Robert Lewandowski ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa FIFA

Kichwa Kichafu

JF-Expert Member
Apr 13, 2017
44,604
188,819
Habari,
Robert Lewandowski amefungua mwaka vyema kwa kuendelea kushinda tuzo yake ya mchezaji bora wa mwaka zinazotokewa na FIFA ambapo alikuwa akichuana na washiriki wenzake ambao ni Lionel Messi na Mohammed Salah.

Lewandowski ameshinda tuzo ya FIFA ya mchezaji bora wa kiume kwa mwaka wa pili mfululizo sasa ambapo sherehe hizi zimefanyika makao makuu ya FIFA huko Zurich siku ya jumatatu leo 17.01.2022.

Mshambuliaji huyu wa Bayern Munich amewapiku waliokuwa wanawania tuzo hiyo ambao ni Lionel Messi na Mohammed Salah kama ilivyokuwa mwaka wa mwisho alivyochukua tuzo ya mchezaji bora wa FIFA December 2020.

Lewandowski alifunga magoli 58 katika mechi 47 kwenye mashindano yote mwaka 2021 ambapo kuliambatana na kuvunja rekodi mbili zilikuwa zikishikiliwa na mshambuliaji legendary wa kijerumani Gerd Muller. Ambazo ni kufunga magoli 41 ndani ya msimu mmoja wa Bundesliga katika timu ya Bayern Munich na magoli 43 ndani ya Bundesliga katika kalenda ya mwaka.

Hadi Sasa amekwisha funga magoli 34 ndani ya mechi 27 kwenye msimu huu, ukijumlisha magoli 9 kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya makundi.

Nawasilisha Mzee Mkoloni.

1642488950767.png

Cc: Kichwa Kichafu.
 
Ata Mess anajua Kuna tuzo mbili au tatu hakustahili Ila hakua na jinsi ya kuzikataa, kwakua mess ni muungwana nadhani kunasiku atatoka hadharani na kulisemea Hilo.
 
Hata ile ya ballon d'or alistahili apewe huyu na wala siyo yule
Hakika sema hawa jamaa wanatoa tuzo pia ku-boost umaarufu wa tuzo zao siwezi kusema haya makosa ya kuwadhurumu baadhi ya wachezaji si jambo la kupangwa.

Ugawaji wa tuzo uma-base sana kwenye biashara zaidi ya watu wanaostaili kushinda tuzo hizo.

Jana pia wamempa CR7 tuzo maalumu ya mchezaji mwenye magoli mechi mechi za kimataifa ambayo kabla wala kwa list haikuwepo.

Hizi ni siasa za mpira na biashara yake kuongeza umaarufu wa tuzo.
 
Ata Mess anajua Kuna tuzo mbili au tatu hakustahili Ila hakua na jinsi ya kuzikataa, kwakua mess ni muungwana nadhani kunasiku atatoka hadharani na kulisemea Hilo.
Hahahaha Hapo Kwa Messi Kutoka Hadharani Sahau Kutokea.
 
Ballon d'or 2019/20 2020/21 hata hii ya 2021/22 mpaka sasa yeye ndio ananafasi kubwa ya kuibeba jamaa wanamfanyia hujuma za waziwazi.
Ngoja wampooze na hizo za fifa
Najiuliza Kwa Nini Africa Na Sisi Tusiwadthamini Wachezaji Wetu Wanaofanya Vizuri Kwa Kuwapa Tuzo Nyingi Kama Wanavyofanya Huko.

Pamoja Na Biashara Tukiweka Pengeni Hakina Messi & Ronaldo Kuna Tuzo Zinapewa Ukiangalia Vizuri Ni Kama Kuwapa Promo Na Appreciation.
 
Hakika sema hawa jamaa wanatoa tuzo pia ku-boost umaarufu wa tuzo zao siwezi kusema haya makosa ya kuwadhurumu baadhi ya wachezaji si jambo la kupangwa.

Ugawaji wa tuzo uma-base sana kwenye biashara zaidi ya watu wanaostaili kushinda tuzo hizo.

Jana pia wamempa CR7 tuzo maalumu ya mchezaji mwenye magoli mechi mechi za kimataifa ambayo kabla wala kwa list haikuwepo.

Hizi ni siasa za mpira na biashara yake kuongeza umaarufu wa tuzo.

Mchezo wa mpira umevamiwa na Biashara.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom