Riwaya: Saa za Giza Totoro

Riwaya: Saa za Giza Totoro

hapana not fair n my lead to legal actions na kwann u ki upload hata mie nakitamani saaaana lakini acha tupambane tukinunue mbona katufanyia fea sana mkuu futa wazo futa nia futa kauli sio tu kuaplodi usimtuie mtu yeyote hata mie nikija pm nishushue
Umenifurahisha sana mkuu! yaani kuna watu wengine mpaka unajiuliza mara mbilimbili, do they have common sense?
 
hapana not fair n my lead to legal actions na kwann u ki upload hata mie nakitamani saaaana lakini acha tupambane tukinunue mbona katufanyia fea sana mkuu futa wazo futa nia futa kauli sio tu kuaplodi usimtuie mtu yeyote hata mie nikija pm nishushue

Wakati anaanza kuiposti humu angesema anafanya matangazo na haitafika mwisho....hata kama alikua anafanya
promo amelipia humu???
 
SEHEMU YA 21


ILIPOISHIA:
“Tunaenda kuvamia benki?” nilijiuliza nikiwa ni kama siamini. Aliendelea kutuchorea mchongo mzima unavyotakiwa kufanyika, na akasema hatutaenda wote, bali watachaguliwa wachache kati yetu watakaoungana na Kikosi A kwa ajili ya kazi hiyo. Moyoni nikawa namuomba Mungu nisiwe miongoni mwa watakaochaguliwa.
SASA ENDELEA...

“Kila mmoja akae tayari, muda wa kuondoka utakapofika mtatangaziwa waliochaguliwa,” alisema Bosi Mute wakati akikamilisha kutupa mchongo wa kazi hiyo. Aliondoka na kutuacha mle ndani, tukawa tunatazamana, kila mmoja akiwa kimya kabisa.

Basi baadaye tulitoka na kila mmoja akaendelea na kazi yake maana licha ya kazi hiyo, kila mtu alikuwa na kitengo chake, mimi nikaelekea kule kwenye kazi yangu ya kuosha magari. Kulikuwa na magari kama matatu hivi yaliyoingia jana yake, basi nikavaa nguo za kazi na kuanza kuyaosha huku mawazo kibao yakiendelea kupita ndani ya kichwa changu.
Ilipofika kama saa tisa hivi za mchana, magari mawili, Toyota Noah, yote yakiwa na rangi nyeusi na vioo vya tinted, yaliwasili na kuingia pale ndani. Nikaona pilikapilika zimeanza, nikajua sasa mambo yamewiva.

Kila mtu aliacha alichokuwa anakifanya na kuanza kuangalia ni nini kinachoendelea, nilimuona Bonta akiwakusanya wale wenzake ambao wote walikuwa wakubwa kwetu. Wakaingia kwenye chumba cha mikutano, sijui walikuwa wakijadiliana nini lakini muda mfupi baadaye, tulianza kuitwa mmojammoja.

Na mimi nilipoitwa, niliacha kila kitu na harakaharaka nikaelekea kwenye kile chumba cha mikutano huku mapigo ya moyo yakinienda mbio kwelikweli. Nilipofika, niliwakuta wenzangu watatu ambao tulikuwa pamoja kwenye Kikosi B, kwa hiyo na mimi nikawa wa nne.

Muda mfupi baadaye, yaliletwa masanduku mawili, yakawekwa pale mezani na Bonta akatuambia kila mmoja anatakiwa kuanza kujiandaa. Masanduku yalifunguliwa, la kwanza lilikuwa na nguo vikiwemo viatu kama vile wanavyovaa wanajeshi na makoti marefu meusi, na lile lingine lilikuwa na bunduki.

Tukaambiwa kila mtu achague vitu vinavyomfaa, tukawa tunatetemeka kwelikweli. Walianza akina Bonta, wakachukua vya kwao, ikafika zamu yetu. Hakukuwa na muda wa kupoteza, kwa hiyo kila mtu alichukua vitu vyake na tukaanza kubadilisha mlemle ndani kama tulivyokuwa tukipewa maelekezo.

Muda mfupi baadaye, kila mmoja alikuwa ameshavaa, kiukweli nguo hizo zilitubadilisha kabisa, sasa tukawa kwenye mwonekano wa kijambazi kwelikweli. Tulipewa pia kofia na miwani myeusi, baada ya kumaliza, Bosi Mute alikuja na kuanza kutukagua mmoja baada ya mwingine.

Ni kama alijua jinsi sisi ambao ndiyo ilikuwa mara yetu ya kwanza tulivyokuwa na hofu, akawa anatutoa hofu na kutuambia tunatakiwa kujiamini. Akaendelea kutupa mchoro wa jinsi kazi inavyotakiwa kufanyika na mwisho akatuambia kwamba Jombi ndiye atakayekuwa kiongozi wa msafara.

