Johnny Sins
JF-Expert Member
- Nov 4, 2019
- 2,536
- 3,883
Msaada wa vocha wasomaji.
Kama una vocha ya Halotel,VodaCom au TTCL nisaidieni niendeleze hadithi
Kama una vocha ya Halotel,VodaCom au TTCL nisaidieni niendeleze hadithi
Story nzuri sana ingawa Msanga hakuna kituo cha polisi.SEHEMU YA 37
Nikiwa naendelea kulia kwa nguvu na kuwafanya vijana wa pale mtaani pamoja na wazee wa mtaani wapate kazi ya kunituliza, nilishtuka baada ya kuona gari la polisi likija pale nyumbani, pombe zote ni kama ziliyeyuka kichwani, nilipogeuka na kutazama pale Bonta alipokuwepo, sikumuona, moyo ukawa unadunda kwa nguvu kuliko kawaida, ni nikiwa ni kama siamini kilichokuwa kinatokea.
SASA ENDELEA...
Naomba maji ya kunywa, ngojeni nikanywe maji,” nilisema huku nikiinuka, uso wangu ukiwa umejawa machozi na kamasi maana nilikuwa nalia kwelikweli ingawa kilio chote kilikatika ghafla baada ya kuwaona wale polisi.
Ujio wao ulionesha wazi kwamba haukuwa wa kawaida, si kawaida polisi kwenda misibani labda katika yale matukio ambayo kifo kimetokea katika mazingira ya kutatanisha, baba hakuwa amekufa kifo cha kutatanisha kwa hiyo ujio huo ulikuwa ni kwa lengo maalum.
Nilitembea harakaharaka huku safari hii hata ile hali ya kupepesuka ikiwa imeisha kabisa, watu wakawa wananitazama huku pia wakitazama kilichonifanya niwe kwenye hali hiyo.
Nilipoingia ndani, nilienda mpaka kwenye dirisha lililokuwa pembeni ya mlango, sikujali waombolezaji waliokuwa wakiendelea kulia, nilijisogeza na kuanza kuchungulia kule nje.
Niliwaona wale polisi wakisogea mpaka pale walipokuwa wamekaa waombolezaji wengine, muda mfupi baadaye nilimuona mwenyekiti wa serikali ya mtaa ambaye naye alikuwa pale msibani, akisimama na kuwafuata wale polisi.
Wakasalimiana kisha wakawa wanazungumza kitu ambacho hata sikuelewa ni nini, nikamuona yule mwenyekiti akigeuka na kuwaoneshea kule ndani, wakaanza kuja. Nilitamani dunia ipasuke na kunimeza, watu wote pale msibani walitulia wakiwa na shauku kubwa ya kutaka kuona nini kilichowaleta askari hao hapo msibani.
Bado sikuwa na majibu, wamefuata nini? Wamejuaje kama nipo pale? Akili za harakaharaka zilinituma kukimbilia kule kwenye chumba kilichokuwa na mwili wa marehemu baba, huko ndiyo mahali pekee ambako hakukuwa na watu. Niliingia mbiombio na kwenda kujifungia mlango kwa ndani, nikawa nautazama mwili wa baba uliokuwa umelala kitandani huku ukiwa umefunikwa sanda, sikuwa najua nini cha kufanya.
Mara nilipata wazo, nililitazama dirisha la chumba hicho ambalo halikuwa limejengwa kwa uimara, nikasogea na kujaribu kulitingisha, niliona likianza kutingishika, nikaona hiyo ndiyo njia pekee ya mimi kujiokoa.
Kumbe wakati mimi nikiwaza hivyo, wale askari tayari walikuwa wameenda mbele zaidi kiakili kuliko mimi, kumbe wakati wengine wakija kule ndani wengine walizunguka upande wa nyuma wa nyuma yetu, wakati nikiendelea kulitingisha kwa lengo la kulivunja ili nitoke na kukimbia, nilimuona askari mmoja akiwa amesimama na bunduki huku akiwa ameilengesha palepale dirishani, kama anayesubiri nitoke tu amalize kazi.
“Mungu wangu, nimekwisha,” nilijisemea huku nikisogea ukutani haraka, mara nikaanza kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu.
