SIRI PART3: MTUNZI PATRICK CK
JASUSI/GAIDI
SEASON 1 : EPISODE 8
Imetimu saa mbili za usiku
Ruby akiwa amejipumzisha
nyumbani kwake gari nne
nyeusi zilifika katika geti la
nyumba yake.Akiwa sebuleni
kwake aliona taa ya kijani
ikiwaka katika kisanduku
kilichokuwa ukutani pembeni
ya runinga iliyounganishwa na
kamera za usalama
zilizofungwa kuzunguka
nyumba yake.Taa ile ya kijani
huwaka pale geti kubwa
linapofunguliwa.Alistuka na
haraka haraka akachukua
kitanza mbali akabonyeza
kamera ya getini akaziona gari
nne zikiingia
“Nani hawa? Mbona sina
ratiba ya kuonana na mtu
yeyote usiku huu?Kwa nini
walinzi wameruhusu watu
kuingia bila kunijulisha?
Akajiuliza
Ruby.Aliogopa.Haraka haraka
akacheza na kompyuta yake na
kuifunga milango yote kwa
ndani halafu akaendelea
kuwafuatilia watu wale kujua
ni akina nani.Gari mbili za
mbele wakashuka watu
waliovalia suti nadhifu na
kulizunguka gari la tatu.Macho
yao hayakutulia waliangaza
kila kona kisha wawili kati ya
wale jamaa wakaelekea katika
mlango mkubwa
wakagonga.Ruby
akawachunguza kwa makini
kwa kutumia kamera ya
mlangoni
“Akina nani hawa?Mbona
siwafahamu?Wanataka
nini?akajiuliza Ruby wale
jamaa wakiendelea kugonga
mlango.Akachukua simu na
kuwapigia walinzi wake getini
kuuliza kwa nini wameruhusu
watu kuingia bila ruhusa yake
na akajibiwa kwamba
wamelazimka kufungua kwani
ni msafara wa Rais.Haraka
haraka Ruby akaenda mlango
akafungua.Wale jamaa wawili
wakaingia ndani wakakagua
sebuleni halafu mmoja wao
akausogeza mkono ake aliovaa
saa karibu na mdomoni wake
akasema
“Clear !
Haikupita hata dakika
moja mlango ukafunguliwa
wakaingia watu wanne kisha
akafuata Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania Dr
Fabian Kelelo
“Hello Ruby” akasema Dr
Fabian akitabasamu
“Mheshimiwa Rais !
akasema Ruby na Rais
akawataka wale walinzi wake
watoke nje
“Umenistua sana
mheshimiwa Rais” akasema
Ruby
“I’m sorry Ruby.Sikutaka
kukueleza kama ninakuja
kwako nilitaka
nikustukize”akasema Dr
Fabian
“Karibu sana.Utapenda
kunywa nini? Akauliza Ruby
“Chochote
utakachoniandalia
nitashukuru”
Ruby akaenda katika
kabati ambalo huhifadhi
vinywaji vikali akachukua
chupa mbili na kuziweka
mezani,akammiminia Rais
kinywaji katika glasi na yeye
akajimiminia
“Karibu”
“Ahsante Ruby”
“Ungeniambia kama
utakuja ili nikuandalie hata
chakula kidogo” akasema Ruby
“Usijali Ruby.Nilitaka
nikustukize nione namna
unavyoishi hapa.Are you
alone?
“Ndiyo niko peke yangu”
akajibu Ruby
“Kwa nini unaishi
mwenyewe?Huna mtu wa
kuishi naye?
“Nina mfanyakazi wa
ndani ambaye kuanzia jana
amepata dharura amekwenda
kumuuguza mama yake
mgonjwa,vile vile nina walinzi
na kama haitoshi nina mbwa
anaitwa Bravo nilipewa na
Mathew ninampenda sana”
akasema Ruby
“Wewe na Mathew
mnaonekana mna ukaribu
mkubwa”
“Ni kweli mheshimiwa
Rais nina ukaribu na Mathew
Mulumbi”
“Vizuri sana.Lakini
unahitaji kuwa na mwenzi
sasa.Utaishi namna hii hadi
lini? Akauliza Dr Fabian na
Ruby akatoa kicheko kidogo
“Mambo hayo
mheshimiwa Rais hayataki
haraka.Muda utakapofika basi
nitakuwa naye lakini kwa sasa
nimejielekeza katika kazi
yangu”
“Kwa hiyo huna
mchumba? Akauliza Dr Fabian
na Ruby akacheka tena kidogo
“Mchumba ninaye ila yuko
nje ya nchi”
“Hongera.Ana bahati sana
huyo aliyekupata.Siku akija
nchini umlete kwangu
nimfahamu”
“Usijali mheshimiwa Rais
nitamleta” akasema Ruby na
ukimya mfupi ukapita
“Ruby nimekuja hapa bila
taarifa kuna suala ambalo
limenileta usiku huu” akasema
Dr Fabian na kunyamaza
kidogo halafu akaendelea
“Ulipokuja ofisini kwangu
asubuhi ya leo hatukuwa na
mazungumzo
mazuri.Nilikutolea maneno
ambayo si ya
kiungwana.Nafahamu
nilikukera hivyo nimekuja
kukuomba msamaha.Siku ya
leo haikuwa siku nzuri kwangu
ndiyo maana nilikuwa katika
hali ile.Nakuhakikishia it won’t
happen again” akasema Dr
Fabian na Ruby akatabasamu
“Mheshimiwa Rais mambo
kama yale ni ya kawaida
kutokea katika sehemu za kazi
hivyo sikushangaa kwa vile
nimekwisha yazoea.Nimefanya
kazi katika ofisi ambayo
inaweza kumpa mtu shinikizo
la damu lakini nilimudu vyema
na ndiyo maana hawakutaka
niondoke hivyo suala lile
lilimalizika pale pale.Mimi pia
ninaomba samahani sana kwa
tabia yangu asubuhi
ile.Nilikosa heshima kwako
mkuu wa nchi,sikupaswa
kuzungumza nawe namna
ile.Nami pia naomba
unisamehe mheshimiwa Rais
hata kama nitakuwa na jambo
limenikaba kooni nitajitahidi
kutafuta namna nzuri ya
kuliwasilisha” akasema Ruby
“Nimekusamehe Ruby”
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais” akasema
Ruby na Dr Fabian
akanyanyua glasi yake
“Friends again?
