RPC wa Dodoma, Afande Muroto aituhumu JamiiForums kwa kupotosha taarifa za kifo cha Sheikh Rashid Bura

JokaKuu

Platinum Member
Jul 31, 2006
30,408
54,886
Sheikh Bura alikutwa amekufa ndani ya ofisi yake. Afande Muroto anasema sababu ya kifo ni moyo wa Sheikh Bura " kufeli. " Taarifa za watu wengine zinadai mwili wa marehemu ulikutwa na majeraha matatu.




Mkuu JokaKuu

kuna msemo usemao '' ni bora kukaa kimya, unaweza kuongea na kuwatoa watu mashaka''

Kuna umuhimu wa viongozi kuchunga kauli zao, na si lazima waongelee kila jambo

Ukimsikiliza kamanda Muroto kuna maswali yanayochagiza udadisi badala ya uelewa
Wasaidizi wanaomshauri hawakumtendea haki kwa kuandaa huu mkutano

1. Kamanda anashambulia Nipashe na JF badala ya kujibu hoja za 'Wanafamilia'' waliokaririwa na magazeti mengine kama mwananchi wakizungumzia uwepo wa majeraha.

Ni muhimu kuijibu Familia, vinginevyo anashambulia messenger na si Message

2. Kamanda anadai wana simu watakazoziangalia kama zina kitu kinachohusiana na kifo Kamanda keshatoa conclusion kwamba kilichomuua ni kufeli kwa moyo.
Simu zitaleta majibu gani tofauti?

3. Kamanda kasema, aliporudi Dodoma alielekea Ofisini kwake.
Wakati huo hakuwa na mawasiliano, je, nani alimuona akielekea Ofisini?

4. Kamanda anasema, kilichomua Bura ni kufeli kwa moyo kulikosababisha ''circulation ya damu'' kukosekeana.

Hiyo ni taarifa inayotolewa na Daktari aliyefanya uchunguzi
a)Kulikuwa na postmortem na kama ilikuwepo kwanini kamanda hakueleza hilo kuondoa utata
b)Kwanini Daktari hakutoa taarifa za kitaalamu ?

Taarifa ya kamanda si ''professional' kwa kuzingatia haya

Kufeli kwa moyo (Heart Failure) si lazima iwe tukio la ghafla. Watu wanaishi na Heart Failure wakipata matibabu. Heart Failure ina maana moyo unashindwa lakini haina maana ni ghafla

Kinachoweza kutokea katika Heart Failure ya ghafla ni Heart attack ambayo huwa ni dharura

Kamanda hajaeleza kama Bura alikuwa na historia ya maradhi ya Moyo. Kama hilo lipo kuna possibility ilisababisha heart attack. Kama hakuna basi inaweza kuwa ni heart attack tu ilitokea

Yote hayo yanaelezwa kwa taarifa ya postmortem ambayo kwa nchi nyingine hutolewa na wataalam kwa kujua suala likienda mahakamani ni Dr tu anayeweza kutetea uchunguzi

Haya ni mambo yanayoelezwa na wataalam na ni magumu sana mbele ya sheria.

Kauli za kamanda mbele ya sheria zitamkwaza. Hivi akiulizwa aeleze patient history, Cardiac anatomy and physiology and pathology of heart failure ataeleza nini?

Akiulizwa Forensic ya kifo hadi kutoa conclusion ya heart failure, ataeleza nini?

Si suala a kusema kufeli kwa moyo.
Heart Failure ni topic pana sana ambayo Kamanda angepaswa kukaa mbali nayo.

Kwahiyo unaweza kuona kauli za kamanda zinavyozidi kuchanganya badala ya uhalisia

kamanda anasema waandishi waende kwa right source ambazo ni Polisi
Pengine kamanda ajiulize kwanini watu wanashaka na taarifa zao

Watu kutafuta habari za mitaani ni dalili ya kupoteza imani na right source.

Pascal Mayalla

Mkuu Nguruvi3,
Kwanza naunga mkono hoja.
Kunapotokea kifo cha utata, taarifa ya polisi ilipaswa kuishia kwenye kuthibitisha mwili umepatikana, ukiwa amekufa na daktari amethibitisha kifo .

