Iko hivi:Serikali iliweka mapingamizi matatu katika rufaa ya Lema,mahakama katika uamuzi wake mdogo (ruling) ilichokifanya leo baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili,ni kuyatupilia mbali ,mapingamizi mawili(dismissal)na kulikubalia moja(uphold).Matokeo ya kulikubali pingamizi moja ni kwamba to some extent rufaa ya Lema ilikuwa na matatizo lakini yanayorekebishika(curable defects).Hivyo Mahakama kwa kuzingatia misingi ya haki imeamua kuiondoa rufaa ya Lema Mahakamani lakini ikatoa nafasi ya kuirudisha tena(The Court of Appeal has decided to struck out the appeal with leave to re-file).Kwa kuwa ruhusa ya kurudisha rufaa imetolew,mahakama ikaona ni vema zitolewe siku 14 tu ili makosa yaliyobainishwa yarekebishwe na rufaa irudishwe.Rufaa ikisharudishwa mahakamani ndani ya siku 14 itapangiwa tarehe nyingine kwa kuzingatia ratiba ya Mahakama ya rufaa.