Ruby akatabasamu na
kusema
“Friends” kisha
wakagonganisha glasi zao.
“Mheshimiwa Rais
ninataka kuuliza na ninaomba
uwe mkweli na muwazi
kwangu”
“Usijali Ruby uliza”
“You did it? Akauliza Ruby
na Dr Fabian akawa kimya kwa
muda halafu akatingisha
kichwa kukubali
“Yes I did it” akasema na
kunyamaza kidogo
“Naomba niwe muwazi
kwako Ruby.Ajali ile ilikuwa ya
kutengeneza kwa lengo la
kuwamaliza familia ya
Akiki.Nina hasira kubwa na
Jenerali Akiki kwa kitu
alichotaka kunifanyia na
niliapa kumfanyia kitu kibaya
sana na hasira hizo ndizo
ambazo zimenipelekea
kuimaliza familia yake namna
ile.Dr Natukunda alikuwa ni
rafiki wa mke wangu na
sikutegemea kama siku moja
ningeweza kumfanyia ukatili
huu lakini ni mume wake
ndiye aliyenifanya niwe na
roho ya ukatili hata
nikalazimika kuimaliza familia
ile yote.Ninataka nimuumize
Akiki.Kama si kwa jitihada
zenu ninyi kuweza kung’amua
mipango aliyokuwa nayo
Jenerali Akiki, hivi sasa tayari
ningekwisha kuwa marehemu
ndiyo maana wewe na
wenzako akina Mathew mnayo
nafasi kubwa ndani ya moyo
wangu kwani mlipambana
kuokoa maisha yangu.Jasiri
Mathew Mulumbi aliweza
kupambana na mtu mwenye
bomu ambalo lililengwa
kuniua.Mimi na Jenerali Akiki
tulikuwa marafiki na tulikuza
mashirikiano kati ya Uganda
na Tanzania.Kila ninapofirikia
kwa nini Akiki ajiunge katika
mpango wa kuniua ninajikuta
ninapatwa na hasira
kali.Hukupendezwa na kile
nilichokifanya kwa familia ya
Jenerali Akiki I’m so sorry
lakini sikuwa na namna
nyingine ya kufanya,roho ya
kisasi ilikwisha niingia”
akasema Dr Fabian na
kunyamaza akanywa funda
moja kisha akasema
“Kuna jambo lingine
ambalo nataka nikufahamishe
leo ambalo ni la siri
kubwa.Tumeufungua ukurasa
mpya hivyo sitaki kukuficha
jambo” akasema Dr Fabian
akanywa tena funda lingine
akasema
“Mapinduzi yaliyofanyika
jana nchini Uganda
yaliyomuondoa madarakani
Jenerali Akiki mimi pia
nimeshiriki katika kuyapanga”
Ruby aliyekuwa ameshika
glasi akiipeleka mdomoni
akajikuta akiishusha haraka
mezani kwa mshangao
alioupata.
“Nimekustua,samahani
kwa hilo lakini nimelazimika
kukueleza ukweli.Kuna kitu
kimoja ambacho unapaswa
ukifahamu kuhusu mimi.Nina
tatizo la kuamini watu ndiyo
maana jambo kama hili
nimelifanya mwenyewe kwa
siri na wewe ni mtu wa kwanza
unalifahamu kwa hapa
nchini.Nimechagua kukuamini
na kukushirikisha katika
mambo yangu nyeti” akasema
Dr Fabiana akanyamaza
akamtazama Ruby
“Dah ! akasema Ruby
“Kama nilivyokueleza
awali kwamba chuki
niliyokuwa nayo dhidi ya
Jenerali Akiki ni kubwa sana
hivyo nilidhamiria
kumuumiza,kumfanya awe na
maisha magumu.Niliwasiliana
na spika wa bunge la Uganda
nikamtaka aje Tanzania kimya
kimya nikazungumza naye kwa
kirefu kuhusiana na mambo
yote anayoyafanya Rais Akiki
naye alishangaa
sana.Hakufahamu kama
James Kasai alikuwa anaishi
jijini Kampala.Nilimpatia
rekodi ile ya Melanie Davis
tukakubaliana aitumie
kumtaka Akiki aachie ngazi
kwa hiari yake na kama
akigoma basi bunge litumike
kumuondoa.Tulitengeneza
mtandao mkubwa na
kumshirikisha pia mkuu wa
majeshi wa Uganda ili endapo
mpango wa kwanza wa
kumtaka aachie ngazi au
kuondolewa na bunge
kushindwa kufanikiwa basi
jeshi lifanye mapinduzi.Kwa
bahati mbaya katika mchakato
huo spika wa bunge la Uganda
aliuawa yeye na familia yake
na ndipo jeshi lilipochukua
nchi” akasema Dr Fabian na
kuchukua glasi akanywa funda
moja kubwa
“Say something Ruby !
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais sijui
niseme nini.Nakushukuru kwa
kunieleza ukweli” akasema
Ruby
“Baada ya kuufahamu
ukweli nini maoni yako?Ni
wewe pekee ambaye una
uthubutu wa kusimama na
kunieleza ukweli.Usiogope
nieleze ukweli”
“Sina maoni yoyote
mheshimiwa Rais” akasema
Ruby na Dr Fabian akanywa
kinyaji kidogo halafu akasema
“Asubuhi wakati
unaondoka ofisini ukiwa
umekasirika ulinieleza
kwamba kwa hiki
nilichokifanya nitasababisha
matatizo
makubwa.Ulimaanisha nini?
“Zilikuwa ni hasira tu
mheshimiwa Rais lakini
sikumaanisha chochote.By the
way yuko wapi Jenerali Akiki
kwa sasa?
