THE SPIRIT THINKER
JF-Expert Member
- Sep 9, 2019
- 392
- 555
HII NI SIMLIZI YA KISAYANSI NA KITEKNOLOJIA. MTUNZI NI YULEYULE TARIQ HAJJ.
HAYA NI MAONO YA MAISHA YAJAYO.
RIWAYA NYINGINE ZILIZO TANGULIZIA NI
1. CODE X
2.CODE. X 2 MCHEZO WA KIFO.
3.COD X 3 ASKARI WA KUTENGENEZWA.
4.CODE X 4 HII MTUNZI NI FRENK MASAI.
NA NYINGINEZO ZA KISAYANSI NA MAPIGANO.
TO THE END (mpaka mwisho)
KITABU CHA KWANZA
1
Na Tariq Hajj
Kalenda ya stela mwaka mia nne na tisini na tisa tokea dunia ilivyobadilisha kalenda yake. Kalenda hiyo imebadilika baada ya dunia kupata wageni kutoka anga za mbali, wageni hao hawakuwa na nia njema na dunia hata kidogo. Hivyo vita kubwa ikazuka na baada ya binadamu kugundua hakuna uwezekano wa kushinda, wachache wakaamua kuungana na wavamizi ili kunusuru maisha yao.
Ni katika nyakati hizo ngumu binadamu wakafanikiwa kupiga hatua moja mbele kiteknolojia. Silaha ya kwanza yenye uwezo wa kuwaumiza wavamizi ikaundwa. Ilikuwa ni robot ambalo liliebdeshwa na binadamu, ilikuwa imebeba silaha nzito ambazo zilikuwa na uwezo wa kusababisha madhara kwa wavamizi.
Hata hivyo halikudumu sana kutokana na marekebisho yake kuwa magumu na yenye kuchukuwa muda. Hata hivyo taratibu binadamu wakaanza kuendelea kiakili na kimwili. Na ni katika huwo binadamu wakagundua uwepo wa chembechembe maalum katika hewa aina 'itharion'.
Chembechembe ambazo ziliwapa uwezo wa ajabu katika kupambana na wavamizi wao. Kwa kupitia majribio mengo hatimae binadamu wakafanikiwa kuunda seli maalum ambazo zilikuwa na uwezo wa kunyonya itharion kutoka katika hewa na kuzisambaza katika mwili wa binadamu.
Hilo likapelekea kuzaliwa kwa kizazi cha kwanza binadamu wapya ambao walitumika kama wanajeshi katika vita dhidi ya wavamizi. Miaka baadae binadamu wakapiga hatua nyingine na kusababisha mageuzi makubwa ya kiteknolojia.
Kwa kutumia vyuma vilivyong'oka kutoka katika mashine za wavamizi walifanikiwa kutengeneza maroboti yenye uwezo wa hali na ustadi mkubwa. Na kutokea hapo vita ikawa nyepesi na pia binadamu wakafungua kurasa mpya katika maisha yao. Kalenda ikabadilishwa na kuitwa kalenda ya stela ikiwa na maana mwaka ambao dunia ilishuhudia uvamizi na pia milango mipya ikafunguka.
**********
Republic of Iron City (mji wa chuma).
Taratibu na maandalizi ya kushherekea siku ya uhuru mwaka mia nne na tisini na tisa ziliendelea. Kila mti alionekana kuzama katika maandalizi hayo.
"Mlemavu anapita" minong'ono ilisikika kila alipokuwa akipita, kijana mwenye nywele nyeusi kuliko na macho ya rangi hazel. Alikuwa akiburuza kitoroli ambacho kilikuwa na maji ya sabuni ndani kwa ajili kufanyia usafi.
"Oooow! Kama sio Baston" kija mmoja mwenye nywele za kijani kibichi akasimama mbele ya kitoroli hicho na kumfanya Baston ashindwe kuendelea na safari yake. "Edward, unataka nini" aliuliza Baston akimuangalia usoni kijana huyo aliesimama mbele yake.
"Inaonekana kipigo cha nyuma hakijakutosha, nilikwambia unaponiona mimi huruhusiwi kuniangalia usoni" aliongea Edward na kuwapa ishara vibwengo wake.
"Inatosha" sauti laini ya mtoto wa kike ikasikika ikitokea mbali kidogo na wakipokuwa wamesimama. Ikafuatiwa na harua za taratibu kabisa ambazo kila zilipokanyaga ardhi zilitoa tafsiri ya mtu huyo aliekuwa anakuja.
"Shanequeen, hilo halikuhusu. Wewe endelea na mambo yako" aliongea Edward akimuangalia binti huyo aliekuwa anatembea kwa mwendo wa madaha.
Shida nyingine iliyozuka baada ya binadamu kugundua uwepo wa itherion ni matabaka. Japo mwanzo yalikuwepo lakini baada ya miaka kadhaa kupita yakaongezeka na kuwa makubwa zaidi. Baada ya miaka miambili wakaanza kuzaliwa watoto ambao moja kwa moja walizaliwa na uwezo wa kunyonya itherion kutoka kwenye hewa.
Hawa waliitwa kizazi cha nne na hilo likapelekea kutokea kwa familia ambazo zilikuwa na uwezo wa kunyonya itherion kwa wingi mno hivyo kuwafanya kuwa na nguvu kuliko wengine wa tabaka hilo na pia kuwa na uwezo zadi kuliko raia wa kawaida.
Yakatengezwa madaraja ambayo yaliwawakilisha watu wenye uwezo wa kutumia itherion. Yalianza na F ambayo iliwakilisha wale wenye uwezo wa chini zaidi ambao hawa walikuwa ni raia wa kawaida.
E iliwawakilisha wale wenye wa juu kidogo kuliko F lakini hawakuwa na uwezo wa kuingia vitani. Hawa wao walikuwa ni kundi lilihusika na marekebisho ya maroboti ya kivita.
D iliwawakilisha wale ambao walikuwa na uwezo wa karibia na kati. Kundi hili lilikuwa la watu waliongia vitani lakini kwa ajili ya kutoa msaada tu.
C iliwawakilisha kundi la wanajeshi wa kawaida, walihusika na kupanda na viumbe wenye uwezo wa chini.
B iliwawakilisha kundi la majenerali, hawa walipambana na viumbe wenye uwezo wa kati.
A iliwawakilisha kundi la makomanda, hawa walikuwa wachache na walikuwa na uwezo wa kupambana na viumbe wenye uwezo wa juu.
S iliwakilisha kundi la asilimia moja tu la binadamu wote, hawa walikuwa na uwezo wa hali ya juu sana na waliweza kupambana na viumbe waliokuwa na uwezo zaidi.
SS, kundi hili lilichangia asilimia sifuri nukta tano ya watu wote duniani, na waliotambulika kuwa katika hili hawakuzidi hata kumi. Ni kundi la watu maalum ambalo halikuwa na mfano wake mpaka wavamizi walikuwa wakiliogopa kundi hili.
Kwa kesi ya Baston, yeye hakuingia katika kundi lolote kati ya hayo nane. Alizaliwa na kutokuwa na uwezo wa kunyonya itherion kabisa. Hivyo kundi la watu kama yeye lilipewa jina la walemavu na uwepo wao haukuwa na tofauti na takataka.
Edward na Shanequeen walikuwa ni daraja A huku Shanequeen akiwa juu kidogo kiuwezo kuliko Edward.
"Ahsante" Baston aliongea na kuvita kitoroli chake nyuma, akapita pembeni na kuelekea ilipo henga namba tano ambako ndipo alipopangiwa kufanya usafi. Katika henga hiyo kulikuwa roboti moja tu ambalo lilikuwa kongwe mno. Pamoja na kutelekezwa huko Baston alihakikisha kila siku analisafisha.
"Fuata upepo, utasafiri katika gharika" ndio maneno yaliokuwa yameandikwa kwenye kifuoa chanroboti huyo. Baada ya usafi, Baston akakaa pembeni ya roboti hilo na kuongea "thamani yako inakuwepo pale unapokuwa na jambo la kuwapa tu" aliongea na kuliangalia.
"Sijui nani alikuwa rubani wako lakini naamini kabisa kipindi chako ulikuwa bingwa" aliendelea na kugusa mkono wa roboti hilo.
"Mpaka sasa nahisi hamu yako ya kuingia vitani", Baston alikuwa akiongea mwenyewe na kufanya kama vile chuma hicho chakavu kilikuwa kinamsikia. "Hata mimi nilikuwa na ndoto ya siku moja kusimama vitani kupigania nchi yangu lakini wachache wakaamua kuwa siwezi kufanya hivyo kutokana na mwili wangu kushindwa kunyonya itherion kutoka katika hewa".
Ghafla kigora kikasikika na taa nyekundu za henga hiyo zikaanza kuwaka, "vikosi vyote katika henga zenu na mjiandae na vita, tunasoma mawimbi ya itherion ya wavamizi" sauti ilisikika kutoka katika speaker maalum ndani ya henga hiyo.
"Wale ambao siyo wanajeshi mnatakiwa kuwa watulivu"
"Vikosi vyote katika henga zenu na mjiandae na vita" kauli hiyo.
"Nichukue vitani, nataka kusimama kwa mara ya mwisho", Baston akasikia sauti lakini eneo hilo alikuwa yeye peke yake na roboti huyo.
"Upweke wangu naona sasa unanifanya kusikia sauti" alijisemea.
