Njemba Soro.
JF-Expert Member
- Oct 5, 2013
- 3,246
- 5,757
alikuwa kichaa bila shaka na nyie mkamsifia sanaaaaa...... akajiona yeye ni bora sana kumbe dishi lilikuwa limeyumba........ AMEJIUA.
Eti jaman? Hata kugegeda tusigegede?Alikuta tatizo gani kwa mabrother hadi akaamua kurudi nyumbani.??
Je Ni lazima binadamu tusali kila sekunde(muda wote) maishani mwetu.?
Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaha mm nimeishia kucheka tuSIMANZI
Godwin Frimin Massawe umeondoka katika Dunia hii
lakini Tutakukumbuka na Tutakuombea.Mwanangu
Godwin naamini Upo kwa Mungu unatuombea zaidi
kwa jinsi kifo chako kilivyotokea. Sijawahi kusikia kifo
cha aina hii zaidi ya kusoma kwenye vitabu vya maisha ya watakatifu. Godiwin alihitimu Kisale secondary 2012,shule ipo mkoani Kilimanjaro wilaya ya Rombo.Alipenda kuishi maisha ya sala,kusoma bibilia kila mara na alifika mahali akasema hakuna anachokitafuta duniani zaidi ya kuishi maisha yatakayomuongoza kufika mbinguni kwa kusoma na kufuata maandiko matakatifu ya bibilia.
Alienda kufanya kazi na Wilvic labour solution kama
data entry. Lakin siku moja aliamua kuacha kazi
akarudi nyumbani. Alipoulizwa kwa nn alisema
"anafanya kazi masaa mengii mnoo mpaka anakosa muda wa kwenda kwenye ibada,kusoma bibilia na
kufanya tafakar" aliendelea kusema "kuliko niendelee na kazi ambayo inaniweka mbali na Mungu halafu nikafa naiacha bora niache nikamtumikie Mungu" Akamwambia baba yake nataka kwenda kujiunga na mabrother niwe nasali mda wote. Akapelekwa.Lakini siku moja akarudi nyumban.
Alipoulizwa akasema kule nilifikiri ni sehemu ya kusali, kuimba na kusoma bibilia mda wote kumbe hapana. Bora nirudi nifanye mda wangu wote wa sala. Siku ya jumapili alienda kanisani na hakurudi nyumbani Alitafutwa kila mahali hakupatkana,Taarifa zilipelekwa mpaka kanisan na kituo cha polisi, Ni mwezi sasa umepita.
Jana taarifa za wazee wanaopasua mbao katikati ya msitu zikasema kuna mtu ameonekana alifariki mda
mrefu na ana bibilia. Taarifa zilipotufikia basi baba
yake anaondoka na polisi leo kuelekea msituni
wakiongozwa na wale wazee wapasua mbao.
Msitu upo Kule katangara,mwisho wa watu kuishi
unaingia ndani mwendo wa masaa manne. Kuna
barid kali sana na wanyama wakali pia. Ndipo
wakamkuta Godiwin amepiga magoti kwenye
gogo, akiwa na Rozary yake shingoni na biblia ipo
chini imefunguliwa kitabu cha SIRA. Godiwin ameshaoza amebaki mifupa tuu na hatoi harufu yoyote. Amevalia nguo zake vilevile. Godiwin alienda msituni kufunga na kusali mpaka akafariki.
Polisi na baba yake wakamchukua na kumpeleka katika chumba cha kuhifadhia maiti kule Huruma hospital.
Taratibu za mazishi zinaendelea.Godiwin aliamua kujitoa kutuombea na kusali na Mungu aliamua tunapomtafuta tusimkute mpaka mapenz yake yatimie.Basi ni majonzi kwa familia na wazazi na wahitimu na wanafunzi wa kisale secondary, wananchi wote wa mashati rombo,kanisa Katoliki na watanzania wote kwa ujumla.
Tumuombee Godwin wakati huu akiwa na malaika na watakatifu mbinguni makao ya kusali na kumsifu
Mungu milele yote.
C&P
KajiuaDuh! Mambo gani haya ya kusali hadi unafia porini. Bibble inasemaje kuhusu hili?
Sent using Jamii Forums mobile app
sio unahis..ni hivyo alikua na shida ya kisaisokolojia..apumzike pemaMMhh nahisi Godwin alikua na tatizo....
(kama nmekosea Mungu anisamehe)
Hapa kuna shida kidogo kwenye simulizi, mtu kaoza,kabaki mifupa,lakini, kashika kitabu kimefunuliwa na ana nguo zake.
Au ndo miujiza hiyo?
Kuna watu wao pesa na maisha si Mali kitu kwao, Kuna watu ambao wameyadharau maisha haya, na ukitafakari sana utagundua kuwa maisha ni utumwa na kuishi ni sawa na kujirisha upepo, lakini Kuna wengine ambao fikra zako na furaha zao wameziweka katika pesa, hawa huwa wanapata tabu sana, kwani pesa ni namba na namba hazina mwisho, nenda Godwin wajinga watakubeza kwa kuwa hawaoni na hawatoweza kujua chochote, kwani moyo wa mtu ni kiza kinene, HERI KUFA KULIKO KUISHI
Sent using Jamii Forums mobile app
Una maanisha nini hapa...???hukumkiri Yesu kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha yako basi ujue ulipoteza muda tu ni heri ungekuwa mzinzi tuui
😂😂😂😂😂😂 Sihami Bongo mm aisee khaaa eti wakamatwe kama wana vibali..jaman nimechek sana..hii ndo Tanzania zaidi ya uijuavyo..!hapa kazi tu😂😂Jana taarifa za wazee wanaopasua mbao katikati ya msitu zikasema kuna mtu ameonekana alifariki mda
mrefu na ana bibilia. Taarifa zilipotufikia basi baba
yake anaondoka na polisi leo kuelekea msituni
wakiongozwa na wale wazee wapasua mbao.
Msitu upo Kule katangara,mwisho wa watu kuishi
unaingia ndani mwendo wa masaa manne. Kuna
barid kali sana na wanyama wakali pia. Ndipo
wakamkuta Godiwin amepiga magoti kwenye
gogo, akiwa na Rozary yake shingoni na biblia ipo
chini imefunguliwa kitabu cha SIRA.
Kwanza hao wazee wakamatwe na waoneshe vibali vya kupasua mbao katikati ya msitu
Pili,hapo nilipokopi pamenichanganya ninavyojua hiyo misitu haikauki mvua au umande na upepo wa hapa na pale ila ya Mungu ni mengi.
M.H.S.R.I.P Godwin
Upo so smart. Marry me before u end up with someone stupidHiyo sio sifa nzuri na wala sio mfano wa kuigwa, marehemu alikua na matatizo ya akili, alistahili atibiwe awe mwanadamu wa kawaida... Religious extremist wapo wa aina nyingi, wapo wanaojilipua mabomu, wapo wanaopinga elimu dunia, wapo wanaona kusali masaa 24 ndio njia sahihi ya kuishi
Huyo alikuwa na matatizo ya akili.Yawezrkana utotoni aliwahi maisha ya mateso makubwa kiasi kuwa tamanio lake kubwa ni kukaa na Mungu tu sio wanadamu waliompa mateso makali waweza kuwa wazazi au aliishi maisha magumu mno kutokana na umaskini mkubwa wa kifamilia.Hiyo hali huwapata wengi hasa wanaopitia mateso makali ya maisha hupenda tu wakae wakisali tu ukimwambia inatakiwa Kazi na Sala haelewi anataka asali tu.Ndio maana hata alippopelekwa kanisani kwa ma brother alishinfikana hakujua kuwa kule ni kazi na Sala sio Sala tu.Ushauri.kila mzazi ajitahidi kutompa mateso ya Aina yeyote ya know ili kiakili au kisaikolojia mtoto hasa akiwa mdogo yaweza pelekea shida mbele