Baada ya hapo taarifa ya kifo kimesababishwa na nini haikupaswa kutolewa na police bali daktari, tena kwa vile mwili ulifanyiwa post mortem, hata familia walipaswa kushauriwa wasizungumzie mwili umekutwajwe (bila nguo, na majeraha, umejaaje) kabla ya forensic report ambayo familia ndio hupewa na kuwa na disclosure liberty.

Marehemu kukutwa bila nguo sio uthibitisho wa crime wala mwili kukutwa na majeraha hayo matatu kwa mujibu wa mtoto wa marehemu pia sio uthibitisho wa crime kama uchunguzi wa forensic ungethibitisha hayo majeraha ni ya nini na ya lini maana mwili umekutwa ukiwa umekaa 3 days dead body in a room, hivyo there is a chance majereha hayo yalikuwa inflicted on dead body baada ya kufariki natural death.

Kitu ambacho sijasikia kikitajwa kwenye kifo hiki ni ambacho mimi nakihisi ni kuwa huyu Marehemu alitoka Dar kwenye mkutano ule ule wa CAG Mstaafu. Ulikuwa ni mkutano wa nini, ulijadili nini, waliohudhuria mkutano ule wajitokeze waseme marehemu alichangia nini kwenye mkutano ule ili tuweze ku connect the dots kama kilikuwa ni kifo cha kawaida or else.

Kwenye uwezo wa polisi wetu na serikali yetu kufanya baadhi ya mambo, unafahamika na niliisha wahi kuuzungumza hapa

Haya mambo ya Ma RPC kutoa taarifa za urongo kwenye media na kutuona sisi wananchi wote kama ni watoto wa darasa la pili, pia niliisha wahi lizungumza humu kwa kumshauri IGP Sirro asiwaache ma RPC waropokaji kama hawa kulichafua jeshi letu safi la polisi

Hili la kifo hiki linahitaji maelezo ya ziada ili lieleweke.
Kwa vile Jamiiforums tumetajwa kwa kushutumiwa kwa uzushi, nashauri uongozi wa jf usikubali na tusikae kimya, hata kama aliyeleta taarifa hizo mwanzo ni just an ordinary member, lakini baada ya tuhuma kwa jf, ni ama huyo member awe equipped kwa kuwa linked na members humu wenye uwezo wa kufanya IJ wamuelekeze cha kufanya ili kuisafisha jf, au jf imtume member mwingine mwenye credentials za kufanya hayo makitu na ukweli ukibainika, ni kamanda Muroto kumpumzishwa tuu kwa uropokaji.

P
Lakini kinachonishangaza ni hiki:

Polisi Tanzania wanao utaalam wa kujua kilichosababisha kifo na kukitangaza?

Au maiti ilishafanyiwa uchunguzi na wataalam husika, na huko ndiko alikotoa taarifa hiyo?

Je, yeye ndie mwenye mamlaka ya kutoa taarifa hiyo?

Ndugu wa marehemu hawakushirikishwa katika uchunguzi uliofanyika? Kwa maana wangeshirikishwa pasingekuwepo na sintofahamu kutoka kwao.

Mimi nadhani kuna umhimu mkubwa kwa Tanzania kurudi kwenye taratibu zinazotambulika katika kufanya mambo kama haya.
Polisi hawezi kujisemea tu chochote anachoona inafaa kisemwe.

"Atawafikeni malaika wa mauti hata mkiwa ktk ngome madhubuti" quran

Rest in peace sheikh Bura

BURA NI NANI

Akimzungumzia marehemu Bura, Mkurugenzi mwenza wa Taasisi ya Dalai Islamic Centre, Abdillah Mboryo, alisema enzi za uhai wake aliwahi kufanya kazi Jeshi la Polisi Kitengo cha Upelelezi katika mikoa mbalimbali.

Mbali na hilo, pia alikuwa Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pia amewahi kuwa mlinzi wa Rais katika utawala wa awamu ya kwanza wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Alisema alizaliwa miaka 60 iliyopita katika Kijiji cha Dalai wilayani Kondoa mkoani Dodoma ambapo ameacha mjane aitwaye Kuruthumu Mohammed na watoto watano.

Alisema mpaka mauti yanamfika alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Dalai Islamic Centre ambayo ilikuwa ikijihusisha na kusafirisha mahujaji kwenda nchini Makka pamoja na kuwa mmoja wa wamiliki wa shule za Zamzam.

Allah amsamehe makosa yake na kumuingiza katika rehema na pepo yake tukufu
Aamiyn

اللهم اغفر له وارحمه وعافه واعف عنه ووسع مدخله واكرم نزله وثبته بالقول الثابت

Zaidi, soma: Polisi: Mmiliki wa shule ZamZam amefariki kwa matatizo ya moyo, hakuna viashiria vya mauaji. Familia yatofautiana na Polisi
 
"Atawafikeni malaika wa mauti hata mkiwa katika ngome madhubuti" quran

Rest in peace Sheikh Bura

BURA NI NANI

Akimzungumzia marehemu Bura, Mkurugenzi mwenza wa Taasisi ya Dalai Islamic Centre, Abdillah Mboryo, alisema enzi za uhai wake aliwahi kufanya kazi Jeshi la Polisi Kitengo cha Upelelezi katika mikoa mbalimbali.

Mbali na hilo, pia alikuwa Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pia amewahi kuwa mlinzi wa Rais katika utawala wa awamu ya kwanza wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Alisema alizaliwa miaka 60 iliyopita katika Kijiji cha Dalai wilayani Kondoa mkoani Dodoma ambapo ameacha mjane aitwaye Kuruthumu Mohammed na watoto watano.

Alisema mpaka mauti yanamfika alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Dalai Islamic Centre ambayo ilikuwa ikijihusisha na kusafirisha mahujaji kwenda nchini Makka pamoja na kuwa mmoja wa wamiliki wa shule za Zamzam.

Allah amsamehe makosa yake na kumuingiza katika rehema na pepo yake tukufu
Aamiyn

اللهم اغفر له وارحمه وعافه واعف عنه ووسع مدخله واكرم نزله وثبته بالقول الثابت
 
Mkuu JokaKuu

kuna msemo usemao '' ni bora kukaa kimya, unaweza kuongea na kuwatoa watu mashaka''

Kuna umuhimu wa viongozi kuchunga kauli zao, na si lazima waongelee kila jambo

Ukimsikiliza kamanda Muroto kuna maswali yanayochagiza udadisi badala ya uelewa
Wasaidizi wanaomshauri hawakumtendea haki kwa kuandaa huu mkutano

1. Kamanda anashambulia Nipashe na JF badala ya kujibu hoja za 'Wanafamilia'' waliokaririwa na magazeti mengine kama mwananchi wakizungumzia uwepo wa majeraha.

Ni muhimu kuijibu Familia, vinginevyo anashambulia messenger na si Message

2. Kamanda anadai wana simu watakazoziangalia kama zina kitu kinachohusiana na kifo Kamanda keshatoa conclusion kwamba kilichomuua ni kufeli kwa moyo.
Simu zitaleta majibu gani tofauti?

3. Kamanda kasema, aliporudi Dodoma alielekea Ofisini kwake.
Wakati huo hakuwa na mawasiliano, je, nani alimuona akielekea Ofisini?

4. Kamanda anasema, kilichomua Bura ni kufeli kwa moyo kulikosababisha ''circulation ya damu'' kukosekeana.

Hiyo ni taarifa inayotolewa na Daktari aliyefanya uchunguzi
a)Kulikuwa na postmortem na kama ilikuwepo kwanini kamanda hakueleza hilo kuondoa utata
b)Kwanini Daktari hakutoa taarifa za kitaalamu ?

Taarifa ya kamanda si ''professional' kwa kuzingatia haya

Kufeli kwa moyo (Heart Failure) si lazima iwe tukio la ghafla. Watu wanaishi na Heart Failure wakipata matibabu. Heart Failure ina maana moyo unashindwa lakini haina maana ni ghafla

Kinachoweza kutokea katika Heart Failure ya ghafla ni Heart attack ambayo huwa ni dharura

Kamanda hajaeleza kama Bura alikuwa na historia ya maradhi ya Moyo. Kama hilo lipo kuna possibility ilisababisha heart attack. Kama hakuna basi inaweza kuwa ni heart attack tu ilitokea

Yote hayo yanaelezwa kwa taarifa ya postmortem ambayo kwa nchi nyingine hutolewa na wataalam kwa kujua suala likienda mahakamani ni Dr tu anayeweza kutetea uchunguzi

Haya ni mambo yanayoelezwa na wataalam na ni magumu sana mbele ya sheria.

