RIWAYA: Siku ya graduation

RIWAYA: Siku ya graduation

SEHEMU YA 13

Tulibaki mule ndani Mimi na Ntahondi, japo nilikua nimefarijika kiasi lakini sikua na amani kabisa maana kengere ya hatari ilikua imeshagonha ndani ya kichwa change, haikuhitaji msaada wa Profesa wa chuo ikuu cha Havard kuja kukuambia kua Pablo aliku ni mtu hatari sana, na kwakua ameshafanikiwa kutoroka sasa itakua ni Mtanange kumpata maana nae sio mjinga kihivyo lazima atajihami kwa umakini wa hali ya juu sana japo Honde ametupa majibu ya uhakika kua atapatikana tu..
Siku hiyo iliisha kimya kimya tukiwa zetu chumbani tukipiga Story na hatimae usiku ukaingia, wahudumu wa humu kwa Mhe Waziri walikua makini kwa kila hatua, pia walikua wakarimu sana, mara kwa mara walikuja kujua usalama wetu mule ndani, na kila muda wa chakula ulipowadia walikua wanakwenda na muda vilivyo,
Baada ya kupata chakula cha usiku, tuliingia kuoga na hatimae tukarudi kulala tu, Ntahondi alionekana kuchoka sana hivyo mapema tu akawa ameshapitiwa na usingizi, lakini hali ilikua tofauti kwangu, Usingizi wote uliparama, nikawa nahesabu tu Paa, mpaka saa saba usioku ndo kwa mbali usingizi ukailainisha mishipa ya kichwa changu na ndani ya muda nikawa nakoroma!!
Asubuhi na mapema ya siku iliyofuata nilikua wakwanza kuamka licha ya kuchelewa kulala mapema, nikaoga haraka haraka, nikamuamsha na Ntahondi nae akaenda kujiswafi mwili, akili yangu ilikua na wahka wa kutaka kujua hatma ya Pablo hivyo nilikua nikisubiri miadi ya Honde kua name nitaenda katika zoezi adhimu la kumkamata Mafia Pablo Mwaki, baba mzazi wa aliekua mchumba wangu Ramla, baada ya Ntahondi kupata maji alijumuika name pale katika meza ndogo kwa ajili ya kupata ‘Stiftahi',
Tulipata kifungua kinywa kile murua tulichoandaliwa na baada ya hapo tukawa sasa tunamsubiri tu Honde
"Na mimi si nitaenda?" aliniuliza Ntahondi
"No.."
"kwanini?"
"Hii imeshakua vita mama, kaa tu utulie usije ukatekwa bure ukaniacha pabaya mimi, jana tu nilitaka kua chizi niliposikia umetekwa"
"Kwahiyo we unavyotaka kwenda huko ukitekwa utakua umeniacha mimi pazuri?"
"Tuachane na hayo, hivi unajua mie simuelewi kabisa Mwl Honde anaonesha dalili za kua nae ni afisa usalama, au we haujashtukia?"
"Kweli mie tangu jana najiuliza maana ujue ni yeye ndie aliekuja na hao vijana anaosema ni maofisa mpaka pale kwenye Tax wakatuteremsha haraka haraka, na wakati nashuka kwenye tax nikaangusha simu chini sasa Honde alipoinama kuiniokotea nikaona ana mguu wa kuku kiunoni"
"Wee, usiniambie!!" "Sure, jamaa Shushushu huyu, haiwezekani mdogo wake tu na waziri mkuu ndo ajue mambo nyeti kiasi hicho chote" "Mhh, mama ya Ngoswe.."
Tuliendelea kubadilishana Story mpaka tukachoka lakini Honde hakutokea, nikaanza kupata hofu, nikajaribu kumpigia kwa simu ya Ntahondi lakini hakupokea, tuliendelea kumsubiria bila mafanikio mpaka jioni ikaingia na giza lililoashiria kuingia kwa usiku nalo likatanda,
Tukaingia zetu kulala, basi hali ilikua hivyo kwa takribani siku nne mfululizo, tuliendelea kuishi mule ndani bila ya kupata mawasiliano ya Kaptain, Honde, wala mtu mwingine yoyote zaidi ya mawasiliano ya simu na baadhi ya ndugu zetu ili kuwatoa hofu juu ya Usalama wetu,
Baada ya siku kama tano hivi mbele ndipo Honde alikuja, kama kawaida yetu hua akifika tunaanza story za kila aina pia hua anatupa taarifa zilizopo huko nje kufuatia tukio zima
"Huko nje habari zimevuja kua Ntahondi anaolewa na Naufal, Ha ha ha mko juu.."
"Ha ha hiyo utakua umeitunga wewe maana hakuna aliewaambia hao watu" Honde na Ntahondi walikua wakitaniana, na mie nikatupia swali langu
"Kwa hiyo kuna habari gani za Pablo?"
"Habari za Pablo sio nzuri sana, kuna mawili, inawezekana ameshatoroka na kakimbilia Kenya ambako atajipanga ili apotelee Dubai nasikia ana mijengo kule, pili inawezekana akawa bado yupo humu nchini ila muda wowote atatokemea"
