Rushwa imeshamiri uhamiaji mkoa wa Kilimanjaro

Rushwa imeshamiri uhamiaji mkoa wa Kilimanjaro

kyagata

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2016
Posts
13,755
Reaction score
25,607
Wakuu
Nimekwenda ofisi za uhamiaji mkoa wa Kilimanjaro nimeshuhudia rushwa iliyokomaa pale. Kuna sample ya watu kama Sajenti Mruma na ASI Sembua Ngesheri na wengine wengi wanaomba rushwa balaa.

Ofisi ni kama haina usimamizi vile kila mtu anajifanyia atakavyo, huwezi kushughulikiwa kazi yako bila kutoa pesa. Wakuu wao wamelala tu wala hawawajibishi hao maofisa wao.

Naomba mamlaka zinazohusika wawaondoe hawa watu haraka sana.
 
huyo mruma na ngesheri nawafahamu.ngesheri kaporomosha bonge la jumba kule bomang'ombe kwa pesa za rushwa.
mruma kuna kipindi nilitaka kumshikisha takukuru akaponyoka.
pale mtu mwema ni mmoja tu mama mmoja hivi anaitwa Lillian huyo ndio mtu poa,wengine wote wala rushwa tu.
 
kuna majitu bado yanaishi zama ziiiileeeeeeee za kipindi kileeee, ss ivi utasikia mzinga unalia.
 
huyo mruma na ngesheri nawafahamu.ngesheri kaporomosha bonge la jumbo kule bomang'ombe kwa pesa za rushwa.
mruma kuna kipindi nilitaka kumshikisha takukuru akaponyoka.
pale mtu mwema ni mmoja tu mama mmoja hivi anaitwa Lillian huyo ndio mtu poa,wengine wote wala rushwa tu.
mkuu,huyo lilian na yeye ni wale wale tu anaomba rushwa sana kama wenzie.
solution ni kufagia watumishi wote wa hii ofisi maana kila mwananchi niliyekutana nae pale analalamika kuwa kaombwa pesa.
 
Wahamishwe wakafanye kazi sehemu ambapo watamulikwa kwa ukaribu na wakipatikana waondolewe kazini kabisa
hao dawa yao ni kufukuzwa tu,maana wakipelekwa kwingine wataenda kuwaambukiza madhambi yao na wengine ambao walikua hawajui kuomba rushwa,mwisho wa siku mtandao wa rushwa utazidi kuwa mkubwa ndani ya Idara ya uhamiaji.
 
mkuu,huyo lilian na yeye ni wale wale tu anaomba rushwa sana kama wenzie.
solution ni kufagia watumishi wote wa hii ofisi maana kila mwananchi niliyekutana nae pale analalamika kuwa kaombwa pesa.
Mkuu kyagata wahusika kama wanapitia humu watakuwa wamepata ujumbe wako.
Lakini naomba nikuulize wewe unahitaji huduma gani katika ofisi hiyo kiasi cha kuwa unazunguka kuwafahamu watumishi wote wa ofisi hiyo kuwa ni wala rushwa?

Au wewe ni mfanyakazi katika ofisi husika? Au ni wakala/ kishoka unaowatafutia watu pasipoti kwa kuwapiga pesa hivyo wamekushitukia na kuamua kukuwekea ngumu hivyo umeamua kumwaga hasira zako huku? Au ni majungu katika ubora wake?

Mkuu Hiyo ofisi ina maana haina hata boss wa kumpelekea malalamiko yako akusaidie kama umenyimwa haki yako?

Rushwa ni adui wa haki usiombe wala kutoa rushwa.
 
Pia uhamiaji Tanga ni problem kubwa kwa Rushwa. Wanashirikiana na wafanyakazi wa mahoteli kuwapa taarifa ya wageni wanolala mahotelini asubuhi na mapema maafisa uhamiaji wanavamia hata wakikutwa na vibali halali husumbuliwa mpaka watoe Rushwa. Naomba wahusika makao makuu walifanyie kazi hili. It's very shame.
 
