Rostam: Umasikini siyo jambo la kujionea fahari

Rostam: Umasikini siyo jambo la kujionea fahari

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,730
Reaction score
4,924
Katika mahojiano maridhawa ya Mwanahabari nguli Tido Muhando wa TBC na Mfanyabiashara "guru" Rostam Abdulrasul Aziz pamoja na kuongea mengi juu ya biashara na siasa, Watanzania tumeshauriwa kutokuuona Umasikini kama jambo la fahari au la kawaida.

Watanzania wengi imesemekana tunauona Umasikini kama hali ya kawaida kabisa na mtu akifanikiwa kutoka kwenye lindi la Umasikini tunatamani kumvuta arudi nyuma tena.

Kuhusu makaa ya mawe: Mfanyabiashara guru amedai kuwa hisa alizonunua hakuuziwa na Serikali ila alizinunua kutoka kwenye kampuni ya nje iliyokuwa inamulikiwa na Mzungu (INTRA ENERGY CORPORATION) ya Australia tena kwa kuzingatia hesabu za soko la hisa za Australia. Katika eneo hili aliongezea kusema kuwa kuna migodi zaidi ya 16 inayomilikiwa na kampuni mbalimbali na yeye bado hajaanza kuvuna makaa hayo katika eneo lake, anakamilisha baadhi ya vitu

Kuhusu Mwadui: Mfanya biashara huyu alisema kuwa hisa alizozinunua zimezingatia ithibati ya soko la hisa la "London" Uingereza London Stock Exchange (LSE) kwa sababu alizinunua kutoka kwenye kampuni ya Uingereza.

Tuje hapa, ule uvumi kuwa Serikali ndiyo iliyomuuzia kwa bei chee kwa maelezo ya Guru huyo wa biashara ni dhahiri unakwenda kukosa mizizi thabiti na kubaki kama aina nyingine ya vumi za kurudishana nyuma.
 
Kama umasikini sio jambo la kujivunia kwanini anawaibia Watanganyika na kuwatia umasikini?

Yaani anatuibia halafu anatucheka kwamba kwanini tumekuwa masikini?

Rostam tunataka migodi yetu na mali zetu, tutakutimua urudi kwenyu huko uturuki sijui utuachie Tanganyika yetu!

Kwanini hutaki kwenda kwenu? unang'ang'ania Tanzania ni yako? ni kwenu?

Rudi kwenu, hatukutakii. Ondokaaa!
 
Je, amezitaja hizo kampuni kwa majina? Pili, hizo kampuni za Uingereza na Australia ni za wazungu au wabongo? Maana kuna wabongo wanasajili makampuni huko nje kisha zinakuja kutubamiza hapa nyumbani.
 
Je, amezitaja hizo kampuni kwa majina? Pili, hizo kampuni za Uingereza na Australia ni za wazungu au wabongo? Maana kuna wabongo wanasajili makampuni huko nje kisha zinakuja kutubamiza hapa nyumbani.
Naam, amezitaja Mkuu
 
Katika mahojiano maridhawa ya Mwanahabari nguli Tido Muhando wa TBC na Mfanyabiashara "guru" Rostam Abdulaziz pamoja na kuongea mengi juu ya biashara na siasa, Watanzania tumeshauriwa kutokuuona Umasikini kama jambo la fahari au la kawaida.

Watanzania wengi imesemekana tunauona Umasikini kama hali ya kawaida kabisa na mtu akifanikiwa kutoka kwenye lindi la Umasikini tunatamani kumvuta arudi nyuma tena.

Kuhusu makaa ya mawe: Mfanyabiashara guru amedai kuwa hisa alizonunua hakuuziwa na Serikali ila alizinunua kutoka kwenye kampuni ya nje ya Australia tena kwa kuzingatia hesabu za soko la hisa za Australia. Katika eneo hili aliongezea kusema kuwa kuna migodi zaidi ya 16 inayomilikiwa na kampuni mbalimbali na yeye bado hajaanza kuvuna makaa hayo katika eneo lake, anakamilisha baadhi ya vitu

Kuhusu Mwadui: Mfanya biashara huyu alisema kuwa hisa alizozinunua zimezingatia ithibati ya soko la hisa la "London" Uingereza London Stock Exchange (LSE) kwa sababu alizinunua kutoka kwenye kampuni ya Uingereza.

