mwanadodoma
Member
- Mar 12, 2024
- 29
- 49
Naandika kwa uchungu mkubwa baada ya Mke wangu kufanyiwa udhalilishaji na huyu kijana mhuni anayeitwa MALIMA ambaye ni Polisi Jamii hapa Kata ya Nala.
Ni kijana ambaye anajiona yeye ni zaidi ya Polisi wa kawaida. Yeye ndie Polisi,yeye ndie Mwanasheria,yeye ndie Hakimu,yeye ndie Magereza. Kazi yake ni kukamata watu na kuwalazimisha wampe pesa akidai ili asiwafikishe Kituo cha Polisi.
Nimesikia Dodoma ameletwa RPC mpya ambaye ni Mwanamama hivyo RPC na RC wote ni wakinamama.
Tafadhali njooni Kata ya Nala itisheni kikao cha wananchi ili tuwaambie malalamiko yetu dhidi ya huyu Polisi Jamii anayeitwa MALIMA.
Ni mnyanyasaji sana kwa Wananchi wanyonge hasa wanawake kwa kuwa hawajui Sheria na Haki zao za msingi.
Haiwezekani mtu mmoja mhuni tu kwa kofia ya upolisi jamii awasumbue wake zetu kwa kumwaga vyakula vyao vya biashara akisema wamechafua mazingira kwa kumwaga maji yenye ukoko wakati ukweli ni kwamba aliwatongoza wakamkataa, na sasa anawakomesha kwa kuwakamata na kutaka wampe pesa akitishia kuwafunga jela.
Diwani anazo taarifa za unyanyasaji unaofanywa na huyu kijana lakini amekaa kimya. Tafadhali RC na RPC mpya Dodoma njooni Nala, itisheni Kikao ili msikie malalamiko yetu dhidi ya huyu mhuni polisi jamii anayeitwa Malima, tafadhali tusaidieni tumechoka na manyanyaso na uonezi wake.
Pia soma - Malima aliyetajwa na JamiiForums kuwa Polisi Jamii awekwa kikaangoni mbele ya mkutano wa hadhara
Ni kijana ambaye anajiona yeye ni zaidi ya Polisi wa kawaida. Yeye ndie Polisi,yeye ndie Mwanasheria,yeye ndie Hakimu,yeye ndie Magereza. Kazi yake ni kukamata watu na kuwalazimisha wampe pesa akidai ili asiwafikishe Kituo cha Polisi.
Nimesikia Dodoma ameletwa RPC mpya ambaye ni Mwanamama hivyo RPC na RC wote ni wakinamama.
Tafadhali njooni Kata ya Nala itisheni kikao cha wananchi ili tuwaambie malalamiko yetu dhidi ya huyu Polisi Jamii anayeitwa MALIMA.
Ni mnyanyasaji sana kwa Wananchi wanyonge hasa wanawake kwa kuwa hawajui Sheria na Haki zao za msingi.
Haiwezekani mtu mmoja mhuni tu kwa kofia ya upolisi jamii awasumbue wake zetu kwa kumwaga vyakula vyao vya biashara akisema wamechafua mazingira kwa kumwaga maji yenye ukoko wakati ukweli ni kwamba aliwatongoza wakamkataa, na sasa anawakomesha kwa kuwakamata na kutaka wampe pesa akitishia kuwafunga jela.
Diwani anazo taarifa za unyanyasaji unaofanywa na huyu kijana lakini amekaa kimya. Tafadhali RC na RPC mpya Dodoma njooni Nala, itisheni Kikao ili msikie malalamiko yetu dhidi ya huyu mhuni polisi jamii anayeitwa Malima, tafadhali tusaidieni tumechoka na manyanyaso na uonezi wake.
Pia soma - Malima aliyetajwa na JamiiForums kuwa Polisi Jamii awekwa kikaangoni mbele ya mkutano wa hadhara