Johnny Sins
JF-Expert Member
- Nov 4, 2019
- 2,536
- 3,883
SEHEMU YA 39
Nilipiga magoti kwa heshima pembeni ya kaburi lake, machozi yakawa yananitoka kwa wingi. Bado sikuwa na majibu kama ile bastola niliyoificha kwenye sanda yake pamoja na fedha alikuwa amezikwa nazo au la!
SASA ENDELEA...
“Pole sana mdogo wangu, naujua uchungu wa kuondokewa na baba, afadhali wewe ameondoka ukiwa umeshakuwa mkubwa, mimi baba yangu alifariki nikiwa bado mdogo sana,” alisema Bonta huku akinipigapiga begani, akawa ananifariji kwa upole na kunitaka nijikaze.
Nilikaa pale kaburini kwa zaidi ya nusu saa, ndugu zangu wengine wote wakaondoka na kuniacha mimi na Bonta, baadaye niliinuka pale nilipokuwa nimepiga magoti na kusogea pale chini ya mkorosho alipokuwa amekaa Bonta, tukakumbatiana huku nikiwa bado naendelea kulia.
“Nilificha mashine na fedha kidogo kwenye sanda ya baba wale polisi walipokuja kunikamata.”
“Najua! Nimekuhifadhia,” alinijibu Bonta na kunifanya nipigwe na butwaa.
“Kwani ilikuwaje, mbona walipofika sikukuona, uliyeyukia wapi?” nilimuuliza Bonta, hakunijibu chochote badala yake, alipandisha mkono wa fulana yake na kunionesha hirizi kubwa aliyokuwa ameivaa.
“Nilikwambia kuhusu hili suala naona mpaka leo hujanipa majibu,” aliniambia, nikashusha pumzi ndefu na kumtazama. Hakuwa amenijibu swali langu, nikamuuliza tena. Aliniambia kwamba akiwa amekaa pale nje, alianza kuhisi hirizi hiyo ikimbana, akalazimika kuondoka haraka na muda mfupi baadaye ndipo askari walipowasili.
“Pombe huziwezi mdogo wangu, siku nyingine utakuja kusababisha matatizo makubwa sana, unatakiwa kuwa makini,” aliniambia na kuanza kunipa somo la jinsi ninavyotakiwa ‘ku-behave’ ninapokuwa mbele ya macho ya watu.
Nilichokuwa nampendea Bonta ni kwamba alikuwa akizungumza na mimi kwa busara sana, alikuwa ananijenga sana kiakili. Aliniambia kama najijua nina kichwa cha panzi, basi nisilewe mbele za watu, nikitaka kunywa bora ninywe kiasi kidogo au kama nataka kulewa basi nijifungie ndani. Nilimuahidi kwamba suala kama hilo haliwezi kujirudia tena na nitakuwa makini zaidi.
“Jioni tunatakiwa kurudi kambini, huku hakufai tena,” aliniambia Bonta, nikatingisha kichwa kuonesha kukubaliana naye. Tuliondoka pale kaburini na kurudi kule nyumbani, tukakaa pale chini ya mti wa mkorosho huku kila mmoja akitafakari mambo yake.
Bado moyo wangu ulikuwa na chuki kubwa kwa wote waliosababisha nishindwe kumzika baba na nilijiapiza kwamba lazima siku moja walipie kwa walichokifanya. Muda uliyoyoma kwa kasi na hatimaye kigiza kikaanza kuingia, nilienda ndani na kukaa na mama, nikawa namfariji kwa sababu bado alikuwa na uchungu mkali ndani ya moyo wake.
“Kuwa makini mwanangu, naomba utafute fedha kwa njia za halali, ukifanya kazi halali utakuwa na maisha mazuri sana kwa sababu inaonekana una nyota inayowaka sana. Ila usipende njia za mkato,” mama aliniambia kwa upole baada ya kumwambia kwamba jioni hiyo natakiwa kurudi Dar es Salaam kwa sababu kesho yake asubuhi natakiwa kazini.
Mama aliongea mambo mengi sana, kwa jinsi ilivyoonesha na yeye alishaanza kuwa na wasiwasi juu ya mwenendo wangu. Alinisihi sana kuachana na ulevi na kunitaka nisimame imara kama kiongozi wa familia.
