Riwaya: Saa za Giza Totoro

Riwaya: Saa za Giza Totoro

SEHEMU YA 24



ILIPOISHIA:
Sijui alitumia ujanja gani, nilishtukia tu mkono wake mmoja ukiwa umeshapenya na kuingia kwenye himaya ya ‘mkuu wa kaya’ na kumkamata, nikapatwa na mshtuko usioelezeka, mapigo ya moyo yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA...
“Tulia basi jamani, mbona unakuwa hivyo,” aliniambia baada ya kuona nimepoteza kabisa utulivu, nilikuwa nahangaika nikiwa hata sijui nataka kufanya nini, kimsingi nilipatwa na msisimko wa ajabu sana. Nilijitahidi kutulia kama alivyonielekeza lakini haikuwa kazi nyepesi.
Alichokifanya, alianza kunitoa magwanda mwilini mwangu, moja baada ya jingine mpaka alipomalizia la mwisho kabisa, na yeye akafanya hivyohivyo! Muda mfupi baadaye, tulikuwa saresare maua.
Aliniongoza nini cha kufanya na muda mfupi baadaye, tulikuwa tukiogelea kwenye bahari ya huba yenye kina kirefu.
Haukupita muda mrefu, nikaanza kutokewa na hali ambayo hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kunitokea, nguvu za mwili zikaongezeka na kunifanya na mimi niongeze kasi ya mchezo, sekunde chache baadaye tayari nilikuwa nimeshakwea kwenye kilele cha mlima mrefu kuliko yote barani Afrika, Mlima Kilimanjaro.
“Ndiyo mara yako ya kwanza eeh?” aliniuliza swali ambalo nilishindwa kulijibu zaidi ya kukwepesha macho yangu kwa aibu. Niliinuka na kwenda bafuni, nikajimwagia maji ambapo angalau akili zilirudi mahali pake, nilipotoka naye alienda kuoga na kurudi pale kitandani.
Kwa mara ya kwanza nilielewa maana ya mapenzi! Ile hofu niliyokuwa nayo ndani ya moyo wangu iliyeyuka na nikajikuta nikitamani kurudia tena na tena sanaa ile ya kikubwa, naye akawa ananipa ushirikiano wa kutosha na kunielekeza nini cha kufanya.
Mpaka tunakuja kulala, ilikuwa ni karibu saa nane za usiku, nikapitiwa na usingizi mzito kiasi kwamba sikuelewa tena kilichoendelea mpaka nilipokuja kuzinduka kukiwa kumeshapambazuka.
Harakaharaka aliamka na kwenda bafuni, akaoga na aliporudi, alijiandaa tayari kwa kuondoka. Nikachukua noti tatu za shilingi elfu kumikumi na kumpa.
“Hizi za nini?”
“Utanunulia mahitaji yako madogomadogo.”
“Aliyekwambia mimi nina shida na fedha zako ni nani? Au unafikiri najiuza?” aliniambia huku akikataa kuzipokea zile fedha. Akachukua mkoba wake mdogo na kuanza kutembea harakaharaka kuelekea kwenye mlango wa kutokea.
Nilibaki namsindikiza kwa macho huku moyo wangu ukiwa na furaha ya ajabu. Alipoondoka, nilienda kufunga vizuri milango, na mimi nikaenda kuoga kisha nikarudi sebuleni na kuwasha runinga, nikawa nachezeachezea simu yangu.
Kilichonishtua ilikuwa ni taarifa ya habari iliyokuwa inaoneshwa kwenye TV kuhusu tukio baya la ujambazi lililotokea Tandika kwenye tawi dogo la benki. Niliacha kila nilichokuwa nakifanya na kuikodolea macho runinga.
Mapigo ya moyo yalianza kunienda mbio baada ya kugundua kwamba kilichokuwa kinatangazwa lilikuwa ni lile tukio tulilolifanya jana yake. Mtangazaji aliendelea kueleza kwamba katika tukio hilo, watu kumi na moja wamefariki dunia, watano kati yao wakiwa ni askari wa jeshi la polisi, wanne walinzi wa kampuni binafsi waliokuwa wakilinda benki hiyo na wawili kati yao ni majambazi.
Nilishtuka sana kugundua kwamba kumbe watu wengi walikuwa wamepoteza maisha kiasi hicho, mwili mzima ukawa unatetemeka, habari zikaendelea kueleza kwamba katika tukio hilo, watu wengine sita wamejeruhiwa vibaya wakiwemo askari na walinzi ambao wote walikimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu.
Pia ilielezwa kwamba majambazi hao waliovamia gari la kubebea fedha kwa kushtukiza na kuanza kupiga risasi hovyo, walikuwa wamefanikiwa kupora jumla ya shilingi milioni mia moja na sitini za Kitanzania na kutokomea kusikojulikana.
“Ni tukio baya sana kuwahi kutokea katika siku za hivi karibuni, tulifanikiwa kuwaua wawili eneo la tukio na msako mkali unaendelea kuhakikisha wahusika wote wanapatikana na kurejesha kiwango hicho cha fedha zilizoibwa.
“Nawaomba wananchi watulie, nawahakikishia kwamba tunaendelea na uchunguzi na tutahakikisha wote waliohusika wanapatikana na kushughulikiwa ipasavyo,” kamanda wa polisi wa kanda maalum ya Dar es Salaam, alisikika akizungumza kutoka eneo la tukio, huku picha za video za eneo la tukio zikipita. Ilikuwa ni habari ya kutisha sana.
Habari hiyo ilifika mwisho na mtangazaji akawa anaendelea na habari nyingine lakini bado akili zangu zilikuwa zimeganda kwenye tukio hilo. Mwili wote ulikuwa umeishiwa nguvu, nilisimama na kuchungulia nje nikihisi pengine naweza kuona hata gari la polisi likiwasili.
Hofu ilinizidi kuliko kawaida, nikaenda chumbani lakini nako nilihisi kama kuna mtu ananitazama, nikarudi tena sebuleni na kukaa lakini bado akili yangu ilikuwa imevurugika. Nilijikuta natamani tena kulewa, niliamini nikipiga ‘vyombo’, ile hofu niliyonayo inaweza kuyeyuka kama ilivyokuwa jana yake.
Swali likawa je, nitatokaje? Niliamua kujilipua kwamba liwalo na liwe. Nilivaa nguo harakaharaka na kichwani nikavaa kofia ambayo niliishusha na kuziba sehemu kubwa ya uso wangu.
Unajua wakati mwingine ni rahisi sana kumtambua mtu mwovu unapokutana naye barabarani na pengine hata vyombo vyetu vya ulinzi vinatakiwa kuelekeza nguvu zaidi katika kufundisha watalaamu wa masuala ya saikolojia.
Nimesema hivyo kwa sababu kwa hali niliyokuwa nayo, kama ningekutana na mtu yeyote anayeweza kusoma sura ya mtu, ingekuwa rahisi sana kunigundua kwamba sikuwa sawa na pengine huo ungeweza kuwa mwanzo mzuri wa kupata ukweli wa kilichokuwa kimejificha nyuma ya pazia.
Nilitoka nikiwa na ‘mawenge’ mpaka mtaa wa pili, nikaingia kwenye kiduka kidogo kilichokuwa kinauza bidhaa mbalimbali za nyumbani, yaani kilijengwa kama ‘supermarket’ flani hivi kwa sababu mle ndani kulikuwa na kila kitu.
Sikuwa nazijua pombe vizuri, kwa hiyo nilichofanya ilikuwa ni kuonesha tu kwa kidole, ‘nataka ile na ile’, mhudumu akanishushia chupa kama nne hivi za pombe tofautitofauti, nikamuuliza bei ambapo aliponitajia tu, nilizama mfukoni na kutoa noti nne nyekundu na kumkabidhi, sikusubiri hata chenji, nikaondoka harakaharaka kurudi kwangu.
Niligundua pia kwamba sikuwa nimekula na nilishasisitizwa na Bonta kwamba ninapotaka kulewa, ni lazima nihakikishe nimekula na kushiba.
Nilipita kwenye kimgahawa kilichokuwa pale jirani, nikamuita mhudumu mmoja wa kike na kumuuliza naweza kupata kitu gani cha kula asubuhi hiyo. Alinitajia orodha ya vilivyokuwepo, nikamwambia nataka supu na chapati nne lakini sina kitu cha kubebea.
“Kwani unaishi mbali?”
“Hapana! Pale kwenye ile nyumba yenye geti jeusi,” nilimwelekeza, akaniambia basi nitangulie ataniletea na vyombo vyake. Nilimshukuru kwa sababu sikuwa nataka kuendelea kuonekana nje, nikatoa noti ya shilingi elfu kumi na kumpa, nikaondoka zangu huku mara kwa mara nikigeuka kutazama kama hakuna mtu anayenifuatilia.
Niliingia ndani na kwa sababu yule dada aliniambia kwamba atakuja muda si mrefu, sikufunga mlango. Nilizibwaga zile chupa za pombe pale chini, nikabadilisha runinga kutoka kwenye ile chaneli ya habari na kuweka muziki, nikaongeza sauti na kukaa pale kwenye kochi, nikafungua chupa moja na kuanza kuigida.
Muda mfupi tu baadaye, tayari nilishaanza kuchangamka, ile hofu niliyokuwa nayo ikaanza kuyeyuka na nikawa najikuta tu nachezesha mwili wangu kufuata midundo ya muziki. Kumbe yule dada alishafika na kugonga mlango lakini kutokana na sauti kubwa ya muziki, wala sikumsikia, ikabidi aingie.
Nilipogeuka, nilishtuka kumuona msichana huyo akiwa amesimama mlangoni, tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake.
