Mkuu Nguruvi3,
Kwanza naunga mkono hoja.
Kunapotokea kifo cha utata, taarifa ya polisi ilipaswa kuishia kwenye kuthibitisha mwili umepatikana, ukiwa amekufa na daktari amethibitisha kifo .
Baada ya hapo taarifa ya kifo kimesababishwa na nini haikupaswa kutolewa na police bali daktari, tena kwa vile mwili ulifanyiwa post mortem, hata familia walipaswa kushauriwa wasizungumzie mwili umekutwajwe (bila nguo, na majeraha, umejaaje) kabla ya forensic report ambayo familia ndio hupewa na kuwa na disclosure liberty.
Marehemu kukutwa bila nguo sio uthibitisho wa crime wala mwili kukutwa na majeraha hayo matatu kwa mujibu wa mtoto wa marehemu pia sio uthibitisho wa crime kama uchunguzi wa forensic ungethibitisha hayo majeraha ni ya nini na ya lini maana mwili umekutwa ukiwa umekaa 3 days dead body in a room, hivyo there is a chance majereha hayo yalikuwa inflicted on dead body baada ya kufariki natural death.
Kitu ambacho sijasikia kikitajwa kwenye kifo hiki ni ambacho mimi nakihisi ni kuwa huyu Marehemu alitoka Dar kwenye mkutano ule ule wa CAG Mstaafu. Ulikuwa ni mkutano wa nini, ulijadili nini, waliohudhuria mkutano ule wajitokeze waseme marehemu alichangia nini kwenye mkutano ule ili tuweze ku connect the dots kama kilikuwa ni kifo cha kawaida or else.
Kwenye uwezo wa polisi wetu na serikali yetu kufanya baadhi ya mambo, unafahamika na niliisha wahi kuuzungumza hapa
Wanabodi Hili ni bandiko la kuhamasisha uzalendo miongoni mwetu sisi wana JF, pale inapotokea serikali yetu imeshindwa jambo fulani, kwa wale wenzetu wenye uwezo, jee tuwajibike kuisaidia serikali yetu au kusubiri mpaka ishindwe, halafu kazi yatu iwe ni kuikosoa tuu, kuibeza na kuizomea kuwa...
Haya mambo ya Ma RPC kutoa taarifa za urongo kwenye media na kutuona sisi wananchi wote kama ni watoto wa darasa la pili, pia niliisha wahi lizungumza humu kwa kumshauri IGP Sirro asiwaache ma RPC waropokaji kama hawa kulichafua jeshi letu safi la polisi
Wanabodi, Hii ni kama barua ya wazi kwa mkuu mpya wa jeshi letu la Polisi, IGP, Kamanda Simon Sirro, kutoka kwa raia mwema, anayemtakia mafanikio mema katika majukumu yake kama IGP mpya, nikimsisitiza karma ya shedding an innocent blood under any circumstances, haijawahi kumwacha mtu salama...
Hili la kifo hiki linahitaji maelezo ya ziada ili lieleweke.
Kwa vile Jamiiforums tumetajwa kwa kushutumiwa kwa uzushi, nashauri uongozi wa jf usikubali na tusikae kimya, hata kama aliyeleta taarifa hizo mwanzo ni just an ordinary member, lakini baada ya tuhuma kwa jf, ni ama huyo member awe equipped kwa kuwa linked na members humu wenye uwezo wa kufanya IJ wamuelekeze cha kufanya ili kuisafisha jf, au jf imtume member mwingine mwenye credentials za kufanya hayo makitu na ukweli ukibainika, ni kamanda Muroto kumpumzishwa tuu kwa uropokaji.
P