Rukwa: Mkuu wa Mkoa asema "marufuku kuachana, kaeni mlee Watoto"

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Bi.Queen Sendiga amepiga marufuku wanandoa kuachana na kuwaagiza viongozi wa serikali za Vijiji na Kata mkoani humo, kuwachukulia hatua kali za kisheria ikiwemo kuwafikisha kwenye vyombo vya dola vijana ambao watabainika kushindwa kulea watoto wao na kuzitelekeza familia zao majumbani.

Bi.Sendiga ameyasema hayo wakati akizindua zahanati ya Kijiji cha Mpona, kilichopo wilayani Sumbawanga, iliyojengwa kwa nguvu za wananchi.

Chanzo: ITV
 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Bi.Queen Sendiga amepiga marufuku wanandoa kuachana na kuwaagiza viongozi wa serikali za Vijiji na Kata mkoani humo, kuwachukulia hatua kali za kisheria ikiwemo kuwafikisha kwenye vyombo vya dola vijana ambao watabainika kushindwa kulea watoto wao na kuzitelekeza familia zao majumbani.

Bi.Sendiga ameyasema hayo wakati akizindua zahanati ya Kijiji cha Mpona, kilichopo wilayani Sumbawanga, iliyojengwa kwa nguvu za wananchi.

Chanzo: ITV
Huwa nampenda sana huyu Queen hivi ameolewa niongeze mke wa pili?

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mimi namuelewa sana Bidada yule, yaani waunganishe vikojoleo vyao alafu kulea matokeo ya tendo aachiwe mmoja haiwezekani...queen wanyooshe wafipa huko
 
Pumbavu Hana lolote huyo tamko jepesi tu hilo halina nguvu kisheria. Kataa ndoa Kataa kuoa ni kauli na Imani kamili na endelevu
 
Suala la mahusiano si la kiongozi kulitolea kauli, kuna wanawake wanateseka, wanapigwa na kunyanyasika na wanaume walio zaa nao, vile vile kwa wanaume, wapo wanaonyanyasika na wake walio zaa nao.

Ni mara ngapi tumesikia matukio ya mtu kuuliwa au kupewa ukilema sababu ikiwa ni mahusiano? Je hamjui kama hayo ni matokeo ya manyanyaso katika ndoa au mahusiano? Je mnafurahia taarifa hizo?

Binafsi me nashauri ukiwa kwenye mahusiano au ndoa ambayo utaona haieleweki, amani ya moyo huna, kutwa kucha we ni mtu wa majonzi ni kheri MUACHANE mapema, maana madhara yake huko mbeleni huwa ni makubwa.

Sasa wewe kaza fuvu uendelee kuumia kila uchwao ety kisa kiongozi fulani katoa tamko fulani, utafamba.
 
Ni jambo jema kuunganisha kuliko kutenganisha.Maandiko matakatifu yanasema alicho kuunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe Mathayo 19 :6,na vile vile yanasema Mungu hapendezwi na kuachana maana kwa maeneo hayo alipo Mkuu Wa mkoa ameona changamoto kubwa ya watoto kuhangaika na ndio maana amekuwa mkali akisisitiza kwa maneno makali ya marufuku kuachana
 
Back
Top Bottom