“Kumbe unajua kucheza,” aliniambia huku akicheka, na mimi nikacheka sana na kukaa. Tayari pombe zilishaanza kukolea ndani ya kichwa changu kwa hiyo nilikuwa na uchangamfu usio wa kawaida.
“Una furaha sana mwenzetu, asubuhi yote hii unacheza muziki,” alisema huku akiinama na kuweka ‘hotpot’ lililokuwa na supu pale mezani, macho yangu yakatua kwenye eneo lake la nyuma.
Sijui nini kilitokea lakini nilijikuta nikivutiwa naye na hapohapo nikatamani nilale naye.
“Kumbe we mzuri kiasi hicho,” nilisema huku nikimsogelea mwilini na katika hali ambayo hakuitegemea, alishtukia nikipitisha mikono yake kwenye kiuno chake. Mshtuko alioupata nusura amwage ile supu, akanigeukia na kunitazama.
“Kwani unaishi na nani humu?”
“Naishi na braza’angu lakini kasafiri kaenda Nairobi, niko peke yangu,” nilimjibu huku nikimvutia kwangu.
“Mh! Mbona kama umelewa?”
“Kwani kuna tatizo lolote mrembo? Fedha siyo tatizo kwangu, kwa hiyo nakula, nakunywa, nalewa muda wowote ninaotaka,” nilisema huku nikiingiza mkono mfukoni na kutoa noti nyingi za shilingi elfu kumikumi.
“Hata wewe ukitaka naweza kukupa,” nilisema, nikamuona ananitazama kwa kunirembulia macho! Nilikuwa na uchawi wa Kizungu.
“Mi nakupenda mwenzio, hivi unaitwa nani?” nilisema huku nikijaribu kumbusu, cha ajabu wala hakuleta ubishi wowote, akaniruhusu nimbusu kwenye shavu lake, akaniambia jina lake anaitwa Neema.
“Njoo basi huku mara moja,” nilisema huku nikimshika mkono na kuanza kumvuta kuelekea chumbani, mwanzo alileta ule ubishi wa kawaida wa kikekike lakini nilipozidi kumng’ang’aniza, alikubali, nikamkokota mpaka chumbani.
Hata sijui nini kilitokea lakini nafikiri kwa sababu ya pombe, ukichanganya na ukweli kwamba tayari nilishajua ladha ya mapenzi, nilijikuta nikipandwa na mzuka wa hatari wa kufanya mapenzi na Neema.
Ilikuwa kazi ngumu kidogo kumshawishi lakini baada ya kumpa noti nyekundu mbili, mwenyewe alikubali lakini akanitaka nisimwambie mtu yeyote kwa sababu bosi wake akijua anaweza kumfukuza kazi.
Harakaharaka nilivua shati langu, nikamsaidia na yeye kuvua zake, nikamvutia kifuani kwangu huku nikiwa na papara zisizoelezeka. Mara nilishtuka kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu, kibaya zaidi ni kwamba sikuwa nimeufunga, nikashtuka kuliko kawaida.
Je, nini kitafuatia?
 
Mamba na wenzie walikuwa na ujasiri sana, walifanya mbwembwe zote msitu wa Kazimzumbwi pasipo kuogopa kambi ya jeshi.
 
SEHEMU YA 25




ILIPOISHIA:
Harakaharaka nilivua shati langu, nikamsaidia na yeye kuvua zake, nikamvutia kifuani kwangu huku nikiwa na papara zisizoelezeka. Mara nilishtuka kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu, kibaya zaidi ni kwamba sikuwa nimeufunga, nikashtuka kuliko kawaida.
SASA ENDELEA...
Kabla hata sijajua nini cha kufanya, nilishtukia mlango wa chumbani ukisukumwa kwa nguvu. Alikuwa ni Bonta na kwa jinsi ilivyoonesha, kulikuwa na tatizo kubwa lililotokea.
“Hebu achana na chochote unachokifanya, binti vaa nguo zako ondoka haraka!” alisema Bonta huku akinitazama, akionesha kutokuwa na hata chembe ya masihara. Harakaharaka nilivaa nguo zangu lakini moyoni nikawa nahisi kama Bonta ameniingilai sana uhuru wangu.
Hata hivyo, nilikiuwa najua kwamba Bonta siku zote ni mtu anayenipenda na kuniheshimu, kwa hiyo lazima kuna sababu iliyomfanya akanifanyia kitendo hicho. Yule msichana alivaa nguo zake harakaharaka akionesha kufadhaika sana, akatoka sebuleni an kuchukua vyombo vyake alivyoniletea supu, akatoka huku akikimbia.
“Kuna tatizo! Hakikisha umefunga nyumba vizuri, tunaondoka,” alisema Bonta huku akizunguka huku na kule, kweli nilifanya kama alivyoniambia, nikafunga chumbani, nikazima kila kitu na wakati natoka, aliona ule mfuko uliokuwa na chupa za pombe.
