Feedback
JF-Expert Member
- Mar 14, 2011
- 7,988
- 4,507
Nafikiri Ruge unajua nini maana ya Copytrights kwenye Music, Demo, Sound track, audio, video nk. Kitendo cha redio Clouds ambayo wewe ni mmiliki wake kutumia sauti ya Sugu kwenye matangazo ya biashara ya fiesta huku ukijua kabisa lengo lake ni kujipatia faida bila idhini ya Sugu kisheria ni kosa la jinai. Mbali ya kuwa kosa la jinai vile vile ni kuonyesha dharau kwa wasanii wadogo kuwa unaweza kufanya kitendo chochote dhidi yao pasipo kuwasiliana nao na wasikufanye kitu chochote.
Kitendo ulichokifanya ni unyanyasaji wa hali ya juu kwa wasanii na hakiwezi kuvumiliwa kwenye ulimwengu wa ustaarabu, huu ni ushahidi tosha wa kile Sugu anachopigania 'maslahi ya wasanii' ambayo kwa mujibu wa Sugu yamehodhiwa na watu wachache 'Empire' ukiwemo wewe na wadosi. Mnawanyonya wasanii wachanga wanaojitafutia ridhiki kwa jasho lao ambao kwa sababu ya uchanga na unyonge wao hawawezi kupaza sauti zao.
Naamini ujumbe aliokutumia Sugu kupitia Clouds umekufikia unachotakiwa ni kujirekebisha na kuheshimu mikataba ya wasanii na si kuwatumikisha na kuwazungusha nchi nzima kwa kisingizio cha matamasha huku ukiwalipa ujira usiostahili wakati wewe na wadosi mkifaidi kupitia migongo yao.
Mimi si mwanamziki au msanii lakini ni mdau wa fani ya muziki kitendo unachokifanya hakikubaliki huwatendei haki wanamziki hasa wanamziki wachanga wanaochipukia-undergrounds. Hii hapa chini ni sauti uliyoitumia bila ridhaa ya mwenyewe na ushahidi wa vipindi vya Clouds kuitumia upo.
[/QUOTE]
Kitendo ulichokifanya ni unyanyasaji wa hali ya juu kwa wasanii na hakiwezi kuvumiliwa kwenye ulimwengu wa ustaarabu, huu ni ushahidi tosha wa kile Sugu anachopigania 'maslahi ya wasanii' ambayo kwa mujibu wa Sugu yamehodhiwa na watu wachache 'Empire' ukiwemo wewe na wadosi. Mnawanyonya wasanii wachanga wanaojitafutia ridhiki kwa jasho lao ambao kwa sababu ya uchanga na unyonge wao hawawezi kupaza sauti zao.
Naamini ujumbe aliokutumia Sugu kupitia Clouds umekufikia unachotakiwa ni kujirekebisha na kuheshimu mikataba ya wasanii na si kuwatumikisha na kuwazungusha nchi nzima kwa kisingizio cha matamasha huku ukiwalipa ujira usiostahili wakati wewe na wadosi mkifaidi kupitia migongo yao.
Mimi si mwanamziki au msanii lakini ni mdau wa fani ya muziki kitendo unachokifanya hakikubaliki huwatendei haki wanamziki hasa wanamziki wachanga wanaochipukia-undergrounds. Hii hapa chini ni sauti uliyoitumia bila ridhaa ya mwenyewe na ushahidi wa vipindi vya Clouds kuitumia upo.
[/QUOTE]
Last edited by a moderator: