Dam55
JF-Expert Member
- Oct 8, 2015
- 5,592
- 11,831
Riwaya: Pasipoti ya Gaidi part 1
Mtunzi: Richard Mwambe
Pasipoti ya Gaidi: Hujuma na Uzandiki
Sura ya I
Ikulu – Dar es Salaam
Saa 10:30 Alfajiri
Wakati giza likijiandaa kutoweka na kuipisha nuru ya asubuhi, miti yote ilikuwa imetulia kana kwamba kuna aliyeiambia ifanye hivyo. ni tausi mmoja mmoja aliyekuwa akilia alfajiri hii tena kwa nyakati tofauti. hawakuwa na zamu ya kufanya hivyo isipokuwa ilitokea tu, ndivyo walivyoumbwa. hawakuwa wakijua lolote linaloendelea katika maisha ya mwanadamu wakati huo, zaidi walisubiri kukuche waendelee kupendezesha mandhari ya eneo hilo. hawa walikuwa kivutio kikubwa sana katika eneo hilo kwa wapiti njia.
Hekaheka katika jengo hilo la makao makuu ya rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania ilikuwa kubwa. vijana wa jeshi la polisi, kikosi maalum cha kutuliza ghasia, walikuwepo wakiwa kimejiweka tayari kwa lolote, ijapokuwa huwa hapo kwa lindo kila siku lakini leo hii walikuwa kivingine kabisa. mbali na wao, eneo hilo, afajiri hiyo lilizungukwa pia na vijana wa jeshi la wananchi waliovalia kombati zao za mabakamabaka, wakiwa na silaha nzitonzito mikononi mwao, kila mmoja akionekana kutingwa na shughuli inayompasa kufanya kwa muda huo. magari ya wagonjwa kutoka jeshi la wananchi yalikuwa yikifanya kazi ya kubeba majeruhi na maiti zilizokutwa ndani ya jengo hilo, hekaheka.
msemaji wa ikulu alikuwa kasimama katikati ya ukumbi mkubwa ndani ya jengo hilo, alikuwa kimya bila kusema lolote, macho yake yalijawa na machozi, midomo yake ilimwemwesa bila kutoa neno.
“samahani mzee!” sauti ilisikika kutoka nyuma yake, alishtuka kama mtu aliyekutana ghafla na mtoa roho, akageuka na kumtazama kijana aliyemwita. mzee huyo alijikuta anashindwa hata kuitikia ile salamu au kuuliza anamwitia nini, badala yake alimfuata yule kijana pindi alipoondoka eneo lile. moja kwa moja walifika kwenye ukumbi mdogo ambao ulikuwa na watu wasiozidi sita, yaani wale wenye vyeo vya juu, wenye dhamana ya ulinzi na usalama wa nchi, pamoja nao kulikuwa na wasaidizi wengine ambao ni maofisa wachache wa ikulu. akaketi katika kiti kilichokuwa wazi, akiwatazama watu hawa kwa zamu, pamoja nao alikuwapo mtu mwenye cheo cha pili kutoka kile cha mkuu wa nchi.
“kama mnavyoona… maofisa kadhaa na wafanyakazi wa ikulu wameuawa,” makamu wa rais aliliambia jopo, “kilichotokea hapa hakieleweki, hakuna anayejua nini kimetokea, ila mke wa rais yaani first lady ametoweka, nafikiri, kwa uwazi kabisa kuwa huu ni uvamizi lakini sijui ni nani au siwezi kuhusisha na kikundi gani kwani uchunguzi ndio kwanza umeanza,” akatulia kimya bila kusema lolote. macho yake yalionekana wazi kutona kwa machozi ambayo hayakutaka kumwagika.
“bila shaka, inawezekana walidhamiria kumteka au kumdhuru rais mwenyewe, walipoona hayupo basi wameondoka na mkewe, first lady. kumbukeni, ikulu ya tanzania ni kati ya majengo machache duniani yanbayolindwa kwa mitambo ya hali ya juu na wanausalama waliokomaa kwenye fani yao, lakini kama tumevamiwa, bila shaka, waliyovamia ni kundi lenye weledi wa juu zaidi katika medani hii ya usalama,” waziri wa ulinzi aliongezea na wajumbe wote wakatikisa vichwa.
“tumepoteza vijana wetu makini kabisa ambao waliaminiwa sana na mkuu. taarifa nimeshamfikishia, na amekatisha ziara yake, anarudi nyumbani kwani hali hii si ya kuvumilika, tunategemea neno la mwisho kutoka kwake,” makamu akalieleza baraza na wote wakaunga mkono.
“mheshimiwa makamu, naomba utoe tamko la wazi kwa sasa juu ya hali hii, maana, tusipoangalia, waandishi wa magazeti kama kawaida yao wataanza kutoa habari zisizothibitishwa,” msemaji wa ikulu alimwambia makamu wa rais.
“ok, naomba ieleweke hivi, ikulu imevamiwa na kundi la kigaidi, walinzi kadhaa wameuawa na bado kuna hali ya sintofahamu. vyombo vya usalama viko katika harakati za kuhakikisha vinategua kitendawili hiki ndani ya saa chache. tunaomba wananchi kuwa watulivu na pia kutoa taarifa polisi pindi unapoona mtu unayemhofia katika maeneo yenu,” makamu wa rais akazungumza. punde tu taarifa ile ikachapwa katika mashine na kusainiwa akakabidhiwa huyo bwana, msemaji wa ikulu ili kuwafikishia wanahabari waliofika alfajiri hiyo katika ukumbi mdogo wa maelezo ulio ndani ya jengo hilo.
***
ikulu ilikuwa haiingiliki mpaka uwe na kibali maalumu, vijana wa jeshi la wananchi waliegesha magari yao upande wa baharini na mengine mawili upande wa hospitali ya ocean road na nyingine zilisimama karibu na ofisi ya hazina. barabara ya magogoni ilifungwa haikuruhusiwa gari wala mtembea kwa miguu kupita eneo lile. juu angani helkopta ya jeshi na polisi zilikuwa zikifanya doria zikishirikiana na zile za jeshi la wananchi.
kwa ujumla jiji la dar es salaam lilikuwa katika misukosuko ya hapa na pale. majira ya saa sita mchana barabara kubwa na ya muhimu zaidi katika jiji hilo ilifungwa kwa muda, ile inayotoka uwanja wa ndege kuelekea mjini. ving’ora vikasikika na gari kama saba hivi zilipita kwa kasi ya ajabu kuelekea mjini. na dakika kumi na mbili tua gari hizo ziliingia katika lango kuu la ikulu na kuegeshwa mahala pake wakati tayari mkuu wa nchi alikuwa amekwishashuka na kuingia ndani ya jengo hilo, moja kwa moja akiwa na walinzi wake alipitiliza na kuteremka ngazi iliyompeleka katika chumba maalum ambacho hufanyia mikutano yake ya siri kilichopewa jina la ‘kilimanjaro square’.
“nimesikitishwa na kilichotokea, hii haiwezekaniki kuivumilia, ni uvamizi,” rais aling’aka huku akizunguka chumba badala ya kuketi chini. watu watano waliokuwa naye ndani ya chumba hicho walibaki kimya kabisa. mkuu wa nchi akarudi na kuketi mezani kwake, akakamata kalamu yake na kutaka kuandika kitu lakini mkono ulikuwa mzito.
“tulikuwa tunakusubiri wewe mheshimiwa rais ili utoe neno lako vijana waingie kazini mara moja,” makamu wa rais alitamka.