Akauvuta na kuchungulia ndani kisha akanitazama, hakusema kitu zaidi ya kuuchukua. Tukatoka mpaka nje, awali nilidhani kwamba Bonta atakuwa amekuja peke yake lakini kumbe alikuwa amekuja na watu wengine kadhaa.
“Ingia nyuma!” aliniambia huku akinipa ishara ya kuingia kwenye siti ya nyuma ya gari dogo lililokuwa limepaki pale nje, mle ndani niliwakuta Jombi, yule jamaa mwingine tuliyeenda naye kwenye tukio Tandika na mwanamke mmoja ambaye sikumjua, yeye alikaa siti ya pembeni na dereva, Bonta ndiye aliyekuwa nyuma ya usukani.
“Bosi Mute ameagiza tuondoke mjini, hali siyo shwari kwa sasa, polisi wanatusaka kwa udi na uvumba,” alisema Bonta wakati akiondoa gari kwa kasi, sasa nikawa nimepata picha ya nini kilichokuwa kinaendelea.
Ilikuwa ni lazima hali hiyo itokee, hamuwezi kusababisha mauaji makubwa kama tuliyoyasababisha sisi, tukamwaga damu za askrai na watu wasio na hatia kisha mambo yaishe hivihivi! Lilikuwa ni jambo lisilowezekana.
Basi tulitoka na kupita Barabara ya Bagamoyo, hii inayopita Mwenge, tukaenda mpaka Njia panda ya Goba na kuchanja kuelekea kule ndanindani, mwisho tukatokezea Mbezi na kuingia Morogoro Road, safari ikaendelea kwa muda mrefu na mwisho tukafika Kibaha.
Japokuwa tulikuwa tukisafiri mchana, hakuna mtu yeyote aliyetutilia wasiwasi na nakumbuka njiani tulipita kwenye vizuizi vingi vya barabarani lakini hatukusimamishwa hata mara moja. Unajua wakati mwingine, polisi huwa wanakosea sana kuamini kwamba wahalifu wote huwa wanatembea usiku tu.
Kwa ushuhuda wa mimi mwenyewe, naweza kukiri kwamba matukio mengi tulikuwa tukiyafanya usiku wa giza totoro lakini pia yalikuwepo matukio mengine mengi ambayo tulikuwa tukiyafanya mchana wa jua kali.
Kuna wakati kwa mfano, tulikuwa tukisakwa na polisi kwa udi na uvumba na wakati huohuo tukawa tunajichanganya mitaani lakini kwa namna ambayo ni vigumu mtu yeyote kukutilia mashaka.
Basi tulipofika Kibaha, tuliiacha barabara ya lami na kuingia mkono wa kulia, safari ikaendelea kwa muda mrefu na mwisho tuliishia kwenye geti kubwa ambalo lilifunguliwa na walinzi wenye silaha.
Tukaingia mpaka ndani nikiwa nashangaashanga
a. Kwa wenzangu, ilionesha kwamba walikuwa wanayajua mazingira kwa sababu gari liliposimama tu, wote waliteremka na kila mtu akaendelea na hamsini zake.
Yaani mle ndani jinsi mlivyokuwa, japokuwa kwa nje ungeweza kudhani labda kumezungushiwa ukuta tu halafu ndani hakuna shughuli yoyote inayoendelea ziaidi ya kilimo lakini ndani kulikuwana ulimwengu mwingine tofauti kabisa. Labda niseme hivi, lile halikuwa shamba kama ambavyo mtu angeweza kuamini baada ya kuona kibao kikubwa pale nje, ilikuwa ni kama kambi ambayo ndani yake kuna shughuli kibao zinazoendelea kimyakimya. Kulikuwa na majengo mengi yakiwa yamejengwa kwa mpangilio maalum.
“Hujawahi kufika huku?”
“Sijawahi kabisa!”
“Hii ni ngome yetu ya siri! Mambo yakiharibika kule mjini huwa tunakuja huku kupumzika na kujipanga upya,” alisema Bonta huku akinitembeza. Ni hapo ndipo tulipopata nafasi ya kuzungumza naye vizuri kwa sababu tangu lile tukio la ujambazi litokee, mimi na yeye hatukupata nafasi ya kuzungumza.
“Unaionaje kazi?”
“Ngumu sana! Daah, braza hii kazi ni hatari sijawahi kudhania.”
“Sisi hatujasoma mdogo wangu, tunakula kutokana na nguvu zetu. Wenzetu waliosoma wameajiriwa huku wanakula maisha, kwa hiyo lazima uipende kazi yako ndipo utakapoiona rahisi.”
“Braza, nitaipendaje kazi ya kuua au kuuawa!”
“Kuua au kuuawa huwa inatokea kama bahati mbaya, hakuna kazi ambayo haina ubaya, cha msingi ni umakini tu. Mbona matukio kibao huwa tunafanya na hafi mtu hata mmoja? Ile ilikuwa bahati mbaya,” alisema Bonta, akaanza kunitolea mifano ya watu kibao ambao walifanikiwa kabisa kubadili maisha yao kwa sababu ya kazi ya kushika mashine.
