Swali zuri kabisa! Nani atamhoji? Kwenye kampeni za Kikwete za mwaka 2005 yeye ndio alikuwa mweka hazina, pesa zote zilizokuwa zinachotwa serikalini zilikuwa zinaingizwa kwenye account zake kwanza kabla ya kuzipeleka kwenye kampeni, wakati huo huo Edward Lowassa yeye ndio alikuwa mwenyekiti wa kamati. Ki ufupi wao ndio waliu-cordinate ule mtandao uliomwingizwa Kikwete madarakani na mbali na hizo fedha za wizi walitoa pia hela zao za mfukoni kuhakikisha ****** anaingia Magogoni. Wengi wa Mawaziri, wabunge na wakuu wa mikoa na wilaya wametokana na mtandao ambao yeye (RA) na Lowassa waliu-cordinate, sasa katika mazingira hayo mkuu unategemea kuna wa kumgusa? Amefanikiwa pia kupenyeza watu wake kwenye system kwa mfano Salva Rweyemam, Mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu , Waziri William Ngeleja na January Makamba ni product za Rostam Aziz. Ku-deal na mtu wa namna hii ni kazi sana hasa ukizingatia kwamba ni kweli wao ndio walimwingiza Kikwete madarakani tena kwa wizi wa pesa za walipa kodi wa Tanzania. Jamaa mtandao wake serikalini , kwenye chama na nje ya hapo unatisha na ana nguvu kubwa ya pesa ndio maana unaona hawamhoji hata baada ya kuandikwa sana na magazeti. Mtandao wa Edward Lowassa ni mkubwa zaidi, sasa ukiwa unganisha pamoja wana nguvu kubwa! Kauli kama za kina Nape Nnauye kwamba hakuna mtu mwenye umaarufu zaidi ya chama au zile za baadhi ya watu kusema Rais anaweza kuwashughulikia ni za kujifariji na kujidanganya tumeshuhudia South Africa, Thabo Mbeki akiwa Rais akishindwa vibaya na Jacob Zuma kwenye uchaguzi wa mwenyekiti wa ANC na hatimaye kupoteza urais. RA, EL na Jakaya Mrisho Kikwete wote ni mafisadi ambao ni nguvu ya umma tu inaweza kuwashughulikia na si vinginevyo!!