Tuje hapa, ule uvumi kuwa Serikali ndiyo iliyomuuzia kwa bei chee kwa maelezo ya Guru hyo wa biashara ni dhahiri unakwenda kukosa mizizi thabiti na kubaki kama aina nyingine ya vumi za kurudishana nyuma.
Anaitwa rostam abdulrasul aziz,ana bachelor degree in economics,exeter university,anaongea kiswahili kizuri,ni mtu anayeifafamu nchi yake vyema.
 
Kama umasikini sio jambo la kujivunia kwanini anawaibia Watanganyika na kuwatia umasikini?

Yaani anatuibia halafu anatucheka kwamba kwanini tumekuwa masikini?

Rostam tunataka migodi yetu na mali zetu, tutakutimua urudi kwenyu huko uturuki sijui utuachie Tanganyika yetu!

Kwanini hutaki kwenda kwenu? unang'ang'ania Tanzania ni yako? ni kwenu?

Rudi kwenu, hatukutakii. Ondokaaa!
Na nyinyi kwanini mtu anawaibia halafu hamumchukulii hatua yoyote ?
 
Kama umasikini sio jambo la kujivunia kwanini anawaibia Watanganyika na kuwatia umasikini?

Yaani anatuibia halafu anatucheka kwamba kwanini tumekuwa masikini?

Rostam tunataka migodi yetu na mali zetu, tutakutimua urudi kwenyu huko uturuki sijui utuachie Tanganyika yetu!

Kwanini hutaki kwenda kwenu? unang'ang'ania Tanzania ni yako? ni kwenu?

Rudi kwenu, hatukutakii. Ondokaaa!
Naunga mkono hoja
 
Ana hoja nyingi nzuri kwa mustakabali wa ukuaji wa biashara nchina na uwekezaji wa ndani. Kusikiliza kila upande ni muhimu kuliko kujifungia au kujichagulia upande wa kusikiliza.
 
Katika mahojiano maridhawa ya Mwanahabari nguli Tido Muhando wa TBC na Mfanyabiashara "guru" Rostam Abdulrasul Aziz pamoja na kuongea mengi juu ya biashara na siasa, Watanzania tumeshauriwa kutokuuona Umasikini kama jambo la fahari au la kawaida.

Watanzania wengi imesemekana tunauona Umasikini kama hali ya kawaida kabisa na mtu akifanikiwa kutoka kwenye lindi la Umasikini tunatamani kumvuta arudi nyuma tena.

Kuhusu makaa ya mawe: Mfanyabiashara guru amedai kuwa hisa alizonunua hakuuziwa na Serikali ila alizinunua kutoka kwenye kampuni ya nje ya Australia tena kwa kuzingatia hesabu za soko la hisa za Australia. Katika eneo hili aliongezea kusema kuwa kuna migodi zaidi ya 16 inayomilikiwa na kampuni mbalimbali na yeye bado hajaanza kuvuna makaa hayo katika eneo lake, anakamilisha baadhi ya vitu

Kuhusu Mwadui: Mfanya biashara huyu alisema kuwa hisa alizozinunua zimezingatia ithibati ya soko la hisa la "London" Uingereza London Stock Exchange (LSE) kwa sababu alizinunua kutoka kwenye kampuni ya Uingereza.

Tuje hapa, ule uvumi kuwa Serikali ndiyo iliyomuuzia kwa bei chee kwa maelezo ya Guru hyo wa biashara ni dhahiri unakwenda kukosa mizizi thabiti na kubaki kama aina nyingine ya vumi za kurudishana nyuma.
takataka
 
Back
Top Bottom