“Kenny! Kennedy,” nilisikia yule mwenyekiti akiniita, nikajua mwisho wangu umewadia. Kitu pekee nilichoweza kukifanya, ilikuwa ni kutoa bastola pale kiunoni nilipokuwa nimeificha pamoja na zile fedha nyingine ambazo nilikuwa nazo mfukoni, achilia zile nyingine ambazo nilipofika tu nilienda kuzificha kwenye chumba kilichokuwa kinatumiwa na ndugu zetu wa kike hapo nyumbani.
“Sasa nitaificha wapi?” niliwaza wakati mlango ukiendelea kugongwa, nilimtazama marehemu baba ambaye bado alikuwa pale kitandani, nikapata wazo la kwenda kuficha vitu hivyo kwenye sanda aliyokuwa amefungwa.
Nilijua hata kama polisi watakuwa na machale kiasi gani, hakuna anayeweza kwenda kuipekua maiti, ndani ya sekunde chache nilikuwa nimeshaifunua ile sanda, nikaichomeka bastola na zile fedha kisha nikairudishia vizuri.
Mungu anisamehe kwa kitendo hicho na hata baba huko aliko naamini atakuwa amenisamehe kwa sababu sikwa na kitu kingine cha kufanya kwa wakati huo, kwani kama ningesema niirushe ile bastola nje, wale askari wangeiona, kama ningesema niifiche sehemu nyingie yoyote mle ndani, lazima wangenipekua na kuiona! Nasisitiza tena sikuwa na cha kufanya.
Baada ya kuhakikisha nimeirudishia ile sanda vizuri, nilisogea pale mlangoni na kufungua mlango huku nikijikamua machozi, nikakutana uso kwa uso na mwenyekiti na wale askari.
“Kijana mwenyewe ndiyo huyu!” alisema mwenyekiti huku akiwaonesha wale askari kwangu, mmoja kati yao akanisalimu kwa kuniita jina langu kisha akaniambia wana mazungumzo na mimi na kabla hata sijajibu chochote, nilishtukia nikivalishwa pingu kwenye mikono yangu kwa mbele.
“Kwa nini unanifunga pingu? Nimefanya kosa gani? Halafu mna mazungumzo gani wakati mimi nipo kwenye msiba wa baba yangu?” nilisema huku nikiendelea kujivisha sura ya majonzi ambayo ilificha kabisa uhalisia uliokuwa nyuma ya pazia.
“Kwani kuna nini? Afande kwani kuna nini baba zangu, mbona mmemfunga mwanangu pingu?” mama aliingilia kati na kuwauliza wale askari huku uso wake ukiwa umejawa na huzuni kubwa kutokana na majonzi ya kuondokewa na mumewe, macho yake yakiwa yanazitazama zile pingu nilizofungwa.
“Tunahitaji kuzungumza na huyu kijana lakini naona analeta ubishi.”
“Mnazungumza naye nini baba zangu wakati mnajua tupo msibani, na mwili wa baba yake bado hata haujaenda kuzikwa? Halafu kwa nini mumfunge pingu? Kwani mmeambiwa huyu jambazi?”
“Mama, siyo kwamba tunamuonea mwanao, tunatekeleza kazi zetu za kisheria, wala hatujafika hapa kwa kubahatisha. Huyu mwanao ni mhalifu, hebu ngoja kwanza tumpekue huku na wewe ukishuhudia,” alisema yule askari, nadhani walishakuwa na uhakika kwamba kuna kitu watanikuta nacho.
Akanishika mikono ambayo tayari ilikuwa na pingu na kuiinua kwa upande wa mbele kisha akaanza kunipapasa mwili mzima lakini hakukuta chochote. Alirudia zaidi ya mara tatu lakini majibu yalikuwa ni yaleyale, wale askari wakawa wanatazamana kisha wakamgeukia yule mwenyekiti.
Mpaka hapo nilishakuwa naelewa ni nini kinachoendelea, ile hofu niliyokuwa nayo ikapungua moyoni kwa sababu niligundua kwamba kumbe wale askari hawanifahamu na hawajui lolote kuhusu mimi isipokuwa kuna ‘mshakunaku’ mmoja amewapigia simu ili waje kunikamata na moyo wangu ulinituma kumhisi yule mwenyekiti.
“Kenny hebu nenda kazungumze nao nje, sitaki mniharibie msiba wa mume wangu, samahani sana,” alisema mama huku akianza tena kulia, sikutaka kumuona mama akilia kwa hiyo ikabidi nikubali haraka kuepusha shari, nikatoka nao hadi nje huku pia tukiwa tumeongozana na yule mwenyekiti ambaye mara kwa mara nilikuwa namkata jicho.
Watu wote pale nje waliacha kila walichokuwa wanakifanya na kuanza kushangaa kuona natolewa na polisi tena nikiwa nimefungwa pingu na kukokotwa mzobemzobe. Niliwasikai baadhi ya akina mama wakianza kuangua vilio kwa sababu ulikuwa ni msiba juu ya msiba.
“Yule mzee mnoko sana yule, sijui anataka mwenzake asimzike baba yake,” nilimsikia kijana mmoja wa pale mtaani akiongea wakati mimi nikitolewa mzobemzobe, wenzake wakawa wanamuunga mkono, hisia zangu kwamba mwenyekiti alikuwa amenichoma kwa polisi zikazidi kuongezeka.
“Halafu umekunywa sana pombe! Yaani asubuhi yote hii umelewa wakati upo kwenye msiba wa baba yako?”
“Nilikunywa jana usiku, siyo asubuhi.”
“Kijana mdogo kama wewe kwa nini unakuwa mlevi kiasi hiki? Halafu hata midomo yako imebadilika rangi na kuwa myeusi, unavuta bangi wewe si ndiyo?”
“Afande eeh! Tuheshimiane basi,” nilimkoromea askari mmoja niliyeona sasa ameanza kuvuka mipaka na kuniuliza maswali yasiyo nakichwa wala miguu. Jambo ambalo walikuwa hawalijui ni kwamba nikiwa kwenye anga zangu, huwa siwaogopi kabisa askari na nilishawafanyia mambo mabaya sana wenzao kadhaa na hata usiku uliopita tu, tulifanya tukio Ubungo tukiwa na Bonta.
Kichwani nilishajengewa itikadi kwamba askari yoyote yule ni adui yangu, awe mwanamke au mwanaume, kijana au mzee, ilimradi ni askari basi hakuna urafikikati yetu.
“Unabishana na chombo cha dola si ndiyo,” alisema yule askari niliyemkoromea huku akigeuka huku na kule kuangalia kama bado watu walikuwa wakitutazama. Ilivyoonesha, kama kusingekuwa na watu wanaotutazama angeweza kunifanyizia kitu kibaya sana.
Na hapa ndipo askari wengi wanapokosea, wapo baadhi ambao wanaamini kwa sababu wamepitia mafunzo ya kiaskari, basi wanayo haki ya kuwaonea au kuwanyanyasa raia na matokeo yake, hata raia wa kawaida, achana na wahalifu kama mimi, wanakuwa na vinyongo na askari na ndiyo maana hata wakisikia wamepatwa na jambo baya, wanachekelea! Hii ni kwa sababu ya ubabe wa baadhi yao.
“Chombo cha dola utakuwa wewe bwana!” nilizidi kumjibu mbovu yule askari, akawa ananitazama kwa kunitamani kwelikweli huku na mimi nikimtazama vizuri kwa lengo la kumkariri sura yake.
Waliniondoa pale msibani mpaka kwenye kituo kidogo ambacho hakikuwa mbali na pale nyumbani, nikaingizwa ndani na kuanza kuhojiwa, madaiyao eti walisema wamepigiwa simu na msamaria mwema kwamba nilikuwa nafanya fujo msibani na kutishia watu bastola.
“Usalama wako utueleze hiyo bastola iko wapi, vinginevyo kazi unayo.”
“Bastola? Bastola gani, umenipa bastola wewe? Halafu we mzee nimekuona kuanzia kule unanifuatafuata sana, sasa dawa yako inachemka,” nilisema kwa kujiamini, uzoefu wa kutumia bunduki, mazoezi niliyokuwa nayafanya kule ngome ukichanganya na pombe kali niliyokuwa nimekunywa na mibange niliyovuta usiku uliopita, vilinipa ujasiri usio wa kawaida ambao uliwafanya wale askari uvumilivu wao ufike mwisho.
“Unasemaje dogo? Mpeni chai huyu maana naona anatuzoea sasa,” alisema mwingine aliyeonekana kuwa na cheo, yule askari ambaye kuanzia kule nyumbani tulikuwa tukijibizana ‘fyongo’, akawa wa kwanza kunisogelea huku akikenua meno yake kama anayeshangilia kwamba hatimaye amepewa ruhusa ya kunishughulikia.
Kufumba na kufumbua, alinipiga ngumi mbili nzito tumboni zilizosababisha nikohoe damu. Je, nini kitafuatia?
Tupo macho, dondosha tu.Amkeni