"Nichukue vitani, nataka kwenda zangu kama shuja na siyo chuma chakavu" alisikia tena sautu. Alipogeuza uso kuangalia akakutana na macho ya roboti huyo yaakiwa yanawaka taa nyekundu.
HAYA NI MAONO YA MAISHA YAJAYO.
RIWAYA NYINGINE ZILIZO TANGULIZIA NI
1. CODE X
2.CODE. X 2 MCHEZO WA KIFO.
3.COD X 3 ASKARI WA KUTENGENEZWA.
4.CODE X 4 HII MTUNZI NI FRENK MASAI.
NA NYINGINEZO ZA KISAYANSI NA MAPIGANO.
TO THE END (mpaka mwisho)
KITABU CHA KWANZA
1
Na Tariq Hajj
Kalenda ya stela mwaka mia nne na tisini na tisa tokea dunia ilivyobadilisha kalenda yake. Kalenda hiyo imebadilika baada ya dunia kupata wageni kutoka anga za mbali, wageni hao hawakuwa na nia njema na dunia hata kidogo. Hivyo vita kubwa ikazuka na baada ya binadamu kugundua hakuna uwezekano wa kushinda, wachache wakaamua kuungana na wavamizi ili kunusuru maisha yao.
Ni katika nyakati hizo ngumu binadamu wakafanikiwa kupiga hatua moja mbele kiteknolojia. Silaha ya kwanza yenye uwezo wa kuwaumiza wavamizi ikaundwa. Ilikuwa ni robot ambalo liliebdeshwa na binadamu, ilikuwa imebeba silaha nzito ambazo zilikuwa na uwezo wa kusababisha madhara kwa wavamizi.
Hata hivyo halikudumu sana kutokana na marekebisho yake kuwa magumu na yenye kuchukuwa muda. Hata hivyo taratibu binadamu wakaanza kuendelea kiakili na kimwili. Na ni katika huwo binadamu wakagundua uwepo wa chembechembe maalum katika hewa aina 'itharion'.
Chembechembe ambazo ziliwapa uwezo wa ajabu katika kupambana na wavamizi wao. Kwa kupitia majribio mengo hatimae binadamu wakafanikiwa kuunda seli maalum ambazo zilikuwa na uwezo wa kunyonya itharion kutoka katika hewa na kuzisambaza katika mwili wa binadamu.
Hilo likapelekea kuzaliwa kwa kizazi cha kwanza binadamu wapya ambao walitumika kama wanajeshi katika vita dhidi ya wavamizi. Miaka baadae binadamu wakapiga hatua nyingine na kusababisha mageuzi makubwa ya kiteknolojia.
Kwa kutumia vyuma vilivyong'oka kutoka katika mashine za wavamizi walifanikiwa kutengeneza maroboti yenye uwezo wa hali na ustadi mkubwa. Na kutokea hapo vita ikawa nyepesi na pia binadamu wakafungua kurasa mpya katika maisha yao. Kalenda ikabadilishwa na kuitwa kalenda ya stela ikiwa na maana mwaka ambao dunia ilishuhudia uvamizi na pia milango mipya ikafunguka.
**********
Republic of Iron City (mji wa chuma).
Taratibu na maandalizi ya kushherekea siku ya uhuru mwaka mia nne na tisini na tisa ziliendelea. Kila mti alionekana kuzama katika maandalizi hayo.
"Mlemavu anapita" minong'ono ilisikika kila alipokuwa akipita, kijana mwenye nywele nyeusi kuliko na macho ya rangi hazel. Alikuwa akiburuza kitoroli ambacho kilikuwa na maji ya sabuni ndani kwa ajili kufanyia usafi.
"Oooow! Kama sio Baston" kija mmoja mwenye nywele za kijani kibichi akasimama mbele ya kitoroli hicho na kumfanya Baston ashindwe kuendelea na safari yake. "Edward, unataka nini" aliuliza Baston akimuangalia usoni kijana huyo aliesimama mbele yake.
"Inaonekana kipigo cha nyuma hakijakutosha, nilikwambia unaponiona mimi huruhusiwi kuniangalia usoni" aliongea Edward na kuwapa ishara vibwengo wake.
"Inatosha" sauti laini ya mtoto wa kike ikasikika ikitokea mbali kidogo na wakipokuwa wamesimama. Ikafuatiwa na harua za taratibu kabisa ambazo kila zilipokanyaga ardhi zilitoa tafsiri ya mtu huyo aliekuwa anakuja.
"Shanequeen, hilo halikuhusu. Wewe endelea na mambo yako" aliongea Edward akimuangalia binti huyo aliekuwa anatembea kwa mwendo wa madaha.
Shida nyingine iliyozuka baada ya binadamu kugundua uwepo wa itherion ni matabaka. Japo mwanzo yalikuwepo lakini baada ya miaka kadhaa kupita yakaongezeka na kuwa makubwa zaidi. Baada ya miaka miambili wakaanza kuzaliwa watoto ambao moja kwa moja walizaliwa na uwezo wa kunyonya itherion kutoka kwenye hewa.
