Rolls-Royce yaunda Ndege inayotumia Umeme

Rolls-Royce yaunda Ndege inayotumia Umeme

Kasomi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
11,027
Reaction score
20,411
35ef02ccbaf7cb5aca8c4fb5c4ebf1a5~2.jpg
Kampuni ya kutengeneza injini za anga na magari ya Uingereza Rolls-Royce imesema imeunda ndege yenye kasi zaidi duniani inayotumia umeme badala ya mafuta na imepewa jina la Spirit of Innovation, spidi yake ya mwisho inazimaliza kilometa 623 kwa saa.

"Kufuatia mpango wa dunia dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi na kulinda mazingira, hii ni hatua nyingine muhimu ambayo itasaidia kufanya 'jet zero' kuwa ukweli na kuunga mkono matamanio yetu ya kuleta mafanikio ya teknolojia ambayo jamii inahitaji kupunguza uchafuzi wa anga, ardhi na bahari”

“Serikali inajivunia kuunga mkono miradi kama hii ili kuongeza uwekezaji wa kibinafsi unaohitajika kufungua ndege safi ambazo zitaruhusu Watu kuruka kama wanavyofanya sasa lakini kwa njia ambayo inapunguza uchafuzi" amesema
Katibu wa biashara wa Uingereza Kwasi Kwarteng.
 
Sawa
Hapa Tanzania Tunaaibika Na Mgawo Huku Tuna

  1. Nyumba Ya Mungu
  2. Hale Pangani
  3. Mtera
  4. Kidato Morogoro
  5. Kihansi Morogoro
  6. Mwalimu Nyerere *
 
Sawa
Hapa Tanzania Tunaabika Na Mgawo Huku Tuna

  1. Nyumba Ya Mungu
  2. Hale Pangani
  3. Mtera
  4. Kidato Morogoro
  5. Kihansi Morogoro
  6. Mwalimu Nyerere *
Hii ndio Bongo
 
Sawa
Hapa Tanzania Tunaabika Na Mgawo Huku Tuna

  1. Nyumba Ya Mungu
  2. Hale Pangani
  3. Mtera
  4. Kidato Morogoro
  5. Kihansi Morogoro
  6. Mwalimu Nyerere *
Wajanja wamerudi
Yule mzee wetu aliyeitwa mshamba, aliyejaribu kuwadhibiti wajanja wasituibie sana tukamuita mshamba mara katoka kijijini.
Mungu akampumzisha sasa tunajuta jijini kila kitu mgao wajanja wanauza mafuta, wajanja wanaingia mikataba, wanapiga hela.

Wajanja hao hao wanasema yule mzee mshamba ndiye amesababisha umeme na maji kuwa mgao, mara kiangazi lakini wanasahau yule mzee alitawala 5yrs na jua lilikuwa linawaka na maji wala umeme haukuwa wa mgao.

Tunyoosheni wajanja wa mjini

Mzee wetu uliyeitwa mshamba Mungu akupe pumziko la milele, wenye kuelewa tunakuombea kwa Mungu. Pamoja na mapungufu yako ulijitahidi
 
Back
Top Bottom