Sikuwa namjua sana huyo Jombi zaidi ya kuwa namuona mara mojamoja pale kambini. Alikuwa ni kipande cha mtu, amekwenda hewani halafu ‘amepasuka’ kwelikweli kutokana na mazoezi. Muda wote macho yake yalikuwa mekundu kama ‘nyanya’ na sikumbuki kama nimewahi kumuona akitabasamu au kucheka tangu nianze kumuona.

Kila mmoja alikabidhiwa bunduki yake, wale wakubwa wakachukua mbilimbili, bunduki kubwa na bastola, sisi tukapewa mojamoja. Baada ya hapo, tulitengeneza kama duara hivi, Bosi Mute akiwa katikati, akawa anaendelea kututoa hofu na kusisitiza kwamba anatuamini na hatuwezi kumuangusha.

Baada ya hapo, tulishikana mikono wote kwa pamoja kisha tukagongesheana ngumi na harakaharaka tulitoka kule nje, yale magari yalikuwa yamesogezwa mpaka mlangoni, tukaingia kwa makundi mawili, kila moja likiwa na mchanganyiko wa wakubwa wawili na wadogo wawili. Ukichanganya na madereva, kila gari lilikuwa na watu watano, safari ikaanza.

Tulitoka kwa mwendo wa kasi huku watu wote wakiwa wanatutazama, tukaingia barabarani na magari yakawa yanakimbia kwa kasi kubwa sana. Sikuwa nawajua madereva ni akina nani lakini walionesha kuwa ni wazoefu sana.

Safari yetu iliishia kwenye mtaa mmoja wenye pilikapilika nyingi, eneo ambalo baadaye nilikuja kulitambua kwamba ni Tandika. Tulisimama kwenye barabara ya vumbi ya mtaa huo, mita chache kutoka kwenye barabara ya lami.

Dakika chache baadaye, tuliona yale magari yanayotumika kubebea fedha na kuzisambaza kwenye benki mbalimbali, likipita kwenye barabara ya lami huku nyuma likiwa linasindikizwa na gari la polisi. Kwa wanaoyajua magari ya kubebea pesa watakuwa wanaelewa vizuri, lilikuwa ni kama Hiace ndogo lakini likiwa limezibwa pande zote.

Harakaharaka madereva walipeana ‘signal’, lile gari la mbele ambalo ndiyo nililokuwa nimepanda mimi, likaondoka kwa kasi na kuingia kwenye barabara ya lami, tukawa tunalifuata lile gari lililobeba fedha na lile gari jingine, liligeuza na kupita mtaa wa pili, sikuelewa linaelekea wapi.

Kulikuwa na magari mengine kadhaa katikati yetu, dereva akawa anajaribu kuyapita kwa fujo, mwisho likabakia gari moja mbele yetu, kisha gari la polisi halafu ndiyo lile gari lililobeba fedha.

Jombi ambaye tulikuwa naye kwenye gari moja, alitoa ishara kwamba kila mmoja ajiandae kwa kazi, huku nikitetemeka, niliitoa bunduki yangu niliyokuwa nimeivaa shingoni na kuificha ndani ya koti refu, nikaishika vizuri na kutoa ‘safety lock’, tayari kwa chochote.

“Gari litakaposimama tu, tunawaangusha kwanza hawa waliopo kwenye gari la polisi, wewe na wewe mtabaki kutoa back-up, hakikisha yeyote anayesogea mnamuangusha,” aisema Jombi huku akinioneshea mimi na yule mwenzangu, tukatazamana huku kijasho chembamba kikiwa kinatutoka.

Lile gari la lilikatiza na kuingia upande wa kulia, gari la polisi nalo likafuatia. Dereva wetu alipunguza mwendo kidogo, akalitoa gari barabarani, tukashuhudia yote mawili yakienda na kusimama nje ya tawi dogo la benki. Askari waliwahi kushuka, wakawatawanya watu wote waliokuwa nje ya ile benki.

Kulikuwa na skari kama sita hivi, wote wakiwa na silaha lakini pia kulikuwa na askari wengine kwenye lile gari lenye fedha ambao wao walivaa nguo za tofauti, tukawaona pia walinzi wa ile benki wakiungana nao kuhakikisha hakuna kinachoharibika.

Hata kabla ya tukio lenyewe, nilishajua kwamba hatuwezi kufanikisha tunachoenda kukifanya kwa sababu kwa hesabu za harakaharaka, wao walikuwa wengi kuliko sisi.

Kumbe dereva alikuwa anasubiri tu maelekezo, Jombi alipotoa ishara tu, dereva alikanyaga mafuta kwa nguvu kisha akakata kona na kuelekea pale wale askari walipokuwa wametanda.

Wakati wale askari wakishtuka na kuelekezea mitutu yao kwenye gari letu, lile gari jingine lilitokea upande wa pili, kwa kasi ileile, kwa hiyo wakawa ni kama wamepatwa na kiwewe, ndani ya sekunde chache tu, wote tulikuwa tumeshashuka kwenye magari yote mawili kwa staili ya kikomando kama tulivyofundishwa kule porini, tukawa tumewazunguka wale polisi na walinzi.

Jombi ndiye aliyekuwa wa kwanza kufyatua risasi, na ya kwanza ilimlenga mmoja kati ya wale askari, tena kichwani! Akadondoka chini kama mzigo, kilichofuata baada ya hapo ilikuwa ni kama uwanja wa vita.

Tuliwafyatulia mvua ya risasi kutoka pande mbili, nao wakawa wanajibu mapigo lakini kwa kuwa tulikuwa tumewazunguka, tuliwazidi ujanja. Ndani ya sekunde chache tu, watu wote walikuwa chini, si polisi, si walinzi, watu waliokuwa jirani wakawa wanakimbia huku wakipiga kelele, kila mmoja akiokoa maisha yake.

Kama tulivyoelekezwa, mimi na yule mwenzangu tulibaki kama ‘back-up’ kuhakikisha hakuna mtu anayesogea kwenye eneo la tukio, Jombi, Bonta na wengine kutoka kwenye lile gari, wakakimbilia mpaka kwenye lile gari huku wakiendelea kufyatua risasi.

Kwa kuwa tayari gari lilishakuwa limefunguliwa na sanduku la fedha kutolewa, hawakupata shida, wakaanza kusaidiana kuliburuza huku risasi zikiendelea kurindima.

Dereva wa lile gari letu alilisogeza mpaka pale karibu na lile sanduku kwa kasi mithili ya magari ya mashindano, Akina Jombi wakalibeba lile sanduku lililoonekana kuwa zito kwelikweli na kuliingiza ndani ya gari. Waliingia ndani ya gari na dereva akaondoka kwa kasi kubwa, sekunde chache tu baadaye tayari walishaingia barabarani.

Kimbembe kikabakia kwetu sisi wawili tuliobaki kutoa ‘back-up’ kama tulivyoelekezwa, lile gari la pili lilikuwa limepaki kama mita hamsini hivi kutoka pale tulipokuwepo, kwa hiyo ilikuwa ni lazima tulikimbilie haraka iwezekanavyo na kuungana na wale wenzetu wawili ambao nao walibaki kama ‘back-up’, kibaya ni kwamba wote tulikuwa ni kutoka Kikosi B.

Tukiwa tunalikimbilia kwa tahadhari kubwa huku tukifyatua ovyo risasi, tulishtukia magari mengine mawili ya polisi yakiingia kwa kasi ya kimbunga, askari wengi wakaruka kabla hata hayajasimama na kuanza kutufyatulia risasi kama mvua.
Je, nini kitafuatia?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii ni kazi sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ilivyo ni kama msimuliaji ameanzia katikati kisha akarudi nyuma hivyo ni rahisi kutabiri mwisho wake!...........


mwisho huyo boss wao atauliwa na huyo dogo sterling, then ataanza kuishi maisha yake na saima!.........
Mkuu unaonekana wewe ni mpenzi wa Indian movie ndio rahasi kuzielewa kabla azijaisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hatar
SEHEMU YA 36