"Sasa nanyi maafisa usalama mmeshindwa kumtia nguvuni kweli?"
"Tafadhali Naufal, aliekuambia mimi ni Afisa usalama ni nani?"
"Ahh, samahani, kwa jinsi unavyopata data najihisi kama niko na mtu wa usalama"
"Ok jitihada zinaendelea kumsaka maana kama atafanikiwa kukimbilia ughaibuni huko na akajificha vizuri, sasa ataanza msako dhidi yenu ili awaue apoteze ushahidi ili hata akikamatwa kesi haitokua nzito sana kwake"
Maneno hayo ya Honde yalinipagawisha zaidi lakini sikua na cha kufanya,
"Kina Ramla na Yule Baunsa nao vipi?"
"Kesho ndo watapandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza kujibu tuhuma za kushiriki kuteka, kutesa, na kupanga njama za mauaji, Hii hawachomoki wale, japo namuonea sana huruma Ramla unajua tayari ujauzito wake unazidi kuchomoza sasa ndo anazidi kuishiwa nguvu"
"Ndo atakoma mshenzi Yule" alijibu Ntahondi kwa hasira
"Sasa ninyi asubuhi muwe tayari tayari kwa ajili ya kuhudhuria mahakamni na kasha baada ya kesi mtarudi huku, nadhani mnaweza kuwasiliana kina mama nao wakaja mkaonana pale mahakamani,
Tulipigasoga sana ili kuvuta muda hatimae Honde akatuaga, akaondoka, tukabaki na sisi tukiendelea kukaa ndani tu kama wafungwa
****
Hatimae siku ya kwenda mahakamani ikawadia, kama ilivyo ada tukawa tumeshaamka mapema na tuko tayari kwa kuhudhuria mahakamani, japo tulikua na hamu ya kuonana uso kwa uso na Ramla ili tumuoneshee kua Mungu ameanza kulipa lakini bado sikua na raha kabisa kwa kutopatika Pablo, haikua muda mrefu san asana ikafika gari nyeusi almaarufu kama Shangingi,
Akashuka Honde na vijana wengine wawili wakiwa wamevalia suti nyeusi, bila shaka nao ni kutoka kitengi cha TISS, Wakatuchukua na safari ya kwenda mahakamani ikaanza, ndani yadika kama thelathini za mwendokasi tulikua nje ya mahakama kuu, tukateremka na kuingia ndani huku tukiwa na watu hawa wa Usalama, tulipofika ndani ya mahakama tuingia chemba huko tukawa tumekaa kwenye viti vidogo vya mbao huku tukisubiri utaratibu, ndipo akaingizwa Ramla, na Yule Baunsa, nilipokutanisha nae macho nikamwambia
"Karibu Baunsa" nae hakunijibu kitu, sasa alikua amesharudiwa na Fahamu lakini alionekana kua mchovu sana nadhani alipewa kiminyo kikali zaidi, Kwan je ya Mahakama watu walikua wamefurika.
Kupitia dirisha dogo niliweza kumuona Mama Ntahondi akiwa amesimama na mama yangu mimi, pia Ntahondi nae aliwatambua baadhi ya wanafunzi wenzao wa IFM, tulipokua mule ndani akawasili Kaptain John Makala, akawa anasalimiana na makarani kisha akaja uswa wetu nasi tukasabahiana nae kwa furaha, na baada ya mawili matatu akamtoa faragha Mwl Honde, sikujua walichokwenda kuongea kwani baada ya muda akarudi Honde peke yake nikamuwahi kwa swali
"Vipi mbona ameondoka?"
"Inasemekana Pablo ndo anataka kutoroshwa muda huu ndo nae anaenda kwenye msako"
"Kwahiyo sisi hatuendi tena?"
"Haina haja sana" Tuliendelea kukaa plae mahakamani kwa muda mrefu bila kesi kusomwa, ikawa ni stori tu baina yetu mpaka nilipochombeza ile habari yangu ya kuokota ile Flash ya Pablo kule ndani ya gari, nilidhani kua jambo lile ni la kwaida sana lakinikumbe ilikua tofauti maana Honde alishtuka na kuniuliza kwa msisitizo "Una uhakika aliiangusha yeye?"
"Ndio.."
"Mbona hkusema muda wote huo?"
"kwani ina nini?"
"Itakua kuna data za muhimu sana mule, we have to do something right now" Honde akatoa simu na akawa anaandika massage kwa muda mrefu na muda mfupi baada ya kumaliza kutuma ujumbe huo,
Simu yake ikaita akapokea na kuongea nakawaelewa kua walikua wakiiongelea ile Flash na kasha akanigeukia mimi
"Eti hiyo Flash iko wapi?"
"Iko kule tunapolala" Baada ya mazungumzo ya Honde na huyo mtu kwenye simu kumalizika alikata simu na kurusi kwangu sasa
"Aisee hiyo Flash ni ya muhimu sana, Kaptain Makala yuko njiani anakuja kutuchuku mimi na wewe tunaenda kuiangalia hiyo flash ila Ntahondi atabaki hapa hapa" Ntahondi alikua akitusikiliza muda wote wa majibizano yetu, nae aliafiki bila kipingamizi kua atatusubiri pale pale mahakani..
Muda mfupi tukaiona gari ile aliyokuja nayo mwanzo Kaptain John Makala lakini alikuwemo dereva tu, tukatoka nje na kuingia ndani ya gari na safari ikaanza, tukarudi kule nyumbani kwa Mhe Waziri,
Tulipofika tu tukawakuta vijana watatu wakiwa wamevaa suti nyeusi, kati yao akiwemo Kaptain Makala ambae baada tu ya kutuona alituonesha kwa ishara kua tufanye hima na haraka, ikabidi tuingie mule ndani kwa mtindo wa Joging, nilipofika Sebuleni maofisa wale wote wakatangulia juu ya meza ambako tayari walikua na Kompyuta ndogo ambayo walikua wameiweka tayari kwa kazi, mie nikaingia ndani kuchukua hiyo Flash, nyuma yangu akinifuata Swahiba wangu Mwl Honde mpaka chumbani,
Nilipofika ndani nikaenda moja kwa moja mpaka kitandani, nikaivuta droo ya kitanda ili nichukue hiyo flasha, nikapigwa na bumbuwazi baada ya kukuta flasha haimo, mikono yangu ikaanza kutetemeka huku ikivuja jasho la uoga, nikainuka haraka na kwenda kwenye Pochi ya Ntahondi aliyoining'iniza juu kiti kidogo kilichomo mule chumbani, nikafungua zipu ya katikati lakini nako Haipo!! Nilizidi kuchanganyikiwa, ghafla Honde nae akanichanganya "Vipi wewe, unaleta upuuzi"
"Hapana Honde siioni flash na niliiweka kwenye droo ya Kitanda"
"Sasa hii unataka kujiletea tabu, unadhani jamaa atakuelewaje?" Sikumjibu kitu Honde, nikafungua katika zipu ya pembeni, pia Haikuwemo!nikawa kama kichaa, nikajikuta najiuliza mwenyewe
"Nani kaichukua sasa?"
"Unaemuuliza nani?" alinihoji Honde, sikumjibu, nikafungua zipu ya upande wa kulia, Nikashusha pumzi, nikaingiza mkono kisha nikaitoa Flash, bila shaka itakua ni Ntahondi ailkua ameihifadhi mule, Honde akanisogelea haraka ili aichukue, hapo hapo namie nikamuuliza "Nini?.."
"Lete haraka twende na muda" "We sio afisa usalama wa taifa, sasa nikupe kama nani?, au amekubali kua nawe ni mmoja wao?" Nikamuachia tabasamu lilionesha kuzidi kumkera halafu mie nikatoka zangu mpaka pale sebuleni, nikaenda moja kwa moja na kumkabidhi Kaptain Makala, nae bila ajizi akaenda moja kwa moja mpaka kwenye Kompyuta yake halafu akaichomeka flash ile na kuanza kuperuzi..
Sikujua Kaptain alikua akiona nini maana kila mara alikua hatulii, yaani utadhani kiti kina miba, inaonekana alikua akiona mambo makubwa nay a ajabu katika kompyuta yake,
Ghafla akamuita Honde na kumuonesha kitu katika Kompyuta yake, Honde nae alipayuka kwa sauti ya mshangao huku akitaja jina la Mhe Kigwaza huku akiitumbulia macho ile Computer, name pia nilishtuka kusikia jina lile maana nilimjua alietajwa, Mhe Andrew Kigwaza,
Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga taifa, Sasa amefanyaje? Sikupata jibu nikiwa sijaelewa kinachoendelea ndani ya Laptop ile tena likatijwa jina jingine lilizidi kunipa hamu na kiu ya kutaka kujua kilichomo
"Johari Kijukuu" alitamka Kaptain, nililijua vema jina hili kwani lilikua ni jina la Jaji aliepangwa kusimamia kesi yetu sasa kama nae ameonekana kua ni mmoja kati ya wana mtandao wa Pablo sijui itakuaje!!,
Wakati wakiendelea kusoma na kupereuzi ndani ya kompyuta mpakato hiyo ghafla Kaptain akainuka na kupiga meza kwa nguvu kisha akasema kwa sauti "Pasword yake hii hapa kaificha huku mshenzi huyu, baada ya hapo akaingiza mkono mfukoni akatoka Modem ya Internet halafu akaipachika kwenye Kompyuta na kuanza kuunganisha mambo pale, Baada ya muda nrefu wa kuperuzi na kudadisi Kaptain alishtuka ten asana, bila shaka alipata jambo jingine kubwa zaidi, akasimama tena pale kwenye kiti, halafu akasema
"Mungu wangu tutwahi kweli!!"
"Wapi?"
