Juzi nikiwa kwenye shughuli zangu hapo Arusha, nilipatwa na mshangao wa mwaka kwa jinsi tapeli anayetafutwa na dola akirandaranda mtaani bila kukamatwa. Issue yenyewe ilikuwa hivi. Kuna mtalii moja raia wa Marekani alifika Arusha akitokea Zanzibar na akafikia hoteli niliyokwepo karibu na hospitali ya Siriani. Alipokelewa KIA na jamaa aliyewasiliana naye kuwa anatoka kampuni ya Green African Tours Tanzania na kumleta hoteli. Mtalii alimlipa jamaa $1,650 kama gharama ya booking ya hoteli na kumpeleka camping kwa siku 3. Mtalii akagikishwa hoteli na kuambiwa wanafuatwa wenzake kama wanne ili waje walale pale hotelini kwa kuwa ameshawafanyia booking ili kesho yake waondoke pamoja kwenda camping. Jamaa hakurudi na baada ya mtalii kuuliza kama kuna booking ya wageni wengine 4 iliyowekwa na jamaa akajibiwa hakuna.Hapo ndo mtalii akajua amepigwa, namba ya simu za kwenye business card hazikupatikana. Tukamshauri mtalii aripoti polisi. Alipofika pale akakuta picha ya jamaa WANTED. Nikajiuliza inawezekanaje mtu WANTED anaweza kujivinjari kwenda KIA kumpokea mmgeni kumleta mjini na kuendelea ma mishemishe zake bila hata kukamatwa.