“Hajulikani
alipo.Alifanikiwa kutoroka
mara tu wanajeshi
walipovamia ikulu.Naamini
hata huko aliko salamu zangu
atazipata.Mali zake zote
zitataifishwa na serikali
atabaki hohehahe.Atapata
mateso makali na atakufa
taratibu”
“Kuna uwezekano
amejificha nchini
Uganda?akauliza Ruby
“Bado haijulikani lakini
jeshi linandelea na uchunguzi
kumtafuta mahala alipo”
akasema Dr Fabian na ukimya
ukapita
“Mheshimiwa Rais mimi
bado si mtaalamu sana wa
mambo ya kiusalama lakini
ushauri wangu ni kufanya kila
linalowezekana kuhakikisha
tunafahamu mahala alipo
Jenerali Akiki na
kummaliza.Kama ataendelea
kuwa hai nina uhakika
mkubwa atajipanga kulipiza
kisasi”
“Jeshi la Uganda
linaendelea na msako na
watanijulisha kila
watakachokipata halafu
tutaangalia nini cha
kufanya.Kwa kuwa ameondoka
madarakani Akiki hana nguvu
tena na hawezi kupanga njama
zozote.Mali zake zote ziko
nchini Uganda na zote
zimetaifishwa na jeshi hivyo
basi hana nguvu yoyote ya
kuweza kupanga shambulio la
aina yoyote ile”
Ruby na Dr Fabian
walikuwa na mazungumzo
marefu hadi ilipotimu saa tatu
za usiku ndipo Rais
alipoondoka kurejea ikulu
WASHINGTON DC –
MAREKANI
Jenerali Akiki alifikishwa
Marekani na kupelekwa katika
nyumba aliyoandaliwa jijini
Washington DC.Ilkuwa ni
nyumba nzuri kubwa na yenye
ulinzi wa kutosha.
“Maisha yana maajabu
sana.Yanaweza kubadilika
ndani ya sekunde moja tu.Jana
nilikuwa Rais,jeshi lote likiwa
chini yangu,nilikuwa na ulinzi
mkali na kauli yangu ilikuwa
ya mwisho lakini leo tazama
mahala nilipo.Niko
ugenini,sina kitu chochote
ninalishwa na kuvishwa,sina
msafara tena,sina timu ya
walinzi na zaidi ya yote sina
familia” akawaza na
kuinamisha kichwa chake kwa
mawazo
“Kila ninapoikumbuka
familia yangu ninapatwa na
uchungu mkubwa
mno.Naamini kabisa kwamba
ajali iliyowaua ni mpango wa
serikali ya Tanzania
inayoongozwa na Dr
Fabian.Anataka kulipiza kisasi
baada ya kugundua kwamba
nilishiriki katika kupanga
mauaji dhidi yake na Patrice
Eyenga.Hata mimi
kupinduliwa naamini ana
mkono wake kwani Spika wa
bunge asingeweza kuipata
rekodi ile ya Melanie.Lazima
aliipata kutoka Tanzania na
mtu ambaye naamini aliyempa
rekodi ile ni Rais Dr Fabian”
akavuta pumzi ndefu alihisi
kizungu zungu akajilaza
kitandani
“Yote haya
ameyasababisha James
Kasai.Yeye ndiye aliyemleta
Melanie kwangu nikamtamani
na kujikuta nikikubali kufanya
kila alichotaka nikifanye.Yule
mwanamke nahisi alikuwa
shetani kwani sikujielewa
nilikuwa nakubali tu
kutekeleza kila
alichonielekeza.Ni aibu kwa
Rais kama mimi kuanguka
penzini na binti mwenye umri
sawa na mwanangu.Ni aibu
kubwa hii” akawaza na
kuinuka
“Natamani hata nijipige
vibao kwa ujinga
nilioufanya.Kwa tamaa zangu
nimekosa kila kitu.Nimemkosa
Melanie,nimeikosa familia
yangu na hata urais wangu
nimeupoteza.Hivi sasa
ninaishi kama mkimbizi”
akaendelea kuwaza huku
akibubujikwa na machozi
“Nilikuwa nikisikia tu
marais wakipinduliwa sikujua
kama huwa wanapata taabu za
namna hii.Mbaya zaidi
nilishiriki katika mpango wa
kumpindua Rais Patrice
Eyenga lakini mpango
haukufanikiwa na kibao
kimenigeukia mimi,jeshi
likanipindua.Nimejifunza
mengi kupitia haya
yaliyonikuta.Kuna muda
ninaichukia siasa natamani
ningebaki jeshini lakini tamaa
za madaraka zikanipeleka
kufanya mapinduzi
nikamuondoa Rais
madarakani na nilichokifanya
ndicho kimenitokea mimi”
akaendelea kuwaza Jenerali
Akiki
“Kuna sauti ninaisikia
ndani mwangu ikiniambia
niachane na siasa nianze
maisha mapya.Nina mali
nyingi nimezichuma ninaweza
kuishi maisha mazuri tu bila
matatizo lakini papo hapo
kuna sauti nyingine ninaisikia
inaniambia nisikubali lazima
nilipize kisasi kwa hawa watu
walionifanyia ubaya.Lakini
hata kama nikiamua kujipanga
kulipa kisasi ni kwa ajili ya
nani? Akajiuliza
“Ngoja niachane kwanza
na haya mawazo kwa sasa.Pale
akili yangu itakapokuwa
imetulia nitajua nini cha
kufanya lakini kwa sasa siwezi
kufanya maamuzi yenye kufaa”
akawaza na kujilaza kitandani
Saa mbili za usiku kwa saa
za Marekani watu sita
wakaingia ndani ya nyumba
alimokuamo Jenerali Akiki
aliyekuwa amejikunyata
sebuleni akitazama
runinga.Watu wale
hawakumsemesha kitu
wakafanya ukaguzi katika
nyumba nzima halafu akaingia
Mark Piller makamu wa rais
wa Marekani.Huyu ni mmoja
wa mwanasiasa kijana sana na
anayetajwa kuwa na ushawishi
mkubwa katika siasa za
Marekani.Jenerali Akiki
akasimama
“Mheshimiwa makamu wa
rais ! akasema Jenerali
Akiki.Hakutegemea kama
Mark Piller angekwenda
kumtembelea usiku ule.
“Jenerali Akiki” akasema
Mark wakasalimiana
“Karibu sana mheshimiwa
makamu wa Rais.Sikutegemea
kukuona hapa mida hii”
akasema Jenerali Akiki
“Nimekuja mida hii kwa
kuwa nisingeweza kuja
mchana kwanza kutokana na
kazi nyingi na pili ni kuhusu
uwepo wako hapa Marekani”
William akanyamaza kidogo
halafu akasema
“Naomba ufahamu
Jenerali Akiki kwamba uwepo
wako hapa Marekani
tumeufanya siri.Wanaofahamu
uko hapa ni watu wachache
sana.Sababu kubwa ya kufanya
jambo hili kuwa siri hatutaki
dunia ifahamu kuwa uko hapa
Marekani hivyo usishangae
kwa masharti ya kutowasiliana
na mtu yeyote.Kwa ujumla
naomba usihofu kitu hapa uko
salama kabisa,ulinzi ni mkali”
“Nashukuru sana
mheshimiwa makamu wa
Rais” akasema Jenerali Akiki
“Jenerali Akiki pole sana
kwa yote yaliyokutokea na
kubwa zaidi tukio la kuipoteza
familia yako” akasema Mark
“Ahsante mheshimiwa
makamu wa Rais.Ninajaribu
kuifanya akili yangu ikubali
kwamba suala hili ni la
kawaida lakini inakuwa
ngumu.Kuondokewa na
familia nzima kwa wakati
mmoja si kitu rahisi hata
kidogo.Itanichukua muda
kulizoea jambo hili na kuliona
la kawaida”
“Pole sana Jenerali
Akiki.Maisha yetu ya kila siku
yamejawa na mitihani mingi
na huu uliokupata ni
mojawapo ya mtihani wa
maisha ambao inakubidi
uushinde.Kwa namna yoyote
ile Jenerali Akiki lazima
ushinde mtihani huu” akasema
Mark
“Ninajitahidi sana
mheshimiwa makamu wa rais
,ninajiahidi lakini ni
ngumu.Itanichukua muda
kulizoea jambo hili.Hata kama
ingekuwa ni wewe ungekuwa
katika hali yangu ungeona
ugumu wa haya
ninayoyaptia.Jana tu nilikuwa
Rais wa nchi nikitembea na
msafara mkubwa,nikitoa amri
na kuheshimiwa na kila mtu
lakini leo hi tazama mahala
nilipo.Hili pekee linatosha
kabisa kukupa ugonjwa wa
moyo lakini kama haitoshi
famili yangu pia
wameuawa.Haya ni mateso
yasiyovumilika hata kidogo
lakini nitajitahidi” akasema
Jenerali Akiki
“Jenerali Akiki moja ya
kile kilichonileta hapa kwako
usiku huu ni kukuhakikishia
kwamba serikali ya Marekani
bado inasimama
nawe.Hatuitambui serikali ya
kijeshi na kesho Rais atatoa
tamko la kutoitambua serikali
hiyo.Marekani ni taifa kubwa
na tukitoa tamko mataifa
karibu yote makubwa
yataungana nasi kuupinga
utawala huo wa
kijeshi.Tutautaka utawala huo
wa kijeshi kurejesha madaraka
kwa serikali waliyoipindua
haraka sana ama sivyo
watakabiliana na vikwazo
vikubwa vya
kiuchumi.Tutazishawishi nchi
kubwa ambazo ni wanunuzi
wakubwa wa mafuta ya
Uganda wapunguze au kuacha
kabisa kununua mafuta ya
Uganda na kuufanya uchumi
wa nchi hiyo kuporomoka kwa
kasi.Tutaweka vikwazo vya kila
aina kushinikiza serikali hiyo
ya kijeshi kurejesha madaraka
kwa serikali
iliyopinduliwa.Naomba usife
moyo Jenerali Akiki sisi
tunakutambua wewe bado ni
Rais wa Uganda na
tutasimama nawe hadi
tuhakikishe unarejea
madarakani” akasema Mark
Piller
“Ahsante sana
mheshimiwa makamu wa
rais.Nimekosa neno la
kushukuru kwa maneno haya
mazito ambayo yamenifariji
sana”
“Usijali Jenerali
Akiki.Karibu sana Marekani
jisikie nyumbani”
“Mungu akubariki wewe
na serikali yako kwa msaada
huu mkubwa” akasema
Jenerali Akikiakiwa ameikunja
mikono yake kifuani
akishukuru
“Jenerali Paul Mukasa !
akasema Mark na kunyamaza
kidogo akamtazama Akiki
“Huyu alikuwa mkuu wa
majeshi.Lazima ni mtu
uliyemuamini sana.Imekuaje
akaamua kukugeuka?akauliza
Rais William.Jenerali Akiki
akavuta pumzi ndefu na
kusema
“Paul Mukasa alikuwa
mwanafunzi wangu
jeshini.Nilimpenda alikuwa
kijana mtiifu na
mkakamavu.Katika kila hatua
niliyokuwa ninapanda jeshini
sikumuacha nyuma niliendelea
kumpigania ili naye aweze
kupanda cheo.Nilipofanya
mapinduzi mtu pekee ambaye
niliamini angeweza kufaa
kuwa mkuu wa majeshi ni Paul
na bila kupoteza muda
nikamteua akawa mkuu wa
majeshi.Tumefanya kazi kwa
mashirikiano makubwa na
sikuwahi hata kuota kama siku
moja Paul angeweza kufanya
kitu kama hiki
alichokifanya.Nilistuka mno
nilipoambiwa kwamba Paul
amejitangaza ndiye Rais wa
Uganda baada ya mapinduzi”
akasema Jenerali Akiki na
kunyamaza akainamisha
kichwa
“Unadhani nini
kimesababisha akafanya hiki
alichokifanya?akauliza Mark
Piller
“Suala hili lazima lina
mkono kutoka nje ya
Uganda.Paul peke yake
asingeweza kufanya hiki
alichokifanya.Alikuwa mtiifu
mno kwangu”
“Unasema kuna mkono wa
mataifa ya nje?Ni taifa gani
unahisi limehusika katika
mpango huu wa
mapinduzi?akauliza Mark
Piller.Jenerali Akiki akafikiri
kidogo na kusema
“Tanzania”
“Tanzania?!