“Baba yako hatunaye tena, wewe ndiyo unatakiwa kuwa kiongozi wa hii familia, ukifanya uzembe ujue kwamba tutakaoumia ni sisi, nakupenda sana mwanangu. Pia baba yako ameondoka lakini tumebaki na madeni mengi makubwa, kama unavyojua kipindi cha mwanzo fedha zote za matibabu tulikuwa tunaazima kwa watu,” alisema mama.
Kuhusu hilo la madeni, nilimwambia nitalimaliza na hakuna tatizo na ili kumfanya awe na amani, palepale tulianza kuorodhesha watu wote waliokuwa wanatudai na viwango vya fedha, tukajumlisha fedha zote kisha nikamhakikishia mama kwamba kabla sijaondoka nitampa akawalipe.
“Unazo hela zote?”
“Ndiyo mama!” nilimjibu kwa kujiamini, basi akashindwa kujizuia, akanikumbatia huku akianza tena kulia. Sijui kwa nini alikuwa akinikumbatia analia sana kwa sababu hiyo haikuwa mara ya kwanza.
Basi nilimhakikishia kwamba nimemuelewa na nitayafanyia kazi mambo yote aliyoniambia, nikainuka na kuelekea kule chumbani nilikokuwa nimehifadhi ule mzigo wa fedha niliokuja nao, nikahesabu kiasi cha madeni yanayotakiwa kulipwa, nikaziweka pembeni kisha zile nyingine nikazifunga vizuri kwenye mfuko, nikarudi kule nilikomuacha mama.
Nilimkabidhi burungutu la hela za madeni, kisha nikampa ulemfuko mwingine uliokuwa na mabunda kadhaa ya fedha, nikamwambia anihifadhie lakini kama kutakuwa na mahitaji yoyote pale nyumbani, asisite kutumia.
“Umepata wapi mihela yote hii mwanangu?” aliniuliza huku akiwa ni kama haamini.
“Nafanya kazi mama, na bosi wangu aliposikia nimefiwa, ameguswa sana na kunipa fedha kwa ajili ya kunisaidia masuala yote ya msiba,” nilimwambia, akanikumbatia tena na kuanza kuzihesabu zile fedha.
Niliona kabisa mikono yake ikiwa inatetemeka kwa sababu fedha zina tabia moja, ukipewa kiwango kikubwa ambacho hujawahi kukishika katika maisha yako, lazima utetemeke. Tena ukiambiwa kwa mfano uzitoe sehemu moja kwenye nyingine ndiyo kabisaa! Fedha nyingi zinaogopesha sana.
Basi baada ya muda, tuliaga, ikiwa ni takribani saa mbili za usiku, kabla sijaondoka niliwagawia fedha ndugu zangu wote, kila mmoja kwa ajili ya mahitaji yake madogomadogo, wakanishukuru sana na kuniona kama mkombozi wao.
Tulitoka na Bonta mpaka kituoni, kwa muda ule, magari yalikuwa ni ya kuvizia kwa sababu muda ulikuwa umeenda sana. Tukiwa pale kituoni tukisubiri gari, Bonta alinipa ile bastola yangu pamoja na zile fedha.
Nilijaribu sana kumdadisi kwamba yeye aliionaje bastola hiyo wakati nilikuwa nimeificha kwenye sanda? Akaniambia kwa watu wanaopata mafunzo kila siku kama mimi na yeye, ni rahisi kwa mmoja kugundua mwenzake anawaza nini haraka.
“Nilijua hawawezi kukukamata na bunduki kwa sababu hata kama ulikuwa umelewa, wewe siyo mjinga kiasi hicho. Walivyoondoka na wewe, mimi nilikuwa mtu wa kwanza kuingia kule chumbani, nikatafuta kila sehemu lakini sikuiona, nikajua lazima itakuwa pale kitandani, na kweli niliiona kwenye sanda,” alisema Bonta na kunifanya niishiwe na maneno.