ILIPOISHIA:
Harakaharaka mama alienda kupewa taarifa, akaanza kuangua kilio kwa sauti ya juu huku akilitaja jina langu, wanawake wengine nao wakawa wanalia kwa huzuni, vilio vikawa vimeamka upya.
“Unatakiwa kujikaza mdogo wangu,” aliniambia Bonta, wakati tukipelekwa kwenye chumba kilichokuwa na mwili wa marehemu.
SASA ENDELEA...
Tuliingia na kukuta mwili wa baba ukiwa umelala na kutulia kitandani, akiwa tayari ameshavalishwa sanda. Ungeweza kudhani baba amelala tu lakini kumbe ndiyo alikuwa ametutoka.
Baba mkubwa ndiye aliyekuja kutufungulia sanda upande wa kichwani, nikamtazama baba, kiukweli nilijitahidi sana kujikaza kiume kama alivyosema Bonta lakini haikuwezekana.
Nilipiga magoti na kuukumbatia mwili wa baba huku uso wangu ukiwa umejawa na machozi, donge kubwa likawa limenikaba kooni kiasi cha kunifanya nishindwe hata kumeza mate, nikaanza kuangua kilio kwa huzuni kubwa huku nikimuita baba.
Kwa kipindi ambacho baba alikuwa mzima, kabla hajaanza kuumwa, alitulea vizuri sana sisi wanaye, alijitahidi kwa kadiri ya uwezo wake kuhakikisha tunapata malezi bora na elimu bora ingawa mambo yalianza kuharibika alipoanza kuugua na kuishia kulala kitandani.
Pengine hata leo hii angegundua ni kazi gani niliyokuwa naifanya baada ya kushindwa kuendelea na masomo kutokana na ukosefu wa karo, pengine angeumia sana ndani ya moyo wake kwa sababu kila sikuwa alikuwa akitusisitiza wanaye kwamba elimu ndiyo kitu pekee kinachoweza kutukomboa maishani.
Kwa zaidi ya dakika kumi na tano nzima nilikuwa nikiendelea kulia tu huku nikiwa nimemkumbatia baba, ikafika mahali ikabidi niondolewe kwa nguvu kwa sababu ningeweza hata kuzimia kutokana na kulia mfululizo kwa muda mrefu.
Nilipotolewa kule chumbani, nilipokelewa na mama ambaye alinikumbatia huku na yeye akianza upya kulia. Ilikuwa ni siku ya huzuni kubwa sana kwangu, mama akawa ananiambia kwamba lichaya mimi kujitahidi kutafuta fedha za matibabu ya baba, alikuwa amekataa kuendelea kukaa nasi na kuamua kurejea kwa Mungu wake. Ilifika mahali, mwili wangu ukawa umeishiwa nguvu kabisa kwa sababu ya kulia, macho yakiwa yamevimba na kuwa mekundu sana.
“Inabidi upate kitu kitakachokupunguzia uchungu ndani ya moyo wako,” alininong’oneza Bonta, akanishika begani na kunikumbatia, akawa ananipeleka nje ambapo ilibidi tujitenge na waombolezaji wengine na kukaa pembeni kidogo ya nyumba, chini ya mti wa mkorosho.
“Changamsha kichwa mdogo wangu, haya ni mambo ya kawaida kabisa, sisi wote hapa duniani ni wapita njia tu, cha msingi tumuombee apumzike mahali pema peponi,” alisema Bonta huku akitoa kichupa kidogo kilichokuwa na ile pombe kali anayopenda kunywa.
Nilikifungua na kupiga funda moja, nilipomeza nilihisi tumbo lote linawaka moto na muda mfupi baadaye, nikaanza kujisikia vizuri. Bonta akawa anaendelea kunisisitiza kuinywa ile pombe. Japokuwa kichupa kilikuwa kidogo lakini nilipofikisha nusu, tayari nilikuwa nimechangamka kwelikweli.
Kuna wakati nilikuwa nasahau kabisa pale ni wapi na nini kimetokea, tukawa tunaendelea na stori za hapa na pale na Bonta, mara Bonta aliingiza mkono mfukoni na kutoa msokoto, akatazama huku na kule kuhakikisha kwamba hakuna mtu yeyote aliyekuwa akitutazama.
Akauwasha na kuvuta kidogo kisha akanipa, na mimi nikavuta huku safari hii nikiwa nimeshaanza kuzoea, ile hali ya kukohoa ikawa imeisha kabisa, nilipovuta mara kadhaa, ndiyo kabisa nilizidi kujiona kama hakuna chochote kilichotokea.
Hata sijui nini kiliendelea, nilishtukia tu nimepitiwa na usingizi mzito, tulipozinduka tayari ilikuwa ni alfajiri. Unajua tatizo la hivi vilevi, kama pombe na madawa mengine ya kulevya, japokuwa watu wengi huwa wanaamini kwamba vinapoteza mawazo, ukweli ni kwamba huwa vinakusahaulisha kwa muda mfupi tu na vikiisha kichwani, matatizo yanarudi palepale.
Japokuwa usiku ule baada ya kupiga pombe kali na kusindikizia na msokoto nilijiona kama nipo dunia nyingine kabisa, kulipopambazuka tu hali ilikuwa imerudi palepale, moyo wangu ulikuwa ni kama una kidonda. Na jinsi pombe zisivyo na adabu, kama ukinywa usiku wa manane, ukiamka asubuhi japokuwa zinakuwa zimepungua sana kichwani lakini bado zinakuwepo.
Kwa hiyo japokuwa ilikuwa ni siku mpya bado kichwa changu kilikuwa na ‘mawenge’ na kwa mtu ambaye ananifahamu vizuri, angeweza kugundua kwamba sikuwa kwenye hali yangu ya kawaida.
“Hapa ni kwenye umati wa watu na kama unavyojua tena kazi zetu hatutakiwi kufanya jambo lolote linaloweza kuwafanya watu waanze kukutilia mashaka.”
“Mimi hapa ni kwetu, wala usiwe na wasiwasi.”
“Kuwa kwenu siyo sababu, polisi wapo kila sehemu, tunaweza kuja kukamatwa hata hapahapa,” alisema Bonta kwa msisitizo lakini aliyokuwa anayazungumza yalikuwa yakiingilia kwenye sikio moja na kutokea kwenye sikio la pili.
“Hebu nipe kwanza nizimue,” nilimwambia Bonta nikimaanisha anipe tena ile pombe kali, akanitazama kwa muda kisha akashusha pumzi ndefu, kumbe alikuwa na vichupa vingine kadhaa vya ile pombe ya Kizungu ambayo hata sijui inaitwaje, akanipa kimoja na kuendelea kunisisitiza kwamba natakiwa kuwa makini tusije kuibua matatizo yasiyokuwa na msingi.
Nilikipiga kile kimoja kwa kasi na licha ya ukali wake, nilipokishusha chini tayari kilikuwa kimeshafika nusu.
“Hapana Snox, hatuendi hivyo,” alisema Bonta huku akinipokonya kile kichupa, akakifunga vizuri na kukirudisha mfukoni mwake. Sikutaka kubishana naye, nikatulia huku nikiisikilia ile pombe ikisambaa mwilini kwa kasi ya ajabu.
Mara nilianza kuhisi kama lile jeraha langu pale mguuni linaniwasha, nikapandisha suruali na kulitazama, sijui ndiyo akili ya pombe au kitu gani, nilijikuta nikitamani kulichubua na kutoa ngozi ya juu ambayo ilikuwa ikilifanya jeraha lionekane limeanza kupona.
Bonta hakushtukia nilikuwa nafanya nini, nikawa nimetulia naendelea kujichubua na cha ajabu hata sikuwa nasikia maumivu. Alipokuja kushtuka, tayari nilikuwa nimemaliza kulichubua lote na kwa sababu kidonda bado hakikuwa kimepona, damu nyingi zikaanza kunivuja mguuni na kulowanisha suruali na kiatu changu.
“Mambo gani umeanzahayo Snox?” alisema Bonta kwa sauti iliyoonesha kwamba alikasirika, wakati hayo yakiendelea, kule upande wa pili vilio vilikuwa vikiendelea kusikika, huku wanawake wengine wakiendelea kupika chai kwa ajili ya waombolezaji.
“Kenny unaitwa ndani,” alisema mtoto mmoja wa jirani, aliyetumwa kuja kuniita. Kama nilivyoeleza awali, jina nililopewa na wazazi wangu ni Kennedy ila wengi walikuwa wakilifupisha na kuniita Kenny, ingawa upande wa pili kwenye kazi haramu, jina langu lililokuwa linafahamika lilikuwa ni Snox.
Niliinuka na kutaka kuelekea ndani lakini cha ajabu, nilijikuta nikipepesuka sana, ni hapo ndipo nilipoelewa kwamba pombe siyo chai, ile pombe niliyokunywa ilikuwa imenichukua kwelikweli, nilijitahidi kujikaza lakini wapi, nikawa naendelea kupepesuka, hali iliyomshangaza kilammoja.
“Huyu si ndiyo mtoto mkubwa wa merehemu?”
“Ndiyo! Si Kenny huyu?”
“Sasa mbona amelewa asubuhi yote hii wakati maiti ya baba yake ipo ndani hata bado haijaenda kuzikwa?”
“Halafu mbona amelowa damu mguuni?” niliwasikia wazee wa pale mtaani ambao walikuwa wamejumuika pale msibani wakinijadili, sikuwajali, nikapita kwa hatua ndefundefu za kilevi na kuingia mpaka ndani.
Japokuwa mama alikuwa kwenye huzuni kubwa, alishtuka sana na hali niliyokuwa nayo, akaacha kulia na kuanza kunitolea macho, akiwa ni kama haamini alichokuwa anakiona.
“Umeanza lini kunywa pombe?” aliniuliza mama kwa mshangao, uso wake ukiwa umelowa kwa machozi na macho yake yakiwa yamevimba na kuwa mekundu kwa sababu ya kumlilia baba.
“Sijanywa pombe!” nilisema kilevi huku nikijitahidi kusimama kikakamavu, kumbe ndiyo nilikuwa nazidi kuharibu.
“Halafu kumbe ile harufu ya bangi iliyokuwa inasikika wewe ndiye uliyekuwa unavuta?”
“Ha..pa...na mama,” nilisema kwa kubabaika, baba zangu wadogo na ndugu zangu wengine waliokuwa wamekusanyika kwenye chumba kimoja kwa ajili ya majadiliano ya kifamilia, walikaa kimya wakisikiliza mazungumzo yangu na mama.
“Tuachane na hayo mwanangu,” alisema mama huku akianza tena kuangua kilio, watu wote wakawa kimya mle ndani, baba mdogo akavunja ukimya.
“Tumeitana kama familia kwa ajili ya kujadili taratibu za mazishi, je, tunataka baba akazikwe makaburini au hapahapa nyumbani, lakini pia tumejipangaje kuhusu gharama za jeneza na matumizi mengine ya msibani?” alisema baba mdogo ambaye ndiye aliyekuwa amepewa jukumu la kuwa msemaji wa familia kwenye msiba huo.
“Nitafanya kila kitu mimi, jeneza shilingi ngapi kwani?” nilisema kwa sauti iliyoonesha wazi kwamba mdomo wangu ulikuwa mzito kwa sababu ya pombe, hakuna aliyenijibu, nikaingiza mkono mfukoni na kutoa burungutu la noti za shilingi elfu kumikumi, hata sikuhesabu nikamkabidhi mama lakini alikataa kuzipokea, akawa anaendelea kulia, ikabidi baba mdogo ndiyo azipokee.
Sijui nini kilitokea, wakati nikijiweka vizuri suruali yangu, bastola iliponyoka kutoka pale kiunoni nilipokuwa nimeificha na kudondoka chini, watu wote wakapigwa na butwaa, kwanza kugundua kwamba nilikuwa na bastola kaini pia kugundua kwamba mguu wangu ulikuwa umelowa damu kuonesha kwamba nilikuwana jeraha kubwa.
Hata mama aliyekuwa akiendelea kulia, alinyamaza nakubaki amepigwa na butwaa, harakaharaka nikainama kwa lengo al kutaka kuiokota ile bastola lakini kwa sababu nilikuwa nimelewa, nilishindwa kuiokota, badala yake nikapepesuka na kutaka kuanguka.
Nilirudia tena kujaribu kuiokota, kweli nikafanikiwa kuiokota na kuirudisha pale kiunoni, bado wote wakawa wanautazama mguu wangu.
“Unatembea na bunduki Kenny? Umepatwa na nini mwanangu? Mbona umebadilika ndani ya muda mfupi na kuwa mtu wa ajabuajabu?” alisema mama, akaanza tena kuangua kilio, nikaona hapo ndani siyo sehemu ya kukaa tena kwani ilionesha ni kama hali niliyokuwa nayo ilikuwa ikimuongezea mama huzuni.
“Mjomba mbona unatudhalilisha?” mambo gani tena haya unayafanya? Kwa nini usisubiri tukamzike baba ndiyo uendelee na mambo yako?” aliniambia mzee mmoja tuliyezoea kumuita mjomba, kauli ambayo iliugusa moyo wangu, nikichanganya na hali niliyomuacha nayo mama chumbani, nilijikuta huzuni kali ikinizonga, nikaanza kulia kwa sauti ya juu. Wasichokijua watu wengi ni kwamba kama umelewa halafu ukaanza kulia, unaweza kulia kwa uchungu mpaka watu wote wakakushangaa, ndicho kilichotokea kwangu.
Nikiwa naendelea kulia kwa nguvu na kuwafanya vijana wa pale mtaani pamoja na wazee wa mtaani wapate kazi ya kunituliza, nilishtuka baada ya kuona gari la polisi likija pale nyumbani, pombe zote ni kama ziliyeyuka kichwani, nilipogeuka na kutazama pale Bonta alipokuwepo, sikumuona, moyo ukawa unadunda kwa nguvu kuliko kawaida, ni nikiwa ni kama siamini kilichokuwa kinatokea.
Je, nini kitafuatia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hatar
SEHEMU YA 49