Alinitolea mfano wa Jombi, yule rafiki yao akasema ni tajiri mkubwa sana mjini, anamiliki baa kubwa nne, hoteli mbili na nyumba kibao kwa sababu ya kazi hiyohiyo!
“Cha msingi ni kuipenda kazi yako tu, halafu pia kuna jambo jingine muhimu sasa sijui wewe imani yako ikoje,” alisema Bonta tukiwa tumeshakaribia kufika kwenye jengo moja lililoonekana kuwa zuri kuliko mengine ndani ya eneo hilo.
Aliniambia kwamba kazi za kushika bunduki, ni lazima mtu uzindikwe na kutoa kafara, vinginevyo uwezekano wa kupigwa risasi na kufa ni mkubwa sana.
Yalikuwa ni mambo mageni kabisa kwangu, aliendelea kunisimulia jinsi yeye na wenzake wanavyopelekwa kwa mganga na Bosi Mute karibu kila mwezi.
“Si unaona hii,” alisema Bonta huku akitoa kitu kwenye waleti yake na kunionyesha! Ilikuwa ni hirizi kubwa nyekundu, akaniambia kwamba kila anapokwenda kwenye kazi ni lazima aichukue na huwa inamkinga sana kwenye matatizo.
Kiukweli mimi sikuwa naamini katika mambo ya ushirikina kwa hiyo nikawa namuitikia tu, yakiingilia kwenye sikio la kushoto na kutokea kwenye sikio la kulia. Tuliendelea na stori, mwisho tukafika pale kwenye lile jengo ambapo palikuwa kama na ofisi fulani hivi.
Tukaingia ndani ambapo kulikuwa na msichana mmoja aliyekaa mapokezi, akamsalimia Bonta kiheshima na kunitazama.
“Huyu ni mgeni eeh!”
“Ndiyo, ni mgeni kiasi lakini ni mwenzetu,” alisema Bonta, nikasalimiana na yule dada.
“Mdogo! Una miaka mingapi?” aliniuliza, nikamgeukia Bonta na kumtazama, nadhani hiyo ilitosha kumfanya aelewe kwamba sijapendezewa na swali lake.
“Siyo kwamba nakudharau, nimekuuliza kwa nia njema tu, mbona hata mimi ni mdogo, tena zaidi yako?” alisema yule msichana huku akijaribu sana kujenga mazoea.
“Mdogo wangu, wewe hujaoa na huyu naye hajaolewa! Muda wote anashinda amekaa tu hapo, kama vipi fahamianeni mi nakuja! Malizia kile nilichokukatisha kule Sinza,” alisema Bonta na kuingia kwenye vyumba vya ndani vilivyoonesha kuwa na watu.
“Unaitwa nani!”
“Kwani we unaitwa nani?”
“Mh! Mbona umekaa kisharishari hivyo jamani, Mungu amekuumba bonge la ‘hendsamu’ halafu unajiharibu, hata hupendezi,” alisema yule msichana baada ya kuona namkazia.
“Do you smoke?” aliniuliza msichana huyo huku akitoa sigara kwenye pakti, akaiweka mdomoni na kuiwasha. Kiukweli nilibaki nimepigwa na butwaa, kwa mwonekano wake sikudhani kama anaweza kuvuta sigara hadharani, nikatingisha kichwa kuonesha kwamba sivuti.
Akahama kule alikokuwa amekaa na kusogea pale nilipokuwa, nadhani alifanya makusudi ili anioneshe shepu yake ambayo ilikuwa imejengeka vizuri kwelikweli, akawa anaendelea kutoa moshi kwa fujo.
“Unajua namna ya kuitumia hii,” alisema huku akitoa bastola yake kiunoni na kuninyooshea. Unajua bado nilikuwa nazidi kujiuliza maswali mengi yasiyo na majibu, nimamtazama usoni kwa lengo la kutaka kujua nia yake maana tulishafundishwa kwamba mtu akishika bunduki, unatakiwa kuwa makini sana kumsoma machoni.
Nilichokifanya, niliipokea ile bastola, nikaiinua juu, nikaikoki na kuchomoa ‘magazini’, risasi zikamiminika chini, nikawa nazidaka na kuziweka vizuri. Niliamua kutumia mbinu hiyo kumuonesha yule msichana kwamba mimi siyo wa mchezomchezo maana alishaanza kama kuniletea dharau.
Nilizirudisha risasi na kuikoki, kisha nikamrudishia, akawa ananitazama machoni huku akitabasamu.
“Nini kilichokufanya ukaingia kwenye hii kazi!” aliniuliza swali ambalo sikulitegemea, nikamtazama, naye akanitazama, tukawa tunatazamana.
Je, nini kitafuatia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 26




ILIPOISHIA:
Nilizirudisha risasi na kuikoki, kisha nikamrudishia, akawa ananitazama machoni huku akitabasamu.
“Nini kilichokufanya ukaingia kwenye hii kazi!” aliniuliza swali ambalo sikulitegemea, nikamtazama, naye akanitazama, tukawa tunatazamana.
SASA ENDELEA...
“Kwani wewe ni nini kilichokufanya ukaingiakwenye hii kazi?”
“Kazi gani? Mimi hapa ni receptionist, mtu wa mapokezi. Kwani kuna ubaya wowote mtu kufanya kazi hii?”
“Receptionist? Wewe ni receptionist?” nilimuuliza huku nikiwa namtazama machoni. Dawa ya mtu anayedanganya ni kumtazama machoni, kwa hiyo kitendo cha mimi kumkazia macho, kilimfanya apoteze pozi, akakwepesha macho yake na kuanza kucheka.
Alikuwa akitaka kuniletea uongo wa waziwazi, bila shaka sote tunawafahamu wale watu wanaofanya kazi mapokezi au kwa kiingereza receptionist. Eti alitaka kuniaminisha kwamba yeye ni mtu wa mapokezi tu, wakati muda mfupi uliopita alinitolea bastola na kuniuliza kama najua kuitumia.
Inawezekanaje mtu wa mapokezi akawa na bastola kiunoni?
“Anyway tuachane na hayo, mi naitwa Kezia, wengi wamezoea kuniita Lady Keys, nafurahi kufahamiana na wewe,” alisema huku akinipa mkono, na mimi nikanyoosha mkono wangu na kumpa.
Kwa mwonekano wake na jinsi alivyokuwa mrembo, ungetegemea kwamba mkono wake utakuwa ‘softi’, lakini niliposhikana naye, nilishtuka kidogo kugundua kwamba alikuwa na mkono mgumu kwelikweli, wakati nikimshangaa, akaniwahi.
“Una mkono mgumu sana, wewe ni mtu wa kazi eeh?”
“Na wewe una mkono mgumu sana receptionist,” nilimjibu, akaishia kucheka tu maana niliamua kuwa ‘kauzu’ sana kwake.
“Karibu ukae,” alisema, safari hii kwa nyodo za kikekike, ule ‘ugumu’ aliotaka kunionesha ulianza kupungua kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele. Bila hata kuniuliza, aliingia kule ndani na kwenda kufungua friji, akatoa chupa mbili za bia na kuja nazo pale akiwa ameshazifungua, moja akanipa huku akiendelea kuvuta sigara na kutoamoshi mwingi.
“Afadhali nimepata mshikaji wa kupiganaye stori, ujue hapa wamejaa watu wa ajabuajabu, hata sina wa kupiga naye stori, isitoshe wengi ni wakubwa na wakija hapa kazi yao ni kunitongoza na kunitishia tu,” alisema msichana huyo ambaye sasa nilikuwa nalijua jina lake, Kezia.
“Usijali, nimefurahi pia kukufahamu Kezia,” nilimwambia huku nikipiga funda moja na kumtazama, akatabasamu.
“Na wewe ulikuwa miongoni mwa walioshiriki tukio la Tandika,” aliniuliza, nikamjibu kwa kutingisha kichwa.
“Mh! Mbona nasikia machalii wote walipigwa ‘gani’ wakatoka wakongwe watupu?” aliniuliza, nikapiga funda jingine kisha nikamtazama tena.
“Mimi nilitoka salama,” nilimjibu huku nikijiinamia, nikacheua povu la bia na kukaa vizuri.
“Daah! Noma sana mshkaji wangu, nakaumbuka na mimi kwenye tukio langu la kwanza nilitoka peke yangu, wenzangu wote tulioingia nao walikula mashine palepale huku nikiwashuhudia, dah! Hizi kazi hizi,” alisema huku naye akipiga funda kubwa na kucheua.
Sasa nilishapata uhakika wa kile nilichokuwa nakihisi! Keshia alikuwa sawa na mimi, hakuwa mtu wa reception wala nini, alikuwa jambazi. Unajua tofauti na zamani ambapo tulikuwa tukiaminikwamba majambazi ni ‘mijitu’ flani hivi ya kutisha, siku hizi huwezi kumdhania mtu kama ni jambazi, mpaka labda akamatwe.
Kwa mwonekano wake, Kezia alikuwa bonge la sistaduu, mzuri wa sura na umbo na anajipenda kwelikweli maana pale pote tulipokaa palikuwa pakinukia pafyumu aliyojipulizia, usingeweza kuamini kama ni mtu wa kazi, kama ambavyo usingeweza kudhani kama na mimi nashika mashine.
“Ilikuwaje?” nilimuuliza kwa udadisi, akashusha pumzi ndefu na kutulia kwa sekunde kadhaa. Akaanza kuniambia kwamba yeye ni mzaliwa wa Musoma, alikuja Dar es Salaam kutafuta maisha lakini siku za mwanzo akawa hana mbele wala nyuma, akawa anaishi kwa kubangaizabangaiza mpaka siku alipokutana na wanawake wawili waliomuunganisha na Bosi Mute.
Aliniambia kwamba Bosi Mute alipokutana naye kwa mara ya kwanza, alionesha kuvutiwa naye sana, akajitolea kwenda kumsomesha kazi ya ureceptionist huku akimilipia kwa kila kitu, akampangia chumba na akawa anampa fedha za kutosha.
“Nilisoma kwa miezi mitatu tu, nikapata cheti na kupelekwa kwenye ofisi yake ya Kariakoo, nikawa nafanya kazi kama receptionist,” aliniambia na kunifungua kichwa kwamba kumbe Bosi Mute ana ofisi nyingine Kariakoo.
Alinisimulia vitu vingi vilivyoendelea mpaka mwisho alipojikuta akiingia kwenye kazi ya kushika mtutu wa bunduki.
“Kiukweli sikulazimishwa ila mazingira tu yenyewe yalinifanya nikose cha kufanya zaidi ya kukubali kujiunga na vijana wa Bosi Mute, tukapelekwa mafunzoni huko Kisarawe ambako nilifundishwa na wenzangu namna ya kutumia bunduki kisha wikikadhaa baadaye, ndiyo tukapangiwa kwenda kufanya tukio Kariakoo, kwenye ofisi za Wahindi fulani waliokuwa wakifanya kazi ya kubadilisha fedha za kigeni.
Alinieleza jinsi walivyovamia wakiwa kama kumi hivi, wakaisimamisha Kariakoo yote kwa dakika kadhaa na kufanikiwa kupora kiwango kikubwa cha fedha kabla ya baadaye polisi kuvamia na kusababisha iibuke vita kali ya kurushiana risasi.
“Wenzangu wanne ambao nilitoka nao mafunzoni walipigwa risasi palepale, wawili wasichana kama mimi na wengine wawili wavulana, yaani sitakuja kuisahau ile siku,” aliniambia huku akitikisa kichwa chake kwa masikitiko.
Stori yake ilikuwa ikifanana sana na ya kwangu, akaendelea kunieleza kwamba baada ya msako kuwa mkali, yeye na wenzake waliotoka salama wakahamishiwa Kibaha na kuanzia siku hiyo ndiyo alipoanza kuishi hapo kambini.
“Sasa hivi kukitokea kazi, tunatoka usiku na kwenda kupiga dili kisha tunarudi hapahapa! Nimeshakuwa mzoefu,” alisema kwa kujiamini. Maelezo yake yalinifanya nivutiwe naye na kumuamini sana, nikaona nimepata kampani ya nguvu.
“Kwa hiyo wewe unaishi hapahapa?”
“Siyo mimi tu, tupo kibao! Utawaona wengine muda ukifika!” aliniambia, tukaendelea kupiga stori za hapa na pale, nikamwambia kwamba jina langu naitwa Kenny au Snox na nikamueleza kwa kifupi kuhusu maisha yangu.
Sikumueleza mambo mengi kuhusu mimi, basi tukaendelea kupiga stori huku tukishushia na bia ambazo alikuwa akienda kuchukua na kuzifungua kwa sababu zilikuwepo za ‘kumwaga’.
Baadaye alienda kuleta chakula, tukala pamoja huku stori zikiendelea. Baadaye, alikuja mwanamke mmoja mtu mzima kiasi, akaniuliza kama mimi ndiyo Kenny, nikamkubalia, akaniambia nimfuate.
“Uje basi ukimaliza,” aliniambia Kezia huku akionesha kuanza kuchangamka kutokana na kilevi, nikamuonesha kwa ishara kwamba nitarudi. Yule mwanamke alinipeleka mpaka kwenye jengo la sita kutoka pale tulipokuwepo, kama nilivyoeleza kulikuwa na majengo mengi yaliyojengwa kwa mpangilio.
“Hapa ndipo utakapokuwa unaishi, hiki ndiyo chumba chako, kina kila kitu ndani na ukihitaji chochote, kuna simu ya mezani utanipigia,” alisema yule mwanamke ambaye baadaye alijitambulisha kwamba yeye ndiyo Matron.
“Nashukuru sana,” nilisema wakati nikipokea funguo, basi akaondoka zake na kuniacha naendelea kukagua kile chumba. Jengo zima lilijengwa kwa mfumo kama wa hosteli hivi, kulikuwa na vyumba vingi ambavyo vilikuwa vinajitegemea. Mle ndani mlikuwa na chumba cha kulala chenye kitanda kikubwa, meza ndogo, friji dogo, kabati la nguo na vyoo na bafu ndani kwa ndani.
Nilishusha pumzi ndefu na kujilaza kitandani, ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kumbe nilikuwa nimeanza kulewa. Niliinuka na kwenda kufungua lile friji dogo, nikakuta ndani kuna maji na chupa kadhaa za pombe! Nikachukua bia moja na kuifungua, nikaendelea ‘kujimiminia’, sikutaka kukumbuka chochote kilichotokea Dar es Salaam.