Kauli za kamanda mbele ya sheria zitamkwaza. Hivi akiulizwa aeleze patient history, Cardiac anatomy and physiology and pathology of heart failure ataeleza nini?

Akiulizwa Forensic ya kifo hadi kutoa conclusion ya heart failure, ataeleza nini?

Si suala a kusema kufeli kwa moyo.
Heart Failure ni topic pana sana ambayo Kamanda angepaswa kukaa mbali nayo.

Kwahiyo unaweza kuona kauli za kamanda zinavyozidi kuchanganya badala ya uhalisia

kamanda anasema waandishi waende kwa right source ambazo ni Polisi
Pengine kamanda ajiulize kwanini watu wanashaka na taarifa zao

Watu kutafuta habari za mitaani ni dalili ya kupoteza imani na right source.

Pascal Mayalla
 
Mkuu JokaKuu

kuna msemo usemao '' ni bora kukaa kimya, unaweza kuongea na kuwatoa watu mashaka''

Kuna umuhimu wa viongozi kuchunga kauli zao, na si lazima waongelee kila jambo

kamanda anasema waandishi waende kwa right source ambazo ni Polisi
Pengine kamanda ajiulize kwanini watu wanashaka na taarifa zao

Watu kutafuta habari za mitaani ni dalili ya kupoteza imani na right source.

Pascal Mayalla
Mkuu Nguruvi3,
Kwanza naunga mkono hoja.
Kunapotokea kifo cha utata, taarifa ya polisi ilipaswa kuishia kwenye kuthibitisha mwili umepatikana, ukiwa amekufa na daktari amethibitisha kifo .

Baada ya hapo taarifa ya kifo kimesababishwa na nini haikupaswa kutolewa na police bali daktari, tena kwa vile mwili ulifanyiwa post mortem, hata familia walipaswa kushauriwa wasizungumzie mwili umekutwajwe (bila nguo, na majeraha, umejaaje) kabla ya forensic report ambayo familia ndio hupewa na kuwa na disclosure liberty.

Marehemu kukutwa bila nguo sio uthibitisho wa crime wala mwili kukutwa na majeraha hayo matatu kwa mujibu wa mtoto wa marehemu pia sio uthibitisho wa crime kama uchunguzi wa forensic ungethibitisha hayo majeraha ni ya nini na ya lini maana mwili umekutwa ukiwa umekaa 3 days dead body in a room, hivyo there is a chance majereha hayo yalikuwa inflicted on dead body baada ya kufariki natural death.

Kitu ambacho sijasikia kikitajwa kwenye kifo hiki ni ambacho mimi nakihisi ni kuwa huyu Marehemu alitoka Dar kwenye mkutano ule ule wa CAG Mstaafu. Ulikuwa ni mkutano wa nini, ulijadili nini, waliohudhuria mkutano ule wajitokeze waseme marehemu alichangia nini kwenye mkutano ule ili tuweze ku connect the dots kama kilikuwa ni kifo cha kawaida or else.

Kwenye uwezo wa polisi wetu na serikali yetu kufanya baadhi ya mambo, unafahamika na niliisha wahi kuuzungumza hapa

Haya mambo ya Ma RPC kutoa taarifa za urongo kwenye media na kutuona sisi wananchi wote kama ni watoto wa darasa la pili, pia niliisha wahi lizungumza humu kwa kumshauri IGP Sirro asiwaache ma RPC waropokaji kama hawa kulichafua jeshi letu safi la polisi

Hili la kifo hiki linahitaji maelezo ya ziada ili lieleweke.
Kwa vile Jamiiforums tumetajwa kwa kushutumiwa kwa uzushi, nashauri uongozi wa jf usikubali na tusikae kimya, hata kama aliyeleta taarifa hizo mwanzo ni just an ordinary member, lakini baada ya tuhuma kwa jf, ni ama huyo member awe equipped kwa kuwa linked na members humu wenye uwezo wa kufanya IJ wamuelekeze cha kufanya ili kuisafisha jf, au jf imtume member mwingine mwenye credentials za kufanya hayo makitu na ukweli ukibainika, ni kamanda Muroto kumpumzishwa tuu kwa uropokaji.