“oh! shiiit, come on, hii ni cold war! let me say cold war, na ntaipigana mpaka mwisho. mtu kukuvamia ndani ya chumba chako na kumchukua mkeo ni matusi, matusi yasiyovumilika!” akang’aka huku akisimama wima kwa hasira, “ni jengo gani au taasisi gani afrika ina ulinzi mkali na makini kama hili jengo hapa? hakuna, ninyi mnajua na dunia inajua. sasa hawa waliokuja na kufanikiwa kufanya madhara haya ina maana wamejuaje njia za kuingia humu na njia za kutokea kama si hujuma?” aliendelea kung’aka kwa sauti. kisha akatulia kidogo huku kijasho kikimtiririka, mwili wake ulimtetemeka kama mtu asikiaye baridi kali. akasimama na kutazamana na mkuu wa majeshi “nataka vijana wako waliobobea kweye michezo hii wahakikishe wanampata first lady ndani ya saas12.
“umesomeka amiri jeshi mkuu,” akajibu mkuu wa majeshi na kusimama akatoa saluti ya utii.
“na ninyi wengine muwe katika kazi zenu za kawaida lakini nyote muangaze macho katika sakata hilo,” akatoa maagizo kwa viongozi wa vikosi vingine. nao wakaitikia wito huo na kila mmoja akaondoka katika jengo hilo lililotukuka. ni dakika hiyohiyo tu ambapo ule ukumbi ulikuwa na watu wawili tu yaani rais na makamu wake.
“inaniuma sana mheshimiwa!” rais alimwambia makamu wake huku mikono yake ikiwa haitulii sehemu moja.
“mimi pia, ukizingatia tumepoteza vijana wenye ujuzi wa hali ya juu sana katika maswala ya usalama,” makamu naye alijibu.
“nina uhakika kwa vijana wetu hawa wa jw, hao wahalifu watapatikana tu,” rais akajibu.
“sawasawa kabisa, lakini unafikiri wao peke yao wataweza kulibaini kundi hilo lililofanya kadhia hii?”
“kwa nini unasema hivyo?”
“kwa sababu kutokana taaluma yao nahisi kama kazi hii inaweza kuwa ngumu,” makamu alikazia.
“hapana! hata mimi nilikuwa mwanajeshi, najua, tuna idara ya upelelezi ya jeshi, na kutokana na uzito wa jambo hili, wao ndio watu muafaka.” akameza mate kisha akaendelea,
“unajua hawa lazima wapambane na mtu anayelingana nao kwa sababu bila shaka ni magaidi sasa gaidi ni levo nyingine, lazima apambane na mtu wa levo yake na hao si wengine ni vijana wa jeshi,” mheshimiwa rais alamwelekeza makamu wake juu ya mpango huo. kikao cha wawili hao kilipomalizika, makamu wa rais akaondoka na kumwacha mkuu wake peke yake ndani ya ofisi hiyo. kitendo tu cha makamu wa rais kutoka na kumwacha mheshimiwa peke yake, simu ya mezani ilianza kuita kwa nguvu na fujo. mheshimiwa rais akaingalia kwa tuo kabla hajaamua kama ainyanyue na kuisikiliza au aiache, lakini tatizo ni kwamba hakujua simu hiyo ilikuwa inahusu nini au inamhusu nani. na mara nyingi simu ya chumba hicho ikiita basi huwa kunakuwa na jambo zito la kiofisi. kwa mkono wa kitetemeshi aliukwanyua mkono wa simu ile na kuiweka sikioni bila kuongea lolote.
“usijaribu kuchukua hatua yoyote kwa kumtafuta mkeo, tunajua unampenda na ndiyo maana tumemchukua, lakini ujue sisi tunachokitaka si fedha wala hatuna ugomvi na wewe. tunahitaji jambo moja tu, toa amri ya kuondoa majeshi yako ya kulinda amani katika kusini mwa nchi ya ngoko. ukilitekeleza hilo, mkeo utampata, na husipotekeleza tutateka na watu wa familia yako waliobakia, na wewe utakuwa wa mwisho…”
“ninyi ni nani? enh! ni nani?” alikatisha simu ile na kurusha swali ambalo halikujibiwa na simu ile ikakatika. rais alibaki amesimama bila kufanya lolote huku simu ile bado ikiwa sikioni, akili ilipomrudia akateremsha mkono taratibu na kuipachika mahala pake. akajitupa kitini nacho kikampokea bila hiyana huku kikinesanesa. mlango wa chumba hicho uliwaka taa ya kijani kwa ndani, akabonyeza swichi iliyo chini ya meza na kijiluninga kidogo kikaonesha mtu aliye upande wa pili.
“chakula kipo mezani mkuu!” akakribishwa lakini alipojitafakari aliona hata njaa hana, akanyanyuka na kutoka nje ya chumba hicho ambapo mlinsi wake namba moja kutoka idara ya usalama wa taifa alimpokea na kumwongoza kuelekea katika ukumbi wa chakula. ndani ya ukumbi huo kulikuwa na watu watatu tu ambao daima alipenda kula nao, hawa ni watu wa karibu sana nay eye, yaani watoto wake, mmoja wa kike na mwingine wa kiume. aliwaangalia watoto wake lakini alijikuta anashindwa kula chakula kile, badala yake aliamua kuondoka na kurudi ofisini, mara hii aliingia ofisi yake ya kawaida, akamwita katibu wake na kumwomba amwitie mkuu wa usalama wa ikulu.
“pole kwa kupoteza vijana wako!” alimpa pole.
“siwezi kupoa mpaka nipate ukweli wa hili,” yule mkuu wa usalama alijibu huku chozi likimdondoka.
“umefika olduvai?” akamwuliza.
“ndiyo mkuu!”
“hakuna madhara yoyote?”
“hakuna mkuu, kule hawajafika kabisa,” yule mkuu wa usalama akampa jibu lililomfanya yule rais kutabasamu kwa mbali.
“sikiliza othman, hili swala si dogo, ni gumu, nimetoa kazi kwa vijana wa jw walikamilishe, lakini nataka na wewe hapa unifanyie uchunguzi juu ya hili, hawa jamaa wamewezaje kuingia hapa ndani pasi na kuonekana?” rais alionesha wasiwasi wa wazi.
“mheshimiwa rais! hicho kitu kinanishangaza mpaka sasa, bado naumiza kichwa kujua ni vipi hawa watu wameweza kuipenya hii ngome ya chuma, sipati jibu. nafikiri inabidi tuwashirikishe wanaintelijensia wa juu kabisa katika hii nyanja,” othman, mkuu wa usalama ikulu alimweleza rais.
“usemalo ni sahihi, je unataka tukodi vyombo vya nje?” akamwuliza mara baada ya kuiinua uso wake.
“inapobidi hatuna budi kufanya hivyo,”
mkuu wan chi akajiinamia tena kwa sekunde kadhaa kisha akamtazama othman.
“sikia othman, ina maana sisi vyombo vyetu vimeshindwa? ni mapema mno kuomba msaada kutoka mataifa ya nje, ngoja tushindwe kabsa hapo hatutakuwa na budi lakini si sasa,” akamwambia.
“ngoja nikwambie kitu, mimi kama mwanausalama nakueleza tu hili swala linaweza kuwa gumu sisi kulitatua, kwa sababu hatujui nini na nini kimetukwamisha katika kugundua hao majahili. isitoshe pamoja na ulinzi mkali wa jengo hili ndio maana unaona vijana wetu wamekufa na kuumia, wavamizi hao wameingia moja kwa moja mpaka ndani ya nyumba yako ilipo ndani ya ikulu hii, hili si la kawaida na halijawahi kutokea popote katika karne hii,” othamn akaongea kwa uchungu sana.
maneno haya yaliifinya akili ya rais kwa muda huo, akatafakari jambo, akamtazama othman, “othman, kati ya vijana wangu wachache ninaoheshimu mawazo yao, wewe ni mmojawapo ndio maana nilikutoa kule ubalozini kukurudisha hapa ikulu, sawa nitalifanyia kazi leo hii, asante,” rais akamshukuru othman, wakaagana.