“Vipi tunaweza kuonana,” nilimwambia Saima, kauli ambayo aliipokea kwa shangwe kwelikweli, akaniambia alikuwa anaisubiri sana nafasi ya mimi kuonana naye. Kwa sababu ya upepo wa bodaboda, hatukuzungumza mambo mengi zaidi ya mimi kumwambia kwamba nitakuwepo Sinza, akaniambia na yeye anaenda kujiandaa kisha nikakata simu.
Nilijikuta nikitabasamu mwenyewe, safari ikaendelea huku nikiendelea kutafakari mambo mbalimbali ndani ya kichwa changu. Yule dereva alinipeleka mpaka Bunju, akaniambia wamepewa maelekezo kwamba waishie hapo.
“Kwa nini usinifikishe nyumbani?”
“Hapana! Unatakiwa kupanda daladala kama wenzako wanavyofanya,” aliniambia, akawa ni kama amenikumbusha kitu muhimu sana kwa sababu tulishapewa maelekezo kwamba njia nzuri ya kuingia mjini salama, ni kwa kutumia usafiri wa umma kwa sababu ni vigumu sana kwa askari wa Dar kusimamisha daladala na kuanza kuwapekua abiria, lakini ni rahisi sana kusimamisha magari binafsi, bodaboda au Bajaj.
Basi nilimshukuru kisha harakaharaka nikavuka upande wa pili wa barabara, nikapanda daladala inayoelekea Makumbusho huku begi langu nikiwa nimeligeuzia mbele na kulikumbatia. Safari ikaendelea huku muda mwingi nikiwa mtulivu sana, gari lilipofika Bamaga niliteremka na kupanda lingine ambalo lilienda kunishusha Sinza Madukani.
Ile nashuka tu, simu ya Saima ikawa inaingia, harakaharaka niliipokea, swali lake la kwanza likawa ni kama nimeshafika au bado.
“Nimeshafika, wewe uko wapi kwani?”
“Naelekea kwenye kituo cha Bajaj, kwa hiyo umesema nishukie wapi?”
“Sinza madukani,” nilimsisitiza, akakata simu. Nilitembea harakaharaka kuelekea nyumbani kwangu, huku nikiwa nimevaa kofia na kuishusha machoni, kiasi kwamba haikuwa rahisi kwa mtu yeyote kunitambua.
Japokuwa nilikuwa najua kwamba hakuna mtu anayenifuatilia, lakini moyo wangu bado ulikuwa na hofu kiasi kwambamarta kwa mara nilikuwa nikigeuka nyuma kuhakikisha niko salama.
Nilifika mpaka pale kwangu salama, nikafungua geti na kuingia mpaka ndani, nikalibwaga begi kwenye sofa kisha nikaanza kuvua nguo zangu kwa ajili ya kwenda kujimwagia maji. Muda mfupi baadaye, tayari nilikua nimeshaoga, nikajilaza kwenye kochi na kuwasha runinga, huku muda wote macho yangu yakiitazama simu.
Dakika chache baadaye, ilianza kuita, nikapokea harakaharaka ambapo Saima alinieleza kwamba tayari ameshashuka kituoni, ikabidi nimuelekeze kwa sababu isingekuwa sawa mimi kutoka tena na kwenda kituoni. Basi akawa anakuja huku nikiendelea kumpa maelekezo na muda mfupi baadaye, nilisikia geti likigongwa, tayari Saima alikuwa ameshafika.
Harakaharaka nikaenda kumfungulia mlango, macho yangu na yake yakagongana, akaachia tabasamu na kutanua mikono yake kama ishara ya kunikumbatia. Huwezi kuamini moyo ulipatwa na mshtuko usio wa kawaida, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
Unajua hakuna mtihani mkubwa kama kukutana na mwanamke mrembo ambaye kwa kumtazama tu unajua kabisa huna hadhi ya kuwa naye! Hicho ndicho kilichonitokea kwa Saima, japokuwa nilikuwa najua kwamba ni mzuri sana, lakini siku hiyo uzuri wake ulikuwa ni kama umezidi kipimo, ungeweza kumfananisha na wale wasanii wa kike wa Kimarekani kwa jinsi alivyokuwa amevaa! Itoshe tu kusema kwamba alikuwa amependeza kwelikweli.
Basi nilijikaza kiume pale, na mimi nikamkumbatia, akanibusu shavuni na kunifanya nizidi kudata. Basi nilimkaribisha ndani na kumuonesha ishara kwamba akae, nikatoka na kwenda kufunga geti vizuri, nikarudi na kufunga pia geti la ndani na kuuacha mlango wa mbao wazi.
“Siamini kama nimekuona tena James,” alisema huku akiniita kwa lilejina bandia nililolitumia kufungulia akaunti.
“Kwa nini Saima jamani? Mimi mwenyewe siamini kama nimekutana tena na wewe,” nilisema huku utulivu ukiwa umeniisha kabisa, nilibaki kuzungukazunguka tu mle ndani, nikiwa hata sielewi nataka kufanya nini.
“Utakunywa nini?”
“Aah James, ndiyo kwanza nimefika unaanza kuhangaika na mimi, kukuona tu kumenifanya nisitamani kitu kingine chochote,” alisema huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake, basi nikaishiwa pozi na kulazimika kurudi pale kwenye kiti na kukaa pembeni yake.
“Kwa nini unakuwa bize kiasi hicho jamani,” alisema huku akinisogelea na kunikumbatia, na mimi nikamkumbatia huku mapigo ya moyo yakinienda mbio kwelikweli. Japokuwa awali nilikuwa nikimsifia sana Kezia kwamba ana shepu nzuri na ‘pigo’ zake ni za kisistaduu, kwa Saima ilikuwa ni funga kazi.