Tuliendelea kusubiri usafiri na kwa bahati nzuri, tulipata lifti kwenye gari lililokuwa limebeba mananasi. Bonta aliniambia kwamba usafiri huo ni mzuri zaidi kwetu kwa sababu hakuna anayeweza kutushtukia, hasa ukizingatia kwamba ilikuwa ni usiku. Basi tuliianza safari, tukiwa tumebanana kule mbele kwa dereva.
Njiani tulisimamishwa na trafiki mara moja tu na wala hakuwa na shida na sisi bali dereva ambaye naye alipompa ‘kitu kidogo’, alituruhusu.
Hatimaye tuliwasili Gongo la Mboto, ikiwa ni karibu saa nne za usiku. Bonta akaniambia kwamba muda huo haukuwa mzuri kwetu kutembea, tukaingia kwenye baa moja iliyopo karibu na barabarani, tukala chakula na kunywa kidogo wakati tukivutavuta muda.
Kwenye kama saa sita kasoro hivi, tuliondoka kwa kutumia bodaboda mbili, tukaenda mpaka nyumbani kwangu, Sinza. Kwa jinsi tulivyokuwa tumechoka, ilibidi tupumzike kidogo, mimi nikaoga na kubadilisha nguo, kwenye kama saa tisa kasoro za usiku, tulitoka na safari ya kuelekea kambini kwa kutumia pikipiki ya Bonta ilianza. Kila kitu kilikuwa kikifanyika usiku kwa usiku.
Saa kumi na moja alfajiri, tayari tulikuwa tumeshawasili kambini Kibaha, tukakuta wenzetu ndiyo wanamalizia kufanya mazoezi. Kama zilivyokuwa taratibu za pale, tulisaini karibu sehemu tatu, kuanzia kule getini, mapokezi na kwa matron kuonesha kwamba tulikuwa tumerudi salama.
Kutokana na uchovu niliokuwa nao, nilienda moja kwa moja chumbani kwangu, nikavua nguo zote na kuzitupa pembeni, nikapanda kitandani na kujilaza na haukupita muda mrefu, nikapitiwa na usingizi mzito.
Nilipokuja kuzinduka, tayari jua lilikuwa kali na kilichonishtua, ni baada ya kuhisi kuna mtu alikuwa amelala pembeni yangu. Niliamka kichovu, kuangalia pembeni nikamuona Kezia akiwa amejilaza pembeni yangu, akiwa amejitanda na mtandio mwepesi bila kuwa na kitu kingine chochote.
“Pole na msiba mume wangu na pole na safari,” aliniambia huku akinikumbatia kwa mahaba na kuanza kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu.
“Ahsante Kezia, asa...nte sa...na,” nilisema huku nikijaribu kujitoa kwenye mwili wake kwa sababu alikuwa akinifanyia uchokozi wa hali ya juu na kwa wakati huo sikuwa kwenye ‘mood’ ya kile alichokuwa anakitaka.
Nilifanikiwa kumtoa, akawa ananitazama usoni kwa mshangao.
“Umepatwa na nini tena, mbona umeumia hivyo?” alisema kwa upole. Kumbe muda wote hakuwa amenitazama vizuri, nikashusha pumzi ndefu na kumjibu kwa kifupi kwamba asiwe na wasiwasi mimi niko sawa.
“Uko sawa kivipi? Angalia jicho moja limevilia damu, usoni una alama nyingi, nani amekufanyia hivi?” Kezia alizidi kunidadisi huku akiendelea kunikagua mwili mzima.
Kiukweli kipigo cha wale askari kilikuwa kimenisababishia maumivu makali sana mwilini, kama isingekuwa uwezo wangu wa kuhimili maumivu, pengine nisingeweza hata kuinuka kitandani.
“Pole sana mume wangu,” alisema Kezia huku akiinuka, akavaa nguo zake harakaharaka na kuniambia nimsubiri. Alitoka na aliporudi, alikuwa na kiboksi cha huduma ya kwanza mkononi huku mkono mwingine akiwa ameshika birika la ‘heater’.
Akafungulia maji kwenye bomba la mle ndani na kujaza kwenye birika, akalichomeka kwenye umeme na kuanza kuchemsha maji. Maji yalipochemka, aliniandaa vizuri kisha akaanza kunichua maeneo yote yaliyokuwa na maumivu. Kiukweli alinisaidia sana kwa sababu nilikuwa na maumivu karibu mwili mzima.
Je, nini kitafuatia?
Nilipiga magoti kwa heshima pembeni ya kaburi lake, machozi yakawa yananitoka kwa wingi. Bado sikuwa na majibu kama ile bastola niliyoificha kwenye sanda yake pamoja na fedha alikuwa amezikwa nazo au la!
SASA ENDELEA...
“Pole sana mdogo wangu, naujua uchungu wa kuondokewa na baba, afadhali wewe ameondoka ukiwa umeshakuwa mkubwa, mimi baba yangu alifariki nikiwa bado mdogo sana,” alisema Bonta huku akinipigapiga begani, akawa ananifariji kwa upole na kunitaka nijikaze.
Nilikaa pale kaburini kwa zaidi ya nusu saa, ndugu zangu wengine wote wakaondoka na kuniacha mimi na Bonta, baadaye niliinuka pale nilipokuwa nimepiga magoti na kusogea pale chini ya mkorosho alipokuwa amekaa Bonta, tukakumbatiana huku nikiwa bado naendelea kulia.
“Nilificha mashine na fedha kidogo kwenye sanda ya baba wale polisi walipokuja kunikamata.”
“Najua! Nimekuhifadhia,” alinijibu Bonta na kunifanya nipigwe na butwaa.
“Kwani ilikuwaje, mbona walipofika sikukuona, uliyeyukia wapi?” nilimuuliza Bonta, hakunijibu chochote badala yake, alipandisha mkono wa fulana yake na kunionesha hirizi kubwa aliyokuwa ameivaa.
“Nilikwambia kuhusu hili suala naona mpaka leo hujanipa majibu,” aliniambia, nikashusha pumzi ndefu na kumtazama. Hakuwa amenijibu swali langu, nikamuuliza tena. Aliniambia kwamba akiwa amekaa pale nje, alianza kuhisi hirizi hiyo ikimbana, akalazimika kuondoka haraka na muda mfupi baadaye ndipo askari walipowasili.
“Pombe huziwezi mdogo wangu, siku nyingine utakuja kusababisha matatizo makubwa sana, unatakiwa kuwa makini,” aliniambia na kuanza kunipa somo la jinsi ninavyotakiwa ‘ku-behave’ ninapokuwa mbele ya macho ya watu.
Nilichokuwa nampendea Bonta ni kwamba alikuwa akizungumza na mimi kwa busara sana, alikuwa ananijenga sana kiakili. Aliniambia kama najijua nina kichwa cha panzi, basi nisilewe mbele za watu, nikitaka kunywa bora ninywe kiasi kidogo au kama nataka kulewa basi nijifungie ndani. Nilimuahidi kwamba suala kama hilo haliwezi kujirudia tena na nitakuwa makini zaidi.
“Jioni tunatakiwa kurudi kambini, huku hakufai tena,” aliniambia Bonta, nikatingisha kichwa kuonesha kukubaliana naye. Tuliondoka pale kaburini na kurudi kule nyumbani, tukakaa pale chini ya mti wa mkorosho huku kila mmoja akitafakari mambo yake.
Bado moyo wangu ulikuwa na chuki kubwa kwa wote waliosababisha nishindwe kumzika baba na nilijiapiza kwamba lazima siku moja walipie kwa walichokifanya. Muda uliyoyoma kwa kasi na hatimaye kigiza kikaanza kuingia, nilienda ndani na kukaa na mama, nikawa namfariji kwa sababu bado alikuwa na uchungu mkali ndani ya moyo wake.
“Kuwa makini mwanangu, naomba utafute fedha kwa njia za halali, ukifanya kazi halali utakuwa na maisha mazuri sana kwa sababu inaonekana una nyota inayowaka sana. Ila usipende njia za mkato,” mama aliniambia kwa upole baada ya kumwambia kwamba jioni hiyo natakiwa kurudi Dar es Salaam kwa sababu kesho yake asubuhi natakiwa kazini.
Mama aliongea mambo mengi sana, kwa jinsi ilivyoonesha na yeye alishaanza kuwa na wasiwasi juu ya mwenendo wangu. Alinisihi sana kuachana na ulevi na kunitaka nisimame imara kama kiongozi wa familia.