***
kusini mwa nchi ya ngoko
Mvua kubwa ilikuwa ikinyesha wanajeshi wa majeshi ya kulianda amani kutoka tanzania walikuwa wamejificha katika msitu huo mnene, wakiwa wamegawana makundi ya askari ishirini ishirini na kuuzungukla msitu huo unaokaliwa na waasi wa x65. waasi hao waliouvamia msitu huo miaka kadhaa nyuma walikuwa sugu na hawakutaka kuondoka kabisa kwa kuwa waliteka migodi ya dhahabu na almasi kwa manufaa yao na waliowatuma.
uamuzi wa tanzania kutoa batalioni moja ya wapiganaji wake mahiri wa jeshi la wananchi ulitokana na ombi la umoja wa nchi za afrika ili kukomesha kabisa uasi huo uliokuwa ukikiuka haki za binadamu kwa watu waishio katika maeneo hayo. mara kadhaa majeshi ya kujitolea yalikwenda huko lakini yalikutana na waasi wenye silaha nzito za kivita hivyo kupelekea kushindwa na kurudi nyumbani bila kutimiza azma yao.
baada ya muda mrefu wa kuwaacha waasi hao, maafikiano ya amani yalishindikana kwa njia ya kidiplomasia kati ya viongozi wa afrika na kiongozi wa wassi hao wa x65 waliokuwa wakipigana vita ya gorilla. vikao vilikaliwa miji mbalimbali ya afrika lakini ilikuwa ngumu kufikia muafaka, waasi hao hawakutaka kabisa kuuachia sit u msitu bali na eneo husika.
“hawa jamaa si wa kuwaonea huruma hata kidogo!” mmoja wa wanajeshi aliyekuwa katika ficho lake huko msituni aliwaambia wenzake.
“ila inaonekana sio tu waasi bali ni wanajeshi waasi kwa maana wanajua vyema mbinu za kivita.
“yeah ni kweli, maana kila tunapowazunguka nao wanakuwa makini, na kila tufanyalo inaonekana kama wanalijua,” askari mwingine wa mstari wa mbele alimjibu mwenzake huku akiweka bunduki yake sawia kifuani pake maana mapambano yangelipuka wakati wowote.
“kumbukeni wenzetu wameshindwa kazi hii na sisi tumeaminiwa kuifanikisha,” kiongozi wao akawaambia.
“aaaa sisi ni jeshi imara la tanzania, hawatuwezi, tunawapanga wadunguaji kisha tunamaliza kazi, hawa waasi ni kuwafutilia mbali tu, aliongea mwanajeshi mwingine aliyekuwa amebeba redio kubwa mgongoni mwake.
“chonjo wasiliana na makundi mengine waambie karibu tunaingia kijijini, hapo lazima tuzunguke kijiji kwa maana hatujui, labda wapo hapo” kiongozi wa kundi akampa maagizo mtaalamu huyo wa redio aliyejulikana kwa jina la chonjo.
***
kutoka katika makundi mengine yote walipata taarifa ile ya redio kupitia vyombo vyao vya kisasa kabisa ambavyo kila mmoja aliweza kusikia kwa wakati wake na aliweza kuongea na mwenzake. askari wale wakajiweka vyema kila mmoja akaiweka tayari bunduki yake kubwa (assault rifle) aina ya m4 carbine kifuani tayari kwa uvamizi. bunduki hii wanajeshi wote walipewa katika operesheni hiyo ukiachana na hiyo bunduki kila mmoja alikuwa na bastola mbili zenye nguvu kwa operesheni za dharula, mabomu ya kutupa kwa mkono ‘fragmentantion granade’, mabomu ya kutoa moshi ‘smoke granade’ kwa ajili ya kumchanganya adui. zaidi ya hapo kila kundi lilikuwa na mtu mwenye lpg, ‘anti-tank weapon’, silaha ya kujitwisha begani inayotumika kuvunja vizuizi wakati wa operesheni. kwa ujumla vijana hawa walitimia kila idara.
kutoka katika maficho walipita chini kwa chini kwenye vichaka vinene kwa minajiri ya kuzunguka kile kijiji cha mpumbutu, wengine wakaenda mlimani na wengine upande wa chini. iliwachukua kama dakika ishirini na tano kuzingira kijiji hicho ambacho mara nyingi waasi walipenda kujificha humo. kisha askari wawili walijitoa chambo kuingia kijijini ili kuwafanya waasi hao kujitokeza kirahisi.
katika moja ya vichaka kulilala watu wawili waliojifunga nyasi kavu na mbichi migongoni na kichwani kiasi kwamba wakilala kifudifudi huwezi kutambua kama ni binadamu, hawa walikuwa ni wadunguaji kitaaluma walikuwa na bunduki kubwa ya kudungulia ‘heavy sniper rifle’ m82a1. walijificha kimya kwenye kichaka kilicho juu ya kilima huku kwa chini wakikiona kile kijiji.
-------------------------------------------------------
epuka corona, waepushe wengine.
kaa nyumbani kama huna ulazima wa kutoka
nawa mikono yako kwa sanitizer au maji yenye dawa au sabuni
#stopcorona
----------------------------------------------------------------
kijiji cha mpumbutu
Shughuli za wanakijiji ziliendelea kama kawaida, watu walikuwa wakijpatia huduma ndogondogo katika maduka na vigenge, wengine wakipata vinywaji na kulewa ili kujisahaulisha shida zao. pembezoni mwa kijiji hicho, ukimaliza tu nyumba za wenyeji kulikuwapo na nyumba nyingine kubwa tu, nyumba hiyo ilikuwa ya tajiri mmoja mfanyabiashara aliyeuawa na waasi na kisha wao kuichukua na kuifanya maskani yao kila waingiapo kijijini hapo. hakuna mtu aliyekuwa akiisogelea nyumba hiyo kwa kuhofia kuuawa. waasi waliitumia zaidi ya kazi hiyo, waliitumia kama dangulo, pale mkubwa wa waasi anapojisikia ashki ya kufanya ngono vibaraka wake walikwenda kijijini na kukamata mwanamke yoyote na kumleta humo ndani. endapo atakataa aliuawa hadharani, hali hii iliwafanya watu wawafungia mabinti na wake zao ndani na wengine hata kukikimbia kijiji hicho.
“hiki ndiyo kijiji cha mpumbutu, wananchi wake hufanyiwa vitendo vya uzazalishwaji na hutendwa kinyume na haki za binadamu, serikali ya ngoko kama haiyaoni haya, tunataka kusafisha waasi kwa mashambulizi ya kimbunga, na si wananchi, hakikisha risasi yako inampiga muasi na shabaha yako isikosee,” sauti ya kiongozi wa vikosi vya ukombozi ilisikika sikioni mwa kila mmoja.
benson boko aliweka jicho lake katika lensi ya bunduki lake kutoka pale alipojificha na kuchungulia, akiangalia lile jumba waliloelekezwa kwenye ramani na kisha taratibu alielekeza kwenye vijia na njia zinazopita katikati ya kijiji hicho. akaondoa jicho na kuangalia saa yake, ilikuwa yapata saa 12 jioni. bado si wanakijiji wala waasi waliokuwa wakijua kuwa wamezingirwa, muda ulikuwa haujafika wa kufanya kazi yao.
tuonane jumamosi
ukiitaka yote ni tsh 4000 tu 0766974865a kuumia, wavamizi hao wameingia moja kwa moja mpaka ndani ya nyumba yako ilipo ndani ya Ikulu hii, hili si la kawaida na halijawahi kutokea popote katika karne hii,” Othamn akaongea kwa uchungu sana.
Maneno haya yaliifinya akili ya rais kwa muda huo, akatafakari jambo, akamtazama Othman, “Othman, kati ya vijana wangu wachache ninaoheshimu mawazo yao, wewe ni mmojawapo ndio maana nilikutoa kule ubalozini kukurudisha hapa Ikulu, sawa nitalifanyia kazi leo hii, asante,” rais akamshukuru Othman, wakaagana.
***
KUSINI MWA NCHI YA NGOKO
MVUA KUBWA ILIKUWA IKINYESHA wanajeshi wa majeshi ya kulianda amani kutoka Tanzania walikuwa wamejificha katika msitu huo mnene, wakiwa wamegawana makundi ya askari ishirini ishirini na kuuzungukla msitu huo unaokaliwa na waasi wa X65. Waasi hao waliouvamia msitu huo miaka kadhaa nyuma walikuwa sugu na hawakutaka kuondoka kabisa kwa kuwa waliteka migodi ya dhahabu na almasi kwa manufaa yao na waliowatuma.
Uamuzi wa Tanzania kutoa batalioni moja ya wapiganaji wake mahiri wa Jeshi la Wananchi ulitokana na ombi la Umoja wa nchi za Afrika ili kukomesha kabisa uasi huo uliokuwa ukikiuka haki za binadamu kwa watu waishio katika maeneo hayo. Mara kadhaa majeshi ya kujitolea yalikwenda huko lakini yalikutana na waasi wenye silaha nzito za kivita hivyo kupelekea kushindwa na kurudi nyumbani bila kutimiza azma yao.
Baada ya muda mrefu wa kuwaacha waasi hao, maafikiano ya amani yalishindikana kwa njia ya kidiplomasia kati ya viongozi wa Afrika na kiongozi wa wassi hao wa X65 waliokuwa wakipigana vita ya gorilla. Vikao vilikaliwa miji mbalimbali ya Afrika lakini ilikuwa ngumu kufikia muafaka, waasi hao hawakutaka kabisa kuuachia sit u msitu bali na eneo husika.
“Hawa jamaa si wa kuwaonea huruma hata kidogo!” mmoja wa wanajeshi aliyekuwa katika ficho lake huko msituni aliwaambia wenzake.
“Ila inaonekana sio tu waasi bali ni wanajeshi waasi kwa maana wanajua vyema mbinu za kivita.
“Yeah ni kweli, maana kila tunapowazunguka nao wanakuwa makini, na kila tufanyalo inaonekana kama wanalijua,” askari mwingine wa mstari wa mbele alimjibu mwenzake huku akiweka bunduki yake sawia kifuani pake maana mapambano yangelipuka wakati wowote.
“Kumbukeni wenzetu wameshindwa kazi hii na sisi tumeaminiwa kuifanikisha,” kiongozi wao akawaambia.
“Aaaa sisi ni jeshi imara la Tanzania, hawatuwezi, tunawapanga wadunguaji kisha tunamaliza kazi, hawa waasi ni kuwafutilia mbali tu, aliongea mwanajeshi mwingine aliyekuwa amebeba redio kubwa mgongoni mwake.
“Chonjo wasiliana na makundi mengine waambie karibu tunaingia kijijini, hapo lazima tuzunguke kijiji kwa maana hatujui, labda wapo hapo” kiongozi wa kundi akampa maagizo mtaalamu huyo wa redio aliyejulikana kwa jina la Chonjo.
***
Kutoka katika makundi mengine yote walipata taarifa ile ya redio kupitia vyombo vyao vya kisasa kabisa ambavyo kila mmoja aliweza kusikia kwa wakati wake na aliweza kuongea na mwenzake. Askari wale wakajiweka vyema kila mmoja akaiweka tayari bunduki yake kubwa (assault rifle) aina ya M4 Carbine kifuani tayari kwa uvamizi. Bunduki hii wanajeshi wote walipewa katika operesheni hiyo ukiachana na hiyo bunduki kila mmoja alikuwa na bastola mbili zenye nguvu kwa operesheni za dharula, mabomu ya kutupa kwa mkono ‘fragmentantion granade’, mabomu ya kutoa moshi ‘smoke granade’ kwa ajili ya kumchanganya adui. Zaidi ya hapo kila kundi lilikuwa na mtu mwenye LPG, ‘anti-tank weapon’, silaha ya kujitwisha begani inayotumika kuvunja vizuizi wakati wa operesheni. Kwa ujumla vijana hawa walitimia kila idara.
Kutoka katika maficho walipita chini kwa chini kwenye vichaka vinene kwa minajiri ya kuzunguka kile kijiji cha Mpumbutu, wengine wakaenda mlimani na wengine upande wa chini. Iliwachukua kama dakika ishirini na tano kuzingira kijiji hicho ambacho mara nyingi waasi walipenda kujificha humo. Kisha askari wawili walijitoa chambo kuingia kijijini ili kuwafanya waasi hao kujitokeza kirahisi.
Katika moja ya vichaka kulilala watu wawili waliojifunga nyasi kavu na mbichi migongoni na kichwani kiasi kwamba wakilala kifudifudi huwezi kutambua kama ni binadamu, hawa walikuwa ni wadunguaji kitaaluma walikuwa na bunduki kubwa ya kudungulia ‘Heavy Sniper Rifle’ M82A1. Walijificha kimya kwenye kichaka kilicho juu ya kilima huku kwa chini wakikiona kile kijiji.
-------------------------------------------------------
Epuka Corona, waepushe wengine.
Kaa nyumbani kama huna ulazima wa kutoka
Nawa mikono yako kwa Sanitizer au maji yenye dawa au sabuni
#StopCorona
----------------------------------------------------------------
KIJIJI CHA MPUMBUTU
Shughuli za wanakijiji ziliendelea kama kawaida, watu walikuwa wakijpatia huduma ndogondogo katika maduka na vigenge, wengine wakipata vinywaji na kulewa ili kujisahaulisha shida zao. Pembezoni mwa kijiji hicho, ukimaliza tu nyumba za wenyeji kulikuwapo na nyumba nyingine kubwa tu, nyumba hiyo ilikuwa ya tajiri mmoja mfanyabiashara aliyeuawa na waasi na kisha wao kuichukua na kuifanya maskani yao kila waingiapo kijijini hapo. Hakuna mtu aliyekuwa akiisogelea nyumba hiyo kwa kuhofia kuuawa. Waasi waliitumia zaidi ya kazi hiyo, waliitumia kama dangulo, pale mkubwa wa waasi anapojisikia ashki ya kufanya ngono vibaraka wake walikwenda kijijini na kukamata mwanamke yoyote na kumleta humo ndani. Endapo atakataa aliuawa hadharani, hali hii iliwafanya watu wawafungia mabinti na wake zao ndani na wengine hata kukikimbia kijiji hicho.
“Hiki ndiyo kijiji cha Mpumbutu, wananchi wake hufanyiwa vitendo vya uzazalishwaji na hutendwa kinyume na haki za binadamu, serikali ya Ngoko kama haiyaoni haya, tunataka kusafisha waasi kwa mashambulizi ya kimbunga, na si wananchi, hakikisha risasi yako inampiga muasi na shabaha yako isikosee,” sauti ya kiongozi wa vikosi vya ukombozi ilisikika sikioni mwa kila mmoja.
Benson Boko aliweka jicho lake katika lensi ya bunduki lake kutoka pale alipojificha na kuchungulia, akiangalia lile jumba waliloelekezwa kwenye ramani na kisha taratibu alielekeza kwenye vijia na njia zinazopita katikati ya kijiji hicho. Akaondoa jicho na kuangalia saa yake, ilikuwa yapata saa 12 jioni. Bado si wanakijiji wala waasi waliokuwa wakijua kuwa wamezingirwa, muda ulikuwa haujafika wa kufanya kazi yao.
Itaendelea....
Mtunzi: Richard Mwambe
Pasipoti ya Gaidi: Hujuma na Uzandiki
Sura ya I
Ikulu – Dar es Salaam
Saa 10:30 Alfajiri
Wakati giza likijiandaa kutoweka na kuipisha nuru ya asubuhi, miti yote ilikuwa imetulia kana kwamba kuna aliyeiambia ifanye hivyo. ni tausi mmoja mmoja aliyekuwa akilia alfajiri hii tena kwa nyakati tofauti. hawakuwa na zamu ya kufanya hivyo isipokuwa ilitokea tu, ndivyo walivyoumbwa. hawakuwa wakijua lolote linaloendelea katika maisha ya mwanadamu wakati huo, zaidi walisubiri kukuche waendelee kupendezesha mandhari ya eneo hilo. hawa walikuwa kivutio kikubwa sana katika eneo hilo kwa wapiti njia.
Hekaheka katika jengo hilo la makao makuu ya rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania ilikuwa kubwa. vijana wa jeshi la polisi, kikosi maalum cha kutuliza ghasia, walikuwepo wakiwa kimejiweka tayari kwa lolote, ijapokuwa huwa hapo kwa lindo kila siku lakini leo hii walikuwa kivingine kabisa. mbali na wao, eneo hilo, afajiri hiyo lilizungukwa pia na vijana wa jeshi la wananchi waliovalia kombati zao za mabakamabaka, wakiwa na silaha nzitonzito mikononi mwao, kila mmoja akionekana kutingwa na shughuli inayompasa kufanya kwa muda huo. magari ya wagonjwa kutoka jeshi la wananchi yalikuwa yikifanya kazi ya kubeba majeruhi na maiti zilizokutwa ndani ya jengo hilo, hekaheka.
msemaji wa ikulu alikuwa kasimama katikati ya ukumbi mkubwa ndani ya jengo hilo, alikuwa kimya bila kusema lolote, macho yake yalijawa na machozi, midomo yake ilimwemwesa bila kutoa neno.
“samahani mzee!” sauti ilisikika kutoka nyuma yake, alishtuka kama mtu aliyekutana ghafla na mtoa roho, akageuka na kumtazama kijana aliyemwita. mzee huyo alijikuta anashindwa hata kuitikia ile salamu au kuuliza anamwitia nini, badala yake alimfuata yule kijana pindi alipoondoka eneo lile. moja kwa moja walifika kwenye ukumbi mdogo ambao ulikuwa na watu wasiozidi sita, yaani wale wenye vyeo vya juu, wenye dhamana ya ulinzi na usalama wa nchi, pamoja nao kulikuwa na wasaidizi wengine ambao ni maofisa wachache wa ikulu. akaketi katika kiti kilichokuwa wazi, akiwatazama watu hawa kwa zamu, pamoja nao alikuwapo mtu mwenye cheo cha pili kutoka kile cha mkuu wa nchi.
“kama mnavyoona… maofisa kadhaa na wafanyakazi wa ikulu wameuawa,” makamu wa rais aliliambia jopo, “kilichotokea hapa hakieleweki, hakuna anayejua nini kimetokea, ila mke wa rais yaani first lady ametoweka, nafikiri, kwa uwazi kabisa kuwa huu ni uvamizi lakini sijui ni nani au siwezi kuhusisha na kikundi gani kwani uchunguzi ndio kwanza umeanza,” akatulia kimya bila kusema lolote. macho yake yalionekana wazi kutona kwa machozi ambayo hayakutaka kumwagika.
“bila shaka, inawezekana walidhamiria kumteka au kumdhuru rais mwenyewe, walipoona hayupo basi wameondoka na mkewe, first lady. kumbukeni, ikulu ya tanzania ni kati ya majengo machache duniani yanbayolindwa kwa mitambo ya hali ya juu na wanausalama waliokomaa kwenye fani yao, lakini kama tumevamiwa, bila shaka, waliyovamia ni kundi lenye weledi wa juu zaidi katika medani hii ya usalama,” waziri wa ulinzi aliongezea na wajumbe wote wakatikisa vichwa.
“tumepoteza vijana wetu makini kabisa ambao waliaminiwa sana na mkuu. taarifa nimeshamfikishia, na amekatisha ziara yake, anarudi nyumbani kwani hali hii si ya kuvumilika, tunategemea neno la mwisho kutoka kwake,” makamu akalieleza baraza na wote wakaunga mkono.
“mheshimiwa makamu, naomba utoe tamko la wazi kwa sasa juu ya hali hii, maana, tusipoangalia, waandishi wa magazeti kama kawaida yao wataanza kutoa habari zisizothibitishwa,” msemaji wa ikulu alimwambia makamu wa rais.
“ok, naomba ieleweke hivi, ikulu imevamiwa na kundi la kigaidi, walinzi kadhaa wameuawa na bado kuna hali ya sintofahamu. vyombo vya usalama viko katika harakati za kuhakikisha vinategua kitendawili hiki ndani ya saa chache. tunaomba wananchi kuwa watulivu na pia kutoa taarifa polisi pindi unapoona mtu unayemhofia katika maeneo yenu,” makamu wa rais akazungumza. punde tu taarifa ile ikachapwa katika mashine na kusainiwa akakabidhiwa huyo bwana, msemaji wa ikulu ili kuwafikishia wanahabari waliofika alfajiri hiyo katika ukumbi mdogo wa maelezo ulio ndani ya jengo hilo.
***
ikulu ilikuwa haiingiliki mpaka uwe na kibali maalumu, vijana wa jeshi la wananchi waliegesha magari yao upande wa baharini na mengine mawili upande wa hospitali ya ocean road na nyingine zilisimama karibu na ofisi ya hazina. barabara ya magogoni ilifungwa haikuruhusiwa gari wala mtembea kwa miguu kupita eneo lile. juu angani helkopta ya jeshi na polisi zilikuwa zikifanya doria zikishirikiana na zile za jeshi la wananchi.
kwa ujumla jiji la dar es salaam lilikuwa katika misukosuko ya hapa na pale. majira ya saa sita mchana barabara kubwa na ya muhimu zaidi katika jiji hilo ilifungwa kwa muda, ile inayotoka uwanja wa ndege kuelekea mjini. ving’ora vikasikika na gari kama saba hivi zilipita kwa kasi ya ajabu kuelekea mjini. na dakika kumi na mbili tua gari hizo ziliingia katika lango kuu la ikulu na kuegeshwa mahala pake wakati tayari mkuu wa nchi alikuwa amekwishashuka na kuingia ndani ya jengo hilo, moja kwa moja akiwa na walinzi wake alipitiliza na kuteremka ngazi iliyompeleka katika chumba maalum ambacho hufanyia mikutano yake ya siri kilichopewa jina la ‘kilimanjaro square’.
“nimesikitishwa na kilichotokea, hii haiwezekaniki kuivumilia, ni uvamizi,” rais aling’aka huku akizunguka chumba badala ya kuketi chini. watu watano waliokuwa naye ndani ya chumba hicho walibaki kimya kabisa. mkuu wa nchi akarudi na kuketi mezani kwake, akakamata kalamu yake na kutaka kuandika kitu lakini mkono ulikuwa mzito.
“tulikuwa tunakusubiri wewe mheshimiwa rais ili utoe neno lako vijana waingie kazini mara moja,” makamu wa rais alitamka.