"Air port, huyu mshenzi anaondoka asubuhi hii kwenda Kenya na ndege ya Shirika la AMNOINA, Ndege ya MHZ 6453 Ndo wanayoitumia"
"Kwahiyo tunafanyaje?"
"Haraka tuondokeni tujaribu kuwawahi" aliposema tu hivyo haraka tukatoka nje na kuingia kwenye magari yetu mawili yaliyokua yameegeshwa pale Nje, tukaondoka kwa kasi ya ajabu kuelekea Airport, tulipokua njiani nilimsikia Kaptain akimuambia Honde apige simu ofisi kuu ya usala kuomba nguvu ya ziada pale uwanjani, tulitembea mwendo wa farasi, mwendo wa kasi, na dakika chache mbele tulikua katika Viunga vya Mwl Julius Nyerere Intanational Airport,
Gari ziliposimama tu tukashuka haraka, nikamuona Kaptain akiikimbilia ndege moja iliyokua ndo kwanza inaiacha ardh na kupaa juu, wote tukamkimbilia mpaka pale lakini haikusaidia kitu MHZ6453 Ilikua ikipotelea hewani,
Abiria wengi walitaharuki wakawa wanakimbia hovyo nadhani walihisi kua sisi ni majambazi au magaidi, tukarudi mpaka pembeni kidogo kulikua na Abiria wa kike kama watano hivi wakiwa wamesiamama na Jeneza lao pembeni huku wakilia, bila shaka walikua wakisafirisha maiti,
Walikua wakiongea kwa lugha ya kingerza, kitu kilichonifanya nijue kua sio watAnzani, Na hata nilipoangalia Lile Jeneza walikua wamelifunika na Bendera ya Ghana, lakini ghafla nikamuona Kaptain akinisogelea na kuniambia nitangulie ndani ya gari, haraka nikawahi kwenye gari, nilipoingia tu nilishangazwa na nilichokiona pale nje,
Kaptain na vijana wake waliwavamia wale wafiwa na kuanza kutembeza kichapo cha nguvu ghafla wakalipitia lile jeneza wakaja nalo kwa kasi mpaka kwenye Gari yetu wakaliingiza nao wakapanda haraka ki dereva akawasha gari tukatoka kwa kasi eneo lile la uwanja wa Ndege
Llikua ni tukio la jabu sana kwa abiria na hata kwangu pia, sikujua kilichofanya Kaptain afanye jambo lile bay asana, basi tukashika kasi barabarani, lakini haikua kazi rahisi maana tayari askari wa pale uwanjani walikua wakitufukuzia kwa kasi huku wakiturushia risasi,
Mji mzima ulichafuka kwa mashambulio yale, Tuliendelea kukimbia mpaka hatimae tukaingia katika viwanja vya mahakama kuu, tukateremka haraka na hapo hapo vijana wa Kaptain wakaliteremsha lile Jeneza na Kaptain akawapa maelekezo vijana wake tukaingia nalo jeneza lile mpaka ndani,na muda huo tayari askari waliokua wakitukimbiza nao walifika mahakamni pale,
Sisi tukaingia mpaka ndani tukakuta watu wengi sana wamejaa kusikiliza kesi, tayari Ramla, Baunsa na baadhi ya viongozi wa jeshi la Polisi wakiwa wamesimamishwa kizimbani huku kesi iikiendelea mbele ya Jaji Johari Kijukuu, ikabidi Mahakam nzima itulie tulivyoingia, ikawa kimya, mara na wale Askari nao wakaingia mpaka ndani.
"Kuna nini?" aliuliza mmoja katika wazee Fulani waliokua wameketi chini ya Jaji, Kaptain hakuwajibu, akienda mpaka kwenye Jeneza hilo na kulifungua
TOBAAAAA
Alikua ni PABLO MWAKI
"Alikua akijaribu kutoroka Airport kwa njia hii ya kujifanya ni maiti, tumemkamata kwa ushirikiano wa maofisa wa Polisi wa pale uwanjani" aliongea kwa kujiamini Kaptain Makala.
Hapo ndipo nilipomvulia kofia Kaptain Makala, sikuamini tukio lile, nilijiuliza mara mbili kua aligunduaje mchezo ule,
Mahakama nzima alishtuka, haraka Mwaki akainuliwa, yeye mwenyewe hakuamini alichokiona, alikua akihema kwa mshangao na Aibu, na hopo sasa Mhe Jaji akaaihirisha kusikiliza kesi hiyo na kupanga tarehe nyingine tena ili kupata utulivu wa tukio hili, japo tulishajua kua hata yeye Johari nae ni katika wafuasi wa mtandao wa mwaki lakini tulimvutia tu Pumzi kwa ajili ya kujipanga kimapambano,
Watuhumiwa wote wakakabidhiwa kwa Askari magereza na msafara wa kwenda KEKO ukaanza huku wahudhuriaji wakitawanyika kwa mshangao na gumzo waliloliona mahakamani, Na mien a Ntahondi tukarudi kwenye gari zetu maalumu kwa ajili ya kurejea mafichoni kwetu!!!