“Baba yako hatunaye tena, wewe ndiyo unatakiwa kuwa kiongozi wa hii familia, ukifanya uzembe ujue kwamba tutakaoumia ni sisi, nakupenda sana mwanangu. Pia baba yako ameondoka lakini tumebaki na madeni mengi makubwa, kama unavyojua kipindi cha mwanzo fedha zote za matibabu tulikuwa tunaazima kwa watu,” alisema mama.
Kuhusu hilo la madeni, nilimwambia nitalimaliza na hakuna tatizo na ili kumfanya awe na amani, palepale tulianza kuorodhesha watu wote waliokuwa wanatudai na viwango vya fedha, tukajumlisha fedha zote kisha nikamhakikishia mama kwamba kabla sijaondoka nitampa akawalipe.
“Unazo hela zote?”
“Ndiyo mama!” nilimjibu kwa kujiamini, basi akashindwa kujizuia, akanikumbatia huku akianza tena kulia. Sijui kwa nini alikuwa akinikumbatia analia sana kwa sababu hiyo haikuwa mara ya kwanza.
Basi nilimhakikishia kwamba nimemuelewa na nitayafanyia kazi mambo yote aliyoniambia, nikainuka na kuelekea kule chumbani nilikokuwa nimehifadhi ule mzigo wa fedha niliokuja nao, nikahesabu kiasi cha madeni yanayotakiwa kulipwa, nikaziweka pembeni kisha zile nyingine nikazifunga vizuri kwenye mfuko, nikarudi kule nilikomuacha mama.
Nilimkabidhi burungutu la hela za madeni, kisha nikampa ulemfuko mwingine uliokuwa na mabunda kadhaa ya fedha, nikamwambia anihifadhie lakini kama kutakuwa na mahitaji yoyote pale nyumbani, asisite kutumia.
“Umepata wapi mihela yote hii mwanangu?” aliniuliza huku akiwa ni kama haamini.
“Nafanya kazi mama, na bosi wangu aliposikia nimefiwa, ameguswa sana na kunipa fedha kwa ajili ya kunisaidia masuala yote ya msiba,” nilimwambia, akanikumbatia tena na kuanza kuzihesabu zile fedha.
Niliona kabisa mikono yake ikiwa inatetemeka kwa sababu fedha zina tabia moja, ukipewa kiwango kikubwa ambacho hujawahi kukishika katika maisha yako, lazima utetemeke. Tena ukiambiwa kwa mfano uzitoe sehemu moja kwenye nyingine ndiyo kabisaa! Fedha nyingi zinaogopesha sana.
Basi baada ya muda, tuliaga, ikiwa ni takribani saa mbili za usiku, kabla sijaondoka niliwagawia fedha ndugu zangu wote, kila mmoja kwa ajili ya mahitaji yake madogomadogo, wakanishukuru sana na kuniona kama mkombozi wao.
Tulitoka na Bonta mpaka kituoni, kwa muda ule, magari yalikuwa ni ya kuvizia kwa sababu muda ulikuwa umeenda sana. Tukiwa pale kituoni tukisubiri gari, Bonta alinipa ile bastola yangu pamoja na zile fedha.
Nilijaribu sana kumdadisi kwamba yeye aliionaje bastola hiyo wakati nilikuwa nimeificha kwenye sanda? Akaniambia kwa watu wanaopata mafunzo kila siku kama mimi na yeye, ni rahisi kwa mmoja kugundua mwenzake anawaza nini haraka.
“Nilijua hawawezi kukukamata na bunduki kwa sababu hata kama ulikuwa umelewa, wewe siyo mjinga kiasi hicho. Walivyoondoka na wewe, mimi nilikuwa mtu wa kwanza kuingia kule chumbani, nikatafuta kila sehemu lakini sikuiona, nikajua lazima itakuwa pale kitandani, na kweli niliiona kwenye sanda,” alisema Bonta na kunifanya niishiwe na maneno.
Tuliendelea kusubiri usafiri na kwa bahati nzuri, tulipata lifti kwenye gari lililokuwa limebeba mananasi. Bonta aliniambia kwamba usafiri huo ni mzuri zaidi kwetu kwa sababu hakuna anayeweza kutushtukia, hasa ukizingatia kwamba ilikuwa ni usiku. Basi tuliianza safari, tukiwa tumebanana kule mbele kwa dereva.