Hawa waliitwa kizazi cha nne na hilo likapelekea kutokea kwa familia ambazo zilikuwa na uwezo wa kunyonya itherion kwa wingi mno hivyo kuwafanya kuwa na nguvu kuliko wengine wa tabaka hilo na pia kuwa na uwezo zadi kuliko raia wa kawaida.
Yakatengezwa madaraja ambayo yaliwawakilisha watu wenye uwezo wa kutumia itherion. Yalianza na F ambayo iliwakilisha wale wenye uwezo wa chini zaidi ambao hawa walikuwa ni raia wa kawaida.
E iliwawakilisha wale wenye wa juu kidogo kuliko F lakini hawakuwa na uwezo wa kuingia vitani. Hawa wao walikuwa ni kundi lilihusika na marekebisho ya maroboti ya kivita.
D iliwawakilisha wale ambao walikuwa na uwezo wa karibia na kati. Kundi hili lilikuwa la watu waliongia vitani lakini kwa ajili ya kutoa msaada tu.
C iliwawakilisha kundi la wanajeshi wa kawaida, walihusika na kupanda na viumbe wenye uwezo wa chini.
B iliwawakilisha kundi la majenerali, hawa walipambana na viumbe wenye uwezo wa kati.
A iliwawakilisha kundi la makomanda, hawa walikuwa wachache na walikuwa na uwezo wa kupambana na viumbe wenye uwezo wa juu.
S iliwakilisha kundi la asilimia moja tu la binadamu wote, hawa walikuwa na uwezo wa hali ya juu sana na waliweza kupambana na viumbe waliokuwa na uwezo zaidi.
SS, kundi hili lilichangia asilimia sifuri nukta tano ya watu wote duniani, na waliotambulika kuwa katika hili hawakuzidi hata kumi. Ni kundi la watu maalum ambalo halikuwa na mfano wake mpaka wavamizi walikuwa wakiliogopa kundi hili.
Kwa kesi ya Baston, yeye hakuingia katika kundi lolote kati ya hayo nane. Alizaliwa na kutokuwa na uwezo wa kunyonya itherion kabisa. Hivyo kundi la watu kama yeye lilipewa jina la walemavu na uwepo wao haukuwa na tofauti na takataka.
Edward na Shanequeen walikuwa ni daraja A huku Shanequeen akiwa juu kidogo kiuwezo kuliko Edward.
"Ahsante" Baston aliongea na kuvita kitoroli chake nyuma, akapita pembeni na kuelekea ilipo henga namba tano ambako ndipo alipopangiwa kufanya usafi. Katika henga hiyo kulikuwa roboti moja tu ambalo lilikuwa kongwe mno. Pamoja na kutelekezwa huko Baston alihakikisha kila siku analisafisha.
"Fuata upepo, utasafiri katika gharika" ndio maneno yaliokuwa yameandikwa kwenye kifuoa chanroboti huyo. Baada ya usafi, Baston akakaa pembeni ya roboti hilo na kuongea "thamani yako inakuwepo pale unapokuwa na jambo la kuwapa tu" aliongea na kuliangalia.
"Sijui nani alikuwa rubani wako lakini naamini kabisa kipindi chako ulikuwa bingwa" aliendelea na kugusa mkono wa roboti hilo.
"Mpaka sasa nahisi hamu yako ya kuingia vitani", Baston alikuwa akiongea mwenyewe na kufanya kama vile chuma hicho chakavu kilikuwa kinamsikia. "Hata mimi nilikuwa na ndoto ya siku moja kusimama vitani kupigania nchi yangu lakini wachache wakaamua kuwa siwezi kufanya hivyo kutokana na mwili wangu kushindwa kunyonya itherion kutoka katika hewa".
Ghafla kigora kikasikika na taa nyekundu za henga hiyo zikaanza kuwaka, "vikosi vyote katika henga zenu na mjiandae na vita, tunasoma mawimbi ya itherion ya wavamizi" sauti ilisikika kutoka katika speaker maalum ndani ya henga hiyo.
"Wale ambao siyo wanajeshi mnatakiwa kuwa watulivu"
"Vikosi vyote katika henga zenu na mjiandae na vita" kauli hiyo.
"Nichukue vitani, nataka kusimama kwa mara ya mwisho", Baston akasikia sauti lakini eneo hilo alikuwa yeye peke yake na roboti huyo.
"Upweke wangu naona sasa unanifanya kusikia sauti" alijisemea.
"Nichukue vitani, nataka kwenda zangu kama shuja na siyo chuma chakavu" alisikia tena sautu. Alipogeuza uso kuangalia akakutana na macho ya roboti huyo yaakiwa yanawaka taa nyekundu.