Dotto C. Rangimoto
JF-Expert Member
- Nov 22, 2012
- 1,985
- 1,286
Kwa kifupi shairi ni matokeo ya shairi la Abbas Lutumbo alilopost ter 1 ya mwez huu ktk wall yke.
Haku muumba kilema, aka mkosesha mwendo,
Huyo ni Mola Karima, mfalme wa vishindo,
Usijifanye yatima, fungua yako mafundo,
Rauka fanya hima, nyumbani haliji windo.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Mwenye kupewa ukwasi, katu hakupendelewa,
Masikini hasiasi, wallahi hakuonewa,
Mitihani ya Qudusi, mola wa majaliwa,
Alichopewa pungusi, chaa hakuruzukiwa.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Rauka wahi kazini, upate yako ijara,
Changamoto za windoni, na zikufanye imara,
Toa simanzi moyoni, tena sifanye harara,
Bosi avimbe kichwani, tuli sipoteze dira.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Ukiri Lutumbo kiri, hebu acha kusonona,
Wazoee waajiri, kama wataka kunona,
Shetwani asikughuri, ingawa dhiki waona,
Subiri kakasubiri, lisilo mwisho hakuna.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Niseme nawaajiri, wenye pembe vichwani,
Wana kifanya kiburi, hawana heri moyoni,
Mbaya hawana habari, shida haina maskani,
Tabu hainatajiri, wala si ya masikini.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Ewe ndugu mwajiriwa, sema na wako moyo,
Jukumu ulilopewa, litimize pasi choyo,
Ridhika na unachopewa, huno wangu mgogoyo,
Rushwa katusi ngekewa, yataka ushinda moyo.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Wote wategemeana, mwajiri na mwajiriwa,
Kubwa kuheshimiana, mwerevu kanielewa,
Pia mkiaminiana, kazi haitachezewa,
Tara mkifanyiana, lengo halitafikiwa,
Riziki ni majaliwa, kuipata si ngekewa.
Njano5.
0784845394
Haku muumba kilema, aka mkosesha mwendo,
Huyo ni Mola Karima, mfalme wa vishindo,
Usijifanye yatima, fungua yako mafundo,
Rauka fanya hima, nyumbani haliji windo.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Mwenye kupewa ukwasi, katu hakupendelewa,
Masikini hasiasi, wallahi hakuonewa,
Mitihani ya Qudusi, mola wa majaliwa,
Alichopewa pungusi, chaa hakuruzukiwa.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Rauka wahi kazini, upate yako ijara,
Changamoto za windoni, na zikufanye imara,
Toa simanzi moyoni, tena sifanye harara,
Bosi avimbe kichwani, tuli sipoteze dira.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Ukiri Lutumbo kiri, hebu acha kusonona,
Wazoee waajiri, kama wataka kunona,
Shetwani asikughuri, ingawa dhiki waona,
Subiri kakasubiri, lisilo mwisho hakuna.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Niseme nawaajiri, wenye pembe vichwani,
Wana kifanya kiburi, hawana heri moyoni,
Mbaya hawana habari, shida haina maskani,
Tabu hainatajiri, wala si ya masikini.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Ewe ndugu mwajiriwa, sema na wako moyo,
Jukumu ulilopewa, litimize pasi choyo,
Ridhika na unachopewa, huno wangu mgogoyo,
Rushwa katusi ngekewa, yataka ushinda moyo.
Riziki nimajaliwa, kuipata si ngekewa.
Wote wategemeana, mwajiri na mwajiriwa,
Kubwa kuheshimiana, mwerevu kanielewa,
Pia mkiaminiana, kazi haitachezewa,
Tara mkifanyiana, lengo halitafikiwa,
Riziki ni majaliwa, kuipata si ngekewa.
Njano5.
0784845394