Haukupita muda mrefu, nikapitiwa na usingizi mzito, nilikuja kuzinduka baada ya kusikia mlango ukigongwa, nilipotoka nilikutana na mzee wa makamo akiwa na sinia lililokuwa na chakula, tukasalimiana kisha akaniambia huo ni msosi wangu.
Sikushangaa sana kwa sababu kwa fedha tulizokuwa tukimuingizia Bosi Mute, alikuwa na haki ya kutuhudumia kama wafalme. Basi niliingia ndani na kuufakamia msosi wote, nikavitoa vyombo nje kama alivyonielekeza yule mzee kisha nikarudi na kwenda kujimwagia maji kupunguza uchovu.
Nilirudi na kujilaza kitandani nikiwa nimejifunga taulo, nikawa nachezea simu yangu, mara nikasikia kitasa cha mlango kikikandamizwa taratibu kuelekea chini, nikakaa makini kutaka kujua ni nani aliyekuwa akiingia. Nilishtuka kugundua kwamba ni Kezia, nikashusha pumzi ndefu na kujiweka vizuri pale kitandani.
Alikuwa amebadilisha nguo na kuvaa kigauni fulani chepesi kilicholifanya umbo lake zuri lionekane vizuri, akaufunga mlango kimyakimya na kumalizia kwa kufunga na funguo kabisa.
“Sitaki wajue kama nipo huku,” aliniambia kwa sauti ya chini huku akicheka, akaja mpaka pale kitandani, akajitupa na kunisogelea.
“Vipi mwanangu, mbona nimekwambia urudi halafu umenichunia,” alisema kwa Kiswahili cha kihuni, nikacheka kidogo na kumwambia kwamba nilikuwa najihisi kulewa, akacheka na kupeleka mkono wake kifuani kwangu.
“Yaani muda mfupi tu niliokaa na wewe nimejikuta nimekuzoea utafikiri tumejuana miaka kumi iliyopita,” aliniambia huku akijisogeza mwilini mwangu. Sikuweza kujizuia, na mimi nikapeleka mkono wangu kwenye kiuno chake na kumshika, akashtuka kidogo halafu akanitazama.
“Nimekuwa mpweke kwa siku zote ninazoishi kwenye hili gereza, leo nimefurahi sana umekuja,” aliniambia huku na yeye akiupitisha mkono wake taratibu kwenye kifua changu.
Kama nilivyosema, Kezia alikuwa sistaduu haswaa! Chumba chote kilikuwa kimejawa na harufu ya marashi mazuri aliyojipulizia. Alikuwa mzuri sana kwa sura na umbo, ukizingatia tayari na mimi nilishaujua utamu wa mchezo wa kikubwa, niliona ujio wake ni kama kuokota dodo chini ya mjohoro.
Tuligusanisha ndimi zetu lakini ukweli ni kwamba sikuwa mjuzi sana wa hayo mambo, jambo ambalo hata yeye aliligundua na kumfanya acheke. Basi akawa ni kama ananifundisha kwa vitendo nini cha kufanya, na mimi nikawa mwanafunzi mtiifu mwenye bidii ya kujifunza.
“Nataka unitoe upweke ndani ya moyo wangu,” alisema huku akijitoa kwenye mikono yangu, nikamshuhudia akilitoa lile gauni jepesi alilokuwa amevaa, cha kushangaza ni kwamba ndani hakuwa na kitu kingine chochote, kwa hiyo ni kama alijiandaa kuja kunijaribu, wakati msimamo wangu siku zote ni kwamba huwa sijaribiwi.
Macho yangu yakatua kwenye kifua chake kilichojaa vizuri, nikalisogeza taulo langu, sasa tukawa saresare maua, macho yake yakatua kwa ‘kiranja mkuu’, akatabasamu na kunitazama.
“Kumbe wewe siyo mdogo kama nilivyodhani mwanzo,” alisema huku akimpapasa kiranja taratibu, jambo lililomkurupusha shetani wangu alikokuwa amejificha, kiranja mkuu akasimama wima kama mwanajeshi anayejiandaa kupiga saluti, nikaipitisha mikono yangu kwenye kiuno chake, akashtuka kidogo na kuanza kujinyonganyonga.
Haukupita muda, nikawa nimeshamuweka vizuri, naye akatii bila shuruti, kipyenga kikapulizwa kuashiria kuanza kwa mpambano usio na jezi wala refa.
Kweli ilionesha alikuwa na upweke wa hali ya juu ndani ya moyo wake, kwani alinipokea kwa bashasha za hali ya juu, nikaanza kufumua mashuti ya nguvu na kusababisha awe analalama kama mtu anayeonewa lakini wakati huohuo akinihimiza kuongeza kasi ya mchezo.
Je, nini kitafuatia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mabaharia msaada wa vocha ya 500 tafadhalini nataka niwapostie vipande vi5 vilivyobaki.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom