Rufaa ya vyeti feki

Rufaa ya vyeti feki

Kweli ndugu, kuja jamaa nimesoma naye tangu O level mpaka chuo, naye jina lake lilitoka ana vyeti feki
tatizo liko hivi mkuu nsekwa, mwingine kweli alisoma labda akapata division 3 sasa anakwenda kuchongesha cheti cha kuonyesha ana division one ili aonekane ni kipanga, na siku ya uhakiki wa vyeti anaonyesha hicho cha kufoji badala ya kile cha kwake halali. Wengi wameingia kwenye mkenge kwa njia hiyo.
 
Sio kila mmoja alifoji, kunawengine vyeti vilikuwa na matatizo mengine, pia ni rahisi sana kumpata mfano kuwaita wote walio submit cheti, ukiwa interview kwa kuwauliza maswali utafahamu tuu.
Unawezaje kukaa miaka yote hiyo bila kugundua tatizo? mimi cheti changu cha form four kilionyesha jina jingine la shule niliyosoma na nilipokwenda kuchukua niligundua straight away nikawaandikia baraza la mitihani wakaniambia nitume kwa registered mail na walipokipata wakanitumia kingine kilichorekebishwa sasa kama mtu hawezi kufuatilia matatizo ya cheti chake ujue kuna walakini hapo.
 
Ndio nilichotaka kusema, watu wamefoji vyeti, walipokamatwa wanaona aibu kukiri kwa jamaa zao, wanadanganya eti wamekata rufaa ili kuwazuga ndugu zao, ndo maana hakuna anayejitokeza kuwa yeye kakata rufaa, kila mtu cheti safiii, sasa kejeli kwa serikali za nini?
Kuna dada mmoja namfahamu alipata zero form four lakini nimeshangaa kuona kamaliza chuo kikuu, kuna rafiki yangu aliniambia kama nakumbuka kuwa huyo dada alikua zero nikasema ndiyo akaniluliza ameonyesha vyeti gani kuingia chuo kikuu? sikua na jibu labda nilidhani chuo kikuu walianza sharia nyingine ya kuchukua watu hata kama walipata zero from four.
 
Sio kila mmoja alifoji, kunawengine vyeti vilikuwa na matatizo mengine, pia ni rahisi sana kumpata mfano kuwaita wote walio submit cheti, ukiwa interview kwa kuwauliza maswali utafahamu tuu.

Tuwekee hayo matatizo mengine tuchangie hoja!!!
 
Unawezaje kukaa miaka yote hiyo bila kugundua tatizo? mimi cheti changu cha form four kilionyesha jina jingine la shule niliyosoma na nilipokwenda kuchukua niligundua straight away nikawaandikia baraza la mitihani wakaniambia nitume kwa registered mail na walipokipata wakanitumia kingine kilichorekebishwa sasa kama mtu hawezi kufuatilia matatizo ya cheti chake ujue kuna walakini hapo.

Tatizi liligundulika mapema 2014, na cheti kilirudi baraza..... wakati wa uhakiki 2016 ofisi haikupeleka utumishi kiambatanisho cha barua ya baraza ko makosa yalitendeka ambayo yamesharekebishwa, ilautumishi ndi inatoa majibu na ofisi ndio inasubiri.
 
Kairuki(waziri wa uhakiki)watendee watu haki angalau kwa kuwajibu rufaa zao
wajue na wapange mipango mingine
Wana familia zinateseka,hata ww ukiambiwa acha uwaziri uendelee na ubunge wako utachanganyikiwa sembuse mtu aliyekua anategea mshaharatu na umefutiwa pini?
Waelezeni watu, mkumbusheni Raisi kama kuna rufaa hazikajibiwa msimsubiri mzee wa watu aseme kila kitu
Hawa mawazr vivuri wamshauri mh? Haya yapo tu kujinenepea nahayajui kama kuna watu wanapitia magumu waliyosababisha wao, utaskia wanasema wanajilizsha, eti serikali makini sijui zilizopita zilikua serikali MAKINIKIA! Matamko ndo kaz yao hawana kngne, bora kumuomba mungu tu amkumbshe Mh JPM lakn sio hawa mawaziri!
 
Weka bayana ndugu, unatumia cheti cha ndugu aliyepo private, mwanasiasa,au cha marehemu? Au baraza wanasema cheti chako kina tatizo gani? Unakuta watu 6 wamekata rufaa, wote cheti chao cha F 4 kina namba moja,
wampe nani? Lakini mngetangaza hadharani mliosoma nao wangewatetea!!

Mwenye original ndio atapona
 
Kweli ndugu, kuja jamaa nimesoma naye tangu O level mpaka chuo, naye jina lake lilitoka ana vyeti feki
Kuna waliobadilisha grades kwa mfano hisabati alipata F form four. Mjini mipango.... Akatafuta cheti kingine na pale kwenye hisabati akaweka B. Hicho cheti ndio kilichotimika kupatia ajira aliyokuwa nayo kabla ya uhakiki.... Wanakula kichwa. Scenario zipo nyingi tofauti tofauti.
 
Vu
Hawa mawazr vivuri wamshauri mh? Haya yapo tu kujinenepea nahayajui kama kuna watu wanapitia magumu waliyosababisha wao, utaskia wanasema wanajilizsha, eti serikali makini sijui zilizopita zilikua serikali MAKINIKIA! Matamko ndo kaz yao hawana kngne, bora kumuomba mungu tu amkumbshe Mh JPM lakn sio hawa mawaziri!
Vivuli hawasikilizwi.
 
Tunawaomba wabunge wetu watuulizie kwa waziri wa utumishi, a.k.a waziri wa feki na uhakiki ni lipi rufaa za walliopinga kuitwa feki zitasikilizwa?
Nimesikia majibu yanaanza kutoka 30/6, na mrufaa anayafuata mwenyewe Idodomya.
 
mi bado sana kukaribia huko kunakoitwa kuisoma namba, nachofanya nilikuwa nakifanya hata kabla huyu anayekuhenyesheni hajapendelewa kuingia majengoni!
 
Kweli ndugu, kuja jamaa nimesoma naye tangu O level mpaka chuo, naye jina lake lilitoka ana vyeti feki
Matokeo yao ya form four walipata madaraja gani?

Je vyeti walivyotumia kuajiriwa na vile walivyopeleka kuhakikiwa ndio vile vyenye matokeo waliopata walipomaliza kidato cha nne?


Ndugu Shukuru Haijakukuta. Kuna Binti namfahamu alitakiwa kufanya Mtihani wa Taifa mwaka 2003 aka omba kuhairisha kutokana na kupatwa na maradhi alikubaliwa na kufanya mwaka unaofatia yaani 2004 kwa namba zake za mwaka 2003 matokeo yake kaitwa anacheti feki.
Je ulize mtu kama huyu serikali itakuwa imemtendea haki?
Je wapo tayari kumlipa fidia kwa kumuaribia sifa kwa jamii?
 
Back
Top Bottom