“oh! shiiit, come on, hii ni cold war! let me say cold war, na ntaipigana mpaka mwisho. mtu kukuvamia ndani ya chumba chako na kumchukua mkeo ni matusi, matusi yasiyovumilika!” akang’aka huku akisimama wima kwa hasira, “ni jengo gani au taasisi gani afrika ina ulinzi mkali na makini kama hili jengo hapa? hakuna, ninyi mnajua na dunia inajua. sasa hawa waliokuja na kufanikiwa kufanya madhara haya ina maana wamejuaje njia za kuingia humu na njia za kutokea kama si hujuma?” aliendelea kung’aka kwa sauti. kisha akatulia kidogo huku kijasho kikimtiririka, mwili wake ulimtetemeka kama mtu asikiaye baridi kali. akasimama na kutazamana na mkuu wa majeshi “nataka vijana wako waliobobea kweye michezo hii wahakikishe wanampata first lady ndani ya saas12.
“umesomeka amiri jeshi mkuu,” akajibu mkuu wa majeshi na kusimama akatoa saluti ya utii.
“na ninyi wengine muwe katika kazi zenu za kawaida lakini nyote muangaze macho katika sakata hilo,” akatoa maagizo kwa viongozi wa vikosi vingine. nao wakaitikia wito huo na kila mmoja akaondoka katika jengo hilo lililotukuka. ni dakika hiyohiyo tu ambapo ule ukumbi ulikuwa na watu wawili tu yaani rais na makamu wake.
“inaniuma sana mheshimiwa!” rais alimwambia makamu wake huku mikono yake ikiwa haitulii sehemu moja.
“mimi pia, ukizingatia tumepoteza vijana wenye ujuzi wa hali ya juu sana katika maswala ya usalama,” makamu naye alijibu.
“nina uhakika kwa vijana wetu hawa wa jw, hao wahalifu watapatikana tu,” rais akajibu.
“sawasawa kabisa, lakini unafikiri wao peke yao wataweza kulibaini kundi hilo lililofanya kadhia hii?”
“kwa nini unasema hivyo?”
“kwa sababu kutokana taaluma yao nahisi kama kazi hii inaweza kuwa ngumu,” makamu alikazia.
“hapana! hata mimi nilikuwa mwanajeshi, najua, tuna idara ya upelelezi ya jeshi, na kutokana na uzito wa jambo hili, wao ndio watu muafaka.” akameza mate kisha akaendelea,
“unajua hawa lazima wapambane na mtu anayelingana nao kwa sababu bila shaka ni magaidi sasa gaidi ni levo nyingine, lazima apambane na mtu wa levo yake na hao si wengine ni vijana wa jeshi,” mheshimiwa rais alamwelekeza makamu wake juu ya mpango huo. kikao cha wawili hao kilipomalizika, makamu wa rais akaondoka na kumwacha mkuu wake peke yake ndani ya ofisi hiyo. kitendo tu cha makamu wa rais kutoka na kumwacha mheshimiwa peke yake, simu ya mezani ilianza kuita kwa nguvu na fujo. mheshimiwa rais akaingalia kwa tuo kabla hajaamua kama ainyanyue na kuisikiliza au aiache, lakini tatizo ni kwamba hakujua simu hiyo ilikuwa inahusu nini au inamhusu nani. na mara nyingi simu ya chumba hicho ikiita basi huwa kunakuwa na jambo zito la kiofisi. kwa mkono wa kitetemeshi aliukwanyua mkono wa simu ile na kuiweka sikioni bila kuongea lolote.
“usijaribu kuchukua hatua yoyote kwa kumtafuta mkeo, tunajua unampenda na ndiyo maana tumemchukua, lakini ujue sisi tunachokitaka si fedha wala hatuna ugomvi na wewe. tunahitaji jambo moja tu, toa amri ya kuondoa majeshi yako ya kulinda amani katika kusini mwa nchi ya ngoko. ukilitekeleza hilo, mkeo utampata, na husipotekeleza tutateka na watu wa familia yako waliobakia, na wewe utakuwa wa mwisho…”
“ninyi ni nani? enh! ni nani?” alikatisha simu ile na kurusha swali ambalo halikujibiwa na simu ile ikakatika. rais alibaki amesimama bila kufanya lolote huku simu ile bado ikiwa sikioni, akili ilipomrudia akateremsha mkono taratibu na kuipachika mahala pake. akajitupa kitini nacho kikampokea bila hiyana huku kikinesanesa. mlango wa chumba hicho uliwaka taa ya kijani kwa ndani, akabonyeza swichi iliyo chini ya meza na kijiluninga kidogo kikaonesha mtu aliye upande wa pili.
“chakula kipo mezani mkuu!” akakribishwa lakini alipojitafakari aliona hata njaa hana, akanyanyuka na kutoka nje ya chumba hicho ambapo mlinsi wake namba moja kutoka idara ya usalama wa taifa alimpokea na kumwongoza kuelekea katika ukumbi wa chakula. ndani ya ukumbi huo kulikuwa na watu watatu tu ambao daima alipenda kula nao, hawa ni watu wa karibu sana nay eye, yaani watoto wake, mmoja wa kike na mwingine wa kiume. aliwaangalia watoto wake lakini alijikuta anashindwa kula chakula kile, badala yake aliamua kuondoka na kurudi ofisini, mara hii aliingia ofisi yake ya kawaida, akamwita katibu wake na kumwomba amwitie mkuu wa usalama wa ikulu.
“pole kwa kupoteza vijana wako!” alimpa pole.
“siwezi kupoa mpaka nipate ukweli wa hili,” yule mkuu wa usalama alijibu huku chozi likimdondoka.
“umefika olduvai?” akamwuliza.
“ndiyo mkuu!”
“hakuna madhara yoyote?”
“hakuna mkuu, kule hawajafika kabisa,” yule mkuu wa usalama akampa jibu lililomfanya yule rais kutabasamu kwa mbali.
“sikiliza othman, hili swala si dogo, ni gumu, nimetoa kazi kwa vijana wa jw walikamilishe, lakini nataka na wewe hapa unifanyie uchunguzi juu ya hili, hawa jamaa wamewezaje kuingia hapa ndani pasi na kuonekana?” rais alionesha wasiwasi wa wazi.
“mheshimiwa rais! hicho kitu kinanishangaza mpaka sasa, bado naumiza kichwa kujua ni vipi hawa watu wameweza kuipenya hii ngome ya chuma, sipati jibu. nafikiri inabidi tuwashirikishe wanaintelijensia wa juu kabisa katika hii nyanja,” othman, mkuu wa usalama ikulu alimweleza rais.
“usemalo ni sahihi, je unataka tukodi vyombo vya nje?” akamwuliza mara baada ya kuiinua uso wake.
“inapobidi hatuna budi kufanya hivyo,”
mkuu wan chi akajiinamia tena kwa sekunde kadhaa kisha akamtazama othman.
“sikia othman, ina maana sisi vyombo vyetu vimeshindwa? ni mapema mno kuomba msaada kutoka mataifa ya nje, ngoja tushindwe kabsa hapo hatutakuwa na budi lakini si sasa,” akamwambia.
“ngoja nikwambie kitu, mimi kama mwanausalama nakueleza tu hili swala linaweza kuwa gumu sisi kulitatua, kwa sababu hatujui nini na nini kimetukwamisha katika kugundua hao majahili. isitoshe pamoja na ulinzi mkali wa jengo hili ndio maana unaona vijana wetu wamekufa na kuumia, wavamizi hao wameingia moja kwa moja mpaka ndani ya nyumba yako ilipo ndani ya ikulu hii, hili si la kawaida na halijawahi kutokea popote katika karne hii,” othamn akaongea kwa uchungu sana.
maneno haya yaliifinya akili ya rais kwa muda huo, akatafakari jambo, akamtazama othman, “othman, kati ya vijana wangu wachache ninaoheshimu mawazo yao, wewe ni mmojawapo ndio maana nilikutoa kule ubalozini kukurudisha hapa ikulu, sawa nitalifanyia kazi leo hii, asante,” rais akamshukuru othman, wakaagana.