Mkuu kyagata wahusika kama wanapitia humu watakuwa wamepata ujumbe wako.
Lakini naomba nikuulize wewe unahitaji huduma gani katika ofisi hiyo kiasi cha kuwa unazunguka kuwafahamu watumishi wote wa ofisi hiyo kuwa ni wala rushwa?

Au wewe ni mfanyakazi katika ofisi husika? Au ni wakala/ kishoka unaowatafutia watu pasipoti kwa kuwapiga pesa hivyo wamekushitukia na kuamua kukuwekea ngumu hivyo umeamua kumwaga hasira zako huku? Au ni majungu katika ubora wake?

Mkuu Hiyo ofisi ina maana haina hata boss wa kumpelekea malalamiko yako akusaidie kama umenyimwa haki yako?

Rushwa ni adui wa haki usiombe wala kutoa rushwa.
mkuu haya sio majungu na wala mimi sio kishoka.nimefika pale wakawa wananipiga dana dana mwishowe huyo sembua akanilengesha kwa mruma anisaidie kumbe mruma na sembua ni genge moja akaniambia eti nitoe laki 2 za sembua kwa ajili ya maji ya kunywa..nilivokataa nae akadhira kunifanyia kazi yangu,na kila ofisa ninaemfata pale ananiambia nimalizane na mruma kwanza.nikaomba kuonana na mkuu wao wakanikatalia.nikajiuliza hii ni ofisi ya umma au kichaka cha wapiga deals.
 
mkuu haya sio majungu na wala mimi sio kishoka.nimefika pale wakawa wananipiga dana dana mwishowe huyo sembua akanilengesha kwa mruma anisaidie kumbe mruma na sembua ni genge moja akaniambia eti nitoe laki 2 za sembua kwa ajili ya maji ya kunywa..nilivokataa nae akadhira kunifanyia kazi yangu,na kila ofisa ninaemfata pale ananiambia nimalizane na mruma kwanza.nikaomba kuonana na mkuu wao wakanikatalia.nikajiuliza hii ni ofisi ya umma au kichaka cha wapiga deals.
Ulikuwa na shida gani ya kufanya wakuombe rushwa?
 
Mtoa post ni mtu wa majungu, baada ya kufatilia taarifa hii, Nimegundua Kyagata alikuwa ni mtumishi wa ofisi ya uhamiaji hapa Kilimanjaro ila kwa sasa hivi amesomewa uhamisho, Na hawa anaowarushia tuhuma Inasemekana wamechangia uhamisho wa Kyagata kutoka na kugeuza ofisi kuwa kama saloon ya kike, Ushauri wangu kwa Kyagata acha wivu wa kike huko uendako ndio kiboko yao!
 
Pia uhamiaji Tanga ni problem kubwa kwa Rushwa. Wanashirikiana na wafanyakazi wa mahoteli kuwapa taarifa ya wageni wanolala mahotelini asubuhi na mapema maafisa uhamiaji wanavamia hata wakikutwa na vibali halali husumbuliwa mpaka watoe Rushwa. Naomba wahusika makao makuu walifanyie kazi hili. It's very shame.
Hii ni kweli asee nilipeleka watalii hotel moja mitaa ya Bombo nashangaa asubuhi PT imeingia eti ooh kuna watu tunawahisi hawana cjui vibali pumba tuu
 
Wakuu
Nimekwenda ofisi za uhamiaji mkoa wa Kilimanjaro nimeshuhudia rushwa iliyokomaa pale. Kuna sample ya watu kama Sajenti Mruma na ASI Sembua Ngesheri na wengine wengi wanaomba rushwa balaa.

Ofisi ni kama haina usimamizi vile kila mtu anajifanyia atakavyo, huwezi kushughulikiwa kazi yako bila kutoa pesa. Wakuu wao wamelala tu wala hawawajibishi hao maofisa wao.

Naomba mamlaka zinazohusika wawaondoe hawa watu haraka sana.


CC: Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro
Rais Magufuli
 
Back
Top Bottom