Je nini kitaendelea?
Usikose mwisho wa riwaya hii ya kusisimua..

Ngekewa ram angelca chacha patrick showtie amina mabata mlyn Angelicious culbby muuza ubuyu princetx Giti VAN HEIST Mng'ongo chwechinyong Sangomwile
 
mkuu Casuist asante sana sasa nioge niende kwwnye ngoma za kinyakyusa ipelo huko
 
Last edited by a moderator:
SEHEMU YA 13

japo tulishajua kua hata yeye Johari nae ni katika wafuasi wa mtandao wa mwaki lakini tulimvutia tu Pumzi kwa ajili ya kujipanga kimapambano,
Mkuu Casuist, Naufal nae amefuata nyayo za akina Mw. Honde? Yaani nae amekuwa afisa usalama?
Hata hivyo ni raha kweli kufuatilia Riwaya hii!
 
Casuist lete uhondo bana, nimekukubali kwa mavituzi.
 
Last edited by a moderator:
aiseeeeee... patamu hapooo... nasikitika kuona kwamba inakwishaaaa
 
Uko juu mkuu Casuist
Hii riwaya ingetengenezewa movie ingekubalika kimataifa aise!
 
Last edited by a moderator:
Imetulia, huko keko wawe macho tu na huyo mtuhumiwa
 
RIWAYA: SKU YA GRADUATION
MTUNZI: MAUNDU MWINGIZI


SEHEMU YA 14

Hatimae ikafika siku iliyokua ikisubiriwa na wengi, Siku ya kumaliza mzizi wa fitna, Siku ya hukumu, Mji mzima ulijawa na shauku ya kutaka kujua kitakachojiri siku hiyo, Kesi nzito hii ilikua imeshawakalia pabaya Pablo Mwaki na washirika wake ambae ni Ramla, Baunsa, na baadhi ya watumishi wa serikalini ambao hawakua waadilifu,
Kesi kubwa ni Kuteka, kutesa, kupanga njama za mauaji dhidi yangu mimi na Ntahondi, Kutekeleza mauaji ya yule dereva Tax, Pia kulikua na kesi zingine nyingi sana zilizokua zikimkabili Pablo ikiwemo ile ya kumuua yule mfanya biashara ambae inasemekana ndio msingi wa utajiri wa Mwaki, pia kujishughulisha na uuzaji wa madawa ya kulevya nchini, na kwa maelezo niliyodokezwa na Mwl Honde ni kwamba tayari Naibu waziri wa ulinzi ameshakamatwa na mpaka sasa yuko chini ya ulinzi kwa kutumia nafasi yake kama kiongozi wa serikali kujihusisha na vitendo viovu vya kutumia baadhi ya maafisa wa jeshi lake kuwadhuru watu, na pia kujihusisha na uuzaj wa madawa ya kulevya, Ushahidi wa kina umeshatimia baada ya kupatikana nyaraka kadhaa kwenye ile flash zikionesha ushiriki wao na mtandao wao mzima..
Kupitia katika upenyo wa dirisha dogo lililopo pale sebuleni niliweza kuona gari nyeusi aina ya Landcruise Vx ikiingia kupitia geti kuu kisha ikaenda kuegesha mbele ya mlango wa kuingilia ndani, punde wakashuka watu wane wakiwa wamevalia Suti nyeusi kila mmoja, kati yao alikuwepo Kaptain John Makala bila shaka hao wengine nao na vijana wake wa kazi, kutoka katika kitengo chake ndani ya Idara ya usalama wa Taifa, niliwajua tu kwa jinsi walivyoingia pale japo sura zao sikuwahi kuziona kabla, na kwakua tayari nilikua nimeshapewa taarifa na Mwl Honde kua wangekuja maofisa hao kwa ajili ya kutuchukua na kutupeleka Mhakamani, nikainuka haraka kutokea pale sebuleni nikakimbilia Chumbani kumita Ntahondi ili tuondoke, muda wote huo Ntahondi alikua kwenye Kioo tu akijremba na kujipodoa, wakati nimesimama Mlangoni namuita Ntahondi tayari Kaptain alikua ameshaingia sebuleni na hpo hapo akiniita kwa mbwembwe za kimombo "Hey.." "Yse Sir" name nilijibu kwa namna ileile aliyoitumia kuniita "Najua taarifa za ujio wetu mlikua nazo, are you ready?" Kabla sijamjibu chochote hapo hapo Ntahondi alitoka chumbani akawa amesimama karibu yangu pale katika mlango wa chumbani, hilo likawa ni jibu murua kwa Kaptain kua tupo tayari kwa safari,, Kaptain alimtupia Jicho Ntahondi, kisha akapepesea macho kwangu halafu akaachia tabasam maridhawa, Tabasamu lile lilikua na maana kubwa, maana ya kwamba hakika tulikua tumependeza sana!! Tukaanza kuongozana na kutoka nje kabisa ilipo gari, tukasalimiana na maofisa wale tuliowakuta pale nje kisha tukaingia ndani ya gari kwa ajili ya kuanza msafara wetu..
