Mmiliki wa gazeti la Rai; Rostam Aziz, ambaye ndiye wengi tunaamini ni mwakilishi wa JK kwenye kashfa ya DOWANS ambayo isipovaliwa njuga italigharimu taifa zaidi ya bilioni 100 ametumia nafasi yake tajwa visivyo alipotumia kumchafua Dr. Slaa na kumwita ni hatari kwa taifa wakati sisi tunaamini yeye Rostam Aziz ndiye hatari kwa usalama wa taifa hili.................................kwa kutuingiza mkenge ili tulipe ufisadi na hivyo kukwamisha jitihada za taifa hili kujitoa kwenye lindi la umasikini............
Aidha Rostam Aziz alidai ya kuwa Dr. Slaa alimzushia kushiriki kikao cha mwanza kilichopanga uchakachuaji wa kura wakati yeye alikuwa safarini Afrika ya Kusini safari ambayo hadi leo Rostam Aziz kashindwa kututhibitishia kuwa kwenye tarehe hizo kweli hakuwa nchini baada ya hata kushindwa kuonyesha kwenye pasi yake ya kusafiria mihuri na viza ya kuingia na kutoka kule Afrika ya Kusini.
Rostam Aziz pia anadai ya kuwa kwa mara nyingine Dr. Slaa amemzushia safari ya kwenda Marekani kwa ajili ya kupanga mipango ya kulipora Taifa hili mabilioni ya fedha kupitia DOWANS huku akishirikiana kwa karibu na swahiba wake JK safari ambayo Rostam Aziz anadai hakwenda..........kwani kwenye tarehe hizo alikuwa humu humu nchini..........Lakini kinyume na awali ambapo Rostam Aziz alionyesha baadhi ya ushahidi ambao uliongeza utata juu ya utetezi wake safari hii hakutoa ushahidi wowote ule kuthibitisha madai yake katika mazingira yanayothibitisha zaidi ya kuwa pengine hata safari hii anasema uongo tu...............Huenda safari hiyo ya marekani alikwenda na sasa anajishauashaua tu..............kujaribu kufunika ukweli.................Upo ushahidi ambao ulitolewa na Tanesco kwa msuluhishi ya kuwa Rostam Aziz ni mwasisi wa kashfa ya DOWANS.......................kama ushahidi huu uliotolewa na tanesco kwenye uamuzi wa DOWANS unavyojieleza..........