Njiani tulisimamishwa na trafiki mara moja tu na wala hakuwa na shida na sisi bali dereva ambaye naye alipompa ‘kitu kidogo’, alituruhusu.
Hatimaye tuliwasili Gongo la Mboto, ikiwa ni karibu saa nne za usiku. Bonta akaniambia kwamba muda huo haukuwa mzuri kwetu kutembea, tukaingia kwenye baa moja iliyopo karibu na barabarani, tukala chakula na kunywa kidogo wakati tukivutavuta muda.
Kwenye kama saa sita kasoro hivi, tuliondoka kwa kutumia bodaboda mbili, tukaenda mpaka nyumbani kwangu, Sinza. Kwa jinsi tulivyokuwa tumechoka, ilibidi tupumzike kidogo, mimi nikaoga na kubadilisha nguo, kwenye kama saa tisa kasoro za usiku, tulitoka na safari ya kuelekea kambini kwa kutumia pikipiki ya Bonta ilianza. Kila kitu kilikuwa kikifanyika usiku kwa usiku.
Saa kumi na moja alfajiri, tayari tulikuwa tumeshawasili kambini Kibaha, tukakuta wenzetu ndiyo wanamalizia kufanya mazoezi. Kama zilivyokuwa taratibu za pale, tulisaini karibu sehemu tatu, kuanzia kule getini, mapokezi na kwa matron kuonesha kwamba tulikuwa tumerudi salama.
Kutokana na uchovu niliokuwa nao, nilienda moja kwa moja chumbani kwangu, nikavua nguo zote na kuzitupa pembeni, nikapanda kitandani na kujilaza na haukupita muda mrefu, nikapitiwa na usingizi mzito.
Nilipokuja kuzinduka, tayari jua lilikuwa kali na kilichonishtua, ni baada ya kuhisi kuna mtu alikuwa amelala pembeni yangu. Niliamka kichovu, kuangalia pembeni nikamuona Kezia akiwa amejilaza pembeni yangu, akiwa amejitanda na mtandio mwepesi bila kuwa na kitu kingine chochote.
“Pole na msiba mume wangu na pole na safari,” aliniambia huku akinikumbatia kwa mahaba na kuanza kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu.
“Ahsante Kezia, asa...nte sa...na,” nilisema huku nikijaribu kujitoa kwenye mwili wake kwa sababu alikuwa akinifanyia uchokozi wa hali ya juu na kwa wakati huo sikuwa kwenye ‘mood’ ya kile alichokuwa anakitaka.
Nilifanikiwa kumtoa, akawa ananitazama usoni kwa mshangao.
“Umepatwa na nini tena, mbona umeumia hivyo?” alisema kwa upole. Kumbe muda wote hakuwa amenitazama vizuri, nikashusha pumzi ndefu na kumjibu kwa kifupi kwamba asiwe na wasiwasi mimi niko sawa.
“Uko sawa kivipi? Angalia jicho moja limevilia damu, usoni una alama nyingi, nani amekufanyia hivi?” Kezia alizidi kunidadisi huku akiendelea kunikagua mwili mzima.
Kiukweli kipigo cha wale askari kilikuwa kimenisababishia maumivu makali sana mwilini, kama isingekuwa uwezo wangu wa kuhimili maumivu, pengine nisingeweza hata kuinuka kitandani.
“Pole sana mume wangu,” alisema Kezia huku akiinuka, akavaa nguo zake harakaharaka na kuniambia nimsubiri. Alitoka na aliporudi, alikuwa na kiboksi cha huduma ya kwanza mkononi huku mkono mwingine akiwa ameshika birika la ‘heater’.
Akafungulia maji kwenye bomba la mle ndani na kujaza kwenye birika, akalichomeka kwenye umeme na kuanza kuchemsha maji. Maji yalipochemka, aliniandaa vizuri kisha akaanza kunichua maeneo yote yaliyokuwa na maumivu. Kiukweli alinisaidia sana kwa sababu nilikuwa na maumivu karibu mwili mzima.
Je, nini kitafuatia?