Ndani ya gari seat ya mbele alikua ameketi mkuu wa msafara Kaptain John Makala akiwa na dreva wake ambae bila shaka nae ni mtu wa usalama pia, Seat tatu za katikati alikua ameketi mmoja kati ya vijana hawa wa Makala, Ntahondi halafu Mimi, na Seat tatu za nyuma zote waliketi vijana hawa waliobakia, Gari ikatoka nje taratibu kisha ilipofika barabarani ikachukua kasi yake, huyu kijana aliekaa karibu na Ntahondi upande wake wa kushoto alikua akimuangalia sana Ntahondi, na nilipomchunguza niligundua kua alikua akimuangalia macho ya tama, macho ya kifedhuli, basi nikajikuta tu namchukia ghafla!!! Kaptain alionekana kujawa na furaha sana tofauti na ilivyo kawaida yake, yaani alishindwa kabisa kuzificha hisia zake, hisia za furaha, na punde akajidhihirisha furaha yake kwa kuanza kuongea tukiwa tunaendelea na dafari ya mahakamani "Thanks to God, Arobain za huyu mshenzi zimetimia" "Nadhani leo Nchi itazizima baada ya hukumu.." na mimi nikajibukwa furaha huku nikimtupia jicho la uchokozi Ntahondi , lakini ghafla nilishtushwa na jibu liliotokea katika seat ya nyuma waliyokaa hawa vijana "NI UPUMBAVU KUAMINI HIVYO!!" Nadhani hata Kaptain nae alishangazwa na jibu la kijana wake huyo, tuakajikuta sasa sot kwa pamoja tumegeuka nyuma kumuangalia
Looh salale!! Afanaleki!!
Sikuamini macho yangu, ilikua ni kama ndoto vile, yaani tulivyogeuka tu tulikutanisha macho yetu na mitutu mitatu ya bunduki kutoka kwa vijana hawa, sura zao zilikua zimeshabadilika kutoka katika ile hali waliyokua nayo mwanzo ya kistaarabu, na sasa alikua kama waliokunywa damu ya binaadamu, nikageuka mbele na kumuangalia Kaptain, lakini nae alikua ameshangaa sana hali ile na alionekana kujawa na hasira na woga pia, nikamsikia Kaptain akiwa tupia swali viajana hawa "Giggs nini tena mbona siwaelewi?" "Shutup Bitch.. Arobain za mwaki bado sana ila leo ni arobaini zenu ninyi" kijana alimjibu Mwaki kwa Wahka "Giggs Am I a bitch to you now?" "Funga bakuli lakao tafadhali takumiminia njugu sasa hivi" Kijana huyu aliendelea kutamba kwa maneno ya kebehi yaliyojaa dharau ya hali ya juu, vijana hawa walikua hawatanii, walionekana kumaanisha wanachosema, Wakati tukio lile likiendelea Ghafla na huyu Afisa mwingine aliekaa karibu na Ntahaondi nae akatoa Pistol yake na kumuelekezea Kaptain huku akitoa maelekezo kwa dereva "Geuza gari fasta tunaelekea Mwenge, ujanja wowote utakaothubutu kuufanya nitakisambaza kichwa chako, Sure I'll blow your ----in headoff" Gari ikageuza uelekeo na sasa tunakwenda Mwenge, sura ya captain ilipwaya na sasa hakua na ujanja tena maana amegeukwa na vijana wake mwenyewe, vijana wenye kujua mbinu hatari za mashambulizi, "Shika barabara ya Mwenge kisha moja kwa moja njia ya Bagamoyo, niliposikia tu Bagamoyo Moyo wangu ukafanya ‘PAA!!' HAPO HAPO NIKAMUONA Ntahondi akibubujikwa na machozi, bila shaka alikumbuka kua huko ndipo ilipo ile kambi ya Pablo ambako tuliteswa na kuponea chupuchupu kuuawa na sasa ndiko tunakopelekwa, Nilijua kua sasa tumefikia tamati, ‘ni lazima tuuwawe tu ili kupoteza ushahidi, amaa kwli niliamini maneno niliyoambiwa kua Pablo Mwaki ni hatari, yaani ana mtandao mpaka kwa maafisa wa usalama wa taifa' Nilijisemea mwenyewe!!
Wakati gari ikiwa imeshabadilisha uelekeo nikamuona Yule kijana aliekua akimuangalia sana Ntahondi akiingiza mkono katika mfuko wa koti lake na kutoa vitambaa vyeusi, akamsogelea Kaptain kwa umakini wa hali ya juu kisha akamfunga machoni, alipomaliza akahamia kwa Ntahondi nae akamfunga, halikadhalika na Mimi wakati huo wale waliopo nyuma yetu walikua bado wametuelekezea bunduki zao, Sasa tukawa hatuoni mbele wala hatuoni muelekeo wetu, Gari ilikua ikikimbia kwa kasi sana mpaka tunayumba Kimya kilitanda ndani ya gari, hapakua na sauti yoyote zaidi ya kilio hafifu kutoka kwa Ntahondi. Kilio kilichokatizwa na karipio kali kutoka kwa huyu kijana aliekua anamuangalia kwa uchu "KELELE WE MALAYA!! Kama una hamu ya kulia subiri tufike utalia mpaka utachoka, Leo tukifika utalala na mimi halafu kesho utalala kuzimu" Maneno haya yalizidi kuuchoma mtima wangu, na sasa nikapoteza kabisa bima ya matumaini
Baada ya mwendo kasi wa takribani saa moja hatimae Gari ilisimama, nikasikia tu mlango ukifunguliwa akashuka mtu sikujua ni nani, tuliendelea kutulia ndani ya gari ile karibu dakika kmi nzima ndipo nikasikia Sauti kali "SHUKENI NYIE NGURUWE PORI, Hi indo himaya ya PABLO MWAKI" Hapohapo nikasikia tu nimevutwa mkono na kuniteremshwa kwenye gari, nikashushwa kibabe kwelikweli baada ya hapo nikaanza kupelekwa kusipojulikana, machoni giza lilitanda kutokana na weusi wa kitambaa kilichoni tait machoni kisawasawa, kwa nyuma yangu nilisikia sauti ya Ntahondi akitonga na kutweta, roho iliniuma sana lakini sikua na cha kufanya, baada ya hatua kadhaa nilisimamisha kidogo halafu nikasika sauti ya mlango ukifunguliwa halafu nikaamriwa niingie ndani, nikaingia bila ya kujua nimeingizwa wapi, nikaongozwa mpaka sehemu Fulani nikaambiwa nisimame kisha Ntahondi nae alikuja mpaka ubavuni mwangu akasimamishwa, nilimjua tu kwa harufu ya marashi yake
Ilikua ni sehemu tulivu sana iliyotawaliwa na ukimya wa kuogofya mno, kwa juu usawa wa kichwani nilisikia mlio wa feni kubwa zikipepea, niakjua tu ni zile za ‘panga boi' Baada ya kusimama kwa dakika kadhaa, nilisikia mtu akinishika maeneo ya kisogoni, nikajua kua alikua akinifungua kitambaa, lakini kabla hajafanya hivyo nilisikia sauti kali, tena ya nguvu, ilionekana ilitokea kwenye Speaker kubwa mule ndani,
"SAPRAAAAAAAAAIZ"
Sauti hiyo ilifuatiwa na sauti kali za watu wakishagalia na kupiga kelele kwa wingi na hapo hapo nikafunguliwa kitambaa change usoni
"Oooh my God"
Nilijisemea mwenyewe kwa sauti, Sikuamini wala kuelewa kilichokua kikiendelea mule ndani, hakika nilistaajabu, kulikua na umati mkubwa wa watu wakiwa wana furaha kubwa, nilipomgeukia Ntahondi nae alionekana kua haamini kinachoendelea kutokea machoni, kwa kifupi tulikua kama Mazuzu tusiojua kinachoendelea. Nilipowageukia wale maofisa usalama niliwaona wote wakiwa wamesimama pembeni huku nao wakicheka kwa sauti huku wakipiga makofi Ghafla nikamuona mama yangu mzazi Bi Shammy akija kwangu na kunikumbatia huku akilia kwa furaha, huku nako namuona Ntahondi nae akikumbatiwa na mama yake kwa furaha kubwa, watu waliofurika ukumbini mule walikua wakiendelea kushangilia tu na kwa mbali Dj aliachia wimbo laini
Amaa kweli hii ni SURPRISE