Manukato aliyokuwa amejipulizia yalikuwa yananukia vizuri kwelikweli kiasi cha kunifanya nizidi kuchanganyikiwa.
“Kazi ndiyo kila kitu mpenzi wangu, bila kazi unafikiri tutaishije mjini hapa? Na afadhali yenu wenzetu mliosoma,” nilisema kwa sauti iliyoonesha kabisa kubabaika, akacheka sana na kuzidi kunikumbatia kwa nguvu.
“Unaishi na nani hapa,” alisema huku akiniachia na kuanza kutazama huku na kule ndani ya chumba changu.
“Peke yangu,” nilimwambia, akawa ni kama anakumbuka kitu. Niliomba isije ikawa majibu yangu yamejichanganya kwa sababu nakumbuka pia kule benki aliniuliza swali hilohilo. Kwa bahati nzuri, hakuendelea kunihoji kuhusu suala hilo, akaanza kunisifia kwamba naishi sehemu nzuri sana.
“Kumbe mwonekano wako wa nje unaendana na maisha yako halisi, ujue wanaume wengi wana kawaida ya ‘ku-fake’ maisha, ukimuona nje anajifanya kupendeza kwelikweli, lakini mahali anapoishi ni vituko,” alisema huku akicheka, moyoni nikaanza kujisikia vizuri.
Mara alisimama, nikapata nafasi ya kulitazama vizuri umbo lake! Saima alikuwa amejaliwa kila kitu, yaani hata sijui nielezee vipi uzuri wake. Upande wa nyuma alikuwa ametanuka sana chini ya kiuno na kukaribia kufanana na namba nane, basi akawa anazunguka huku na kule mle ndani, akiwa anathaminisha kila kitu kilichokuwemo.
“Huku ndiyo chumbani kwako?” alisema huku akiwa anaelekea kule chumbani, basi ikabidi nisimame na kumfuata ili nimuoneshe na kule ndani kulivyokuwa, kama mwenyewe alivyokuwa anataka, kweli nikamfungulia mlango, akaingia chumbani huku akiendelea kuangaza macho huku na kule, tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake.
Katika sekta ya kujikamilisha pale ndani, nilikuwa najiamini kwa sababu ni kweli ndani kwangu kulikuwa kuzuri kwelikweli, kukiwa na vitu vingi vya thamani ambavyo ni vigumu sana kwa mtu wa umri wangu kuwa navyo, pengine hata wengine walioanza maisha muda mrefu na wanaonizidi umri, hawakuwa na ubavu wa kuishi maisha kama yale.
“Hapa ndipo unapolala,” alisema huku akijirusha kwenye kitanda kikubwa na cha kisasa kilichokuwa kimechukua sehemu kubwa ya chumba cha kulala, basi wote tukawa tunacheka huku akiendelea kunisifia.
Pale alipojirusha, sketi fupi aliyokuwa amevaa, ilipanda juu kidogo na kunifanya niyaone mapaja yake mazuri, yenye weupe wa kung’aa, mapigo ya moyo yakawa yanazidi kunienda mbio huku moyoni nikijisemea ‘kweli leo nimepatikana’.
Basi nilikaa pembeni yake, tukawa tunatazamana huku bado akiwa ameachia tabasamu pana kwenye uso wake, lililomfanya azidi kuonekana mrembo.
“Pole kwa matatizo yaliyokupata,” nilisema, akashusha pumzi ndefu na kuinuka, tukawa tumekaa kitako, akaanza upya kunisimulia kila kilichotokea huku akiwa ananitazama sana machoni.
“Sijui alinigundua jana tulipotazamana naye kule benki?” nilijiuliza mwenyewe moyoni huku mara kwa mara nikiwa nakwepesha macho yangu, basi aliendelea kunielezea kila kitu, akanionesha mchubuko mdogo aliokuwa ameupata kwenye mguu wake wa kushoto.
“Hapa nilichubuka baada ya kuanguka niliposikia risasi zikipigwa huku watu wote tukiamrishwa kulala chini,” aliniambia, moyoni nikawa nazidi kupata hofu kwa sababu hata huyo mtu aliyeanza kufyatua risasi na kuamrisha watu wote walale chini, nilikuwa ni mimi.
Kuna wakati nilihisi huenda ananieleza hivyo ili kunitega ili aujue ukweli, lakini na mimi nikawa mjanja sana wa kujifanya kila alichokuwa ananisimulia ni kigeni kabisa.
“Vipi kuhusu kidani chako?” nilimuuliza kwa mtego nikitaka pia kujua ni nini alichokuwa anakihisi moyoni mwake, basi akaanza kunielezea jinsi kidani hicho kilivyotaka kumuingiza matatizoni.
“Kwa bahati nzuri baba’angu mkubwa yupo kwenye ofisi ya mpelelezi mkuu, yeye ndiye aliyesaidia sana kulimaliza soo, vinginevyo na mimi ningekuwa ndani sasa hivi,” alisema huku uso wake ukibadilika.
“Nikuulize kitu James?”
“Niulize tu Saima.”
“Unajua mimi bado sijaelewa mazingira yaliyosababisha kidani changu kiokotwe pale nje, au labda kuna mtu ulimuazima?”
“Hapa...na! Hapana Saima, siwezi kumuazima mtu kitu cha thamani ulichonipa, yaani hata mimi sielewi. Nahisi labda pengine nilikiangusha pale nje ile siku uliponipa.”
Je, nini kitafuatia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom