEMA HILI JAMBO LIKAWA NA TIME FRAME ili watu waweze kuwa na uhakika na ajira zao.

Tusidili na mambo makubwa tu huku kwenye msingi mambo yanaharibika na nchi inapata aibu kubwa hasa kwa wageni trafiki wanaongoza hasa tangu road license iondolewe... Shame shame shame on them.. Rushwa ya kulazimisha mpaka buku! Tena anaombwa mgeni.

Vijana wa usalama waluojazwa kwingine wapelekwe na huko nilikotaja na wakafanye kazi kwa weledi, tutaona maajabu lakini kwa sasa hali ni mbaya
 
Mtani ninakushangaa unavyolalamika ati Rushwa imekithiri,Kwani zile Bilioni nane za Kivuko kibovu zilikuwa nini??Au kuhonga nyumba za serikali kwa nyumba ndogo??

Aliyeweza kukwapua raslimali zetu akiwa na cheo kidogo atakwapua zaidi akiwa na cheo kikubwa.

Rushwa Keisha mpaka tupate Kiongozi aliyekuwa muadilifu na anayechukia rushwa na ufisadi toka ndani yake na si kuigiza.

Hakuna wa kupiga na na rushwa hapo, ni blah blah za kupiga zaidi.
 
Mhh,Mkuu umeamsha dude,kuna watakaokubaliana na watakaokupinga kutegemeana na "ukanda aliko,undugu,ukabila,itikadi,kiburi,imani potofu,madaraka nk.) . Ila haya ni mambo mazito sana ya kujadili kama ni kweli.
 
Umesema kweli tupu..

Hali ni mbaya sana.

Trafiki Polisi ndio wamekuwa manyang'au au niseme ni wakora kwa wananchi. Kosa dogo tu wanataka hela(rushwa) au unaona anaanza kuprint ile fine. Toka kufutwa kwa road license kila Trafiki barabarani anataka kadi ya gari.

Lakini hili na makosa mengine ni makosa ambayo mtu anaweza kupewa onyo au elimu. Sio kila kosa Lazima mtu awe penalised.. Shame kabisa.

Kwenye madawa huko nyepesi nyepesi ni deni la MSD kwa serikali ni Mabilioni mengi tu. MSD has lost its purchasing power na hayo maduka yatakufa tu. Ambapo hayajafunguliwa ni Ndoto kufunguliwa.

Hospitalini huduma ovyo na morali ipo chini.

Wapo busy kumsaidia Lipumba kumaliza CUF na UKAWA..
Shame.
 
Watanzania ni wajinga! Wanauawa kimyakimya lakini bado wanavumilia! Magufuli ameua taasisi zote za fedha. Hakuna mtumishi anae staafu aliye lipwa mafao yake karibu mwaka mmoja sasa. BIMA, NSSF, PSPF, LAPF , NHIF Wote wamefilisika.Halmashauri nyingi zimebaki kama shule za sekondari! No money, hata karatasi wanaomba ! Mpaka 2020 haspitali zote na vyuo vya ualimu vitabaki magofu.
 
Mtani ninakushangaa unavyolalamika ati Rushwa imekithiri,Kwani zile Bilioni nane za Kivuko kibovu zilikuwa nini??Au kuhonga nyumba za serikali kwa nyumba ndogo??

Aliyeweza kukwapua raslimali zetu akiwa na cheo kidogo atakwapua zaidi akiwa na cheo kikubwa.

Rushwa Keisha mpaka tupate Kiongozi aliyekuwa muadilifu na anayechukia rushwa na ufisadi toka ndani yake na si kuigiza.

Hakuna wa kupiga na na rushwa hapo, ni blah blah za kupiga zaidi.

LOWASA?
 
Wapingaji kazini. Somebody somewhere is controlling us. Ngoja waje waliotumwa na kuwekwa wajibu.
 
Rushwa imezaliwa upya! Upya kabisa, afadhali ya serikali iliyopita, wala rushwa walikuwa na ka uoga/aibu.
Kila mtu anasema liwalo na liwe maadamu hakuna ushahidi wa kunifunga
 
Daah!mkuu umesema kweli,halmashauri rushwa imeota mizizi,unaombwa ili upewe haki yako.

Dont settle for less
 
Watanzania ni wajinga! Wanauawa kimyakimya lakini bado wanavumilia! Magufuli ameua taasisi zote za fedha. Hakuna mtumishi anae staafu aliye lipwa mafao yake karibu mwaka mmoja sasa. BIMA, NSSF, PSPF, LAPF , NHIF Wote wamefilisika.Halmashauri nyingi zimebaki kama shule za sekondari! No money, hata karatasi wanaomba ! Mpaka 2020 haspitali zote na vyuo vya ualimu vitabaki magofu.

Huu ni ukweli mchungu mkuu thanks kwa kuusema. Unachukua vyanzo vyote vya mapato vya halmashauri na kuwaacha hohehahe what do you expect? Halafu kituko kingine kwa kuwa kazi zilizokuwa zinafanywa na Halmashauri zimechukuliwa na TRA nimewasikia TRA wametangaza nafasi za kazi mpya 400 lakini sijasikia Halmashauri zikipunguza watu. Hakuna kazi siku hizi halmashauri zaidi ya kupiga soga tu. Lets wait and see ila tunakoelekea si salama tuuachie muda utatupa majibu.
 
kwa hili nakubaliana asilimia zote...halmashauli.ya ilemela kitengo cha arizi ni aibu!! yani unaweza kusimama dilishani masaa mawili wahudumu wapo wanajitafutisha mafaili tuuu kaaa....yote tisa kumi nilipeleka barua ya kubadilisha umiliki ya nyumba tangu trh 30hadi leo hakuna kushughulikiwa...nimefatilia hadi nimechoka ...hakiananani nchi hii inaelekea shimoni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom