Roho yangu nimemkabidhi MUNGU - Nape

Nipe tano

Senior Member
Jun 16, 2011
100
27
Nimesoma gazeti la JAMBO Leo limemnukuu Nape AKISEMA Roho yake ameikabidhi kwa MUNGU katika wakati huu MGUMU WA vita dhidi ya mapapa CCM
 
keshatolewa kwenye reli huyu.. lowasa yeye roho na mwili kavikabidhi zamani sana.. si mlimuona kule nigeria?
 
Thursday, 04 August 2011 19:55 newsroom
https://www.jamiiforums.com/index.p...hdGlkPTc3OnBlcnNvbmFsLXRlY2gmSXRlbWlkPTE3Ng==https://www.jamiiforums.com/index.p...hdGlkPTc3OnBlcnNvbmFsLXRlY2gmSXRlbWlkPTE3Ng==https://www.jamiiforums.com/index.p...t=default&page=&option=com_content&Itemid=176https://www.jamiiforums.com/index.p...t=default&page=&option=com_content&Itemid=176https://www.jamiiforums.com/index.p...nchi&format=pdf&option=com_content&Itemid=176https://www.jamiiforums.com/index.p...nchi&format=pdf&option=com_content&Itemid=176

NA BASHIR NKOROMO
HATUA ya kuwataka watuhumiwa wa ufisadi wapime na kuchukua uamuzi wa kuondoka katika vikao vya maamuzi ya CCM, kutakifanya Chama kuaminiwa zaidi na wananchi. Hayo yalisemwa jana mjini Dar es Salaam na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alipokuwa akizungumza na viongozi wa Kampuni ya Africa Media Group, inayomiliki vyombo kadhaa vya habari, kikiwemo kituo cha Televisheni cha Chanel Ten. Alisema, maamuzi ya CCM yanalenga zaidi maslahi ya nchi na wananchi wake na si maslahi ya mtu mmoja mmoja. Alisema, kutokana na misingi iliyowekwa na waasisi wake, CCM bado ina kila sababu ya kuendelea kuongoza nchi kwa kutekeleza yale yote ambayo yamo ndani ya Ilani ya Chama hicho.

Nape alisema, mazingira yaliyokuwapo ndani ya Chama hivi sasa, yamekilazimu kufanya mabadiliko ili kukabiliana na changamoto mbali mbali. Alisema, mabadiliko hayo ambayo yalipitisha maamuzi zaidi ya 20, ni miongoni mwa mengi ambayo CCM imekuwa ikiyafanya tangu wakati wa TANU na hivyo watu wasichukue muda mwingi kuyashangaa bali washiriki katika kuyaenzi kwa kufanya utekelezaji. Hata hivyo, alikiri kuwa mabadiliko hayo yanaweza kuwaathiri baadhi ya watu, lakini hilo halitakuwa jambo la ajabu kwa sababu mabadiliko yoyote yanapotokea, wapo watakaoathirika katika kipindi kifupi, lakini wakafaidika kwa muda mrefu. "Siwezi kusema hakuna watakaoathiriwa na mabadiliko haya, wale waliokuwa wananufaika na mfumo holela uliokuwa unawapa mwanya kufanya mambo kwa manufaa yao hata kama yanaathiri taifa, lazima wataguna na kujaribu kufanya sarakasi za kupinga mabadiliko haya," alisema Nape. Alisema kutokana na sababu hizo, ndio maana zimetokea changamoto za hapa na pale katika mapokeo ya mabadiliko yaliyofanywa na CCM, ikiwemo baadhi kujaribu kujitokeza na kusema hadharani kwamba mabadiliko haya hayana maana.

Nape aliwataka Watanzania na hasa vyombo vya habari, kuacha kuyafanyia kazi maneno ya mitaani, hasa yanayokihusu Chama cha Mapinduzi. Alisema CCM inaendeshwa kwa vikao na hata wanahabari wanapaswa kuripoti kile kilichozungumzwa ndani ya vikao.

Alisema milango ipo wazi kwa kila mwenye hoja mbadala inayohusu maamuzi yanayofanyika hivi sasa. Ziara hiyo ya kutembelea vyombo vya habari, ni mwendelezo wa ziara za Mwenezi huyo alizoanza kuzifanya mwezi uliopita.
 
Da! Mkuu Achebe mbona short cut sana kiongozi??
Sijui kwa nini hakuleta habari kamili soma hii kutoka Raia Mwema.
Kikwete aipa nguvu Sekretariati mpya
Katika kikao hicho cha CC, Rais Kikwete alirudia kuipa nguvu Sekretarieti ya chama hicho kwa kuwapinga moja kwa moja wanaoibeza wakiwamo baadhi ya wenyeviti wa mikoa ambao wamekuwa wakisema inapotosha uamuzi wa NEC.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari, Rais Kikwete alitamka ndani ya kikao cha Kamati Kuu akisema; "there are some stupid guys (wajinga fulani)," wanaosema Sekretariati hiyo inakivuruga chama kwa namna wanavyosimamia utekelezaji wa uamuzi wa NEC; hasa wa kujivua gamba.
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa moja kwa moja kuwa ni kuwapuuza baadhi ya viongozi wanaodai kuwa Sekretariati imekuwa ikisimamia uamuzi wa kujivua gamba, kinyume cha matakwa ya Halmashauri Kuu, Kamati Kuu imeipongeza Sekretariati hiyo.
Hatua hiyo inatajwa kuwa ni pigo kwa baadhi ya viongozi wa sasa wa chama hicho, wakiwamo wanaopaswa kujiuzulu nafasi za uongozi katika chama hicho - Chenge na Lowassa; huku Rostam naye akijiuzulu kwa kulalamikia Sekretariati hiyo akisema inaendesha siasa uchwara.
Wengine katika orodha ya kuishambulia Sekretariati hiyo na hasa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ni John Guninita, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM-Dar es Salaam na Hamisi Mgeja Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, wote wakitajwa kuwa karibu na viongozi wanaotakiwa kujiuzulu.
Taarifa kutoka ndani ya kikao cha Kamati Kuu zinaeleza kuwa Rais Kikwete ni kati ya viongozi walioweka wazi msimamo wao kuhusu mwenendo wa Sekretariati, akimtaja kwa jina Nape Nnauye.
 
Mpatieni Nape nakala za Mwananchi na The Citizen 4/8/11, ataona picha halisii. na kwa taarifa tu ni kwamba wana-ccm wanamuunga mkono jamaa wa pande ingine!
 
Kila muwamba ngoma........Too little too late!
 
tatizo hawa magamba maneno mengi utendaji hamna.Wote hawana meno
 
nn anaweza kuhamia upinzani mda wowote iwapo ataendelea kunyimwa ushirikiano.mia
 
Nimesoma gazeti la JAMBO Leo limemnukuu Nape AKISEMA Roho yake ameikabidhi kwa MUNGU katika wakati huu MGUMU WA vita dhidi ya mapapa CCM
We mungu kaona naye wapi? mpaka amkabidhi ROHO YAKE.?
Tuseme kaisha kufa sasa au yamaanisha nini???!!
AU yu mahututi. ??,Je anaumwa.?
Lakini yeye sianataka kuona pepeo kwa kukemea dhambi.?
Je ni msafi kiasi kile.??

Mpaka awanyoshee kidole na kuwapiga mawe wenzake
?
 
Gamba zuri huvuka bila kuchanika........hili la CCM lilichanika kabla ya kuvuka.......na halijavuka bado
 
Back
Top Bottom