Sasa Nilianza kupata picha kua hatukua tumetekwa bali ilikua ni mpango maalum wa kutuleta huku kwa mtindo wa kutushtukiza maana sasa nilianza kuwaona watu wengi niliowajua, nilimuona Mwl Honde akiwa ameshika Mic nadhani ni yeye ndie aliesema ‘Surprise', nikawaona baadhi ya rafiki zake na Ntahondi kutoka chuoni kwao, kwa mbali nikwaona wazee Fulani hivi na ndani ya dakika kadhaa nikawakumbuka, walikua ni wale wazee wa kule kijijini walikotuokoa na kumpigia simu Oscar, ukumbi ulijaa ndugu, jamaa, na marafiki, Furaha sasa name ilianza kutamalaki usoni mwangu japo nilijishangaa nikishindwa kujizuia na ghafla machozi yakawa yaanitiririka mashavuni Mama yangu akawa ananifuta, NDIPO sasa Mc Mr Honde akautuliza ukumbi uliokua bado umelipuka kwa shangwe, Akashika mic na kuanza kuongea huku sasa ukumbi mzima ukiwa kimya!!!
"Mabibi na Mabwana, Ndugu waalikwa wote, sasa huu ndio muda maalum tuliokua tukiusubiri kwa hamu na tayari vijana wenu wameshawasili ukumbini, Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kwamba Naufal na Ntahondi ni viajana waliojitengenezea histori ya kipekee kufuatia mkasa wa kusikitisha na kuumiza sana uliowakumba, japo waliumizwa nafsi na miili yao kwa kuteswa na kutwezwa lakini kwa ujasiri na jitihada walizozitumia kupambana na kujiokoa Mungu aliwasaidia na kuwaopnesha nja na hatimae leo tupo nao hapa, Hakika wameweza kuishinda nguvu kubwa ya fedhuli na nduli Pablo Mwaki, Kwa mliohudhuria jana mahakamani mlipata wakati mzuri kusikiliza mwenendo wa kesi ulivyokua, mlipata kujua uhalifu mkubwa uliokua ukifanywa na Mwaki na baadhi ya viongiozi serikalini ambao nao walitiwa nguvuni na kuhukumiwa pamoja, mlishuhudia PABLO A akihukumiwa adhabu ya kifo, na baadhi ya wapambe wake wakihukumiwa kifungo cha maisha jela, Pia mlishuhudia Ramla akihukumiwa miaka Tisini jela pamoja na kazi ngumu kutokana na kushiriki na kupanga njama chafu akiwa na Bwana wake Pablo amabe baadae imegundulika kumbe alikua ni bwana wake, najua kuna mengi ya kujifunza kwenye tukio hili kwa kila mwenye akili timamu, hivyo tumekutana hapa kwa pamoja kuwapa pole vijana hawa na kuwapongeza kwa ujasiri wao tangu mwanzo wa kesi mpaka iliposhia, sina haja ya kuirejea tena hapa kwa kua nilishaisimulia hapo awalai" Baada ya maneno hayo tena kwa mara nyingine ukumbi ulilipuka kwa nderemo na vifijo huku tukiwa tumekumbatiwa na wazazi wetu, sasa nilipata picha kua kumbe huku ilikua jana yake, japo sikujua kwa nini hatukupelekwa mahakamani, nikiwa bado natafakari, utadhani Honde alinisikia akaendelea kufungukua "Jana haikua rahisi kuwaleta vijana hawa mahakamani kwa sababu walikua wakiwindwa ili wauawe kupoteza ushahidi lakini kwa kua ushahidi ulikua umekamilika hivyo hiyo haikuweza kuathiri mwenendo wa kesi na hatimae hukumu kutolewa, sasa tukiwa tunajiandaa kuachia muziki laini huku mkipata vinywaji na maakuli napenda kutumia fursa hii kuwasemea jambo mjoa Naufal na Ntahondi" Ukumbi mzima ulitulia kimya kujua ni nini hasa tunataka kusemewa!!
"Ndani ya muda waliokua pamoka katika tabu hatimae vijana hawa wameamua kua pamoja kwa maana ya kua Mke na Mume, hivyo siku yaleo watajitambulisha kwenu kama wachumba, watavishana pete za uchumba, na kwa kua jambo hili wameliridhia wote kua wana nia ya kufunga ndoa hivyo basi Mhe Waziri Mkuu ambae ni kaka yangu mimi ametoa gharama zote za kumaliza shughuli ya ndoa yote hii ambayo tumepanga ifanyike Kesho katika ukumbi wa SEFLAVA" Ukumbi mzima ulilipuka kwa makelele ya kupongeza, nikamuona mama yangu anamsogelea mama yake na Ntahondi akamkumbatia, hapo hapo nasi huku tukakumbatiana huku waalikwa wakiserebuka muziki mzuri uliowekwa na Dj

Maundu Mwingizi, 2014


MWISHO!!!
 
mkuu hadithi ni nzuri na yakusisimia sana,pokea pongezi ila umetuacha kwenye mning'inizo kwani ingekuwa vzr ungeendelea had kwenye maisha mapya ya hao wanandoa,ni hayo tu mkuu
 
Back
Top Bottom