“Ndiyo” akajibu Jenerali
Akiki
“Tanzania na Uganda ni
nchi marafiki wakubwa.Iweje
Tanzania ishiriki katika
kuipindua serikali ya
Uganda?akauliza Rais William
na Jenerali Akiki akawa kimya
“Jenerali Akiki unadhani
kwa nini Tanzania ikashiriki
katika kuipindua serikali ya
Uganda? Kama unafahamu
chochote nieleze tafadhali”
akasema Mark Piller
“Nitakueleza ukweli Mark
Piller lakini naomba kile
nitakachokuambia kisivuke nje
ya kuta za nyumba hii”
“Niamini tafadhali”
akasema Mark Piller
“Kulikuwa na mpango wa
mapinduzi kuiondoa
madarakani serikali ya
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo na mimi nilishiriki
katika mpango huo”
“Mlitaka kuipindua
serikali ya jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo?Mark
Piller akauliza
“Ndiyo.Nilishiriki katika
mpango huo wa kumuondoa
madarakani Rais Patrice
Eyenga”
“Kwa nini mlitaka
kumuondoa madarakani Rais
Patrice Eyenga? Akauliza Mark
Piller
“Mheshimiwa makamu wa
Rais naamini unajua kwamba
vita iliyokuwa inaendelea
katika jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo ilikuwa
na manufaa makubwa kwa
nchi tajiri”
“Hilo nalifahamu.Nchi
nyingi tajiri zimefaidika sana
kwa vita iliyokuwa inaendelea
nchini Congo” akasema Mark
Piller
“Uganda pia ilifaidika
katika mapigano yale kwani
sisi tulikuwa tunamfadhili
James Kasai.Alipoingia
madarakani Rais Patrice
Eyenga alimaliza machafuko
yaliyodumu kwa miaka mingi
na kukata ile mirija yote
iliyokuwa inazifaidisha nchi
mbalimbali.Majenerali wa
jeshi la Congo
hawakufurahishwa na kile
alichokifanya Patrice Eyenga
kwani walikuwa wakifadikika
kutokana na mapigano yale
hivyo waliandaa mpango wa
mapinduzi kumuondoa
madarakani Patrice
Eyenga.Hilo lilikuwa kundi la
kwanza lakini kulikuwa na
kundi la pili ambalo liliandaa
mpango wa mapinduzi ambalo
ndilo nilishirikiana nalo”
akasema Jenerali Akiki na
kumueleza Mark Piller kila
kitu kuhusiana na mpango ule
wa Melanie Davis wa kuwaua
marais Patrice Eyenga na Dr
Fabian Kelelo.
“Hivyo ndivyo ilivyokuwa
mheshimiwa makamu wa
Rais” akasema Jenerali Akiki
“Nilisikia kuhusu mpango
ule wa kuwaua marais wa
Tanzania na Congo kwa bomu
la kujitoa mhanga lakini
sikujua kama wewe nawe
ulishiriki katika mpango
ule.Ahsante kwa kunieleza
ukweli” akasema Mark Piller
na ukimya ukapita.
“Jenerali Akiki sahau hayo
yote yaliyotokea na hapa
umekuja kuufungua ukurasa
mpya.Kabla sijakueleza
chochote nataka kukuhakisha
kwamba mimi binafsi niko
tayari kukusaidia lakini nataka
kujua tutaanzia wapi
kukusaidia.Nataka kusikia
mipango yako.Je unataka
kurudi tena Uganda? Bado
unataka kukalia kiti cha Urais?
Nieleze mipango yako
tafadhali” akasema Mark Piller
“Mheshimiwa makamu wa
Rais kwa kweli mpaka sasa
sifahamu nini hasa
ninakihitaji.Akili yangu naona
kama imefika mwisho wa
kufikiri” akasema Jenerali
Akiki
“Akiki wewe ni
mwanajeshi usiruhusu akili
yako ikashindwa kujua hatima
yako.Katika maisha kuna
kuanguka lakini ukianguka
simama haraka endelea
mbele.Nawe pia umeanguka
hivyo unapaswa kusimama na
kusonga mbele.Hukufika hapa
ulipofika kwa bahati
mbaya.Ulipambana ukafika
hapa ulipofika hivyo usikubali
kirahisi watu hawa wakaharibu
kila kitu ulichokipigania kwa
muda mrefu.Umeijenga
Uganda usiwape nafasi watu
hawa ya kuiharibu Uganda na
kuvuruga yale yote
uliyoyajenga.Unapaswa
kupambana”
“Mheshimiwa makamu wa
Rais sitaki tena
kupambana.Nataka nibadili
maisha yangu”
“Maisha ya namna gani
unataka kuishi Jenerali Akiki?
“Sitaki tena kurejea
Uganda.Nataka nipate sehemu
niishi maisha yaliyotulia yenye
amani.Ninafahamu mnao
uwezo wa kunirejesha
madarakani lakini sitaki tena
urais.Nimeponea tundu la
sindano sitaki tena kurejea
Uganda.”
“Nimekuelewa jenerali
Akiki na mimi nakuahidi
kukusaidia kwa hilo lakini
naomba ufahamu kwamba
hautakuwa na maisha yenye
furaha na amani unayoyataka
kama wale watu ambao
wamekuondoa madarakani
wataendelea kusalia
madarakani.Kokote
yanakofanyika mapinduzi
kuna mambo mawili tu
ambayo humtokea Rais
anayepinduliwa.Kuuawa au
kufungwa gerezani na mali
zake zote hutaifishwa awe
amezipata kihalali au
kifisadi.Akibahatika kukimbia
Rais huyu hugeuka mkimbizi
na wakati mwingine anaweza
akaishi ugenini kwa maisha
yake yote yaliyobaki.Paul
Mukasa na wenzake
wataendelea kukusaka kujua
mahala ulipo.Hii inakufanya
uwe katika hatari kubwa lakini
nakutoa hofu kwamba hapa
Marekani utakuwa
salama.Utapewa uraia wa
Marekani na utaishi maisha
mazuri yenye hadhi yako”
“Nashukuru sana makamu
wa Rais”
“Jenerali Akiki kama
umechagua kutorejea tena
Uganda hayo ni maamuzi yako
na tunayaheshimu,hata hivyo
kuna jambo ambalo lazima
tulifanye.Wasaliti wale
waliokupindua hatuwezi
kuwaacha hivi hivi lazima
tuwafunze adabu” akasema
Mark
“Nini unakitaka
mheshimiwa makamu wa
Rais?akauliza Jenerali Akiki
“Nataka Uganda
isitawalike.Nataka wananchi
wa Uganda wauchukie utawala
wa kijeshi na wapaaze sauti
kuukataa utawala huo na
kutaka kurejeshwa kwa serikali
ya kiraia.Mambo
yatakapokuwa magumu
wanajeshi watalazimika
kurejesha madaraka kwa
serikali ya kiraia.Unaonaje
wazo hilo? Akauliza Mark
Piller
“Ni mpango mzuri sioni
tatizo lake” akasema Jenerali
Akiki
“Ahsante kwa
kukubali.Kinachotakiwa ni
kuzusha vurugu kubwa nchini
Uganda zitakazolilazimisha
jeshi kutumia nguvu na
kupelekea umwagikaji
mkubwa wa damu na hii
itajenga chuki kubwa kati ya
utawala wa kijeshi na
wananchi.Jumuiya ya
kimataifa haitakaa kimya
itapaaza sauti kuutaka utawala
wa kijeshi kuondoka na
kuachia madaraka kwa serikali
ya kiraia.Jenerali Akiki nataka
unisaidie mawazo ni namna
gani tunaweza kuchafua hali ya
amani nchini Uganda ili
tuweze kuidhoofisha serikali
ya kijeshi iliyokuondoa
madarakani?akauliza Mark
Piller.Jenerali Akiki alichukua
muda kidogo akatafakari na
kusema
“Kikubwa inachotegemea
serikali kwa sasa ni mafuta
ambayo yanaipatia Uganda
fedha nyingi sana.Tunaweza
kuwadhoofisha kwa kuondoa
chanzo hiki kikubwa cha
mapato.Kuna bomba la mafuta
ambalo linatoka Uganda
kwenda Tanga
Tanzania.Bomba hili
likilipuliwa nchi itakosa
mapato na watashindwa
kuendesha serikali.Nashauri
tuwadhibiti katika mafuta
mheshimiwa makamu wa rais”
akasema Jenerali Akiki
“Jenerali Akiki tukilipua
bomba la mafuta linalokwenda
Tanzania bado hatutakuwa
tumefanya kitu.Ninachotaka
mimi ni kuleta machafuko
nchini Uganda ambayo
yatapelekea vurugu kati ya
jeshi na wananchi.Nataka
damu imwagike” akasema
Mark Piller.Jenerali Akiki
akamtazama Mark kwa muda
halafu akasema
“Mark Piller nimekueleza
ukweli wangu wote kwa nini
nimepinduliwa.Nataka nawe
unieleze ukweli.Kwa nini
unataka itokee vurugu
Uganda? Ni kweli vurugu hizo
unazozizungumzia ni kwa ajili
ya kuidhoofisha serikali ya
kijeshi au ni kwa maslahi
yenu? Akauliza Jenerali Akiki
“Jenerali Akiki
usizungumze kuhusu ninyi bali
sema ni kwa maslahi
yetu.Wewe tayari ni mmoja
wetu na kwa kuwa u mmoja
wetu nitakueleza ukweli” Mark
Piller akanyamaza kidogo
halafu akasema
“Nchi ya Uganda ina
mafuta mengi mno kuliko nchi
nyingine yoyote Afrika.Akiba
ya mafuta ya Uganda
iliyogunduliwa ni kubwa sana
kuzidi hata zile nchi
zinazofahamika kwa uzalishaji
mkubwa wa mafuta.Unaonaje
kama tukichukua kiasi kidogo
cha mafuta ya Uganda na
kuongeza katika akiba yetu ya
mafuta? Akauliza Mark
Piller.Jenerali Akiki akafikiri
kidogo kisha akasema
“Mheshimiwa makamu wa
Rais sasa nimepata picha
nzima kuhusiana na haya
mazungumzo yetu.Kila kitu
tulichokizungumza hapa
msingi wake ni mafuta ya
Uganda”
“Ndiyo Jenerali Akiki”
akajibu Mark Piller na ukimya
ukapita
“Usiogope Jenerali
Akiki,tayari wewe ni mwenzetu
na kiasi kidogo cha mafuta
tutakachokichukua na
kuongeza katika akiba yetu ni
kwa ajili ya ndugu zako
wamarekani.Ukiwa kama mtu
mwenye mchango mkubwa
katika jambo hili utanufaika
sana.Utaishi maisha ya
kifahari sana hapa Marekani
yenye hadhi yako.Umefanya
kazi kubwa sana katika nchi
yako,umeiweka Uganda
ikaonekana katika ramani ya
dunia lakini hakuna thamani
yoyote unayopewa,hata mali
zako zimechukuliwa na lengo
lao ni ili uishi maisha magumu
ya taabu.Hustahili kutendewa
hivyo.Hapa Marekani
tunakuthamini na utaishi
mazuri yaliyojaa amani na
furaha.Hutatamani tena
kurejea Afrika” akasema Mark
“Mheshimiwa makamu wa
Rais hilo unalotaka nilifanye ni
usaliti mkubwa kwa nchi
yangu na bara la afrika.Huo ni
unyonyaji mkubwa” akasema
Jenerali Akiki na maneno yale
Mark Piller hakuonekana
kuyapenda
“Jenerali Akiki,kauli kama
hizo zilizungumzwa miaka
mingi na viongozi wazalendo
kwa bara la Afrika mfano Rais
wa kwanza wa Tanzania Julius
Nyerere na wengineo ambao
walikuwa na uchungu wa kweli
na bara la Afrika lakini kwa
wewe hupaswi kutamka
maneno kama hayo.Hauna sifa
hiyo ya uzalendo kwa nchi au
bara lako.Umemfadhili James
Kasai kiongozi wa waasi
ambaye aliua watu
wengi.Kiongozi mwenye
uzalendo kwa bara lake hawezi
akafanya kitu kama
hicho.Ulishiriki katika mpango
wa mauaji ya maraisi
wenzako,kiongozi mzalendo
huwezi ukafanya jambo kama
hilo.Jenerali Akiki hivi sasa
hauna kitu chochote,hauna
mahala pa kwenda na hakuna
nchi wanayoweza
kukupokea.Serikali ya
marekani imekupokea kwa
mikono miwili na kukupa
makazi ya kama haitoshi
utapata mara mbili ya kile
ulichokipoteza baada ya
mapinduzi.Ni juu yako ukubali
au ukatae.Ukikubali utakuwa
raia wa Marekani na kufaidika
lakini endapo utakataa basi
hatutakuwa na namna
nyingine zaidi ya kukuruhusu
ukatafute hifadhi nchi
nyingine au tutakurejesha
Uganda.Chaguo ni lako
jenerali Akiki.Labda nikuweke
wazi kwamba Marekani
inapokea watu wale ambao
watakuwa na manufaa kwa
nchi.Kama nawe unataka kuwa
raia wa Marekani lazima uwe
na faida kwa nchi hii” akasema
Mark Piller na kumtazama
Jenerali Akiki
“Nini unakitaka Jenerali
Akiki? Unataka kuwa raia wa
Marekani au unataka kurejea
Afrika?akauliza Mark Piller
“Sitaki kurejea
Afrika.Nitaishi hapa
Marekani”
“Kama unakubali kuishi
hapa Marekani huna budi
kukubaliana na haya
niliyokueleza” akasema Mark
Piller
“Kama mpango ni
kuchukua mafuta basi vurugu
ndani ya Uganda pekee
hazitasaida kufanikisha
mpango huo.Bomba la mafuta
linaanzia Uganda na kwenda
katika bandari ya Tanga nchini
Tanzania.Ili mpango huo
ufanikiwe lazima eneo lote la
Afrika Mashariki liingie katika
machafuko ndipo itawezekana
kuchukua mafuta hayo katika
bandari ya Tanga” akasema
Jenerali Akiki
“Hapo sasa
tunazungumza.Ni vipi basi
tunaweza kuliweka eneo la
Afrika Mashariki katika
machafuko ili tuweze
kufanikiwa kudhibiti mafuta?
Akauliza Mark Piller
“Kuna njia moja tu
ambayo inaweza ikatumika
kuleta machafuko makubwa
katika eneo zima la Afrika
Mashariki” akasema Jenerali
Akiki
“Nakusikiliza Jenerali
Akiki.Ni jambo gani hilo?
Akauliza Mark Piller
“Ni kwa kutumia dini”
“Dini?
“Ndiyo.Tukitumia dini
inaweza ikaleta machafuko
makubwa si Uganda peke yake
bali eneo lote la afrika
Mashariki”
“Hebu nifafanulie namna
dini inavyoweza ikaleta
machafuko Uganda na Afrika
mashariki” akasema Mark
Piller
“Kiongozi mkuu wa
waislamu nchini Uganda
atauawa na watu
wasiojulikana.Baada ya mauaji
hayo,tutazungumza na kikundi
cha kigaidi cha IS ambao
watafanya mashambulio ya
mabomu katika makanisa na
mashule yanayomilikiwa na
dini ya kikristu.IS wataeleza
kwamba mashambulio hayo ni
ya kulipiza kisasi kwa mauaji
ya kiongozi mkuu wa waislamu
nchini Uganda” akasema
Jenerali Akiki
“Subiri kidogo Jenerali
umesema kuhusu kushirikiana
na kikundi cha kigaidi cha IS?
Akauliza Mark Piller
“Ndiyo mheshimiwa
makamu wa Rais !
“Hilo
haliwezekani.Marekani katu
haiwezi kushirikiana na
magaidi kwa namna yoyote
ile.Magaidi ni maadui zetu na
tunawasaka kwa udi na
uvumba kila mahala walipo na
kamwe,narudia tena kamwe
hatuwezi kushirikiana nao
katika jambo lolote”
“Kama mnahitaji mafuta
ya Uganda basi mashirikiano
na IS ni kitu cha lazima.Si IS
pekee bali kikundi chochote
cha kigaidi iwe Alshabaab au
Boko Haram” akasema
Jenerali Akiki
“Hebu nieleze namna
unavyotaka kuwatumia IS
katika suala hili”
“Kama nilivyo tangulia
kusema kwamba kikundi ha IS
kitashambulia makanisa na
shule za taasisi za kidini na
kusababisha vifo
vingi.Tutamtafuta mtu ambaye
atatumika kuchochea na
kuwapandisha hasira wakristu
ili wakalipize kisasi kwa
waislamu na hapo tutakuwa
tumepanda mbegu ya chuki
kwa waumini wa dini hizi
mbili.Machafuko ya kidini
yakianza ni kama moto wa
petroli,jeshi halitaweza
kuyazuia.Yatasambaa nchi zote
za Afrika mashariki”akasema
Jenerali Akiki
“Lakini uislamu
haukubaliani na matendo ya
kigaidi.Watakanusha kwamba
waliofanya mashambulio hayo
katika makanisa na misikiti
hawauwakilishi uislamu”
akasema Mark Piller
“Ni kweli. Lakini maelezo
watakayoyatoa baada ya
mashambulio hayo
hawatajitaja kuwa ni kundila
IS bali watasema ni kikundi
cha waislamu”
“Hilo ni wazo zuri pia.Ni
vipi kama akristu
hawatachukuah atua zozote
baada ya mashambulio hayo
kutokea katika nyumba zao za
ibada?akauliza Mark
“Hapa kuna watu ambao
lazima tuwatumie ili kuamsha
hasira kwa waumini wa dini ya
kikristu na kuchochea
machafuko.Kuna mwanasiasa
mmoja anaongoza chama cha
upinzani ambaye
tutazungumza naye na yeye
ndiye atakayewapanga
viongozi wa dini
watakaowachochea waumini
wao kuanzisha mashambulizi
dhidi ya watu wa dini
nyingine.Hawa nao lazima
muwape hifadhi hapa
Marekani.Baada ya machafuko
wataondoka Uganda na kuja
huku kimya kimya huku
wakiacha moto ukiendelea
kuwaka Uganda”
“Hilo halina tatizo.Lazima
wataangaliwa kwa namna ya
kipekee kabisa” akasema Mark
Piller
“Machafuko haya
yatakuwa makubwa
yatasambaa katika miji
mingine ya Uganda na
hatimaye nchi nzima.Uganda
ikiingia katika
machafuko,tutahamia Tanga
Tanzania.Ili kuweza kuchukua
mafuta lazima jiji la Tanga
liingie katika machafuko
pia.Nina uhakika mkubwa
sana kama tukitumia dini
kuwagombanisha wakristu na
waislamu basi machafuko
yatakuwa makubwa na damu
itamwagika.Machafuko
yatakapokuwa makubwa
mtakuwa mmepata kigezo cha
kupeleka majeshi yenu Afrika
Mashariki kwa lengo la
kulinda amani na mtafanikiwa
kuchukua kila mkitakacho
lakini ili mpate sababu ya
kutosha ya kupeleka wanajeshi
Afrika Mashariki kuna jambo
lazima lifanyike ambalo sina
hakika kama mtakubaliana
nalo”
“Jambo gani Jenerali
Akiki? Akauliza Mark Piller
“Ubalozi wa Marekani
ulioko Kampala inabidi
ulipuliwe”
“Kulipua ubalozi wa
Marekani?! Mark Piller
akashagaa
“Ndiyo Mark.Lazima
iwepo sababu ya kupeleka
wanajeshi Uganda na Afrika
mashariki hivyo ili kuongeza
uzito lazima ubalozi wa
Marekani Kampala ulipuliwe
na raia wa Marekani kuuawa”
akasema Jenerali Akiki.Mark
Piller akafikiri kidogo halafu
akasema
“Sawa nitaunda timu
maalum ya kulishughulikia
suala hilo”
“Mtu ambaye
atahamasisha machafuko
kutokea anaitwa Joshua
Lulangwa.Huyu ni
mwanasiasa anayeongoza
chama cha upinzani
kijulikanacho kama chama cha
ukombozi wa Uganda.Huyu
ndiye atakayewaandaa
viongozi wa dini ambao
watahamasisha wafuasi wao
kushambuliana.Ataandaa
kiongozi mmoja mwenye
ushawishi upande wa wakristu
na mwingine upande wa
waislamu.Narudia tena hawa
watakaochochoa machafuko
mnatakiwa muwape hifadhi
Marekani.” akasema Jenerali
Akiki
“Hilo halina tatizo Jenerali
Akiki tutalitekeleza” akasema
Mark Piller.
KISIWA CHA
VITI LEVU – FIJI
Baada ya matembezi
marefu katika msitu mnene
Mathew Mulumbi na Najma
walirejea kupumzika katika
hoteli walikofikia.Mara tu
walipofika mapokezi Mathew
akajulishwa na muhudumu wa
mapokezi kwamba wakati
wamekwenda kutembea
msituni kuna mtu alifika
kumtafuta.Mathew alistushwa
kidogo na taarifa ile hakujua
nani aliyekuwa
anamtafuta.Hakufahamiana
na mtu yeyote katika kile
kisiwa kwani walikuwa na siku
tatu tu toka wamefika katika
kisiwa kile kwa mapumziko.
“Hakutaja jina lake huyo
mtu aliyekuja kunitafuta?
akauliza Mathew
“Hapana hakutaja jina lake
ila alisema atarejea tena
baadae” akasema Yule
muhudumu kisha Mathew
akaelekea chumbani kwake
“Abu kuna nini alikuwa
anakwambia Yule mwanadada
wa mapokezi?akauliza Najma
ambaye alimuacha Mathew
akizungumza na muhudumu
wa mapokezi akaelekea
chumbani.
“Alikuwa ananipa taarifa
kwamba kuna mtu alikuja
kunitafuta” akasema Mathew
“Nani huyo aliyekuja
kukutafuta? Hakutaja jina
lake? Kuna mtu unafahamiana
naye hapa?
“Hakutaja jina
lake.Nashangaa kwa kuwa
hakuna mtu anayetufahamu
huku ugenini.Tutamfahamu
mtu huyo kwani aliahidi
kurudi tena baadae” akasema
Mathew kisha wakaoga na
kwenda kupata chakula cha
mchana.
Kwa muda wa miezi
mitatu Mathew na mpenzi
wake Najma wamekuwa katika
mapumziko wakizunguka
sehemu mbali mbali duniani
kutalii.Baada ya kurejea
kutoka Dar es salaam ambako
alifanikiwa kumuua james
Kasai na Khalid Sultan
Khalid,Habiba Jawad kwa
kufurahishwa na kazi
aliyoifanya Mathew alimtaka
yeye na Najma wakazunguke
sehemu mbali mbali duniani
kwa muda wa miezi minne ili
kuweka akili sawa kabla ya
kuingia katika misheni
nyingine.Kwa kipindi cha
miezi mitatu Mathew na
Najma wamekuwa
wakizunguka sehemu mbali
mbali duniani wakifanya
utalii.Walifika sehemu nyingi
maarufu kwa utalii duniani na
siku tatu zilizopita walifika
katika kisiwa cha Fiji
wakiendelea na mapumziko
yao.Kwa muda huo wa miezi
mitatu Mathew Mulumbi
alijitahidi kujiweka mbali na
runinga au simu.Hakutaka
kutazama au kusikia kitu
ambacho kingeweza kuharibu
mapumziko yao.
Baada ya kupata chakula
walirejea chumbani kwao
kupumzika kabla ya jioni ya
siku ile kwenda katika
matembezi ya miguu
ufukweni.
Saa moja za jioni walirejea
hotelini ndipo walipokutana
na Yule mtu aliyekuwa
akiwatafuta.Ni mmoja kati ya
walinzi wa Habiba Jawad
wakamkaribisha katika
chumba chao kikubwa
“Tulijiuliza sana
tulipoambiwa kuna mtu
amekuja kutuulizia kwani
hatuna mtu tunayefahamiana
naye hapa Fiji” akasema
Mathew
“Hata mimi nilijua
mtastuka na sikutaka kutaja
jina langu makusudi ili
kuwastua” akasema Malik na
wote wakaangua
kicheko.Chakula kikaletwa
wakala na maongezi rasmi
yakaanza
“Abu Zalawi nimetumwa
na mama Habiba anawahitaji
mrejee nyumbani.Amenituma
niwaombe samahani kwa
kukatisha mapumziko yenu”
akasema Malik
“Kuna tatizo
ganinyumbani?akauliza Najma
“Hakuna tatizo lolote
lakini amenituma hivyo”
akasema Malik
“Kama hakuna tatizo kwa
nini mama anatusumbua
katika mapumziko
yetu?akauliza Najma
“Hajatusumbua kwani
tumekuwa na mapumziko
marefu sana.Kwa miezi mitatu
tumekuwa angani na majini
tukistarehe.Ni wakati wa
kurejea nyumbani” akasema
Mathew
“Tunaondoka usiku
huu.Ndege iko tayari uwanja
wa ndege wa Nadi kwa ajili ya
kuelekea Saudi
Arabia”akasema
Malik.Hakukuwa na muda wa
kupoteza Mathew na Najma
wakaanza kujiandaa kwa ajili
ya kurejea Saudi Arabia japo
Najma hakuonekana kufurahia
kuondoka mapema kisiwani
Fiji.