P
 
1. Aliwahi fanyakazi ofisi ya CAG

2. Anahusika katika taasisi ya Dalai Islamic center ambayo hata CAG mstaafu yupo.

3. Kabla ya kifo alikuwa safaarini kuhudhuria kwenye kikao cha tasisi yao ambacho CAG mstaafu alikuwepo ambaye naye ilisemekana alitekwa baada ya kutoka kwenye kikao hicho.
 
Kunapotokea kifo cha utata, taarifa ya polisi ilipaswa kuishia kwenye kuthibitisha mwili umepatikana, ukiwa amekufa na daktari amethibitisha kifo .
Ukitazama video Kamanda ametumia muda mwingi kueleza yasihusiana na tukio, mfano Nipashe, JF na habari za ''hapa na pale'' za ndugu kumtafuta.

Kamanda hakueleza mwili ulipatikana vipi, nani alitoa taarifa, polisi waliona nini.

Katika kifo cha namna hiyo lazima maelezo yasiache shaka ya Foul play.

Hakueleza taarifa zilifika saa ngapi na kutoka kwa nani. Na ilikuwaje ikatokea hivyo.
Baada ya hapo taarifa ya kifo kimesababishwa na nini haikupaswa kutolewa na police bali daktari, tena kwa vile mwili ulifanyiwa post mortem, hata familia walipaswa kushauriwa wasizungumzie mwili umekutwajwe (bila nguo, na majeraha, umejaaje) kabla ya forensic report ambayo familia ndio hupewa na kuwa na disclosure liberty.
Hapa kuna hoja kubwa sana.

Dr pamoja na Wanafamilia walitakiwa wasimame na Kamanda kuthibitisha taarifa.

Dr angeeleza Foresinc ilifanyika wapi na kwa Idhini ya Familia

Kamanda angeeleza tukio la kifo kwa kuhusisha maelezo ya Dr na Idhini iliyotolewa na Familia kutoa habari za Kifo

Next of Kin au mwanafamilia aliyepewa jukumu ndiye angesimama na maelezo ya Kamanda.

Kilichofanyika ni Kamanda kutoa maelezo yake akiaminisha umma ni right source.
Haiwezekani kuwa na ''right source'' bila ushahidi wa kutoshakutoka kwa Dr na Familia.
Marehemu kukutwa bila nguo sio uthibitisho wa crime wala mwili kukutwa na majeraha hayo matatu kwa mujibu wa mtoto wa marehemu pia sio uthibitisho wa crime kama uchunguzi wa forensic ungethibitisha hayo majeraha ni ya nini na ya lini maana mwili umekutwa ukiwa umekaa 3 days dead body in a room, hivyo there is a chance majereha hayo yalikuwa inflicted on dead body baada ya kufariki natural death.
Mtu pekee aliye na dhamana ya kuufahamisha umma kuhusu hayo uliyosema ni Daktari.

Yeye angeweza ku defend kila hoja kitaalamu na kwa kutumia Forensic examination.
Uwepo wa majeraha au kutokuwepo kungethibitishwa na Dr kitaalamu
Kitu ambacho sijasikia kikitajwa kwenye kifo hiki ni ambacho mimi nakihisi ni kuwa huyu Marehemu alitoka Dar
Kamanda alitaja Bus na seat number aliyokaa marehemu pamoja na mmiliki wa Bus.

Hii ni katika kuthibitisha kuwa Marehemu alisafiri kutoka Dar.

Tatizo linajitokeza Kamanda anaposema baada ya kushuka marehemu alikwenda Ofisini.
Nani alimuona akienda Ofisini?

Inaeleweka marehemu alipoteza mawasiliano na ndugu.
Je, Kamanda ana ushahidi upi unaoonyesha Marehemu akielekea Ofisini na si kwingine.
Kwenye uwezo wa polisi wetu na serikali yetu kufanya baadhi ya mambo, unafahamika
Kama kungelikuwa na private investigator, kamanda angekuwa katika wakati mgumu sana kisheria.

Kwa maelezo yake nachelea kusema cross examination ingemtia matatani sana.

Kwa mfano, amefikia conclusion ya mgonjwa kufa kwa heart failure iliyosabanisha ''circulation ya damu ..''.

Swali, maelezo hayo ni ya Daktari au ni yake?
Je, ana uhakika heart failure inazuia mzunguko wa Damu?
Je, marehemu alikuwa na heart failure au alipata heart attack?
Je, marehemu alikuwa na pre existing condition?
Je, marehemu alikuwa na maradhi mengine yanayoweza kusababisha kifo cha ghafla?
-Asthma, Kisukari n.k. kwa uchache tu wa kutaja

Kikubwa zaidi Kamanda anasema simu za marehemu zilikuwa zimezimwa.
Je simu zilimwa au zilikwisha charge?
Wakati wanazichukua zilikuwa na charge?Kamanda alionaje kwamba zimezimwa?

Halafu kamanda anachunguza simu za nini ikiwa tayari amefikia conclusion ya kifo cha heart failure. Kwa mfano, ikigundulika jambo jingine , je Kamanda atafuta kauli ya heart failure?
Haya mambo ya Ma RPC kutoa taarifa za urongo kwenye media na kutuona sisi wananchi wote kama ni watoto wa darasa la pili, pia niliisha wahi lizungumza humu kwa kumshauri IGP Sirro asiwaache ma RPC waropokaji kama hawa kulichafua jeshi letu safi la polisi
Sijui kwanini Kamanda alichukua hatu hiyo, ni dhahiri hakuwa na taarifa za kutosha.

Alichukua jukumu kukanusha bila kujua athari zake. Watanzania wa leo wana uelewa mkubwa sana. Wanaweza kutosema lakini si Wajinga. Hili limetia shaka badala ya kuondoa

Mbele ya sheria Kamanda ana wakati mgumu.
Kila sentensi aliyotoa katika cross examination itamweka pagumu

Haiwezekani atoe conclusion ya heart failure halafu aseme uchunguzi unaendelea
Tena kasema heart failure ilizuia circulation, kwa uhakika.
Hili la kifo hiki linahitaji maelezo ya ziada ili lieleweke.
Vinginevyo kitaacha maswali yasiyo na majibu na hasa kutokana na kauli za RPC ambazo kitaalam iwe Polisi au Udaktari au kijamii hazieleweki hata kidogo. Zimezidi kuvuruga badala ya kujenga.

Kwa hili kamanda ameliwekea 'hamira' maelezo yake yanatia shaka kuliko kuondoa
Kifo ni tukio linaloweza kutokea popote na wakati wowote.

Kifo kikielezwa kwa usahihi hakuna tatizo, kinapolezwa kwa namna kamanda alivyofanya, maswali ni mengi kuliko majibu.

Mh Rais Magufuli aliwahi kutoa angalizo ''Jeshi la Polisi lijisafishe''. Kwa hili nadhani kauli ya Mhe Rais inaingia bila shaka. Maelezo ya Kamanda yanaliweka jeshi mahali pasipotakiwa

tindo Mag3 JokaKuu
 
Kuna magazeti yameandika leo kuwa familia imekataa maelezo ya polisi

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa ndio Muroto anapo angukia pua. Kijana wa marehemu amekataa version ya Muroto na kusisitiza kuwa mwili wa Mzee wake ulikutwa hauna nguo na una dalili ya majeraha. Labda kama nae amezushiwa kusema hivyo, vinginevyo taarifa ya polisi ina walakini na JF ina msingi wa kuleta taarifa iliyoletwa.

Nafikiri Jeshi letu la Polisi kwenye uwazi na ukweli (in Mkapa's voice) wana matatizo makubwa hadi wanafungua kesi ambazo hazipo, wanatoa reporti ambazo si sawa.
 
Back
Top Bottom