***
kusini mwa nchi ya ngoko
Mvua kubwa ilikuwa ikinyesha wanajeshi wa majeshi ya kulianda amani kutoka tanzania walikuwa wamejificha katika msitu huo mnene, wakiwa wamegawana makundi ya askari ishirini ishirini na kuuzungukla msitu huo unaokaliwa na waasi wa x65. waasi hao waliouvamia msitu huo miaka kadhaa nyuma walikuwa sugu na hawakutaka kuondoka kabisa kwa kuwa waliteka migodi ya dhahabu na almasi kwa manufaa yao na waliowatuma.
uamuzi wa tanzania kutoa batalioni moja ya wapiganaji wake mahiri wa jeshi la wananchi ulitokana na ombi la umoja wa nchi za afrika ili kukomesha kabisa uasi huo uliokuwa ukikiuka haki za binadamu kwa watu waishio katika maeneo hayo. mara kadhaa majeshi ya kujitolea yalikwenda huko lakini yalikutana na waasi wenye silaha nzito za kivita hivyo kupelekea kushindwa na kurudi nyumbani bila kutimiza azma yao.
baada ya muda mrefu wa kuwaacha waasi hao, maafikiano ya amani yalishindikana kwa njia ya kidiplomasia kati ya viongozi wa afrika na kiongozi wa wassi hao wa x65 waliokuwa wakipigana vita ya gorilla. vikao vilikaliwa miji mbalimbali ya afrika lakini ilikuwa ngumu kufikia muafaka, waasi hao hawakutaka kabisa kuuachia sit u msitu bali na eneo husika.
“hawa jamaa si wa kuwaonea huruma hata kidogo!” mmoja wa wanajeshi aliyekuwa katika ficho lake huko msituni aliwaambia wenzake.
“ila inaonekana sio tu waasi bali ni wanajeshi waasi kwa maana wanajua vyema mbinu za kivita.
“yeah ni kweli, maana kila tunapowazunguka nao wanakuwa makini, na kila tufanyalo inaonekana kama wanalijua,” askari mwingine wa mstari wa mbele alimjibu mwenzake huku akiweka bunduki yake sawia kifuani pake maana mapambano yangelipuka wakati wowote.
“kumbukeni wenzetu wameshindwa kazi hii na sisi tumeaminiwa kuifanikisha,” kiongozi wao akawaambia.
“aaaa sisi ni jeshi imara la tanzania, hawatuwezi, tunawapanga wadunguaji kisha tunamaliza kazi, hawa waasi ni kuwafutilia mbali tu, aliongea mwanajeshi mwingine aliyekuwa amebeba redio kubwa mgongoni mwake.
“chonjo wasiliana na makundi mengine waambie karibu tunaingia kijijini, hapo lazima tuzunguke kijiji kwa maana hatujui, labda wapo hapo” kiongozi wa kundi akampa maagizo mtaalamu huyo wa redio aliyejulikana kwa jina la chonjo.
***
kutoka katika makundi mengine yote walipata taarifa ile ya redio kupitia vyombo vyao vya kisasa kabisa ambavyo kila mmoja aliweza kusikia kwa wakati wake na aliweza kuongea na mwenzake. askari wale wakajiweka vyema kila mmoja akaiweka tayari bunduki yake kubwa (assault rifle) aina ya m4 carbine kifuani tayari kwa uvamizi. bunduki hii wanajeshi wote walipewa katika operesheni hiyo ukiachana na hiyo bunduki kila mmoja alikuwa na bastola mbili zenye nguvu kwa operesheni za dharula, mabomu ya kutupa kwa mkono ‘fragmentantion granade’, mabomu ya kutoa moshi ‘smoke granade’ kwa ajili ya kumchanganya adui. zaidi ya hapo kila kundi lilikuwa na mtu mwenye lpg, ‘anti-tank weapon’, silaha ya kujitwisha begani inayotumika kuvunja vizuizi wakati wa operesheni. kwa ujumla vijana hawa walitimia kila idara.
kutoka katika maficho walipita chini kwa chini kwenye vichaka vinene kwa minajiri ya kuzunguka kile kijiji cha mpumbutu, wengine wakaenda mlimani na wengine upande wa chini. iliwachukua kama dakika ishirini na tano kuzingira kijiji hicho ambacho mara nyingi waasi walipenda kujificha humo. kisha askari wawili walijitoa chambo kuingia kijijini ili kuwafanya waasi hao kujitokeza kirahisi.
katika moja ya vichaka kulilala watu wawili waliojifunga nyasi kavu na mbichi migongoni na kichwani kiasi kwamba wakilala kifudifudi huwezi kutambua kama ni binadamu, hawa walikuwa ni wadunguaji kitaaluma walikuwa na bunduki kubwa ya kudungulia ‘heavy sniper rifle’ m82a1. walijificha kimya kwenye kichaka kilicho juu ya kilima huku kwa chini wakikiona kile kijiji.
-------------------------------------------------------
epuka corona, waepushe wengine.
kaa nyumbani kama huna ulazima wa kutoka
nawa mikono yako kwa sanitizer au maji yenye dawa au sabuni
#stopcorona
----------------------------------------------------------------
kijiji cha mpumbutu
Shughuli za wanakijiji ziliendelea kama kawaida, watu walikuwa wakijpatia huduma ndogondogo katika maduka na vigenge, wengine wakipata vinywaji na kulewa ili kujisahaulisha shida zao. pembezoni mwa kijiji hicho, ukimaliza tu nyumba za wenyeji kulikuwapo na nyumba nyingine kubwa tu, nyumba hiyo ilikuwa ya tajiri mmoja mfanyabiashara aliyeuawa na waasi na kisha wao kuichukua na kuifanya maskani yao kila waingiapo kijijini hapo. hakuna mtu aliyekuwa akiisogelea nyumba hiyo kwa kuhofia kuuawa. waasi waliitumia zaidi ya kazi hiyo, waliitumia kama dangulo, pale mkubwa wa waasi anapojisikia ashki ya kufanya ngono vibaraka wake walikwenda kijijini na kukamata mwanamke yoyote na kumleta humo ndani. endapo atakataa aliuawa hadharani, hali hii iliwafanya watu wawafungia mabinti na wake zao ndani na wengine hata kukikimbia kijiji hicho.
“hiki ndiyo kijiji cha mpumbutu, wananchi wake hufanyiwa vitendo vya uzazalishwaji na hutendwa kinyume na haki za binadamu, serikali ya ngoko kama haiyaoni haya, tunataka kusafisha waasi kwa mashambulizi ya kimbunga, na si wananchi, hakikisha risasi yako inampiga muasi na shabaha yako isikosee,” sauti ya kiongozi wa vikosi vya ukombozi ilisikika sikioni mwa kila mmoja.
benson boko aliweka jicho lake katika lensi ya bunduki lake kutoka pale alipojificha na kuchungulia, akiangalia lile jumba waliloelekezwa kwenye ramani na kisha taratibu alielekeza kwenye vijia na njia zinazopita katikati ya kijiji hicho. akaondoa jicho na kuangalia saa yake, ilikuwa yapata saa 12 jioni. bado si wanakijiji wala waasi waliokuwa wakijua kuwa wamezingirwa, muda ulikuwa haujafika wa kufanya kazi yao.
tuonane jumamosi
ukiitaka yote ni tsh 4000 tu 0766974865a kuumia, wavamizi hao wameingia moja kwa moja mpaka ndani ya nyumba yako ilipo ndani ya Ikulu hii, hili si la kawaida na halijawahi kutokea popote katika karne hii,” Othamn akaongea kwa uchungu sana.
Maneno haya yaliifinya akili ya rais kwa muda huo, akatafakari jambo, akamtazama Othman, “Othman, kati ya vijana wangu wachache ninaoheshimu mawazo yao, wewe ni mmojawapo ndio maana nilikutoa kule ubalozini kukurudisha hapa Ikulu, sawa nitalifanyia kazi leo hii, asante,” rais akamshukuru Othman, wakaagana.
***
KUSINI MWA NCHI YA NGOKO
MVUA KUBWA ILIKUWA IKINYESHA wanajeshi wa majeshi ya kulianda amani kutoka Tanzania walikuwa wamejificha katika msitu huo mnene, wakiwa wamegawana makundi ya askari ishirini ishirini na kuuzungukla msitu huo unaokaliwa na waasi wa X65. Waasi hao waliouvamia msitu huo miaka kadhaa nyuma walikuwa sugu na hawakutaka kuondoka kabisa kwa kuwa waliteka migodi ya dhahabu na almasi kwa manufaa yao na waliowatuma.
Uamuzi wa Tanzania kutoa batalioni moja ya wapiganaji wake mahiri wa Jeshi la Wananchi ulitokana na ombi la Umoja wa nchi za Afrika ili kukomesha kabisa uasi huo uliokuwa ukikiuka haki za binadamu kwa watu waishio katika maeneo hayo. Mara kadhaa majeshi ya kujitolea yalikwenda huko lakini yalikutana na waasi wenye silaha nzito za kivita hivyo kupelekea kushindwa na kurudi nyumbani bila kutimiza azma yao.
Baada ya muda mrefu wa kuwaacha waasi hao, maafikiano ya amani yalishindikana kwa njia ya kidiplomasia kati ya viongozi wa Afrika na kiongozi wa wassi hao wa X65 waliokuwa wakipigana vita ya gorilla. Vikao vilikaliwa miji mbalimbali ya Afrika lakini ilikuwa ngumu kufikia muafaka, waasi hao hawakutaka kabisa kuuachia sit u msitu bali na eneo husika.
“Hawa jamaa si wa kuwaonea huruma hata kidogo!” mmoja wa wanajeshi aliyekuwa katika ficho lake huko msituni aliwaambia wenzake.
“Ila inaonekana sio tu waasi bali ni wanajeshi waasi kwa maana wanajua vyema mbinu za kivita.
“Yeah ni kweli, maana kila tunapowazunguka nao wanakuwa makini, na kila tufanyalo inaonekana kama wanalijua,” askari mwingine wa mstari wa mbele alimjibu mwenzake huku akiweka bunduki yake sawia kifuani pake maana mapambano yangelipuka wakati wowote.
“Kumbukeni wenzetu wameshindwa kazi hii na sisi tumeaminiwa kuifanikisha,” kiongozi wao akawaambia.
“Aaaa sisi ni jeshi imara la Tanzania, hawatuwezi, tunawapanga wadunguaji kisha tunamaliza kazi, hawa waasi ni kuwafutilia mbali tu, aliongea mwanajeshi mwingine aliyekuwa amebeba redio kubwa mgongoni mwake.
“Chonjo wasiliana na makundi mengine waambie karibu tunaingia kijijini, hapo lazima tuzunguke kijiji kwa maana hatujui, labda wapo hapo” kiongozi wa kundi akampa maagizo mtaalamu huyo wa redio aliyejulikana kwa jina la Chonjo.
***
Kutoka katika makundi mengine yote walipata taarifa ile ya redio kupitia vyombo vyao vya kisasa kabisa ambavyo kila mmoja aliweza kusikia kwa wakati wake na aliweza kuongea na mwenzake. Askari wale wakajiweka vyema kila mmoja akaiweka tayari bunduki yake kubwa (assault rifle) aina ya M4 Carbine kifuani tayari kwa uvamizi. Bunduki hii wanajeshi wote walipewa katika operesheni hiyo ukiachana na hiyo bunduki kila mmoja alikuwa na bastola mbili zenye nguvu kwa operesheni za dharula, mabomu ya kutupa kwa mkono ‘fragmentantion granade’, mabomu ya kutoa moshi ‘smoke granade’ kwa ajili ya kumchanganya adui. Zaidi ya hapo kila kundi lilikuwa na mtu mwenye LPG, ‘anti-tank weapon’, silaha ya kujitwisha begani inayotumika kuvunja vizuizi wakati wa operesheni. Kwa ujumla vijana hawa walitimia kila idara.
Kutoka katika maficho walipita chini kwa chini kwenye vichaka vinene kwa minajiri ya kuzunguka kile kijiji cha Mpumbutu, wengine wakaenda mlimani na wengine upande wa chini. Iliwachukua kama dakika ishirini na tano kuzingira kijiji hicho ambacho mara nyingi waasi walipenda kujificha humo. Kisha askari wawili walijitoa chambo kuingia kijijini ili kuwafanya waasi hao kujitokeza kirahisi.
Katika moja ya vichaka kulilala watu wawili waliojifunga nyasi kavu na mbichi migongoni na kichwani kiasi kwamba wakilala kifudifudi huwezi kutambua kama ni binadamu, hawa walikuwa ni wadunguaji kitaaluma walikuwa na bunduki kubwa ya kudungulia ‘Heavy Sniper Rifle’ M82A1. Walijificha kimya kwenye kichaka kilicho juu ya kilima huku kwa chini wakikiona kile kijiji.
-------------------------------------------------------
Epuka Corona, waepushe wengine.
Kaa nyumbani kama huna ulazima wa kutoka
Nawa mikono yako kwa Sanitizer au maji yenye dawa au sabuni
#StopCorona
----------------------------------------------------------------
KIJIJI CHA MPUMBUTU
Shughuli za wanakijiji ziliendelea kama kawaida, watu walikuwa wakijpatia huduma ndogondogo katika maduka na vigenge, wengine wakipata vinywaji na kulewa ili kujisahaulisha shida zao. Pembezoni mwa kijiji hicho, ukimaliza tu nyumba za wenyeji kulikuwapo na nyumba nyingine kubwa tu, nyumba hiyo ilikuwa ya tajiri mmoja mfanyabiashara aliyeuawa na waasi na kisha wao kuichukua na kuifanya maskani yao kila waingiapo kijijini hapo. Hakuna mtu aliyekuwa akiisogelea nyumba hiyo kwa kuhofia kuuawa. Waasi waliitumia zaidi ya kazi hiyo, waliitumia kama dangulo, pale mkubwa wa waasi anapojisikia ashki ya kufanya ngono vibaraka wake walikwenda kijijini na kukamata mwanamke yoyote na kumleta humo ndani. Endapo atakataa aliuawa hadharani, hali hii iliwafanya watu wawafungia mabinti na wake zao ndani na wengine hata kukikimbia kijiji hicho.
“Hiki ndiyo kijiji cha Mpumbutu, wananchi wake hufanyiwa vitendo vya uzazalishwaji na hutendwa kinyume na haki za binadamu, serikali ya Ngoko kama haiyaoni haya, tunataka kusafisha waasi kwa mashambulizi ya kimbunga, na si wananchi, hakikisha risasi yako inampiga muasi na shabaha yako isikosee,” sauti ya kiongozi wa vikosi vya ukombozi ilisikika sikioni mwa kila mmoja.
Benson Boko aliweka jicho lake katika lensi ya bunduki lake kutoka pale alipojificha na kuchungulia, akiangalia lile jumba waliloelekezwa kwenye ramani na kisha taratibu alielekeza kwenye vijia na njia zinazopita katikati ya kijiji hicho. Akaondoa jicho na kuangalia saa yake, ilikuwa yapata saa 12 jioni. Bado si wanakijiji wala waasi waliokuwa wakijua kuwa wamezingirwa, muda ulikuwa haujafika wa kufanya kazi yao.
Itaendelea....